Kama sio tajiri na huna asset, kusomesha watoto shule za gharama ni ujinga unaongeza umaskini kwenye ukoo

Kunandungu yangu anasomesha kwa milion 5 kwa mwaka,watoto watatu wameanzia la kwanza private ad form four wa kwanza anamaliza mwaka huu

Hua napiga maesabu hizi milion 5 kwa mwaka Hadi wafike chuo sio chini ya milion 60 ad 80,hizi Hela ukiwanunulia madogo Kila Mmoja Kosta wakimaliza versity siwatakuja kuzipigia kazi kujiajiri kuliko kutumia nguvu nyingi mwanzo wakishamaliza utaskia mzazi anamwambia mtoto Mimi kazi yangu ya kukusomesha nishamaliza pambana kivyako
 
Mambo yanabadilika na Kila nyakati zina namna yake fanya Yake. Fanya yalio ndani uwezo wako ungekuwa umewahi kuwa kwenye panel ya interview Ukiona vijana wavyoteseka kisa lugha tu.

Hata law school pale kinachowafelisha wengi lugha inachangia . Wakenya kinawabeba lugha tu Ila wa kawaida tu Kama sisi sana

watalamu wanakubali kuwa mtoto aelewe vizuri anachofundishwa lazima afundishwe kwa mother tongue.
Nimewahi kufundisha kidato Cha kwanza yaan wtt wanateseka Sana na kukata tamaa mm nashauri serekali iitishe kura ya maoni tuamue lugha ya kufundisha primary mpaka chuo kikuu. Kwa waliowahi kufundisha watalikubali hili.
 
Noma hiv unaanzaje kumpeleka mtt wako shule ina walimu 10 wanafunzi 600+ walimu wenyewe wanamtumia mtoto wako ndo awauzie biashara zao za kababu na barafu shuleni
Hatujadharau Ila shule ya jirani hapa wapo 160 + darasani la nne wtt inabidi mzazi uwe na Muda kutosha kumfatilia mwanao Mungu amjalie ajitambue vinginevyo.
 
Ni kweli kwamba uwezo wa mtu unaweza onekana popote ila sio vibaya kumpa mwanao elimu nzuri.
 
Tatizo ya tz tuna watu wanamawazo ya biashara za survival mode tuu. Hayo unayosema wewe hututaki na kwa kuwa hatutaki basi tukubali kuwa watumwa wa wadhungu mpaka pale yesu atakaporudi
 
Huwaga wanawadai wazazi wao kazi..
 

Kwenye paragraph yako ya mwisho, elimu nayo ni asset. Pia curriculum na syllabuses ni zile zile.
Elimu hii hii ya kibongo mkuu?
 
Hii mbinu ijaribishe kwako mkuu, yaan uanze kusave m5 kila mwaka afu ununue Costa uone kama ni rahisi, kilimo cha tikiti kwenye karatasi ni rahisi sana
 
Tatizo watanzania wengi ni bendera fwata mkumbo. Hawafanyi vitu kwa kutumia akili zao wenyewe, kufanya uchambuzi wa kina na kuangalia uhalisia wa maisha yao, ndio maana mwisho wa siku, wanajikuta wana nasa. Yani watanzania ni watu wa kuigaiga tu. We angalia jinsi wanavyoigana kununua magari, kwamfano gari kama nissan dualis, subaru forester, toyota crown athlete, escudo etc etc.

Kuna watu wanachukua mikopo mikubwa mikubwa benki ili wasomeshe watoto wao shule za gharama, ili waonekane na wao wako fresh, mwisho wa siku wanaumia tu, nyumba zinauzwa na mabenki kila siku, na asilimia kubwa wanaoleta haya matatizo yote ni wanawake, wanaharibu sana watoto.
 
Hii mbinu ijaribishe kwako mkuu, yaan uanze kusave m5 kila mwaka afu ununue Costa uone kama ni rahisi, kilimo cha tikiti kwenye karatasi ni rahisi sana
Mkuu save Hela madogo zije ziwasaidie baadae kujiajiri,tatizo wazazi wamekalili mtoto asome aje kua dakatari,injinia,wakishamaliza wanabaki wanabaki wamejishikiza na vimshahara vya laki 2,kwasasa supply ni kubwa mno kuliko demands,na madogo wanafaulu kweli,wakati unasomesha usisahau kusevu Hela kwa ajili ya madogo baadae,sio unatumia nguvu nyingi mwanzoni akimaliza unamtelekeza
 
Me nadhani bora huku kwenye elimu ya chini ndo uwekeze zaidi kwa mtoto uko juu anakua tayari keshajitambua lkn pia anamsingi mzuri uliomjengea tangu awali anaweza akaandelea vzr tuu
 
Mshahara haueleweki, unakuta mtumishi anasomesha watoto watatu shule ya mabasi ya njano, Kivumbi na jasho.

Sehemu nyingine familia haina kipato Cha uhakika mathalani ni wafabiashara ndogondogo nao huingiwa na ulimbukeni kupeleka watoto huko matokeo yake ni madeni na maisha ya aibu.

Wazazi wengine huenda mbali zaidi mpaka kuuza ardhi ya familia Ili wapate ada ya shule.
 
Namba moja naomba ukiwa nikumbuke kwenye uwaziri wa afya hakika una kitu na utafika mbali

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Point nzuri sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…