Kama unataka kuondoka kwenye umasikini, waepuke masikini kama ukoma

Nikiwaambia muache kuuliza maswali ya kijinga mnakimbilia kupaniki.
Nimekupa maelekezo hapo, bado unalazimisha kile unataka wewe.
Ndiyo maana nasema pata pesa na maswali ya kijinga kama haya hutasumbua nayo watu.
Kila la kheri.
 
Nikiwaambia muache kuuliza maswali ya kijinga mnakimbilia kupaniki.
Nimekupa maelekezo hapo, bado unalazimisha kile unataka wewe.
Ndiyo maana nasema pata pesa na maswali ya kijinga kama haya hutasumbua nayo watu.
Kila la kheri.
Sawa mkuu asante.
 
Mnataka kuwa matajiri, kwani hamkuambiwa ni vigumu tajiri kuuona ufalme wa mbinguni mithili ya ngamia kupenya kwenye tundu la sindano? 😂😂 Natania.
 
Dk Makirita bado una kazi kama mitazamo ya watu ndio kama hii mmmh kuna safari ndefu bado ya watu kupata ufahamu wa Elimu ya Maisha na Mafanikio!
 
Masikini waliowengi huwa wanashauriana mambo ya kwenda kunywa pombe kutafuta Madanga na kuosha rungu, kudiskasi mambo ya Diamondi na Simba na Yanga.

Siku imeisha hiyo siku ya pili ni kulalamika kuwa Raisi demu hafai.
Sure kabisa yani.
 
Dk Makirita bado una kazi kama mitazamo ya watu ndio kama hii mmmh kuna safari ndefu bado ya watu kupata ufahamu wa Elimu ya Maisha na Mafanikio!
Acha tu mkuu,
Yaani hii kitu bado ni ngumu mno kwa watu.
Sasa naelewa kwa nini hii nchi inashindwa kupiga hatua licha ya kuwa na rasilimali.
Mitazamo ambayo watu wanayo ni ya hovyo sana.
 
Habari za sijui kuutafuta utajiri utazisikia sanasana kwenye nchi maskini kama Bongo. Ila nchi zilizoendelea ukiachana na Marekani (Nasemea hasa hasa nchi za Ulaya), huwezi kusikia hizi swagga za kutafuta utajiri maana system ya nchi yenyewe ipo katika hali ya kuwafanya watu wote waishi maisha karibia sawa. Kitakachomtofautisha mwenye pesa nyingi sana na mtu mwingine ni kuhusu tu makazi. Kwamba mtu mwenye pesa nyingi ataishi kwenye nyumba inayojitegemea na mtu wa kawaida anaishi kwenye apartments. Ila mambo mengine wapo sawa tu maana hakuna gap kubwa kati ya maskini na tajiri.

Unakuta wote wanapata mahitaji yao kwenye supermarket moja. Siyo kama Bongo wanaonunua mahitaji Mliman city ni wenye pesa zaidi. Unakuta pia Ulaya huduma za afya ni sawa kwa watu wote siyo kama Bongo mwenye pesa anapata matibabu Agakhan na makabwela wanaenda Mwananyamala. Elimu nchi nyingi za Ulaya ni bure na baadhi unalipia pesa kidogo kwa chuo kikuu. Siyo kama Bongo mwenye pesa anapeleka watoto wake Internanational school makabwela wanapeleka watoto wao Shule ya msingi Buza. Mahakama zinatenda haki kwa watu wote, siyo kama Bongo mwenye pesa anaweza kununua haki na kabwela akafungwa hata kwa ushahidi wa uongo.

Unakuta pia hata anayefanya kazi ya usafi analipwa mshahara unaomtosha kulipa bills zote kwa mwezi na kubakisha chenchi. Yaani mfanya usafi anaweza kusafiri hata kwa ndege siyyo kama bongo ili usafiri kwa ndege mpaka uwe tajiri. Sasa nchi kama hizi mtu anatafuta utajiri wa kazi gani? Hizi stori zipo tu nchi maskini.

Kwa kuhitimisha, mie huwa naona watu wanaohimiza sana watu kuwa matajiri wanataka tuendelee kuwa na mfumo wa kutengeneza nchi ya wenye nacho na wasio nacho hivyo kuendelea kumkandamiza mtu maskini. Any way... Ngoja niishie hapa kwanza kwa sasa..
 
Kuna ukweli ila kuna mdau kagisia happ mtaji wa tajiri ni haohao maskini. Labda mfanye mtaji na si rafiki.
 
Tuhimizane;
1) Kufanya kazi kwa bidii na kuacha uvivu maana ka-nchi ketu bado kana shida nyingi za huduma za kijamii
2) Tuwahimize viongozi kuweka sera za usawa kwa watu wote katika nyanja za kijamii, kisiasa na kiuchumi
3) Watu wenye vipaji wavitumie vipaji vyao ili kuifanya dunia (nchi) yetu kuwa sehemu nzuri ya kuishi muda huu mfupi tuliokopeshwa kuishi hapa Duniani (miaka yenyewe michache tu 60-80 years).

Haya mambo ya kulishana upepo wa kupeana hamasa za kuutafuta utajiri hapa Duniani ni kulishana upepo ambao hauna manufaa yoyote. Tunawajengea watu nadharia vichwani kwamba kuutafuta utajiri ndio mambo yote kwenye maisha hali inayopelekea vijana kutafuta utajiri kwa njia ambazo pengine hazina mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi mfano betting na mambo mengine yanayofanana na hayo.

Kingine ni kuwa, hizi hamasa za kuwafanya watu wapate hisia za kuutafuta utajiri kunawafanya watu wapate stress na depression kwenye maisha pale wanapoona hawawezi kutimiza hizo hisia za kuwa tajiri.

Focus isiwe kuwafanya watu waone utajiri wa mapesa mengi ndio ufahari wa maisha. Tuzingatie point 3 hapo juu kama nilivyoandika.

NB: Mtoa mada; unaweza kuniambia kwa nchi zilizoendelea siku nyingi kama Sweden, Finland, Denamarak, Netherlands zina mabilionea wangapi ukilinganisha na idadi nyingine ya watu? Mana tulitegemea kwakuwa wao wameanza kusoma vitabu tangia zamani na wamefanikiwa tangia zamani basi kungekuwa na Mabilionea wengi zaidi kuliko watu wengine wa kawaida kama hiki mnachotueleza kwenye hivyo vitabu vya motivation vya wafanyabiashara wa vitabu wa huko Marekani ni kweli.

Naomba ulete takwimu za Mabilionea wa hizo nchi nilizozitaja tuone graph ikoje. Angalau onesha kuanzia miaka 50 huko nyuma tuone trend ilivyo.
 
Nimesoma vizuri lakini nikaona mwenye biashara ya kitabu yeye mwenyew ajani shauri bado sana tajiri sio dalali
 
Mkuu kwanza mtoa mada hataki kuelezea nini maana ya utajiri kwa mujibu wake na kitabu..

Pengine utajiri anaokusudia yeye ni kuwa na uwezo wa kufikiri na wewe unagusia utajiri wa mapesa.

Pengine utajiri anaogusia mtoa mada ni uwezo wa kutongoza mademu wengi lakini wewe unagusia utajiri wa pesa nyingi.

Pengine utajiri anaokusudia mtoa mada ni kuwa na vitabu vingi vya kiswahili vilivyoandikwa na makirita amani kumbe wewe unakusudia utajiri wa mapesa mengi.
 
Matajiri wengi wazinzi tu ..hamna lolote hapo. Hiyo ni biashara ya kitabu unafanya. Utajiri ni Neema ya Mungu tu. Kuna wenye juhudi nyingi za kuupata lakini wameambulia hasara tu.
Ha ha haa. Kutafuta utajiri ni nadharia zilizowekwa vizuri kwenye maandishi ya wauza vitabu wa Marekani. Vitabu vingi vinavyoelezea mambo ya utajiri vimeandikwa huko Marekani.

Ila Ulaya hizi habari huwezi kuzisikia kiviiile. Watu wa Ulaya hawana makuu na purukushani nyingi za kutafuta hela. Wanaangalia ni jinsi gani wanaweza kumudu bills za mwezi basi.

Masuala sijui ya kuwa Bilionea utayasikia kwenye nchi maskini kama Bongo. Tupambane kuhimizana kufanya kazi kwa bidii kila mtu kwa nafasi yake ili Serikali ikusanye kodi na kuimarisha huduma za kijamii. Vilevile tupaze sauti Serikali iweke mazingira ya usawa katika huduma za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Haya mambo ya kutafuta utajiri ni kulishana upepo tu.
 
Matajiri wengi wazinzi tu ..hamna lolote hapo. Hiyo ni biashara ya kitabu unafanya. Utajiri ni Neema ya Mungu tu. Kuna wenye juhudi nyingi za kuupata lakini wameambulia hasara tu.

Hao wanaoutafuta utajiri bila kuupata hawatumii njia sahihi,unatakiwa ufanye vitu vya tofauti(unique) na sisi wabongo kinachotuponza ni ubishi usio na maana,
 
Matajiri wengi wazinzi tu ..hamna lolote hapo. Hiyo ni biashara ya kitabu unafanya. Utajiri ni Neema ya Mungu tu. Kuna wenye juhudi nyingi za kuupata lakini wameambulia hasara tu.

Mtu anapewa fursa itakayompa kesho yake halafu anakuwa mbishi then anaenda kuwauliza walioshindwa ili wampe ushauri ,unafikiri mtu aliyeshindwa atakushauri nin?mim nilikuwa maskin sana nalala njaa na familia yangu lakin baada ya kufanya maamuz angalau nimetoboa naweza kuingiza dola 6000 kwa wiki
 
Na ndefu ndiyo inayodumu.
Mchicha unaota ndani ya siku 3, hauwezi kudumu hata mwaka.
Mbuyu unaota miaka 7, unadumu mpaka miaka 100.
Hivyo tuweke nguvu zetu kwenye vitu vitakavyodumu.

Kweli kabisa wabongo wengi wanapenda kitonga
 
Kitecho cha kwenda kwenye kijiwe cha pombe na kuwaambiwa wanywaji waache kabisa tabia ya kunywa pombe tena waepuke walevi sio watu wazuri......hakuna mlevi atakayekupenda.......

hapa jf wengi ni watu wa maisha ya chini ambao mtu yeyote ambae atafundisha somo la kuhusu ishu ya uchumi lazima wajue kuhusu level ya maisha yake!



ona comments zao[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
una akili sana bro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…