Mtoa mada umenena vyema kabisa, tena ukiambiwa laki 3 beba 6, na zifiche kwa kugawa makundi, tafuta kipensi cha jinsi shonea mifuko migumu kwa fundi cherehani wako then zigawe hela, pili epuka mazoea kisa tu umemsikia mtu anaongea kiswahili, wengi wao sio watu tena, wanafosi maisha so mswahili mwenzio kukuua ni chapu sana.
Epuka watu haswa waswahili wasijue mfumo wa maisha yako.
Kuhusu tax ama daladala hakunaga konda so jitahidi sana ukae siti za katikati kama bado hujapazoea. Uwe na uwezo mkubwa wa kukariri mazingira, hili ni muhimu sana.
Nimeingia south kupitia beitbridge, (Zimbabwe na south border, Kopfontein/Tlokweng, Botswana na south, Martin drift, Botswana na south, ktk boda hizo nashauri pitia za Botswana na south, Beitbridge ukiingia tu unaanza kukutana na usela mavi wa wasouth pale misina.
Kiufupi south kila mtu ana stress, anatamani maisha mazuri ya shortcut.
Usimuamini askari au polisi mia kwa mia nao no wezi wakubwa sana tu. South ya leo nenda kibiashara utoke sio pa ku hustle tena.
Mwaka mpya kuingia 23 saa 10 jioni nilipigwa visu vitatu mkononi na pajani kimoja kisa simu tu.
Kiufupi sio salama kabisa na napachukia sana, kama huendi kibiashara eti ni ku hustle aisee nashauri hustle hapahapa bongo.