Kama ushawahi kuachwa kihivi, njoo utupe mkasa

Kama ushawahi kuachwa kihivi, njoo utupe mkasa

Kuna manzi niliachana nae mwaka Jana lkn chaajabu sikumbuki niliachana nae kisa Nini😂 nishadownload mafaili yote kichwani kumbukumbu zote lkn sikumbuki ila maugomvi mengine kabla ya kuachana nayakumbuka! ila kisa cha kuachana hata kuhisia tu NO!
mara ya mwisho alinitext sikumjibu!
Sijui nini kimekula kumbukumbu hiyo duh!
 
miaka kama mitano iliyopita nilikuwa na mahusiano na dada mmoja wa jirani na mahali ninapoishi, mimi nilimsumbua sana kuingia kwenye mahusiano name ila akawa hataki, siku moja nilibahatika kupata kazi dar nikahama nilikokuwa mwanzo, nikiwa kule dar nikaja kujua kwamba naye amechaguliwa chuo cha sehemu ile ile nikaendeleza kumuomba tuwe na mahusiano (hapo tunchat kwa simu)

miezi imeenda akawa anasafiri kwenda bukoba nakumbuka niliamka asubuhi sana nimuwahi ubungo pale, nikamuwahi nikampa na zawadi mbili tatu, baadaye akaja kunikubalia.

Nikiwa likizo kazini nikarudi nyumbani kwetu nje ya dar, usiku mmoja nikapokea simu kwa namba ngeni kuuliza nani naongea naye nikajibiwa kuwa “mpenzi wako” mnhh nikiwaza ninao kama watatu na sikumbuki sauti zao vyema kwa sababu alibadili sauti, nikamwambia wewe ni anna (daah nikataja demu mwingine) bais akaniuliza uko wapi maana nimerudi kwetu huku, nikamjibu nipo hapa hapa likizo, akasema unafanya nini name kiutani nikamjibu kuwa nakunywa pombe, daah akaniacha pale pale hata sikuamini, mzigo sijala, mahusiano yamedumu kwa miezi kadhaa tu, looh, nikamuomba sana msamaha wapiii!!!
mwaka jana ameshuhudia tu pciha za ndoa yangu na mke wangu mzuri, akaishia kukomenti hongera best, ila najua pengine anaumia sababu aliniacha kwa kosa la kijinga ambalo lililkuwa linazungumzika, namshukuru akanifanya nikutane na huyu mama kija wangu mpenzi!

Wakati mwingine ukiachwa kubali tu huenda unapelekwa kwa mtu sahihi zaidi!
 
Nilikua nina mpenzi ambae tulipendana sana
Nilimpenda
Alinipenda

Ilitokea ikafika siku ya kuzaliwa kwake (birth Day) na kutokana na kua nilitingwa na shughuli nyingi za kikazi nilisahau kumuwish (tulikua tunaishi mikoa tofauti) lakini niliwasiliana nae kwa maongezi ya kawaida tu…

Ilipofika jioni aliniambia leo ilikua birthday yangu na hujaniwish chochote na nimeumia sana so naomba tuachane tu and so and so..

Nilimuomba msamaha kwamba nilipitiwa lakini aligoma na tukaishia kuachana for real!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mleta uzi badili kichwa cha uzi. Iwe ULISHAWAHI KUACHWA KIMASIHARA?.

Mimi hata sitaki kabisa kurudia kukumbuka, ila wanaume huwa tunajikaza tu ilakini moyoni maumivu yake hayaelezeki. Labda itokee kwamba huyo aliyekuacha hakuwa 1st wala 2nd priority kwako. Kuna mtu mnakutana na mnaendana kwa kila kitu, ila inatokea ng'ombe fulani na pembe zake, inayachona mapenzi yenu.
 
Back
Top Bottom