Kama unataka kuondoka kwenye umasikini, waepuke masikini kama ukoma

shida ni kua kitabu kinaandikwa ulaya kinatafasiliwa bongo ambao mifumo ya nchi haimruhusu kabisa mtu kufanya hayo
 
Yaani dah watu wengine sijui wakoje eti anatuuzia kitabu cha jinsi mbinu ya kuwa tajiri lakini yeye sio tajiri
 
Matajiri wengi wazinzi tu ..hamna lolote hapo. Hiyo ni biashara ya kitabu unafanya. Utajiri ni Neema ya Mungu tu. Kuna wenye juhudi nyingi za kuupata lakini wameambulia hasara tu.
Kama ni Neema ya mungu na wewe muombe mungu uwe billionea.

Tafuta helA upunguze stress
 
Noma sana!
 
ndio maana kwenye maskini kuna maskini
 
Ukikaa na watu masikini utavutwa kwenye umasikini hivyo hivyo ukikaa na matajiri. Umasikini ni roho ya laana za ukoo ambazo Kazi yake kuu ni kufunga akili.
 
Ufukara ni moja ya Adui aliyezishinda Serikali karibu zote za Kiafrika.

Sijui kama tutamuweza Adui huyu
Wanashindwa kwa interest zao za kisiasa.
Wanawafanya wengi wawe masikini Ili wawatawale. Pia ni nature kwa maana hakuna mwafrika anaeweza mletea maendeleo mwafrika mwenzake. Pia waafrika hawana uwezo wa kuongoza Jamii ikastawi.
 
Urope ime
Urope imelala,
Urope ipo stagnant,
Wale zama zao zilishapita.
Ndiyo maana innovations zote sasa zinatokea US.
Hatuwezi kujilinganisha na Europe.
Sisi bado tupo kwenye hustling stage.
 
Msiweke nchi yoyote ya Europe kwenye hizi comparisons zenu.
Watu tunaweza kujipima nao ni Asia, kama China, Korea na wengine.
Ambao tulianzia pamoja miaka siyo mingi.
Unajilinganisha na nchi ambazo wakati babu zetu wanavaa ngozi wao tayari walikuwa na viwanda vya nguo?
Hamuwezi kuwa serious.
Angalieni hatua ambazo China inapiga, pamoja na mapungufu yake mengi, bado inapiga hatua kubwa.
Ndiyo tunapaswa kukaa huko.
 
Mkuu, mbona una mawazo mgando sana.
Unashindwa kuelewa mambo madogo hivi huo utajiri utauweza kweli?
Tumeshajadiliana na kumaliza lako, lakini bado una nyongo tu.
Get a life mkuu, utakufa siku siyo zako.
And by the way, Get Money, #NothingElseMatters
 
shida ni kua kitabu kinaandikwa ulaya kinatafasiliwa bongo ambao mifumo ya nchi haimruhusu kabisa mtu kufanya hayo
Mbona suti inavaliwa ulaya na bongo mnavaa.
Mbona burger zinaliwa Marekani na hapa bongo mnakula?
Mengine yote ya wezekane ila kwenye fedha ndiyo ishindikane?
Huu ndiyo ujinga unawafanya wengi kubaki kwenye umasikini.
Soma kitabu uvue huu ujinga.
 
Yaani dah watu wengine sijui wakoje eti anatuuzia kitabu cha jinsi mbinu ya kuwa tajiri lakini yeye sio tajiri
Kama padri anavyofundisha na kufungisha ndoa wakati yeye hana ndoa.
Unaionaje hiyo?
 
Mkuu, mbona una mawazo mgando sana.
Unashindwa kuelewa mambo madogo hivi huo utajiri utauweza kweli?
Tumeshajadiliana na kumaliza lako, lakini bado una nyongo tu.
Get a life mkuu, utakufa siku siyo zako.
And by the way, Get Money, #NothingElseMatters
Mkuu mimi na wewe tumeshamalizana.

Huonekani kama mtu mstaarabu wa kupokea mawazo tofauti badala yake unakuwa mtu wa misimamo ya hasira na kuamini kila anayekuhoji analengo la kukukwamisha,
hizo ni mindset za kimasikini sana ambazo unatuonesha hapa.

Wewe mwenyewe unaonekana una uchungu na hasira ya pesa ndio maana hutaki kuhojiwa kuhusu kitabu.

Na wewe endelea kutafuta pesa utaacha kuwasumbua watu kuhusu kununua kitabu.

Matajiri akina modewji hawalazimishi watu kununua bidhaa zao kama unavyofanya wewe hapa.
 
Urope ime

Urope imelala,
Urope ipo stagnant,
Wale zama zao zilishapita.
Ndiyo maana innovations zote sasa zinatokea US.
Hatuwezi kujilinganisha na Europe.
Sisi bado tupo kwenye hustling stage.
Wewe kwakuwa ni msomaji najua utakuwa ni mfuatiliaji pia wa mambo mengi ya kidunia. Unamfahamu Senator mmoja wa US anaitwa Bernie Sanders? Unafahamu itikadi za siasa zake za US? Jaribu kumfuatilia vizuri siasa zake na maandishi yake juu ya Siasa za US na maono yake anavyolinganisha mfumo wa uchumi wa US na ule wa nchi za Ulaya.

Fuatilia pia comments kwenye pages zake kwenye social media uone maoni ya watu wa kawaida wa Marekani tofauti na Matajiri wachache wanaomiliki uchumi wa Marekani. Uwe unatembelea pia mtandao wa Quora kujifunza watu wengine Duaniani wana maono yapi kuhusu uchumi wa nchi za Ulaya na ule wa Marekani. Mwisho kabisa fuatilia mwenendo wa SIASA za chama cha Democrat uone maono yao juu ya uchumi wa Marekani.
 
Urope ime

Urope imelala,
Urope ipo stagnant,
Wale zama zao zilishapita.
Ndiyo maana innovations zote sasa zinatokea US.
Hatuwezi kujilinganisha na Europe. Sisi bado tupo kwenye hustling stage

Nimewahi kusoma andiko lako huko nyuma unasema una maono ya kuwa Rais wa nchi yetu siku moja. Kama haya ndio maono yako kuhusu uchumi wa nchi yetu basi tuna changamoto kubwa kama Taifa. Mie nakuomba uendelee kujifunza zaidi hasa katika nchi za wenzetu waliotangulia. Uone walianza vipi, wako wapi sasa na wanamaono ya kufika wapi hapo baadae. Ujifunze changamoto wanazopitia na u-digest hizo changamoto kwa kuonesha namna gani sisi tunaweza kuepuka hizo changamoto katika safari yetu. Usiwe mbaguzi wa kujifunza , usiegemee kusoma vitabu vya motivation speakers wa Marekani peke yake. Soma na makala nyingine ikiwemo mtandao kama Quora uone maoni ya watu wengine walio wasomi na wananchi wa kawaida Duniani.
 
Hakika, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...

Masikini nae mtu hata kama hana kitu...
 
CHINA inapiga hatua kwa kuhamasisha watu wake wawe Mabilionea kama unavyotaka kutushawishi na sisi ?

Wewe kama msomaji wa vitabu uliyebobea, Je, unadhani focus ya sasa ya nchi yetu iwe kuwahamasisha watu kutafuta utajiri au watu wafanye kazi kwa bidii na kulipa kodi kisha Serikali kutumia vizuri hizo kodi kuboresha huduma za kijamii?

Je, kwenye huko kusoma kwako, umewahi kujiuliza kwanini nchi nyingi zinazoongoza kwa watu wake kuwa na furaha duniani ni nchi za Ulaya na siyo Marekani?

Kwa misingi hiyo, Je, ungependa nchi zipi ziwe role model wetu?

Nakuomba ufafanue na sisi wavivu wa kusoma vitabu tujifunze kupitia hapa JF.
 
Utajiri unapatikana kwa kununua vitabu vya Makirita Amani
Nunueni vitabu kwa wingi ili mumsaidie Makirita Amani kua tajiri zaidi na apate kutunanga zaidi sisi masikini [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…