Kamata kamata haiwezi kuwa Suluhu. Mzee Kikwete asikilizwe

Kamata kamata haiwezi kuwa Suluhu. Mzee Kikwete asikilizwe

Ama kweli dunia inakwenda kasi sana.

Kwamba Dkt. Slaa, balozi wa Hayati Magufuli leo yuko korokoloni tena chini ya awamu ya 6?

Ikumbukwe hata kina Mbowe hayakuwakuta ya kuwakuta kwenye awamu ile.

View attachment 2717325

Kwa hakika Mh. Kikwette, hata asipoyasemea kwa mara nyingine tena.

Chonde chonde enyi mlioko madarakani:

Kikwette na asikilizwe!
Mkuu kongole. Mimi nimefahamu kwamba watu waachiwe watoe maoni, yaangaliwe, na yafanyiwe kazi. Hakuna tatizo ktk hilo. Tatizo ni pale unapoenda zaidi na kuhamasisha watu waichukie serikali, kufanya uchochezi na zaidi kuhamasisha kuondoa uongozi ulioko madarakani kwa nguvu (kufanya mapinduzi).
 
Mkuu kongole. Mimi nimefahamu kwamba watu waachiwe watoe maoni, yaangaliwe, na yafanyiwe kazi. Hakuna tatizo ktk hilo. Tatizo ni pale unapoenda zaidi na kuhamasisha watu waichukie serikali, kufanya uchochezi na zaidi kuhamasisha kuondoa uongozi ulioko madarakani kwa nguvu (kufanya mapinduzi).

Mkuu haya ya kufanya uchochezi na kuhamasisha watu kufanya Mapinduzi yanatoka wapi?

Kumekuwa na mawazo kuwa kwenye suala hili tumegawanyika. Haijulikani ni nani wapi salama.

"Kwamba imekuwa ni udini, uzanzibari na utanganyika?"

1. Hivi ndugu zetu kina Mwaipopo au Assad na wa namna hiyo hawaioni hoja ya kisheria hapa?

2. Hivi ndugu zetu wazanzibari kina Zawadini au Fatma karume kulikoni kufumba macho leo dhidi ya kamata kamata hIzi na hata kuona kuna uhaini hapa? Si kuwa kumbe panakuwapo damu iliyo nzito kuliko maji hapa?

3. Kulikoni suala hili kuwa ni Zanzibar dhidi ya Tanganyika? Kulikoni kuwa ni suala la bandari za bara lakini si Zanzibar?

Kwamba Zanzibar hawalioni hilo na kuwa mlipo sasa mnatushangaa mno tunapopaza sauti kuuonyesha kutokuridhishwa kwetu?

Haya ya kupakaziana uhani si ni yale yale yakiwasibu Maalim, CUF, masheikh wa uamsho nk sote tukiyapigia kelele tokea enzi za Mkapa?

Ndugu zetu katika mapambano, nini kimebadilika au kinewasibu leo?

Ni kwa vile kuna mzanzibari, mwanamke au mwislamu madarakani anayeyafanya yale yale leo?

Kwamba nyie leo mmeuona huu ni uhaini?

Bwana Zawadini nikiamini wewe kama mmoja wa wale wajumbe nguli aliye muadilifu katika mapambano tokea pande za huko, nini kimekupata ndugu yangu?

"Nini kimewapata ndugu zetu? Kulikoni kigugumizi hiki?"

Kwa hakika leo nakuona kama walivyonishangaza Prof. Assad na Fatma Karume.

"Umeniacha njia panda."
 
Haisaidii chochote.
Panapofuka moshi, ukitaka kuufuta zima moto chini( by Justine Kalikawe)
 
Mkuu kongole. Mimi nimefahamu kwamba watu waachiwe watoe maoni, yaangaliwe, na yafanyiwe kazi. Hakuna tatizo ktk hilo. Tatizo ni pale unapoenda zaidi na kuhamasisha watu waichukie serikali, kufanya uchochezi na zaidi kuhamasisha kuondoa uongozi ulioko madarakani kwa nguvu (kufanya mapinduzi).
Nani huyo aliyehamasisha mapinduzi? Tuwekee ushahidi hapa nasi tuuone.

Serikali inachukiwa kwasababu imeshindwa kuja na majibu ya maswali inayoulizwa kwa wakati, tena inapokuja, inakuja na majibu ya dharau, kuziba masikio, unataka wale wanaojibiwa hivi waipende hiyo serikali isiyowajibika kwao?
 
Kuna gross mismanagement ya uchumi na matumizi ya anasa ya serikali inafanya nchi ionekane uchumi wake upo hoi na ili serikali iendelee kutekeleza anasa zake za kutumia magari ya kifahari ikiwemo anasa zilizopindukia za mafisadi unafanya a desperate move ya kuuza na kuweka rehani rasilimali muhimu za nchi.​
 
2. Hivi ndugu zetu wazanzibari kina @Zawadini au Fatma karume kulikoni kufumba macho leo dhidi ya kamata kamata hIzi na hata kuona kuna uhaini hapa? Si kuwa kumbe panakuwapo damu iliyo nzito kuliko maji hapa?
Mkuu; mimi leo nitaangazia haya mawili ya Zawadini.
Kule mwanzo nilikupa kongole kwa kuona wasia wa Mhe. Kikwete ni wa kuufanyia kazi na nikasema kongole. Kikwete amesema watu waachwe watoe maoni na ikionekana kuna la kulifanyia kazi lifanyiwe kazi.

Haiingii akilini kwamba kwa watu kuwa huru kutoa maoni washajiishe watu kupinga serikali iliyopo madarakani, kuchochea watu kufanya fujo (uhalifu) na zaidi kushajiisha mapinduzi. Haya ndo ninayoyasemea.
Bwana @Zawadini nikiamini wewe kama mmoja wa wale wajumbe nguli aliye muadilifu katika mapambano tokea pande za huko, nini kimekupata ndugu yangu?
Mikuu; Zawadini bado ni yuleyule. Huenda tunatofautiana kwenye namna tunavyoyatafsiri haya matukio. Uadilifu wangu kwenye kutafuta haki ya kila mmoja wetu bado haujabadilika na sitarajii kwamba utabadilika.

Ni vizuri kila mmoja wetu atambue mipaka yake kwani sisi tunaongozwa na sheria.
 
Nani huyo aliyehamasisha mapinduzi? Tuwekee ushahidi hapa nasi tuuone.
Aliyehamasisha hayo amewekwa humu JF na kila mtu aliyepata nafasi alisikia. Rejea kwenye ule uzi kwani sina nafasi ya kukulisha kwa kijiko.
 
Aliyehamasisha hayo amewekwa humu JF na kila mtu aliyepata nafasi alisikia. Rejea kwenye ule uzi kwani sina nafasi ya kukulisha kwa kijiko.
Huyo mtu nilimsikiliza na sikuona neno lolote baya alilotamka, hasa kuipindua serikali usemavyo, amekuwa akihimza maandamano kama njia ya kufikisha ujumbe kwa msaliti aliyetuzibia masikio..

Hayo kwako ndio kutaka kuipindua serikali? au maandamano hayatambuliki kisheria siku hizi?
 
Tanzania ina laana fulani hivi mbaya:
1. Mkapa aliwekwa na Nyerere lakini hakumsikiliza na akamgeuka vibaya.
2. Magufuli aliwekwa madarakani kwa msaada wa Mkapa lakini hakumsikiliza Mkapa akamgeuka.
3. Samia aliwekwa madarakani kwa msaada wa Jakaya lakini naye naona yuko mbioni kumgeuka.

NB: Swali la muhimu ni hili: Samia ataweza kweli kumgeuka Jakaya mtoto wa Mjini kirahisi tu?
Haingii akilini ukae kwenye majukumu makubwa kama hayo alafu uwe mtumwa wa mtu mmoja... nafsi inakusuta!
 
Nani huyo aliyehamasisha mapinduzi? Tuwekee ushahidi hapa nasi tuuone.

Serikali inachukiwa kwasababu imeshindwa kuja na majibu ya maswali inayoulizwa kwa wakati, tena inapokuja, inakuja na majibu ya dharau, kuziba masikio, unataka wale wanaojibiwa hivi waipende hiyo serikali isiyowajibika kwao?
Hayo masuala ya ushahidi mahala pake ni Mahakamani sio hapa
 
Mkuu; mimi leo nitaangazia haya mawili ya Zawadini.
Kule mwanzo nilikupa kongole kwa kuona wasia wa Mhe. Kikwete ni wa kuufanyia kazi na nikasema kongole. Kikwete amesema watu waachwe watoe maoni na ikionekana kuna la kulifanyia kazi lifanyiwe kazi.

Haiingii akilini kwamba kwa watu kuwa huru kutoa maoni washajiishe watu kupinga serikali iliyopo madarakani, kuchochea watu kufanya fujo (uhalifu) na zaidi kushajiisha mapinduzi. Haya ndo ninayoyasemea.

Mikuu; Zawadini bado ni yuleyule. Huenda tunatofautiana kwenye namna tunavyoyatafsiri haya matukio. Uadilifu wangu kwenye kutafuta haki ya kila mmoja wetu bado haujabadilika na sitarajii kwamba utabadilika.

Ni vizuri kila mmoja wetu atambue mipaka yake kwani sisi tunaongozwa na sheria.

Kuacha kuyaangazia #1 na #3 kwa mawazo yangu ni kutojitendea haki wewe mwenyewe.

Nikurejee hapo kwenye #2 kwenye kumwangazia Zawadini:

a) Kongole kumhusu Mzee Kikwette hilo hakuna jipya. Kwani tumekuwa hilo tukilipagania sote tokea enzi za akina Maalim na wengi wengine wakiwa TANU, ASP na hata CCM.

Ikumbukwe pia hata Kikwette hakuwaacha salama Maalim, CUF, masheikh wa uamsho, katiba ya warioba wala maoni yote ya watu.

b) Kwamba harakati za leo wewe waziona ni Mapinduzi? Wakati tulikuwa sote hapa:



Maajabu ya Mussa!

Utamwaminisha nani kuwa Zawadini huyu ni yule yule ati tofauti ni tafsiri za matukio tu?

Ama kwa hakika kama chini hapa ni maoni ya Zawadini na haya ya leo nayo ni ya Zawadini huyo huyo? Basi tuna matatizo makubwa zaidi!

Screenshot_20230815-105131.jpg


Screenshot_20230815-105154.jpg
 
Ama kweli dunia inakwenda kasi sana.

Kwamba Dkt. Slaa, balozi wa Hayati Magufuli leo yuko korokoloni tena chini ya awamu ya 6?

Ikumbukwe hata kina Mbowe hayakuwakuta ya kuwakuta kwenye awamu ile.

View attachment 2717325

Kwa hakika Mh. Kikwette, hata asipoyasemea kwa mara nyingine tena.

Chonde chonde enyi mlioko madarakani:

Kikwette na asikilizwe!
Matope
 
He was silent killer,nikikumbuka sakata la uamsho namna alivyowasotesha ndani cna hamu nae.
Kikwete nilikuwa anatisha kuliko Magufuli, kwa wenye kumuelewa. Msione anacheka cheka tu, ndiyo sura yake ilivyo siyo kuwa anacheka kweli.
 
Tanzania ina laana fulani hivi mbaya:
1. Mkapa aliwekwa na Nyerere lakini hakumsikiliza na akamgeuka vibaya.
2. Magufuli aliwekwa madarakani kwa msaada wa Mkapa lakini hakumsikiliza Mkapa akamgeuka.
3. Samia aliwekwa madarakani kwa msaada wa Jakaya lakini naye naona yuko mbioni kumgeuka.

NB: Swali la muhimu ni hili: Samia ataweza kweli kumgeuka Jakaya mtoto wa Mjini kirahisi tu?

Kaka, Dark Days itakupa majibu kama anauwezo wa kumkabili Born town ama anajichetua tu?
 
Back
Top Bottom