Kama unasafiri Kilometa zaidi ya 800 kwa basi wewe ni masikini tafuta hela

Watu bwana sasa kuna watu wanapiga dar to LUSAKA ,dar to lubumbashi kwa basi tena kwa mwezi hata mara mbili na wana mawe na gari wamepaki home ila wanapanda basi hao nao .Iga jambo lenye faida sio unapata kihela kidogo tu unaanza kuona watu maskini.Watu wanamitaji mpaka wa dola 70000$ lakini wao ni basi tu.
 
Hayo masaa wanayopoteza njiani,plus risks za ajali,plus usumbufu tunduma....wajitafakari kama kweli bank wana zaidi ya USD 70000
 
Mkuu si kila anayefanikiwa ni mwizi, kuna watu wabunifu sana katika kutafuta pesa.

Wewe jua hilo
Kwa bongo na Afrika huenda uka wataja akina dangote na wengine wachache,zaidi ya hapo ni wale waiba kodi za wavuja Jasho wa kweli ambao wanalazimishwa kubakia kuwa maskini.
 
Hayo masaa wanayopoteza njiani,plus risks za ajali,plus usumbufu tunduma....wajitafakari kama kweli bank wana zaidi ya USD 70000
Inawezekana ww sio mpambanaji hivi kweli mm naenda zangu Kitwe zambia niwashe gari. kwanza mpaka unafika uchovu wa ku drive plus usumbufu wa trafic na cost ya mafuta. lakini km basi nafika ndani ya siku moja na nusu nimeepusha gharama kubwa ya ndege na gari binafsi.Kujali mda bila kuangalia faida na kipato unachopata ni upuuzi saving money ni bora sana kuliko kujimwambafai.
 
Daaaaah maskini tunasakamwa sana mwezi huu, kuna mwamba huko nae katwambia tusioe,... aseeeh njooni maskini wenzangu tusikitike na tushirikiane kwa pamoja kupinga hoja ya mleta mada...otherwise mleta mada una masikhara sana, hizo nauli za ndege tu kwa route moja ni mshahara wa mtu, hata kama ni safari ya kikazi katumwa na ofisi per diem yake yote haitoshi nauli ya ndege...kwa kifupi ukijudge umaskini wa waTz kwa kupanda ndege basi tuna maskini wengi sana
 
Sijui huwa naonaje nikiona mwanaume anajiona ana Hela kisa kapanda ndege!🤦🤦🤦waafrica bado tuna safari sana......no wonder ATCL mpya ikiingia kunakuwa na maandamano ya mapokezi na ngoma zinachezwa
 
Magufuli alikuwa masikini?
 
Ukishaongelea swala la gharama ujue umesuport uzi,bado unajitafuta,huna hela,endelea kutafuta hela bro
 
Ruvuma na Mtwara hatuna uwanja wa Ndege wa maana , kumbuka huku kuna uswahili na umaskini, huku hatusomi na wanetu wanaishia darasa la saba na kuozeshwa;Ndoa za utotoni zinaongoza huku,.
Hatuna utaratibu wa kurudi kwetu kama Wachagga , ndege itamleta nani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…