Kama unajitafuta nje ya Dar es salaam, sahau kuhusu utajiri

Kama unajitafuta nje ya Dar es salaam, sahau kuhusu utajiri

Mtoa mada are you serious kwa hichi ulicho andika,nenda tunduma,kahama,makambako,Mwanza Mbeya,nenda mafinga nenda katoro uone vijana wapo simple in appearance lakini account inasoma 9 digits na hawana ngebe,shauri yako ukiwa na mtazamo huu utaishia kutazama magorofa ya wahindi hapo Dar huku wezako wakiwa wanajenga ya kwao mikoani.
 
Inategemea na shughuli unayoifanya.kila mkoa unafursa yake ambayo unaweza kuifanyia kazi na ukafanikiwa vizuri tu
 
Mikoani Kuna madini unajichimbia tu popote maisha yanaenda vipi Dar Pana madini gani
 
Dar matajiri wengi utajiri wao wameutolea mikoani, wengine wamehamia baada ya kutoboa kimaisha.
Wewe ambae unategemea kuishi kwa ujanja ujanja kwa kigezo eti dar huwezi kulala njaa, utazeeka unatafutia tumbo lako na kujidai unamjua kila tajiri kwenye vijiwe vya kahawa

Jioni ikifika unaenda kuoga kwenye bafu lisilo na mlango unaweka Shuka mlangoni.
Weekends wazee wa harakati hawapo mjini ,utawakuta Morogoro ndani ndani,ifakara huko,handeni hapo mkata ,mradi kuna mahala wanaenda check maendeleo ya uwekezaji ,j3 kama kawa wapo mzigo
 
Ila Wewe pole sana Tena mikoani kutoboa rahisi kuliko dar
Though Mimi ni mzaliwa wa Dar from newborn to college mpk kazi na maisha ila Niko Mkoa Kwa Sasa Kwa short time bwanaa ukitulia fursa zipo abundantly Rudi Mpwayungu nikuoneshe machimbo
Mkuu unabishana na mtu anaye Jutia jinsia yake?
 
Huu ndo ukweli vijana wenzangu ambao mnapambana kucha kutwa kutafuta unafuu wa maisha ndani ya Bongo hii ila mkiwa nje ya mkoa wa Dar Es salaam ahsee kuja kutoboa sio simpo kihivyo.

Sio kwamba hakuna waliotoboa ila walifanikiwa kwa kuchelewa huku wakiwa wamechoka sanaa, ukiwa kijana wa sasa kizazi kipya inabidi akili yako iwe very smart inayoendana na ushindani na ubunifu wa kisayansi au teknolojia.

Ndani ya jiji la Dar es salaam population rate inakupa nguvu ya kutafuta maana wateja ni watu huwez kwenda kutafuta lindi kwenye watu wachache waliofulia unaacha mji wa kibiashara kama Dar es Salaam

Vijana tupambane kuukataa umasikini, maisha ya sasa niyakukimbizana vibaya mno yaani, tumia akili kutafuta sio nguvu.

Mwisho kabisa fanya kazi zote ila sio Ile ya halmashauri.
20231112_073835.jpg

Sawa mwalimu tunajitafuta
 
Kuna wengine pia tunaamini ukiwa Tz ni ngumu kutoboa, bila makandokando na kuwa chawa wa chama au mtu fulani maarufu, nahisi ni imani tu popote kambi.
 
Wanaandika pumba.
Endeleeni kuamini ni Pumba! Lakini Dar watu wanabadili maisha ila wanaopotea ni wengi kuliko wanafanikiwa!
Hapa Dar usipojisimamia kila siku madeni na kuishi maisha ya kusadikika huku mob psychology ndo uangamivu wa vijana wengi!
 
Kwa hiyo walioko dar wote wanatuzidi maisha tuliopo shy n.k
Dar kuna watu wenye maisha mabovu kazi kurundikana mabondeni tu!
Yaani vijana wa Kahama au Njombe uwalinganishe na vijana wa Dar wanaokaa Mazense au Kigogo kweli wanaoshindia vibarua vya elfu 8!
 
Back
Top Bottom