Kamanda Muliro please trade carefully na wananchi. Polisi waishi ndani ya Katiba, Sheria na PGO imani irudi

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Kamanda Muliro nafahamu unasoma hapa jukwaani.


Inawezekana mmejiundia ama kujijengea kasumba kwamba wanasiasa wanafurahia kazi yenu ya kutumia nguvu bila mizania. Mmekuwa mkiwakandamiza na kuwadharau sana wananchi wanapoonewa na askari wa chini yenu.

Mmejipa majukumu ya kisiasa kinyume na Katiba. Mnatoa matamko bila mizania ya matokeo yake.

Mimi kama raia ninatoa ushauri kwenu kwamba, makachero mliowamwaga mitaani kuwasaka wakosoaji na wapinzani wanaochipukia hawawezi kufagia wote. Wanachokipata sasa ni kukosa ushirikiano na hiyo kupelekea taarifa nyingi kupikwa ili malkia aendelee kuamini kuwa mna uwezo wa KUWAZIMA wananchi wanaolilia haki zao.

Tamko ulilolitoa ni budi ikalirejea kwa uzingativu wa alignment kwa Katiba, Sheria na kanuni rasmi. Afisa ama mtumishi wa umma anayekiuka utaratibu anapotekeleza majukumu yake anakuwa ametenda makosa ambayo yanagharimu Haki, Utu na kuichafua serikali.

Askari anapomvamia na kumkwapua raia anayetuhumiwa bila kuzingatia taratibu za ukamataji salama ni wazi anatenda kosa. Wananchi wengi wametekwa haujaleta majibu ya uchunguzi. Ametekwa Ali Kibao kwa mitutu mizito mchana kweupe na kwenda kuuawa mpaka leo hakuna ripoti ya uchunguzi wala waliokamatwa.

Hivyo unavyowatishia wananchi ili waendelee kuwa kondoo wanapotekwa nyara na vyombo vya dola ni wazi kwamba mmeshakolea na kujiamini kwamba matendo ya kigaidi wanayofanyiwa raia ni sawa tu.

Mkuu Muliro, tumia ulimi na ufahamu wako kwa tija na siyo kututishia kwani chuki dhidi yenu imeshaenea vya kutosha. Asiwepo wa kuwasha utambi
 
Mkuu Muliro, tumia ulimi na ufahamu wako kwa tija na siyo kututishia kwani chuki dhidi yenu imeshaenea vya kutosha. Asiwepo wa kuwasha utambi
Your browser is not able to display this video.
 
Mkuu Muliro, tumia ulimi na ufahamu wako kwa tija na siyo kututishia kwani chuki dhidi yenu imeshaenea vya kutosha. Asiwepo wa kuwasha utambi
Heshima sana mkuu 'Msanii'. Laiti kama ange kuwa anawasilishiwa maandiko muhimu kama hili lako, nadhani hata yeye kama binaadam wengine angetulia na kulipa fkra muhimu

Ni jambo la kusikitisha kwamba hawa viongozi wa polisi wanapo kuwa kwenye nafasi hizi za uongozi ni kama wana sahau kwamba na wao ni binaadam tu kama wengine.

Mimi bado sielewi umuhimu wa hili wimbi jipya la utendaji kazi ya kipolisi. Hivi kuna sababu zipi hasa za polisi kufanya kazi nje ya taratibu zilizopo? Kwa nini pawepo na umuhimu wa kundi la kuteka watu? Hili mimi bado sijalielewa vizuri?

Chukua mfano wa kutekwa kwa marehemu mzee Kibao. Kulikuwa na sababu zipi hasa za kumteka yule mzee. Kwani kama palikuwepo na uhalifu alio shukiwa kuufanya, isinge kuwa bora kumkamata tu kwa taratibu zilizopo? Alihusishwa na kitu gani kibaya kiasi cha kumuua kikatili vile?

Sasa basi, kwa mfano huo; huyu Afande Muliro anafikiri watu waendelee tuu kukubali kutekwa na hatma zao zisijulikane zitaishia wapi, mauti, au kutojulikana kabisa? Kwa nini Muliro aone kuwa hii ndiyo inayo faa kwa kazi zao?
 
Mkuu
Hata hizi hoja za ushauri tunazowapa hawa kaka na dada zetu in uniforms wanazichukulia kama insults.

Tunatimiza wajibu huku tukiwindwa. Hatuogopi maana vyombo vya dola havijishughulishi tena na usalama wa raia na mali zao
 
Murilo atambue tu kwamba ule ni mwanzo tu. Watu tunahasira za kupotelewa ndugu zetu. Angejua hii itakua hatari kwa watekaji na watekwaji. Twende kazi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…