Kama Yesu Kristo alikufa Msalabani ili tukombowele katika utumwa wa Dhambi mbona bado dhambi zinazidi kuongezeka?

Kama Yesu Kristo alikufa Msalabani ili tukombowele katika utumwa wa Dhambi mbona bado dhambi zinazidi kuongezeka?

Sio kila kitu kipo kwa ajili ya kila mtu, ukiona huelewi ujue hicho sio kwa ajili yako..
 
Masikini vijana hawasomi kabisa Neno la MUNGU.

Biblia Ina Majibu yooote ya Swali lako.

Soma Bible UTAPATA majibu.
Kizazi cha ajabu sana hiki, ndiyomaana kimebakia kutafuta miujiza tu ili kupata baraka za kiuchumi, afya n.k badala ya kujikita katika kuyachunguza Maandiko Matakatifu ya Mungu wajue kilicho sahihi.
 
kwa jinsi nilivyoielewa biblia inatuambia yeye ni kweli nauzima kila amwaminiye atapata uzima wa milele , ila utashangaa wahubili wanavyo watisha waumini kuhusu dhambi na bwawa liwakalo motto na kibiriti hii yote kuwafanya watu wawe watiifu nawanyenye kevu kupita uhalisia ili waweze kukusanya mapato kiurahisi
 
Mkuu ni swali zuri, ila jiulize swali dogo, wewe kama mzazi unajitoa kufanya kazi ili familia na wewe uie, je ulishawahi kumaliza njaa?

kwa wote wenye mwili na roho, ukombozi unakuja kwa juhudi yako, kwa maana utahukumiwa kwa kadiri ya matendo yako.

Ukombozi hauji kwa kusali sana au kukesha makanisani wakati unafanya matendo mabaya. Matendo yako na si kitu kingine
Msilete janja janjajanja jibu swali kwanini dhambi bado zipo huku Kristo alisulubiwa kwa ajili yetu?
 
Yesu hakufa kwaajili ya kuwakomboa, hata hivyo biblia inasema alikuja kwaajili ya kondoo waliopotea wa nyumba ya israel ama wana wa kabila zake waliopotea, hivyo uwepo wake dunian ilikuwa ni kwaajili ya watu wa asili yake na jamii yake tu, ninyi wengine hamuhusiki acheni shobo.

Hakukuwa na ulazima wa yeye kufa msalaban ili awakomboe[emoji16][emoji23] bali chuki za wale aliokuwa anawahubiria ndio zilisababisha afe kwa kupewa makosa hivyo kifo chake kisiwe sabbu ya kusema ni ukombozi.

Hata hivyo kama yeye kwel alikuja kwaajil ya kuikomboa dunia basi isingetumika nguvu kubwa kueneza neno lake, hususan Afrika ambako mamilion ya watu walikufa wakilazimishwa kuamin huo upuuzi wa kidini na kushika mafundisho ya ukristo, pia hakukua na ulazma wa imani kuenea kwa njia ya vita za msalaba zilizokuwa na malengo ya kueneza hiyo imani ya Yesu wenu.

Pia hakuna Ushahidi wa yesu kukomboa wala kusaidia jambo lolote zaid ya uzushi wa wafia dini.

Yesu hajawai kuwepo, aliundwa na wakatoric miaka ya 300A.D kwa kuchukua historia za miungu ya wamisri, wahindu, then kuleta jina jipya la Yesu kutoka kwa Yeshua ama Zeus/Azazel ama Osiris mungu mwana wa kiume wa kimisri..

Tafuta dunia nzima hautapata historia ya uwepo wa yesu wala hao mitume wake kuishi dunian, zaid ya uzushi huo utaupata ktk vtabu vya kidini vinavyolazimisha mtu aamini bila kutumia fikra kupambanua mambo.

Yesu angekuwepo kwel basi angesharudi kitambo sana maana hata ktk maneno yake alikuwa akiwashuhudia baadhi ya watu wake kuwa angerejea muda si mrefu na kwa dalili ilionesha ni kipindi chake[emoji23][emoji23] yuko wapi sasa?

Yesu angekuwepo basi dhambi zinazoongozwa kutendwa na wafia dini za ulawiti, uuwaji, ubakaji na ushirikina makanisan haya zisingekuwepo.

Yesu angewafia wanadamu basi isingekuwa na haja ya kutueleza sana maana kila mtu angeshajua bila kuforciwa na dini.

Yesu hatorudi, mtakesha mkisubiri hatorudi maana hajawai kuwepo na hatowai kuwepo.

Jina la Yesu liloundwa na wazungu wa kirumi kisiri kwa kumaanisha SUN/SON ama mwana wa shetan/nyota ya asubuh ambaye ni aina ya Pepo lenye muundo wa kondoo dume, pepo hilo lina nguvu kubwa ya kutenda mazingaombwe kwa wanaoliita kupitia makafala ya damu(damu ya yesu), pia kutaja majina yake ya asili ama kificho pepo hilo linaweza kutenda maajabu.

Pepo hilo ndio aina ya yale sign of 666 ambayo ndio hayo yatatumika kuwaingia watu kama chapa ya akili kwa kuwapotosha na kuwafunga kiakili na kiroho wasiweze kutambua Muumba wa kweli ni yupi, na badala yake kuwafanya watu waamini maajenti wa hili pepo ambao ndio hao wachungaji wenu na dinu zote za ulimwengu zote ziko chini ya hiki kiumbe kushirikiana na mapepo wengine(666) ambao kama watakuingia basi sahau kuhusu Kupona ktk Hukumu, maana utakuwa mmoja wa waabudu sanamu.

Dini zote ni uongo, dini zote zinamuabudu kiumbe mmoja kupitia mikanganyiko ya kuwafanya watu wasijue kweli kwa kufarakana na kutofautiana ktk mafundisho yao.

Muumba wa kweli hana haja ya sisi kuwa na dini na hajawai kumtuma huyo yesu aje awafie wanadamu, dhambi kutoka kwake ni wew kuomba mthamah na kuacha FULL STOP.
 
Ndio maana wayahudi wanasema Yesu bado hajaja.

Maana wanadamu tuiahidiwa Yesu Kristo atazaliwa na atakufa msalabani. Kifo chake kitakuwa alama ya ukombozi kwa Mwanadamu kutoka ktk utumwa wa dhambi.

Mbona sasa maovu, maasi na dhambi ndio kwanza zinazidi kuongezeka. Au aliyekuja na kufa sio Yesu Halisi
Bado unaamini kwenye hizi ngano za waarabu na wayahudi na wazungu!
 
Mtu asiyeamini uwepo wa Mungu aliwahi kunipa changamoto kwenye kipindi cha televisheni. "Damu ya Yesu imekuwepo kwa miaka 2,000," alisema, "na kama kungekuwa na nguvu yoyote ndani yake kama unavyodai, ulimwengu usingekuwa katika hali ya uovu kama hii."

Nikamjibu, "Ndugu, siku hizi pia kuna sabuni karibu kila sehemu, lakini watu wengi bado ni wachafu. Sabuni haimfanyi mtu kuwa safi kwa kuwa karibu, hata kama anafanya kazi katika kiwanda cha sabuni - lakini jioshe nayo.

Tumia damu ya Yesu kwa maisha yako ya dhambi na utajiunga na mamia ya mamilioni ya watu wanaoimba na kusema 'Kuna nguvu, nguvu, nguvu ya ajabu katika damu ya Mwanakondoo." Mungu akubariki.

Marehemu REINHARD BONNKE
Acha uongo...hiyo damu ya yesu inapatikana wapi?? Huyo yesu kwa mujibu wenu alikufa zaid ya miaka2000 iliyopita je hiyo dam anatoa wapi kuwakomboa mpka leo hii?

Kuhusu sabuni tunaamini zipo na zilikuwepo maana znaendelea kutengenezwa kila siku, sas damu ya yesu iko wapi? Kama ni huko rohon mnakosingiziaga basi huyo yesu alikuwa na mapipa mangapi ya damu kuwatosha mpaka leo? Na ujuwe kuwa kiumbe wa rohoni hana sifa ya kuwa na damu wala mwili wenye sifa za kibinadamu, je hizo damu mnaomba zinatoka wapi?? Ama anajiuwa tena ili mpate damu?[emoji23]

Haya maswali mnayakimbia sana kwa visingizio ambavyo hata biblia zenu hazijaeleza.

Elezen ukwel kuwa kifo cha yesu ambacho hakikuwai kuwepo ni aina ya stori zinazohusu Tambiko la kumwaga damu ya kiumbe, na damu hii ni sadaka kwa mashetan, na damu hii unapoomba itatolewa kwa hayo mashetan ya kimatambiko kupitia damu za sadaka za wanyama ama wanadamu, unaweza usitoe wew iyo sadaka ya damu lkn hao viumbe wanajua wanapoipata kupitia washirika wao, hivyo unapoomba damu ya yesu ikutakase unakua unashiriki tambiko la imani za wazungu wa kale waliobadili matambiko hayo kuwa dini na damu iyo uombapo itakupa miujiza kama utakavyo ama isikupe jibu lolote,.

yesu kama kweli angekuwepo basi isingekuwa na haja ya kutumia maombi ya damu wala sadaka, maana alishamaliza kifo chake kwaiyo hata maovu yasingekuwepo maana alimalizana nayo kifoni.

Kwakuwa Yesu katungwa na wazungu kwa kuiba historia za Miungu wa afrika ya kale, hivyo msitegemee mabadiriko yoyote mtatopata maana mnaomba kiumbe ambacho hakijawai kuwepo zaid ya stori za biblia
 
Majira ya yesu haukufanyika wokovu wowote ndo maana akasema katika mathayo 22:24 “Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”

Maana vyote alivyokuja navyo Yesu viliibiwa na yeye kuuliwa nje ya shamba ila hakuliongea hilo kulinda imani rejea mathayo 21:33-41

Paka ufalme wa baba yake ulipokuja juu ya nchi Zekaria 14:9 na ufunuo 21:3
 
Nilishasema haya mambo ni fix, hakuna Mungu wa kweli anaemtwaa mwanae kafara. Kafara ni za kibinadamu.
 
Ndio maana wayahudi wanasema Yesu bado hajaja.

Maana wanadamu tuiahidiwa Yesu Kristo atazaliwa na atakufa msalabani. Kifo chake kitakuwa alama ya ukombozi kwa Mwanadamu kutoka ktk utumwa wa dhambi.

Mbona sasa maovu, maasi na dhambi ndio kwanza zinazidi kuongezeka. Au aliyekuja na kufa sio Yesu Halisi
Unategemea dhambi itakoma kwa namna hii ya kila siku mnahubiri dhambi badala mema. Angalia Yesu alipokuja alifanya na kuhubiri nini. Lakini sasa ninyi kila uchao mnatamka hizo dhambi mara 1,000 huku mema mkitamka mara. Haijalidhi makanisani, misikitini au mitaani

Badilikeni kifkra
 
Ndio maana wayahudi wanasema Yesu bado hajaja.

Maana wanadamu tuiahidiwa Yesu Kristo atazaliwa na atakufa msalabani. Kifo chake kitakuwa alama ya ukombozi kwa Mwanadamu kutoka ktk utumwa wa dhambi.

Mbona sasa maovu, maasi na dhambi ndio kwanza zinazidi kuongezeka. Au aliyekuja na kufa sio Yesu Halisi
Labda sio yeye tusubiri tena kidogo [emoji3], maana hata ujana wake hatujauona
 
Hilo nalo neno kweli
Unategemea dhambi itakoma kwa namna hii ya kila siku mnahubiri dhambi badala mema. Angalia Yesu alipokuja alifanya na kuhubiri nini. Lakini sasa ninyi kila uchao mnatamka hizo dhambi mara 1,000 huku mema mkitamka mara. Haijalidhi makanisani, misikitini au mitaani

Badilikeni kifkra
 
Majira ya yesu haukufanyika wokovu wowote ndo maana akasema katika mathayo 22:24 “Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.”

Maana vyote alivyokuja navyo Yesu viliibiwa na yeye kuuliwa nje ya shamba ila hakuliongea hilo kulinda imani rejea mathayo 21:33-41

Paka ufalme wa baba yake ulipokuja juu ya nchi Zekaria 14:9 na ufunuo 21:3
Sawa sawa
 
Back
Top Bottom