Kama shule za Private zikifanikiwa kumfanya kila mtoto wa primari kupata A nini kitatokea?

Kama shule za Private zikifanikiwa kumfanya kila mtoto wa primari kupata A nini kitatokea?


Sasa kama unajua Hilo mbona nyuzi nyingi humu zimekuwa za kulaumu hizi shule. Ni kama ndo chanzo Cha matatizo ya mfumo wetu wa elimu?
Mkuu, tatizo la mfumo wetu wa Elimu unaharibiwa na serikali. Kwa maana hiyo tatizo moja huzaa jingine.
Mfano.
Kutokana na sera ya elimu ya serikali kulazimisha wanafunzi wasome tuu bila kurudia/kukariri madarasa imepelekea shule nyingi za private kushindwa kujipambanua kitaaluma,njia pekee iliyobaki kwenye hizi shule ni kuhakikisha hata wale wanafunzi wasiojiweza kwenye madarasa husika wanafaulu hata kuliko wanaojiweza.
Hali hii imeziua hata zile shule za vipaji maana wanapokea wanafunzi wasio type yao.
Tatizo hili limezifanya shule za private kuwa biashara. Huku tatizo serikali ikifurahia kodi wanazolipa na afisa uhamiaji wakifurahia rushwa za walimu na watumishi wasio wenyeji wa ttanzania kwenye shule hizi.
Hilo ni tatizo ndio maana nikasema tunaandaa bomu la majobless na incopetent working class kupitia mambo makuu mawili.
Elimu shule za private ni biashara.
Elimu shule za serikali ni siasa.
**thamani halisi ya elimu haipo tena.
 
Back
Top Bottom