Kamanda wa Polisi Katavi: Edgar Mwakabela (Sativa255) anasema alichukuliwa Dar hadi Arusha na kisha kutupwa Katavi

Kamanda wa Polisi Katavi: Edgar Mwakabela (Sativa255) anasema alichukuliwa Dar hadi Arusha na kisha kutupwa Katavi

Bashite ndiye bosi wa kundi la wasiojulikana hivyo walienda Arusha kumuonyeha kuwa kazi uliyotutuma hii hapa naye akatoa maelekezo wamuue kisha wakamtupe katavi aliwe na wanyama kupoteza ushahidi.
Hapana naamini ni Mr DJ huyo wa Chadema ndio mtuhumiwa wa ugaidi
Yule mtu ni mafia sana
 
JamiiForums imemtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Kaster Ngonyani kuhusiana na tukio hilo ambapo amesema "Ndio ni kweli, taarifa za tukio hilo lipo na tayari tumeshaenda eneo la tukio na Mgonjwa sasa hivi yupo Hospitali ya Wilaya ya Mlele eneo Mpigwe Kibaoni

SACP Ngonyani amesema Sativa aliokotwa Usiku wa Kuamkia Juni 27, 2024 Barabarani maeneo ya Pori la Hifadhi ya Taifa ya Katavi (Barabara ya Msimbwe Majimoto inayoelekea Mpanda.

Pia soma: Sativa225 (Edgar Mwakabela) kijana maarufu kwa kukosoa serikali X apatikana, baada ya kutekwa na watu wasiojulikana

Ameongeza "Mgonjwa ameongea Mwenyewe japo kwa shida amesema alikamatwa na Watu Juni 23 Mbezi kwa Msuguri, kisha akapelekwa Mkoani Arusha katika sehemu ambayo haijui na baadaye kuletwa Katavi ambapo alipigwa na kitu chenye ncha kali ambacho anasema kilitokea mdomoni kisha Wakamtupa kwenye msitu huo na kutoweka

Amesema "Mgonjwa alijikokota kutoka Porini hadi Barabarani ambapo Wasamaria wema walimwona na kumpakia kwenye gari kisha kumpeleka Hospitali. Aliongea kidogo sana kwa sasa haongei. Tunasubiri taarifa ya Daktari kuhusu alichomwa na kitu gani.
Hivi Wanasiasa wana roho na mioyo ya kawaida kweli! Yaani kirahisi tu unafikia hatua ya kujeruhi au kuyaondoa kabisa maisha ya binadamu mwenzako, kisa tu hutaki kukosolewa!!
 
Mtekaji huyu hapa
 

Attachments

  • IMG_2832.jpeg
    IMG_2832.jpeg
    221.6 KB · Views: 8
Huko X wakosoaji wengi wako hatarini, humu kwenyewe watu wawe makini hamko safe km mnavyofikiria.
 
i
Hicho kitu chenye ncha kali kilichotokea mdomoni,kiliingilia eneo gani la mwili wake mpaka kikatokea mdomoni?
itakuwa risasi, cha kushukuru Mungu si ukute risasi haijagusa hata mfupa wala mshipa, Mungu mkubwa. hata kama mtu amekukosoa vibaya na kwa uwongo, ndio ufanye hivi jamani? ubinadamu upo wapi? hii dunia juu mbinguni huko kuna mbabe wa kila mtu, God is watching, msijiona wababe sana, yupo Mungu mbinguni.
 
Huko X wakosoaji wengi wako hatarini, humu kwenyewe watu wawe makini hamko safe km mnavyofikiria.
Tangu Mello ateuliwe kwenye kamati ya ulinzi wa nn sijui hakuna tena uhakika wa uhuru humu.
 
Aulizwe mwenyekiti wa uvccm kagera Faris Buruhan.
 
"Chezea ndevu usichezee dola "

Alisema nani huu ushauri?

Huu ni upumbavu, unakwenda kumteka, kumuumiza mtu mdogo kama huyu ambaye hana madhara yoyote zaidi ya kubwabwaja Tu mitandaoni.

Haya ni matumizi mabaya ya Dola.
 
Kutekateka watu eti kwasababu wanakosoa huo ni ushamba tu na uoga.

Wanaofanya hayo matukio na wanaowatuma wajue tu wamelaaniwa wao na uzao wao, madhara wanaweza wasiyaone kwao lakini watoto wao wanaowapenda na kuwasomesha kwa gharama na vipato vinavyotokana na huo ujinga wao watakuja kuishi maisha magumu ajabu pamoja na Mali wanazowaachia.
 
Huu ni upumbavu, unakwenda kumteka, kumuumiza mtu mdogo kama huyu ambaye hana madhara yoyote zaidi ya kubwabwaja Tu mitandaoni.

Haya ni matumizi mabaya ya Dola.
Sativa alikuwa anatukana utadhani hakuzaliwa na mwanamke
20240627_190455.jpg
 
Alaa kumbe mambo yaliyasisiwa na Mwendazake bado tunayaenzi.

Haya mambo yanatufanya tuonekane uncivilized nation.

Kama ana makosa sheria & mahakama zipo wazi.
 
Back
Top Bottom