OMOYOGWANE
JF-Expert Member
- Dec 30, 2016
- 4,701
- 11,920
- Thread starter
-
- #81
Now atakuwa na adabu ya kutoshaKuna mshikaji mmoja alikuwa jeuri sana kwa mabosi zake. Alikuwa ana uwezo wa kujibu nyodo anavyojisikia. Hapo ni kazi anafanya Serikalini. Baadae mambo ya dharau yalivyozidi waliamua kumuhamisha na akawekwa chini ya mtu ambapo pamoja na dharau zake alikuwa hawezi kufurukuta. Na ajabu zaidi hakupewa JD yoyote akabaki anauza sura tu ofisini. Baada ya miezi kadhaa akaamua kuacha kazi na kwenda kwenye kampuni nyingine. Hiyo kampuni akahama tena akapata nyingine. Kabla hajaanza hiyo kampuni ya nyingine ikabidi wafuatilie background ya jamaa kote alipopita. Walimchafua vibaya sana.
Sasa jamaa ana zaidi ya mwaka hana kazi. Nauli tu imekuwa ni shida sana.
Umenena msg...Habari wakuu!!
Huu ni ushauri kwa watu wote waliopo kwenye ajira sehemu mbali mbali serikalini au makampuni binafsi n.k,
Haiijarishi wewe ni polisi, mwanajeshi, Mwalimu, daktari, mhasibu, sekretari, mwandishi wa habari, kiongozi wa kisiasa, Modetator JF n.k hata kama unalipwa elfu moja kwa siku, heshimu sana kazi yako na ipende kama unavyompenda mke wako au watoto wako.
Siku ukipoteza hiyo kazi sio ajabu kujikuta unapoteza na vitu vingine vya muhimu kama vile mke, heshima, marafiki ndugu hata biashara uliyoamua kuianzisha nayo ikafa kifo cha mende,
Hakuna watu wanafiki kama walio maofisini, hakikisha hupotezi kazi baki huko huko na wanafiki wenzio maana siku utakapopoteza kazi hakuna atalayehangaika na wewe hapo ofisini kwako ulipo sasa ama huko utakakokuwa unapereka vyeti na CV zako narudia tena hskuna atakayehangaika nawewe,
Siku ukitaka kujitolea watapokea CV zalo ulizotype na kuprint kwa pesa ya msaada kama umezipereka private watakuambia watakupigia simu na hiyo ndio bye bye, kama ni serikalini hayupo mkurugenzi, au mkuu yeyote atakayehangaika na makaratasi yako yatawekwa kwenye faili yaungane na barua za wenzako za mwaka juzi ambazo hazijajibiwa,
haijarishi unalipwa laki moja au mbili kwa mwezi, haijarishi unalipwa mamilioni, haijarishi unatembea kwenye gali zuri la serikali au kampuni, nguvu uliyonayo sasa ndiyo inayokufanya uheshimike na kuchangamkiwa unapokwenda kikazi kwenye taasisi zingine,
UMASIKINI HAUNA TOFAUTI NA MAKALIO YA MBWA!
Wasio na kazi au ajira hawajapenda au kutaka wawe hivo bali ni competition kali iliyopo mitaani
kijana kama wewe ni boda boda umeoa unawatoto na unarisha familia heshimu sana hiyo kazi
Mwenye macho na asome kisha atafakari
Nawasilisha.
Umemaliza kila nilichotaka kuandika. Kiukweli kuongeza chanzo kingine cha mapato ndo jambo litakalomweka mtu huru. Na ili kuongeza kipato inahitaji roho ngumu na mipango thabiti ya muda mfupi na mrefu. Umeongelea hili tatizo la waajiriwa wengi anapata mshahara na kukimbilia kukopa ili ajenge au kununua gari. Sio jambo baya lakini kibiashara haiko sawa sana kwasababu hela iliyowekezwa hairudi na kuishia kuishi maisha magumu sana yenye kitanzi cha mkopo. Nawashauri watu wazingatie hii comment yakoMentality ya Kuajiriwa naona ndio inatuweka kuwa watumwa,....sisemi kuwa kuajiriwa ni kubaya la hasha. Nasema, unaajiriwa na kuanza mchakato wa kuangalia mbele baada ya miaka kadhaa malengo yangu ni yapi? Kwenye kuajiriwa kuna fanya mwaajiriwa kutofikiri nje ya Box, kwa maana kua anaangalia mwisho wa mwezi atapata mshahara, hata kama hautoshi(Na hautatosha maisha yote), yeye atajituma muda woote kufanya kazi ya kuajiriwa!
Sasa basi, suluhisho ni, tumia kazi ya kuajiriwa kama ngazi ya kuanza kujijenga, ukitumia kipato cha kazini, anza kuchukua mkopo wa kuanzisha kijibiashara.....usianze biashara kubwa, anza kitu kidogo kama hata kibanda cha kuuza vocha na soda. baada ya kumaliza mkopo huo, biashara inakua yako na ndio faida......chukua mkopo mwengine, anzisha biashara nyengine, hata kinyozi na kuendelea.
Baada ya miaka michache, utakuta umekua mjasirimali na vibiashara kadhaa. Anza kulea na kuboresha hizo biashara.
Itafika wakati, hizo biashara zako zinakupa zaidi ya mshahara............hapo sasa ndio unaweza kuachia pole pole huo utumwa.
Tatizo wafanyi kazi wengi huanza na kuchukua deni kununua gari...kujenga nyumba, kununua makochi..na kadhalika!
Kuajiriwa ni Slavery ndungu zangu.........mimi ni muajiriwa, lakini, ningepata ushauri mapema, ningekua Muajiri kwa sasa!
Yani amekuchoka sana.., hapo ni week tu imekata 😅😅😅Na akifika oficin mda wa lunchtime
Stori na marafiki zake ni wewe anaomba ushauri akufanyaje maana huna mbele wala nyuma
Ndio hivyo hawajaumbwa kutoa ila kupokeaYani amekuchoka sana.., hapo ni week tu imekata 😅😅😅
Tupe experience yako mkuuSibishani Mpwa wala sikatai ila naamini kwamba kila binadamu ana uwezo wa ku--survive kutokana na mazingira! Kikubwa usikate tamaaa. Mimi ni mfano
Ndio hivyo hawajaumbwa kutoa ila kupokea
Tumewaendekeza kwa kuwasogeza mpaka jikoni mkuuMnawaendekeza tu, mie wangu anatoa vizuri na anaelewa kuwa maisha ndivyo yalivyo
Yeah eti oh wanawake ni watu wa kupokea tu! Kama unakula zangu na zako lazma nizile ndio mfumo wa lifeTumewaendekeza kwa kuwasogeza mpaka jikoni mkuu
Kuna utofauti kati ya kuogopa na kuwa makini, huu uzi ni wa tahadhari tu,Kuogopa Kufukuzwa Kazi ni uoga wa maisha
Nani kasema. Marafiki zangu wote ni wa shuleni, mtaani rafiki ningempata wapi sasaHata shuleni,
Hahahaah niliwahi kuandika Mara nyingi ila kwa kirefu zaidi niliandika I think 2015-2016 hapo sikumbuki! Ila ninachoweza kukushauri ni kwamba, mshukuru Mungu saana sana unapokosa kazi ujue kuna milango mingine mwenyezi Mungu anakupa nafasi kujua mema makubwaTupe experience yako mkuu
Mhhm!!!!,hivi kuna kazi inayoweza kukufanya mtumwa kweli???.Kazi isikufanye mtumwa.
Sisi ma atheist, matumaini yetu tunaweka kwenye logic na science 😃Hahahaah niliwahi kuandika Mara nyingi ila kwa kirefu zaidi niliandika I think 2015-2016 hapo sikumbuki! Ila ninachoweza kukushauri ni kwamba, mshukuru Mungu saana sana unapokosa kazi ujue kuna milango mingine mwenyezi Mungu anakupa nafasi kujua mema makubwa
Whatever, tumia hio hip Logic and science kujua kuwa kuna fursa nyingi nje ya ajira (kuajiriwa)!!Sisi ma atheist, matumaini yetu tunaweka kwenye logic na science 😃
Sio tuu kustaafu bali akiishiwa Salio mwisho wa mweziWaajiriwa wengi hawana ujanja wa kuishi nje ya mshahara thus wakistaaafu ni lzm wafe mapema