Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

1.Nacho amini, uwezi unyesha kila kitu ulichonacho utawapa advantage maadui wako
2.Nchi zilizokua za kikomunist ziliwekeza sana kwny jeshi bila kujitangaza, ila ikitaka kazi ziguse ndo utajua uwezo wao.
3.Kwa jwtz hii ndo outing yao kubwa kitaifa kwahiyo wansheherekea wakiwa pamoja nasi lkn bila kuuza siri za kazi.
4.Nachowapendea zaidi jwtz ukiwa nao wanajitambulisha kama JESHI LENU sio JESHI LETU.
Mfano: jeshi lenu litaenda Kongo kulinda amani, na sio hutaenda au jeshi letu litaenda ........
ALL IN ALL JWTZ NI MOJA YA MAJESHI YENYE NIDHAMU SANA DUNIANI.
Jeshi la watawala. Jeshi la CCM. Nidham kwa kwa watawala
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
kagame pale alikuwa anatuchora tu,.sisemi kwamba Rwanda itatushinda, ila kwa siku hizi, zana hizo wameonyesha ni za mwisho kabisa kutumiwa kwenye battle, kama Rwanda wanazo zana za kisasa za drones toka Israel, hizo wanakupiga vizuri tu ukienda kichwakichwa, ndio walitaka wazitumie kipindi kile watuaibishe, na wangetupa surprise kwelikweli.

sisi pia, tunatakiwa kuwa na akili, Uturuki ambao kwa sasa ni marafiki zetu sana, wametengeneza drones bora sana za kivita ambazo unazituma tu kule zinateketeza askari, Armenia imeshindwa vita na Azerbaijan, Azerbaijan ilikuwa nchi iliyoonewa sana na armenia iliporwa hata maeneo, armenia ilikuwa mbali sana kivita kuwazidi, wakaingia na mavifaru, azerbaijan wakapewa msaana na uturuki wakatumia drones tu ambazo waturuki wanatengeneza, waliwatandika waamenia hadi wakanyosha mikono na wakarudisha maeneo yao yote yaliyokuwa yameporwa. ni juzi tu hivi.

kwa hiyo na sisi utachane na masilaha ya aina hii, tunaweza kua nayo machache tu ila mengine tutumie technolojia ya kisasa zaidi, sio kwamba tuacha haya ila tuangalie nchi za wenzetu wanatumia nini.

though, kwa sasa Tanzania haiihitaji hata kupoteza pesa kununua silaha kwasababu sidhani kama kuna adui mkubwa ambaye ni nchi ni threat kwetu, hata Rwanda kipindi cha JK walikuwa wanaoogopa mno kwasababu tungewapiga au wangetupiga (jambo ambalo ni gumu kwao), they could not stand to live with a monster besides their country for therest of their lives, wasingeweza kustahimili kuishi na adui pembeni yao miaka ya mbeleni, hasa kagame ambaye anajua tungeweza kuweka hata rais mwingine akitokea Tanzania kama tukitaka kama tulivyofanya kwa m7.waasi wake wangekuja tu hapa na kuanzia safari hapa.
 
Hayo mawazo yako ila ukweli ni kwamba Tanzania huwa hawaonyeshi silaha zake mpya waziwazi. Kuanzia sasa ufahamu hilo!View attachment 2038324
Baada ya hii ndiyo yakafanywa manunuzi ya silaha (picha za awali nilizo kuwekea juu). Mi 17 zilinunuliwa zikiwemo air defensive system S-300 kutoka Russia na hizi nilizozitaja ni baadhi tu.
Hiyo screenshot sijaiona ila hakuna S300 hapa nchini. Misri na Algeria wanazo, Ethiopia ilinunua ikazipanga zizunguke anga la Grand Renaissance Dam kwa vile wana mgogoro na Misri na technically inaweza taka kulishambulia.

Mi 17 jana asubuhi imemuua CDF wa India na mke wake kwenye ajari. Na crew ya wengine 11
 
Hayo mawazo yako ila ukweli ni kwamba Tanzania huwa hawaonyeshi silaha zake mpya waziwazi. Kuanzia sasa ufahamu hilo!View attachment 2038324
Baada ya hii ndiyo yakafanywa manunuzi ya silaha (picha za awali nilizo kuwekea juu). Mi 17 zilinunuliwa zikiwemo air defensive system S-300 kutoka Russia na hizi nilizozitaja ni baadhi tu.
Screenshot nimeiona sasa. Kuna mahali unaona tumenunua Mi 17 transport helicopter au S300. Sisi Tanzania?
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Rais keshasema hatuma maadui dunia hii .... wasiwasi wa nini?

Badala ya kununua vifaru na ndege bora tu wanunue vifaa vya mahospitali zetu!
 
Mara nyingi ni vigumu kujua order zilizowekwa ni zipi labda ziwe ni kubwa na zimewekwa wazi. Ila wakati wa delivery ndio inajulikana. Haya mambo sio magumu inategemea na mtu anafatilia nini.

Watu wanafatilia utajiri wa mtu, mali zake, hisa na madeni sembuse silaha zenye regulations. Mimi hushangaa watu hujuaje vikosi, nakuwa nimekaa naangalia let's say Liverpool Vs Man City alafu mchezaji anapasha nje watu wanashangilia mtoe huyo X. Najiuliza wamejuaje X ndio atatoka na ni kweli anatoka yeye, wamejuaje X anapwaya. Huwezi ona nachangia kwenye mpira maana sijui.
Sawa Tank 14

Peace [emoji3577]
 
Uko sahihi lakini sijui unachonibishia ni nini. Unajua kama wakati huu kuna watu wako training ya silaha ambazo ni toleo jipya na hazijaoneshwa hapo uwanjani? Unajua kama kuna silaha tunazo na watu wameshapewa mafunzo tayari lakini hazijaoneshwa hapo?

Unasemaje kama silaha ndo hizi basi hatuna kitu?

Ukubali ukatae kuna silaha hununuliwa kwa dharura kulingana na mahitaji achilia mbali long term plan unazozizungumzia wewe.

Unajua kuwa kuna tabia ya soko la siri la silaha hasa baina ya nchi marafiki? au kwa kulinda maslahi ya nchi ngeni katika nchi yenye vita?

Mambo ni mengi linapokuja suala la vita. Si tu eti mikataba ya kuuziana silaha pia kuna kufake mikataba hiyo kuficha kufahamika kuwa nchi fulani ina silaha fulani.

Kwa kifupi tu.
Sipingi lolote hapa ila ujue exceptions are rare and few. Kwanza budget tu inaonesha ni silaha gani mtanunua, bado kuna operation costs and maintenance. Alafu bado kuna marupurupu sijui mishahara kwa bajeti hiyo hiyo ambayo haizidi trilioni 2.
 
Rais keshasema hatuma maadui dunia hii .... wasiwasi wa nini?

Badala ya kununua vifaru na ndege bora tu wanunue vifaa vya mahospitali zetu!

Rais keshasema hatuma maadui dunia hii .... wasiwasi wa nini?

Badala ya kununua vifaru na ndege bora tu wanunue vifaa vya mahospitali zetu!
Maonesho ya silaha ya leo lengo lake ni nini sasa!?
 
Nasema usidharau nchi hii kisa hizi siasa za kiccm ila Kuna mambo mengi hufanyika kulinda hii nchi sema Raia tunalaumu vile nchi yetu inausiri mkubwa kuliko unavoweza kufikiria.
Naamini tuko vizuri hvi vya Leo ilikuwa display tu kidogo, pia ukisema tujilinganishe sijui na USA mara Russia ni sawa na kulinganisha mbingu na ardhi
Sisi hatulaumu jeshi wala hatusemi ni dhaifu, wala hatulidharau. Sisi tunapaza sauti tuwe tiyari kila idara. Ni kama mtu akija kusema TANESCO wawe imara haambiwi anaidharau au hana uzalendo. Ingekuwa vyema tukajua ni jeshi la WANANCHI, sio jeshi la kikundi fulani wala wanajeshi wenyewe. Sisi wananchi tulipiganie liwe na nyenzo za kutulinda. Waliotakiwa kuhakikisha lina nyenzo ni hawa akina Musukuma na Babu Tale.
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Unachokisema halina maana Sana katika mbinu za kivita kwa sababu zifuatazo:-
1. Ukubwa Silaha hutokana na aina ya Maadui unao walenga au walio kuzunguka.
2. Uchumi wa nchi pia, maana kuna Silaha ambazo Zina ghalama kubwa kuanzia ununuaji Hadi utunzaji wake.
3. Ukubwa wa jeshi pamoja na technology.
Kwa hiyo Silaha ulizoziona zinaendana kabisa nguvu ya adui wa Tz, Tambua adui yetu kimapigano hawezi kuwa marekani,Urusi Wala China.
N:B vita haina bajeti( siku kikinuka utaona Silaha zaidi ya hizo ulizo ziona)
 
Ulinzi ni pamoja na kuonesha uwezo ulionao. Kwa silaha zilizooneshwa kusema kweli ni hafifu. Zimepitwa ma wakati. Uganda na Kenya wana silaha bora kutuzidi.
We are weak compared to them.
Labda Uganda ,, Kenya ni wenzetu sanaa[emoji3]
 
Kuna amani ni kwa sababu ya ukondoo wa watanzania. Na pia rushwa katika jeshi. Kimsingi jeshi limetekwa na CCM na watawala na kuwasaliti wananchi.
Usichanganye siasa za CCM na Chadema ukajua ndio jeshi lipo hivyo....
 
Back
Top Bottom