Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

Kama silaha zilizooneshwa ndio za Jeshi letu, bado tupo nyuma sana

Hujui hata mambo ya jeshi then unazarau jeshi la nchi yako linalolinda mipaka, mkuu punguza ujuaji wa kijinga.
Sio dharau mkuu. Nikisema fulani ana elimu ya darasa la saba na huyu ana PhD utasema namdharau mwenye la saba B. Yani kuwa muwazi kibongo inaitwa dharau. Nchi nyingine zinaita tenda inajadiliwa na bunge na vyombo vya habari vinahoji, watu wanaanzisha debate kushindanisha silaha gani wanunue kwa fungu walilonalo. Watu wanatoka wanaenda Dubai Airshow, Army Expo, MAKS Airshow na wakirudi wanasema ukweli walioona nchi inaamua.

Last week mpaka leo kuna matukio kadhaa. India kasaini mkataba wa kutengeneza assault rifle za Kalashnikov ya Russia. UAE imenunua Rafales 80 kutoka Ufaransa kwa zaidi ya trilioni 43 za kibongo. Finland imesaini kununua F-35 kutoka Marekani. Hizi zote zinafanyiwa mchuano mkali na tenda zinakuwa wazi na wananchi wana haki ya kuhoji.

Sisi hapa tukisema tunaitwa wajuaji na wajinga. Maana ya jeshi la wananchi haipo wala haizingatiwi. Ila Afrika ndo ilivyo hata ndoto tunazoota sidhani kama wazungu huota hivi
 
Wewe ndio muongo kupindukia. Unaona jinsi ambavyo dereva wa Fuso atapata ugumu kumwambia shika semi uendeshe mpaka Burundi? Sasa huo ugumu ni mdogo sana kulinganisha na tank driver wa T-59 ambayo ni type ya 1960s alafu umwambie aendeshe model ya 1990s. Silaha zinatengezwa kiasi kwamba ambaye hajafundishwa hiyo silaha haitumii. Kwenye kununua silaha kuna mkataba wa kufundisha na kutoa spares, South Africa walinunua Saab Jas 39 Gripen fighters miaka ya 2010s mwishoni ila mwaka huu wameziground kisa hawana spares na training inasuasua. Syria alinunua air defence kutoka Russia ila mafunzo ya kuzitumia yalizidi miaka miwili. Hapo kama ni adui amesubiri umalize mafunzo?

Kwanza huwezi nunua silaha leo ukapewa leo. Hizo J-7G tuliagiza mwaka 2012 zikaja 2014. Kwa nini msiache kuongea ambayo hamjui. Eti kombe la dunia linaanza mwezi huu, alafu wewe ndio unatafuta wachezaji kwenye vilabu
Uko sahihi lakini sijui unachonibishia ni nini. Unajua kama wakati huu kuna watu wako training ya silaha ambazo ni toleo jipya na hazijaoneshwa hapo uwanjani? Unajua kama kuna silaha tunazo na watu wameshapewa mafunzo tayari lakini hazijaoneshwa hapo?

Unasemaje kama silaha ndo hizi basi hatuna kitu?

Ukubali ukatae kuna silaha hununuliwa kwa dharura kulingana na mahitaji achilia mbali long term plan unazozizungumzia wewe.

Unajua kuwa kuna tabia ya soko la siri la silaha hasa baina ya nchi marafiki? au kwa kulinda maslahi ya nchi ngeni katika nchi yenye vita?

Mambo ni mengi linapokuja suala la vita. Si tu eti mikataba ya kuuziana silaha pia kuna kufake mikataba hiyo kuficha kufahamika kuwa nchi fulani ina silaha fulani.

Kwa kifupi tu.
 
Sio dharau mkuu. Nikisema fulani ana elimu ya darasa la saba na huyu ana PhD utasema namdharau mwenye la saba B. Yani kuwa muwazi kibongo inaitwa dharau. Nchi nyingine zinaita tenda inajadiliwa na bunge na vyombo vya habari vinahoji, watu wanaanzisha debate kushindanisha silaha gani wanunue kwa fungu walilonalo. Watu wanatoka wanaenda Dubai Airshow, Army Expo, MAKS Airshow na wakirudi wanasema ukweli walioona nchi inaamua.

Last week mpaka leo kuna matukio kadhaa. India kasaini mkataba wa kutengeneza assault rifle za Kalashnikov ya Russia. UAE imenunua Rafales 80 kutoka Ufaransa kwa zaidi ya trilioni 43 za kibongo. Finland imesaini kununua F-35 kutoka Marekani. Hizi zote zinafanyiwa mchuano mkali na tenda zinakuwa wazi na wananchi wana haki ya kuhoji.

Sisi hapa tukisema tunaitwa wajuaji na wajinga. Maana ya jeshi la wananchi haipo wala haizingatiwi. Ila Afrika ndo ilivyo hata ndoto tunazoota sidhani kama wazungu huota hivi
Point
 
Uko sahihi lakini sijui unachonibishia ni nini. Unajua kama wakati huu kuna watu wako training ya silaha ambazo ni toleo jipya na hazijaoneshwa hapo uwanjani? Unajua kama kuna silaha tunazo na watu wameshapewa mafunzo tayari lakini hazijaoneshwa hapo?

Unasemaje kama silaha ndo hizi basi hatuna kitu?

Ukubali ukatae kuna silaha hununuliwa kwa dharura kulingana na mahitaji achilia mbali long term plan unazozizungumzia wewe.

Unajua kuwa kuna tabia ya soko la siri la silaha hasa baina ya nchi marafiki? au kwa kulinda maslahi ya nchi ngeni katika nchi yenye vita?

Mambo ni mengi linapokuja suala la vita. Si tu eti mikataba ya kuuziana silaha pia kuna kufake mikataba hiyo kuficha kufahamika kuwa nchi fulani ina silaha fulani.

Kwa kifupi tu.
Silaha mpya ilizonunua TZ ni zipi!? A-100 hatujaziona zimeenda wapi!?
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Hebu kazijaribu hizo silaha, kwani hazi ui?
 
Vijana wengi wanaangalia movies zinawachanga sana, hawajui mambo kwa ground ni tofauti kabisa.

Tanzania ni nchi ya Kijamaa, mambo yake mengi ni siri, hicho wanachoonyesha sicho kilichopo...

Kila Mwaka bajeti ya wizara ya Ulinzi na usalama inatengwa tena ya kutosha, umewahi kusikia wametangaza kununua hiki ama kile...

Ukiona umekaa sehemu unashushia bia na nyama choma tena kwa amani kabisa jua kuna wanaume hawalali huko.
Yaani hii ni kwel aisee... kuna kipindi tulikuwa tunatoka doria usiku ya maliasili. Njia tukiyopita ilikuwa ikatisha kwenye kambi ya jeshi sasa bhana tukasimamish2a huo usiku. Siku ndo nikaelewa kweli kuna wakati wazalendo wanatulinda usiku kucha sisis tumelala tu kama ngedere, tunachekelea tu amani tuliyonayo.... ila kimsingi nchi yetu inalindwa kwa dhati na ari ndo maana vyombo vya ulinzi na usalama siwez wadharau hata siku moja... akinikuta barabarani akanipa tena ntamshukuru...

Imagine watu wanahoj mtu kukamatwa kwa jamaa kabla ya kutenda uhalifu halafu, mtu mwingine anahoji kwani amefanya kosa gani hadi akamatwe.... jaman jaman... tuipende amani yetu na tuilinde kwa hali na mali... i wish hata nngetaman kuwa sehemu ya usalama... ili nam nionyeshe mchango wngu kwa nchi wa moja kwa moja...
 
Heshima yako mkuu!

Kabla sijasoma post yako hata mimi nlichangia hoja hapa kuwa kuna nchi kama Kenya na Ethiopia. Hizi nchi ktk ukanda wetu zimepiga hatua kubwa mno ktk uwekezaji jeshini.

Hatuwez leo kusema tuna kikosi bora kwa kuwa tuliwapiga M23 au waasi wengine, ilishawahi kutokea miaka ya nyuma Tz tukashika namba ishirin na kitu kwenye vikosi bora ulimwenguni, watu tukasifia mno.

Lakini huwez amini mkuu, China, Korea zote mbil n.k hawamo mle ndan, je kusema sisi ni bora kulia wao? Tumekuwa watu wa kusifia hiki chombo lakini kiuhalisia hakina sifa ambazo zinazo.

Kwa zama hizi tuna jeshi la kawaida mno, tena tusije thubutu jifananisha na majeshi mengine hapa Afrika.
Hilo jeshi la Ethiopia unalosifia..mbona limechezeshwa segere na Tigray
 
Vijana wengi wanaangalia movies zinawachanga sana, hawajui mambo kwa ground ni tofauti kabisa.

Tanzania ni nchi ya Kijamaa, mambo yake mengi ni siri, hicho wanachoonyesha sicho kilichopo...

Kila Mwaka bajeti ya wizara ya Ulinzi na usalama inatengwa tena ya kutosha, umewahi kusikia wametangaza kununua hiki ama kile...

Ukiona umekaa sehemu unashushia bia na nyama choma tena kwa amani kabisa jua kuna wanaume hawalali huko.
Kuna amani ni kwa sababu ya ukondoo wa watanzania. Na pia rushwa katika jeshi. Kimsingi jeshi limetekwa na CCM na watawala na kuwasaliti wananchi.
 
Sio dharau mkuu. Nikisema fulani ana elimu ya darasa la saba na huyu ana PhD utasema namdharau mwenye la saba B. Yani kuwa muwazi kibongo inaitwa dharau. Nchi nyingine zinaita tenda inajadiliwa na bunge na vyombo vya habari vinahoji, watu wanaanzisha debate kushindanisha silaha gani wanunue kwa fungu walilonalo. Watu wanatoka wanaenda Dubai Airshow, Army Expo, MAKS Airshow na wakirudi wanasema ukweli walioona nchi inaamua.

Last week mpaka leo kuna matukio kadhaa. India kasaini mkataba wa kutengeneza assault rifle za Kalashnikov ya Russia. UAE imenunua Rafales 80 kutoka Ufaransa kwa zaidi ya trilioni 43 za kibongo. Finland imesaini kununua F-35 kutoka Marekani. Hizi zote zinafanyiwa mchuano mkali na tenda zinakuwa wazi na wananchi wana haki ya kuhoji.

Sisi hapa tukisema tunaitwa wajuaji na wajinga. Maana ya jeshi la wananchi haipo wala haizingatiwi. Ila Afrika ndo ilivyo hata ndoto tunazoota sidhani kama wazungu huota hivi
Nasema usidharau nchi hii kisa hizi siasa za kiccm ila Kuna mambo mengi hufanyika kulinda hii nchi sema Raia tunalaumu vile nchi yetu inausiri mkubwa kuliko unavoweza kufikiria.
Naamini tuko vizuri hvi vya Leo ilikuwa display tu kidogo, pia ukisema tujilinganishe sijui na USA mara Russia ni sawa na kulinganisha mbingu na ardhi
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Ndo maana walichakazwa vibaya sana walipoenda kukabiliana na magaidi wa Mocambic pale Kitaya, wakatelekeza vifaru
 
Hakuna cha movie hapa Mzee. Jeshi letu lipo outdated. Tunatakiwa ku modernize. Tunaona display za silaha kwa majirani zetu. Uganda na Kenya.
Hao Waganda na Wakenya wanahenyeshwa na vijana kutoka Somalia si mchezo
 
Tofautisha silaha za maonyesho na za kivita.zile ni za kuonyeshea
 
Here again mzee!

Mkuu wewe ulitaka kujua Jwtz imenunua nini na ukajua? 2017 hadi 2020 kwa mfano
Mara nyingi ni vigumu kujua order zilizowekwa ni zipi labda ziwe ni kubwa na zimewekwa wazi. Ila wakati wa delivery ndio inajulikana. Haya mambo sio magumu inategemea na mtu anafatilia nini.

Watu wanafatilia utajiri wa mtu, mali zake, hisa na madeni sembuse silaha zenye regulations. Mimi hushangaa watu hujuaje vikosi, nakuwa nimekaa naangalia let's say Liverpool Vs Man City alafu mchezaji anapasha nje watu wanashangilia mtoe huyo X. Najiuliza wamejuaje X ndio atatoka na ni kweli anatoka yeye, wamejuaje X anapwaya. Huwezi ona nachangia kwenye mpira maana sijui.
 
Ndo maana walichakazwa vibaya sana walipoenda kukabiliana na magaidi wa Mocambic pale Kitaya, wakatelekeza vifaru😀
Magaidi wanastukiza na sio kuweza kupigana, Hakuna kundi lolote la kigaidi lenye kuweza kupigana na jeshi, Ingekuwa rahisi hivyo, serikali nyingi zingeshaanguka,gaidi ni SAwa na panyaroad wao uvizia na ushambulia
 
Nimetazama maazikisho ya miaka 60 ya Uhuru. Kwa silaha tulizoonesha zinanipa wasiwasi na uwezo wa jeshi letu.

Vitu vingi vilivyooneshwa ni silaha zilizotumika kipindi cha USSR.
Kuna BM 21. Kwa kweli tunatakiwa Ku modernize jeshi letu. Bado lipo nyuma sana.
Jeshi la Mwaka 47
 
Back
Top Bottom