Kama una mpango wa kuja South, zingatia mambo haya sita kabla ya kuanza safari yako

Ndugu yangu domokeka alizamia huko miaka 15 iliyopita mpaka leo hatujawahi wasiliana nae. Sijui mzima au ashachinjwa. Maana na yeye aliendekeza sana usela mavi. Si unajua watoto wa tandale kwa tumbo tena!
 
Abiria wote ni makondakta unampa jirani yako nauli na unachukua chenji yako kama ipo, wa mwisho ambaye amekaa karibu ya dereva anamkabidhi dereva pesa kamili na ikipungua ni juu yako kufidia, vinginevyo utasurubiwa na dereva.
Huu ni ujinga wa kusululishana bila sababu ya msingi ingelikua huku bongo dereva wangelikua wanasikosa pesa zote kwa mfumo huu.
 
Wale ambao hatupendi kuwa watumwa wa lugha za wakoloni ndo basi tena?
 
Ni mfumo wa zamani sana ndo unaotumika kwetu. Lakini sometimes naelewa. Nchi zetu bado hazijaendelea. Watu wengi wanategemea usafiri wa umma ambao kuupanda kwake tu ni kwa fujo, kubanana na kujaza kupita kiasi ili kila mmoja awahi anapokwenda hasa makazini asubuhi, na nyumbani jioni.

Ukiwawekea ustaarab wa huku wa kujikusanyia hela wenyewe, inamaana wengi hawatolipa na dereva hatoweza kujua idadi ya waliopanda daladala. Maana ni mwendo wa kugombania, kubanana nk.
 
Are you new in town🤣🤣😂 unabaki unakodoa macho
 
Ndugu yangu domokeka alizamia huko miaka 15 iliyopita mpaka leo hatujawahi wasiliana nae. Sijui mzima au ashachinjwa. Maana na yeye aliendekeza sana usela mavi. Si unajua watoto wa tandale kwa tumbo tena!
Inawezekana akawa ashakufa, yupo jela au mtaani ila kapoteza na kuacha kuwasiliana na familia. Kama yupo hai basi kuna siku tu utapata habari zake.
 
Naskia wazulu ndio wakurya wa south africa wanapenda fujo na ubabe balaa
Wakurya ni watoto wadogo sana mbele ya hawa jamaa. Wakurya wanafujo za mmoja mmoja hasa akikukuta raia ni mnyonge. Ila wakurya hawana ujanja wa kulianzisha kupambana na serikali.

Ila hawa jamaa tukianza kwenye historia mfalme wao Shaka Zulu ndio aliekuwa na nguvu kuliko mfalme yoyote katika nchi zote za kusini mwa Afrika. Aliwahenyesha wazungu mpaka wakaja na style ya kioo 🤣🤣🤣 (kweli mzungu noma)

Wazulu chini ya uongozi wa Shaka Zulu walitembeza kipigo kwa kila aliekuwa sio mzulu mpaka ikapelekea wangoni kusambaratika wengine wakakimbilia Tanzania, wengine wakakimbilia Malawi, wengine Zambia nk. Kama hiyo haitoshi wakavamia mpaka Msumbiji tena mji mkuu maputo wakateka watu na kwenda kuwafanya watumwa wao na wengine kuwazalisha. Kama hiyo haitoshi wakatembeza kipigo kwa jamii nyingine iliyokuwa karibu yao hadi jamii hiyo ikakimbilia katika eneo ambalo leo hii ndio linaitwa Swaziland.

Kama hiyo haitoshi wakatembeza kipigo tena kwa jamii nyingine ya Ndebele hadi jamii hiyo ikakimbilia Zimbabwe na kuanzisha makazi na kuwa kabila rasmi la Zimbabwe. Hapa hapa tu walianzisha fujo mwaka 2019, baada ya raisi mstaafu ambae ni wa kabila lao kukamatwa. Fujo hiyo ilikuwa kubwa hadi kupelekea kutumwa jeshi la taifa kuingilia kati baada ya vyombo vyote vya ulinzi kushindwa kuwatuliza.

Sasa kabila la namna hiyo unawezaje kulifananisha na wakurya ambao hawana historia yoyote. Leo hii popote utapokwenda iwe nchi yoyote ya Afrika, Ulaya au Marekani ukiuliza kuhusu makabila ya South kila mtu atakutajia wazulu. Jamaa wanashika mila zao balaa, wana umoja balaa. Fikiria wana mpaka dini yao ya shembe na inatambulika kitaifa. Sometimes mpaka viongozi wa kitaifa ambao ni kabila lao na imani yao huudhuria ibada zao mchana kweupe.
 
Aisee chief natamani ungekuwa unanipa hii story live maana kuandika kunachosha ...hio story ya shaka zulu na wazungu kutumia staili ya kioo iko vipi maana sijaielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…