zerominus10
JF-Expert Member
- Aug 25, 2022
- 8,142
- 13,721
Naona Walevi wamepigwa spana mara 2+1 Kor 6:9-11 SUV
Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi.
Sawa Mama Mtumishi emu nipe Neno la leo linasemaje leo Jumatatu yangu nataka iwe na upako nikutunukie na taji la uzima km zawadiHahaa, soma kwa makini, mkuu. Hiyo ya kwanza ni WEVI(WEZI/WAIBAJI/THIEVES)
Katika mijadala na malumbano ya hoja hapa JF, kuna watu wengi waliojaa hasira vifuani mwao. Wanakasirishwa na maneno au vitendo vidogo vinavyoweza kuepukika...Usiseme natukana watu, soma mpaka mwisho utajua kwanini kichwa cha uzi kimeandikwa hivyo.
Katika mijadala na malumbano ya hoja hapa JF, kuna watu wengi waliojaa hasira vifuani mwao. Wanakasirishwa na maneno au vitendo vidogo vinavyoweza kuepukika.
Yafuatayo ni baadhi ya mambo madogo ambayo mara nyingi humfanya mtu aliyejaa hasira akasirike:
Mambo ni mengi, ongezea na wewe...
- Akiulizwa maswali magumu – Wakati wa mijadala, mtu anaweza kuulizwa maswali yanayohitaji ufafanuzi wa kina au uthibitisho wa madai yake. Badala ya kuchukulia maswali hayo kama fursa ya kueleza hoja yake vizuri, mtu aliyejaa hasira anaweza kuhisi kama anashambuliwa au anawekewa mtego wa kumfanya ashindwe kujibu. Anaweza kuona kama anaonewa, anadharauliwa au kulazimishwa kukiri kuwa uzi wake hauna mashiko
- Akikosolewa uandishi wake – Akikosea kuandika na watu wakalenga tu kuonyesha makosa hayo badala ya hoja yake, anachukia na kukasirika.
- Akitajwa jina au akiona emoji ya kejeli – Emoji kama 😂, 🤦♂️, au 😏 zinaweza kumuudhi sana. Na akitajwa jina lake, anaweza kuona kama vile anapigwa vita moja kwa moja na kwa sababu hiyo anajaa hasira.
- Akipachikwa jina la dharau – Akiitwa majina kama "mjinga," "chawa” au "hater," anapandwa na hasira haraka.
- Akiambiwa akapime afya ya akili – Anaweza kuona kama amedharauliwa au kutiliwa shaka akili yake.
- Akishutumiwa kwa lengo ambalo hana – Mfano, akionekana kama ana ajenda fulani ya siri, anaweza kujihami kwa hasira.
- Akijibiwa tu kwa "OK" au "Sawa" badala ya maelezo marefu – Anaweza kuona kama amepuuzwa au hajaheshimiwa na hivyo anajaa hasira.
- Akishambuliwa na kundi kubwa – Akiona watu kadhaa wanamshambulia kwa mpigo, anaweza kulipuka kwa jazba.
- Akijibiwa kwa “meme” badala ya hoja – Picha za utani zinapotumika kujibu hoja yake anayoiona ya maana, anachukia na kukasirika.
- Akiambiwa "huna pointi" au “hujui unachosema,” – Anakasirika na kuona kama amedhalilishwa.
- Akiambiwa "acha kuandika kwa kukurupuka" – Anakasirika akifikiri wanamaanisha hajui kitu chochote alichoandika.
- Akipewa "reaction" ya kicheko😂 kwenye hoja yake “serious” – Anakasirika kwa kuhisi amefanyiwa mzaha.
- Mada anayoitetea ikipuuzwa – huku nyingine anazoona hazina uzito zikipewa kipaumbele, anakasirika na kuona kama kuna upendeleo.
- “Moderator” au "Content Manager" akiunganisha au kuuhamishia panapostahili uzi wake – Anakasirika na kuhisi kama ananyamazishwa kwa makusudi.
- Akiambiwa amewekwa kwenye “ignore list” – Anakasirika sana na kumchukia huyo aliyemwambia hivyo.
Kama umegundua mojawapo ya mambo hayo yanakukasirisha, basi fahamu kuwa mbele za Mungu unahesabika “mpumbavu.” Biblia inasema: "Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu."(Mhubiri 7:9).
Hiyo mental frame work mmekaa jopo la watu wangapia mkakubaliana kuwa iwe ivyo?Usiseme natukana watu, soma mpaka mwisho utajua kwanini kichwa cha uzi kimeandikwa hivyo.
Katika mijadala na malumbano ya hoja hapa JF, kuna watu wengi waliojaa hasira vifuani mwao. Wanakasirishwa na maneno au vitendo vidogo vinavyoweza kuepukika.
Yafuatayo ni baadhi ya mambo madogo ambayo mara nyingi humfanya mtu aliyejaa hasira akasirike:
Mambo ni mengi, ongezea na wewe...
- Akiulizwa maswali magumu – Wakati wa mijadala, mtu anaweza kuulizwa maswali yanayohitaji ufafanuzi wa kina au uthibitisho wa madai yake. Badala ya kuchukulia maswali hayo kama fursa ya kueleza hoja yake vizuri, mtu aliyejaa hasira anaweza kuhisi kama anashambuliwa au anawekewa mtego wa kumfanya ashindwe kujibu. Anaweza kuona kama anaonewa, anadharauliwa au kulazimishwa kukiri kuwa uzi wake hauna mashiko
- Akikosolewa uandishi wake – Akikosea kuandika na watu wakalenga tu kuonyesha makosa hayo badala ya hoja yake, anachukia na kukasirika.
- Akitajwa jina au akiona emoji ya kejeli – Emoji kama 😂, 🤦♂️, au 😏 zinaweza kumuudhi sana. Na akitajwa jina lake, anaweza kuona kama vile anapigwa vita moja kwa moja na kwa sababu hiyo anajaa hasira.
- Akipachikwa jina la dharau – Akiitwa majina kama "mjinga," "chawa” au "hater," anapandwa na hasira haraka.
- Akiambiwa akapime afya ya akili – Anaweza kuona kama amedharauliwa au kutiliwa shaka akili yake.
- Akishutumiwa kwa lengo ambalo hana – Mfano, akionekana kama ana ajenda fulani ya siri, anaweza kujihami kwa hasira.
- Akijibiwa tu kwa "OK" au "Sawa" badala ya maelezo marefu – Anaweza kuona kama amepuuzwa au hajaheshimiwa na hivyo anajaa hasira.
- Akishambuliwa na kundi kubwa – Akiona watu kadhaa wanamshambulia kwa mpigo, anaweza kulipuka kwa jazba.
- Akijibiwa kwa “meme” badala ya hoja – Picha za utani zinapotumika kujibu hoja yake anayoiona ya maana, anachukia na kukasirika.
- Akiambiwa "huna pointi" au “hujui unachosema,” – Anakasirika na kuona kama amedhalilishwa.
- Akiambiwa "acha kuandika kwa kukurupuka" – Anakasirika akifikiri wanamaanisha hajui kitu chochote alichoandika.
- Akipewa "reaction" ya kicheko😂 kwenye hoja yake “serious” – Anakasirika kwa kuhisi amefanyiwa mzaha.
- Mada anayoitetea ikipuuzwa – huku nyingine anazoona hazina uzito zikipewa kipaumbele, anakasirika na kuona kama kuna upendeleo.
- “Moderator” au "Content Manager" akiunganisha au kuuhamishia panapostahili uzi wake – Anakasirika na kuhisi kama ananyamazishwa kwa makusudi.
- Akiambiwa amewekwa kwenye “ignore list” – Anakasirika sana na kumchukia huyo aliyemwambia hivyo.
Kama umegundua mojawapo ya mambo hayo yanakukasirisha, basi fahamu kuwa mbele za Mungu unahesabika “mpumbavu.” Biblia inasema: "Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu."(Mhubiri 7:9).
Neno la leo ntakupa, ila tambua kuwa atakayetoa taji ya uzima ni BWANA peke yake(2 Timotheo 4:8).Sawa Mama Mtumishi emu nipe Neno la leo linasemaje leo Jumatatu yangu nataka iwe na upako nikutunukie na taji la uzima km zawadi
Pasipo msaada wake BWANA sisi hatuwezi kufanya lolote linalompendeza Mungu.Dah! Hizi sala nyingine bhana! Yan unamtaka Mungu na Ukuu wake wote ule eti afanye kazi ya kuudhibiti ulimi wa Sweety Candy ili usinene matusi!!!.
Mi nadhani tumsubiri Mungu amalizane kwanza na yale ya Russia vs Ukraine, Israel vs Gaza/Palestine, Amani huko Congo DRC, Watanzania wasio na hatia wanaotekwa na kupotezwa, Ukame unaotunyemelea Hapa Tz n.k.
Mambo ya matusi mbona wapo akina Musa na Haruni(Wachungaji, Mashekhe, Manabii, Mitume na watumishi wa Mungu. Asipowasikia hao, basi hatamsikia hata Mungu akinena naye.
sawa mkuuChangamsha ubongo. Acha uvivu wa kusoma.
Ahsante Mama MTUMISHI, naomba namba nichangie Sadaka ya Neno km hutojaliNeno la leo ntakupa, ila tambua kuwa atakayetoa taji ya uzima ni BWANA peke yake(2 Timotheo 4:8).
Kabla ya Neno, tafadhali omba (kwa kufuatisha kwa moyo wako wa dhati) sala hii ya toba. Omba hivi:
“Ee Mungu Baba, nimetambua mimi ni mkosaji, nimekutenda dhambi nyingi sana. Leo nakuja mbele zako nikiomba msamaha wako. Natubu dhambi zangu zote na kuziacha. Nakiri kuwa Yesu Kristo ni Bwana, na Yeye ndiye Mwokozi wa ulimwengu. Yesu Kristo karibu moyoni mwangu utawale maisha yangu kuanzia leo. Naomba unipe nguvu ya kushinda dhambi na kuishi maisha matakatifu. Namkataa shetani na kazi zake zote. Asante Yesu kwa kuniokoa. Katika Jina la Yesu Kristo, ninaomba na kushukuru. Amen.”
Kama umeomba sala hiyo kwa moyo wako wa dhati, tayari umeokoka. Anza kusoma Biblia kila siku na kumuomba Mungu akusaidie kuendelea vizuri kiroho. Anza pia kwenda katika Kanisa lolote linalohubiri wokovu na kufundisha utakatifu watakupa msaada zaidi wa jinsi ya kukua kiroho.
Nakuachia sasa Neno la leo lenye upako:
“Bwana atakutangulia, Yeye atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope, wala usifadhaike." – Kumbukumbu la Torati 31:8
Nini wewe Semenya.Wahaya utawajua tuu, iphone karume???
Halafu we jamaa si nilisikia Watu washaanika maturubai/kula ubwabwa?
Namba yako kwa ajili ya maombi ya usiku Mama MchungajiSadaka utapeleka hilo Kanisa utakaloenda
Napenda uniongoze maombi ya usiku Mama MtumishiKama kweli umeamua kuokoka, anza sasa kujizoeza kuomba mwenyewe, Mungu anasikia na atakujibu. Soma Mt 7:7-8
Sawa Mama Mtumishi nimekuelewaMungu anasikia wakati wote sio usiku tu
Huu ni mfano(mwongozo tu) wa jinsi unavyoweza kuomba asubuhi, mchana au usiku:Napenda uniongoze maombi ya usiku Mama Mtumishi