Kamata kamata haiwezi kuwa Suluhu. Mzee Kikwete asikilizwe

Kamata kamata haiwezi kuwa Suluhu. Mzee Kikwete asikilizwe

Kaka, Dark Days itakupa majibu kama anauwezo wa kumkabili Born town ama anajichetua tu?
Born town alikuwa yule Mfabian wa Scotland, alikuwa mjanja, mwerevu na mwenye nguvu isiyo kawaida ndani na nje ya mipaka ya hii nchi ila wapi. Bakari na ujanja wake naye ameshatangulia mbele ya haki, minong'ono inasema tatizo ni hili-hili la Dubai. Lakini, hebu tusubiri tuone mwisho wake.
 

Kama hao mawakili wenu wanadhani kwamba hizi kauli ndizo zitakazowafunga wakina Dr Slaa kwa kosa la uhaini (Treason), basi kazi ipo. Wangejikita tu kwenye makosa yao ya Uchochezi (Sedition), ila huku wanakoenda watasababisha mengine. Mathalani, kauli kama hizi zimekuwa zikitolewa Tanzania tokea miaka ya 90's uliporudishwa mfumo wa vyama vingi nchini.

Dr Slaa hii siyi mara yake ya kwanza kutoa kauli tata kama hizi. Kuelekea mwaka 2015 alishawahi kusema hadharani kwamba "Tutahakikisha nchi haitatawalika", tena akaenda mbali akawahamasisha vijana waanzishe makundi ya kihuni kuiga mfumo wa Italia wa Red-Brigade ambalo lilikuwa ni kundi la wanamgambo waliopambana na serikali. Walishitakiwa kwa makosa ya uchochezi.

Hivi ninyi mnafahamu hata maana ya uhaini kweli, au mnapelekwa tu na mihemko, ???
 
Ikumbukwe pia hata Kikwette hakuwaacha salama Maalim, CUF, masheikh wa uamsho, katiba ya warioba wala maoni yote ya watu.
Ni kweli, na hawa wala hawakuwahi kusema wanataka kuiondoa serikali na yakawafika haya, seuze wanaosema hadharani, sio JF ambako kuna voro; tutarajie nini? Kumbuka masheikh walikaa ndani kwa zaidi ya miaka tisa. Jee hawa wa leo ikitokea hivyo itakuwaje? Masheikh kosa lao lilikuwa ni kuukataa muungano hadharani, jambo leo, baada ya swala la bandari limekuwa ndo wimbo.
Kwamba harakati za leo wewe waziona ni Mapinduzi? Wakati tulikuwa sote hapa
Sio mimi kuziona ni mapinduzi harakati zao. Nimesema huwezi kuhamasisha na kufanya uchochezi na kuhamasisha kuiondoa serikal na mengine halafu useme ni uhuru wa kutoa maoni. Hayo wanayo/waliyofanya/wanayotuhumiwa kufanya ni makosa kwa mujibu wa sheria za nchi na mahakama ndo itaamua walifanya au hawakufanya na wala sio mimi Zawadini.
Ama kwa hakika kama chini hapa ni maoni ya @Zawadini na haya ya leo nayo ni ya @Zawadini huyo huyo? Basi tuna matatizo makubwa zaidi!
Mkuu hayo ni maoni yangu na siajaona ambapo nimesema au kuunga mkono kuiondoa serikali, uchochezi au kuhamasisha mapinduzi.

Mimi, Zawadini msimamo wangu haujabadilika katika kuona haki inapatikana kwa kila mmoja bila kufikiria kuiodoa serikali kinyume na sheria
 
Tulipofika ni pazuri
Dunia imejua

Kwa ufupi dp world Samia na ukoo wake watajua dunia ni ya nani?
 
Ni kweli, na hawa wala hawakuwahi kusema wanataka kuiondoa serikali na yakawafika haya, seuze wanaosema hadharani, sio JF ambako kuna voro; tutarajie nini? Kumbuka masheikh walikaa ndani kwa zaidi ya miaka tisa. Jee hawa wa leo ikitokea hivyo itakuwaje? Masheikh kosa lao lilikuwa ni kuukataa muungano hadharani, jambo leo, baada ya swala la bandari limekuwa ndo wimbo.

Sio mimi kuziona ni mapinduzi harakati zao. Nimesema huwezi kuhamasisha na kufanya uchochezi na kuhamasisha kuiondoa serikal na mengine halafu useme ni uhuru wa kutoa maoni. Hayo wanayo/waliyofanya/wanayotuhumiwa kufanya ni makosa kwa mujibu wa sheria za nchi na mahakama ndo itaamua walifanya au hawakufanya na wala sio mimi Zawadini.

Mkuu hayo ni maoni yangu na siajaona ambapo nimesema au kuunga mkono kuiondoa serikali, uchochezi au kuhamasisha mapinduzi.

Mimi, Zawadini msimamo wangu haujabadilika katika kuona haki inapatikana kwa kila mmoja bila kufikiria kuiodoa serikali kinyume na sheria

Kwamba Kwenye list unakubali yaliwakuta kina Seif na wote wale kinyume cha utaratibu na tumekuwa sote, bega kwa bega kupinga yaliyowakuta?

Kwamba unajifariji kuwa hao walikaa ndani muda wote na hawakuwa wamesema neno Mapinduzi? Maajabu ya Mussa!

Huko mbona kutakuwa ni kujidanganya ndugu yangu?

Wewe hujui walibambikiziwa ugaidi. Kwani walisema ugaidi? Wewe hujui ufundi wa mamlaka zetu Kwenye kubambikiziana kesi?

Au ilichoona au mapendekezo ya tume ya haki jinai hukuyasikia? Au ungependa wewe kubambikiziana ipi? Kwani wanao upungufu wa kesi za kubambikizia watu?

Nchi hii ikitaka kukutia ndani au hata kukuuwa kwani inashindwa wapi? Wako wapi kina Ben, Azory au Mosses Lijenje? Au kumbe nani walikuwa wale marehemu kwenye viroba?

Kwamba ni kwa mujibu wa sheria zipi unazotaja kuzihalalisha wewe leo walizozikiuja kina Slaa hapa ambazo wewe au ninyi leo kumbe mwaziheshimu mno?

Kwamba Leo mahakama na polisi ndiyo unaziona tuziheshimu tu zitatupa tafsiri sahihi? Kuwa tusubiri hayo huko na kuwa si wewe kutoa maoni kwani hizo ni kazi za kitaalamu na utalaamu huo uko mahakamani?

"Hapa naweza kuyaelewa sasa yale matatizo ya wengi na Zitto, ACT na hata na wazanzibari. Ya kuwa mko unprincipled!

"Ninyi si wa kualalia mlango wazi."

Kwa kiswahili - mu wumanafiki!

Kwamba mkuki Kwa nguruwe siyo? Kwamba udini, uzanzibari, jinsia au njaa?

Kwamba huku wewe ukiona hakukuwa na vionjo vya kuiondoa serikali?



Kwani serikali isiyokidhi matakwa ya watu wake kuiondoa madarakani kwanini iwe haramu?

Mbona Amini tulimfurusha madarakani kama ilivyokuwa wakoloni, au walivyofurushwa kina Mengistu, Mubarak, Bokassa, Bashir na wengi wa namna hiyo?

Kwa maoni yako ninaelekea kukubaliana na wanaoona wazanzibari si washirika wa kutumainiwa kwenye kudai haki zetu.

Udini, uzanzibari na kuwa rais Sasa hivi ni mwenzenu basi ndiyo kusema fyongo zake zote hamzioni na kweli mlipo sasa mnatushangaa?

Kwa mwendo huu suala hili litakuwa ni la watanganyika.

Kwamba pilipili msizozila ziwawashe ninyi vipi?
 
Msaliti wa UKAWA hiyo ndo adhabu yake kura yangu ilipotea sababu yake wamshughulikie haswaa maana uhuni aliotufanyia hatujausahau.
 
Msaliti wa UKAWA hiyo ndo adhabu yake kura yangu ilipotea sababu yake wamshughulikie haswaa maana uhuni aliotufanyia hatujausahau.

Maoni ya maccm na mijitu isiyojulikana hayajifichi.

Hatudanganyiki!

Habari ndiyo hiyo.
 
Kwamba Kwenye list unakubali yaliwakuta kina Seif na wote wale kinyume cha utaratibu na tumekuwa sote, bega kwa bega kupinga yaliyowakuta?

Kwamba unajifariji kuwa hao walikaa ndani muda wote na hawakuwa wamesema neno Mapinduzi? Maajabu ya Mussa!
Hapana shaka kwamba hawakuwahi kusema neno mapinduzi. Mara zote walilalamikia kubadilishwa matokeo ya uchaguzi, na hili unalielewa. Sikupata kusikia au kuona mtandaoni ndgu zetu akina brazaj wakilisema hili.
Huko mbona kutakuwa ni kujidanganya ndugu yangu?
Sijaona kujidanganya katika hili. Kwenye ukweli lazima tuseme.
Wewe hujui walibambikiziwa ugaidi. Kwani walisema ugaidi? Wewe hujui ufundi wa mamlaka zetu Kwenye kubambikiziana kesi?
Maalim Seif wala wanasiasa kutoka upinzani wakati hule hawakubambikiziwa ugaidi. Waliobambikiziwa ugaidi ni masheikh wa Uamsho nao huo ubambkiziwaji ulitoka JMT na sio Zanzibar. Tuweke kumbukumbu vizuri.
Au ilichoona au mapendekezo ya tume ya haki jinai hukuyasikia? Au ungependa wewe kubambikiziana ipi? Kwani wanao upungufu wa kesi za kubambikizia watu?
Hapa sijaelewa.
Nchi hii ikitaka kukutia ndani au hata kukuuwa kwani inashindwa wapi? Wako wapi kina Ben, Azory au Mosses Lijenje? Au kumbe nani walikuwa wale marehemu kwenye viroba?
Hawashindwi ila katika hili la sasa mbona watu wameonekana na kusikika,
Kwamba ni kwa mujibu wa sheria zipi unazotaja kuzihalalisha wewe leo walizozikiuja kina Slaa hapa ambazo wewe au ninyi leo kumbe mwaziheshimu mno?
Mkuu hapa swala sio kuridhika au kutoridhika, kuziheshimu au kutokuziheshimu bali swala ni kwamba sheria zipo na hivyo ni lazima kufuatwa. Kuzivunja kunapelekea kuchukuliwa hatua.
Kwamba Leo mahakama na polisi ndiyo unaziona tuziheshimu tu zitatupa tafsiri sahihi? Kuwa tusubiri hayo huko na kuwa si wewe kutoa maoni kwani hizo ni kazi za kitaalamu na utalaamu huo uko mahakamani?
Hawa ndo wanatakiwa kutoa tafsiri ziwe sahihi au zisiwe sahihi na nini cha kufanya pale mtu asiporidhika zimewekwa, ni wajibu wetu kuzifuata.
Hapa naweza kuyaelewa sasa yale matatizo ya wengi na Zitto, ACT na hata na wazanzibari. Ya kuwa mko unprincipled!
Hawa ulotutaja tuko unprncipled kwa maoni yako. Unao uhuru wa mawazo huenda ukweli utajulikana kwamba walioko unprincipled
Ninyi si wa kualalia mlango wazi."

Kwa kiswahili - mu wumanafiki!
Huenda haya unayodai ya unafiki ni kwasababu ya kutofanya yale unayoyataka wewe. Ni ajabu!! Hivi wewe hali (status) yako ni ipi? Jee wewe ni kiherehere, kitimbakwiri au nani hasa?
Kwamba mkuki Kwa nguruwe siyo? Kwamba udini, uzanzibari, jinsia au njaa?

Kwamba huku wewe ukiona hakukuwa na vionjo vya kuiondoa serikali?
Si swala la mkuki kwa ngurue, Uzanzibari, udini wala njaa. Pia si swala la kuona vionjo vya kuiondoa serikali bali swala ni kutamka hadharani swala la kuiondoa serkakali.
Kwani serikali isiyokidhi matakwa ya watu wake kuiondoa madarakani kwanini iwe haramu?
Ni kichekesho na ni akili za kitoto kudhani kwamba kuiondoa serikali kinyume cha sheria ni halali. Huku ni kuishiwa na hoja, kushindwa na kukosa hekima. Haifanani kwako kuyadai haya. Nakusihi fikiri kwanza kabla hukuanza kuandika.
Mbona Amini tulimfurusha madarakani kama ilivyokuwa wakolon
Hili nalo ni kukosa na kuishiwa na hoja. Hivi unamfananisha Amini na mama Samia? Huku ni kukosa uelewa na kutokufikiri. Tafakari.
Kwa maoni yako ninaelekea kukubaliana na wanaoona wazanzibari si washirika wa kutumainiwa kwenye kudai haki zetu.

Udini, uzanzibari na kuwa rais Sasa hivi ni mwenzenu basi ndiyo kusema fyongo zake zote hamzioni na kweli mlipo sasa mnatushangaa?
Kwa mwenendo huu na utaratbu huu ni kweli Wazanzibari, kama mimi, siko tayari kuwa mshirika katika hili

Mkuu kama ni udini basi wewe brazaj unaongoza na haya maandiko yako yanathibitisha hayo. Hivi la kuwa rais ni mwenzetu linkuja sasa? Mlikuwa wapi wakati watu waliponyanyaswa nanyi mukakaa kimya kwa kuwa wao ni Wazanzibari?

Nakukumbusha tu akina Juma Duni walishitakiwa kwa uhaini sikumsikia brazaj akipaza sauti hadi pale mahakama lipoamua hakuwezi kufanyika Zanzibar kwa kuwa sio nchi? Ulikuwa wapi wakati masheikh waliposhiliwa kwa miaka zaidi ya tisa? Huo haukuwa udini, haukuwa ubaguzi, haukuwa umajimbo? Iweje leo liwe jambo kwasababu tu wanaoshikiliwa ni wale wenye imani moja nawe, ni wale wenye asili moja nawe?

Mimi Zawadini nitaendelea kuunga mkono juhudi za kupata haki kwa kutumia njia za kistaarabu na kamwe staunga mkono wabaguzi wa aina yoyote. Hatuna budi siku zote jembe tuliite jembe

Zawadini
 
Hapana shaka kwamba hawakuwahi kusema neno mapinduzi. Mara zote walilalamikia kubadilishwa matokeo ya uchaguzi, na hili unalielewa. Sikupata kusikia au kuona mtandaoni ndgu zetu akina brazaj wakilisema hili.

Bila shaka unafahamu wote hao wamewahi kushitakiwa kwa njama za mapinduzi na pia kutamka neno mapinduzi na shtaka hilo ni vitu viwili tofauti.

Kama sivyo basi serikali ya CCM utakuwa ungali huijui.

Kwamba hukuwahi kuwasikia kina brazaj kulisemea hili Kwa hakika itakuwa kutojitendea haki.

Izingatiwe jukwaani humu tunatembea na ID fiche Labda kama wewe ni verified member. Pili brazaj anatembea humu tokea 26 July 2016. Rejea zako ni kutokea wapi? Umeyaangalia mabandiko yangu kuihusu Zanzibar na kadhia za huko tangia muda huo na vipindi vyote vya chaguzi za huko kujiridhisha kabla ya kuiandika fyongo yako hii?

Sijaona kujidanganya katika hili. Kwenye ukweli lazima tuseme.

Kujidanganya ni kwenye kudhani waliobambikiziwa kesi ni wazanzibari tu ila si hawa na eti kuwa kwa hawa ni halali yao.

Maalim Seif (rip) asingekubaliana nawe kwenye hilo.

Maalim Seif wala wanasiasa kutoka upinzani wakati hule hawakubambikiziwa ugaidi. Waliobambikiziwa ugaidi ni masheikh wa Uamsho nao huo ubambkiziwaji ulitoka JMT na sio Zanzibar. Tuweke kumbukumbu vizuri.

Kubambikiziwa kesi ndiyo iliyo hoja kuu. Kubambikiziwa hakujali ni kesi ipi kwa maana mwenye kulifanya hilo ni kwa discretion yake si mbambikiziwa kesi. Kwani nani anachagua abambikiziwe kesi ipi?

Kwatenganisha JMT na SMZ wote hao chini ya CCM ni kutaka kujidanganya kwingine mchana mchana.

Kwani waliomtambua mtoto wa nyoka ni nyoka walikosea?

Hapa sijaelewa.

Majuzi kati rais aliteua tume ya haki jinai. Kama hiyo nayo huielewi angalia hapa kujiridhisha:


Nitazijibu hoja zako zote hapa ila nichape kazi kidogo kwanza.
 
Bila shaka unafahamu wote hao wamewahi kushitakiwa kwa njama za mapinduzi na pia kutamka neno mapinduzi na shtaka hilo ni vitu viwili tofauti.

Kama sivyo basi serikali ya CCM utakuwa ungali huijui.
Bila shaka unafahamu wote hao wamewahi kushitakiwa kwa njama za mapinduzi na pia kutamka neno mapinduzi na shtaka hilo ni vitu viwili tofauti.

Kama sivyo basi serikali ya CCM utakuwa ungali huijui.
Swala la maalim Sef kushtakiwa kwa mapinduzi halipo na haljawahi kuwepo.

Kuhusu serikali ya CCM kutokuijua vizuri utakuwa wewe, kwa mwenendo huu, ndo huenda pia huijui vizuri.
Izingatiwe jukwaani humu tunatembea na ID fiche Labda kama wewe ni verified member.
Hili la kutembea na ID fiche unaalitambua wewe. Mimi najadilana na brazaj wa humu JF kwa sasa. Siku nyingine nitag kwamba huyu wa sasa ni brazaj katika ID fiche ili nisiseme hujachangia na kumbe umechangia ukiwa umejifunika kizoro.
Pili brazaj anatembea humu tokea 26 July 2016. Rejea zako ni kutokea wapi? Umeyaangalia mabandiko yangu kuihusu Zanzibar na kadhia za huko tangia muda huo na vipindi vyote vya chaguzi za huko kujiridhisha kabla ya kuiandika fyongo yako hii?
Katika hili, Zawadini yumo humu tokea 2012 kwa hivyo Zawadini katika hili ni mzoefu zaidi.
Kubambikiziwa kesi ndiyo iliyo hoja kuu. Kubambikiziwa hakujali ni kesi ipi kwa maana mwenye kulifanya hilo ni kwa discretion yake si mbambikiziwa kesi. Kwani nani anachagua abambikiziwe kesi ipi?
Hapa nilikuwa najadili madai yako kwamba maalm Seif walibambikiziwa kesi ya ugaidi. Kama ni vingine, jaribu kuwa mahususi (specific) kwani mimi najadili maandiko siangalii kichwani mwako kuna nini. Na huu ndo utaratibu.
Kwatenganisha JMT na SMZ wote hao chini ya CCM ni kutaka kujidanganya kwingine mchana mchana.

Kwani waliomtambua mtoto wa nyoka ni nyoka walikosea?
Kwamba leo SMZ na JMT ni moja kwa sababu tu najenga hoja? Si ni nyinyi munaosema ni kitu, utawala, serikali nyingine? Nikuite kigeugeu?
Kama hiyo nayo huielewi angalia hapa kujiridhisha:
Hapa nilikuwa sikuelewa umeandika nini. Mimi najadili kitu kichoandikwa kwa ufasaha na sio kukurupuka tu. Jitahidi kuandika kwa ufasaha ili tujadili kwa ufasaha.

Baada ya hayo nakushukuru na nakutakia majadiliano mema yenye heshima na busara.
 
Hawashindwi ila katika hili la sasa mbona watu wameonekana na kusikika,

Kama hawashindwi si ndiyo haya waswahili huita akutukanaye hakuchagulii tusi ndugu? Lini watataka kumbambikizia nani nini huo ni uchaguzi wao.


Mkuu hapa swala sio kuridhika au kutoridhika, kuziheshimu au kutokuziheshimu bali swala ni kwamba sheria zipo na hivyo ni lazima kufuatwa. Kuzivunja kunapelekea kuchukuliwa hatua.

Hata mkoloni sheria alikuwa nazo. Ndiyo maana kutwa kucha tunapogania katiba mpya Ili kuwa na sheria za haki Enye kukubaliwa Kwa haki na sote.

Sheria mbaya hukataliwa. Sheria hazitoku Kwa mwenyezi Mungu. Miito ya kuziangusha serikali Kwa mujibu wa Katiba haliwezi kuwa haramu.

Hawa ndo wanatakiwa kutoa tafsiri ziwe sahihi au zisiwe sahihi na nini cha kufanya pale mtu asiporidhika zimewekwa, ni wajibu wetu kuzifuata.

Hawa ndugu wanashikiliwa kinyume cha sheria. Hakuna shaka kuwa unajua mtu akikamatwa ndani ya masaa 24 inabidi awe kafikishwa mahakamani. Kumbe wewe nani kutofuata yeye sheria unakuona wewe ni sawa?
Hawa ulotutaja tuko unprncipled kwa maoni yako. Unao uhuru wa mawazo huenda ukweli utajulikana kwamba walioko unprincipled

Asante Kwa kutambua ni Kwanini ninalazimika kuwaita unprincipled na kwamba si from nowhere!

Huenda haya unayodai ya unafiki ni kwasababu ya kutofanya yale unayoyataka wewe. Ni ajabu!! Hivi wewe hali (status) yako ni ipi? Jee wewe ni kiherehere, kitimbakwiri au nani hasa?

Mimi ninasimama na ndugu huyu ambao ndiyo ulio ukweli mchungu:

F3k78Z8a0AAldWM.jpeg


Si swala la mkuki kwa ngurue, Uzanzibari, udini wala njaa. Pia si swala la kuona vionjo vya kuiondoa serikali bali swala ni kutamka hadharani swala la kuiondoa serkakali.

Kwa hiyo kwako wewe haipo tofauti ya kutamka mapinduzi na kupanga mapinduzi? Kwamba kumbe hawa wanashtakiwa Kwa kutamka mapinduzi Wala si kupanga mapinduzi?

Ni kichekesho na ni akili za kitoto kudhani kwamba kuiondoa serikali kinyume cha sheria ni halali. Huku ni kuishiwa na hoja, kushindwa na kukosa hekima. Haifanani kwako kuyadai haya. Nakusihi fikiri kwanza kabla hukuanza kuandika.

Uhalali wa serikali ni upi? Seif alipokuwa hamtambui SheIn hadharani, uliwahi kudokeza popote au kumuasa kuwa ulikuwa ni uhaini? Au ilikufikirisha kwanini hakukamatwa kwa uhaini?

Hili nalo ni kukosa na kuishiwa na hoja. Hivi unamfananisha Amini na mama Samia? Huku ni kukosa uelewa na kutokufikiri. Tafakari.

Amini na wote wafanyao yoyote kinyume na matakwa ya umma hawawezi kujinasibu kuwa ni tofauti. Wote ni wahalifu kama wowote.

"Zingatia kibaka ni kibaka TU hata kama yuko kwenye V8."

Kwamba wewe unayo tofauti ya tafsiri ya neno kibaka?

Uhalali wa serikali unakoma unapojinyakulia haki za raia na uka geuka kuwa wabakaji. Jiridhishe kuhusiana na kadhia ya bandari za bara kukabidhiwa dp world lakini Siyo za Zenji. Hiyo ikiwa bila ya ridhaa ya wabara.

Kwamba ni hoja yako tutulie tuli mbakaji amalize starehe zake Kwa amani? Kwamba hiyo ndiyo hoja yako Bora kabisa kwenye hili?

Kwamba unakwazija kuona tunasimama kuupinga ubakwaji huu? Bado tusijiulize nini kimekupata wewe au wenzetu tokea Zanzibari huko?


Kwa mwenendo huu na utaratbu huu ni kweli Wazanzibari, kama mimi, siko tayari kuwa mshirika katika hili

"Hapa ndipo hatutaacha kukumbushana ya Martin Luther."

Hii ni Leo na hata milele!

Mkuu kama ni udini basi wewe brazaj unaongoza na haya maandiko yako yanathibitisha hayo. Hivi la kuwa rais ni mwenzetu linkuja sasa? Mlikuwa wapi wakati watu waliponyanyaswa nanyi mukakaa kimya kwa kuwa wao ni Wazanzibari?

Nikukumbushe tena mrejee brazaj tangia 26 Nov 2016 alipotia timu. Kulikoni kutaka kumnyooshea kidole ndugu huyu kabla ya siku hiyo pasipo na kufahamu kabla ya hapo alikuwa wapi na hata kama alikuwa Bado kuzaliwa?

Nakukumbusha tu akina Juma Duni walishitakiwa kwa uhaini sikumsikia brazaj akipaza sauti hadi pale mahakama lipoamua hakuwezi kufanyika Zanzibar kwa kuwa sio nchi? Ulikuwa wapi wakati masheikh waliposhiliwa kwa miaka zaidi ya tisa? Huo haukuwa udini, haukuwa ubaguzi, haukuwa umajimbo? Iweje leo liwe jambo kwasababu tu wanaoshikiliwa ni wale wenye imani moja nawe, ni wale wenye asili moja nawe?

Ninakukumbusha Tena kuyarejea maandiko ya brazaj tokea 26 Nov 2016 kuhusu haki. Bila
kusahau kuihusu Zanzibar, Maalim Seif na wote uliowataja wakiwamo masheikh wa uamsho. Ya nini kuandika mate?

Nipende kukutaarifu brazaj hakuwahi kukaa kimya au kuacha kukerwa na ubaguzi wowote na hata kama mbaguzi huyo alitaka kuwa zawadini ambaye mapema nikimtambua kama mshirika mwaminifu wa siku zote kabla ya maandiko yako haya.

Lini nimewahi kuwa na simile na wabaguzi tokea kokote watokako hata kama ingekuwa mbinguni? Kama wao kama wewe sitakufumbia macho kwenye hili!

Kwenye hili nitakuwa mchoyo wa fadhila kutokuwafahamisha kuwa: "mme boogie!"

Mimi Zawadini nitaendelea kuunga mkono juhudi za kupata haki kwa kutumia njia za kistaarabu na kamwe staunga mkono wabaguzi wa aina yoyote. Hatuna budi siku zote jembe tuliite jembe


Hayupo anayetaka Shari. Hata hivyo waliotambua amani kutopatikana ila kwa ncha ya upanga hawakukosea.

Kwamba tunataka haki? Kwamba iwe kwa vipi? Hayo hayawezi kuwa Kwa utashi au uchaguzi wa maadui zetu.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu kwa huyu ndugu yenu na hasa kama mwampenda.

FuOaIYLXgAAoFSO.jpeg


Atatawala si kwa matakwa yake, bali Kwa mujibu wa Katiba!
 
Ni kwenye sakata hili hili mkuu. Sakata linanuka uvundo ajabu bi mkubwa hausikii.
Hivi ni sahihi kwa mkuu wa mkoa wa Dar kuwatishia wanaopinga mkataba tata wa bandari?

Hivi ni maadili mema ya kiongozi kama mkuu wa mkoa wa Dar aliyepo sasa hivi kuwaonesha jeuri wananchi kwamba hakuna mtu anayeweza kumpanda juu ya kipara chake? Kwamba wakome kama walivyokoma kunyonya maziwa ya mama zao? Mamlaka ya uteuzi bado tu inamfuga akijikweza kwa mshahara wa kodi zao?
 
Swala la maalim Sef kushtakiwa kwa mapinduzi halipo na haljawahi kuwepo.


Kama kumbukumbu huna huwa unaweza hata uka google kujiridhisha:

Screenshot_20230818-123137.jpg


Ya nini kukuruka kama kibwengo ndugu?

Kuhusu serikali ya CCM kutokuijua vizuri utakuwa wewe, kwa mwenendo huu, ndo huenda pia huijui vizuri.

Hadi hapo nina haja ya kujieleza zaidi mgeni wa serikali ya CCM ni nani?

Hili la kutembea na ID fiche unaalitambua wewe. Mimi najadilana na brazaj wa humu JF kwa sasa. Siku nyingine nitag kwamba huyu wa sasa ni brazaj katika ID fiche ili nisiseme hujachangia na kumbe umechangia ukiwa umejifunika kizoro.

Kumbe wajua wajadiliana na brazaj? Basi mrejee brazaj tokea 26 Nov 2016 si kabla ya hapo.

Katika hili, Zawadini yumo humu tokea 2012 kwa hivyo Zawadini katika hili ni mzoefu zaidi.

Hapa nilikuwa najadili madai yako kwamba maalm Seif walibambikiziwa kesi ya ugaidi. Kama ni vingine, jaribu kuwa mahususi (specific) kwani mimi najadili maandiko siangalii kichwani mwako kuna nini. Na huu ndo utaratibu.


Hadi hapo utakuwa umetambua uzoefu wako wa ki analogu haufui dafu kwenye wa mamboleo almaarufu - kidijitali.

Aghalabu ni kuwa waungwana husema 1+1 = 2 haijali ni wazoefu wa wajinga wangapi wanasema ni 5.

Kwamba leo SMZ na JMT ni moja kwa sababu tu najenga hoja? Si ni nyinyi munaosema ni kitu, utawala, serikali nyingine? Nikuite kigeugeu?


Wapi na lini, au mimi na nani tulisema zi tofauti?

IMG_20230818_124534.jpg


Lini tumeacha kuwanyooeshea vidole hao ndugu? Au wewe hujausikia ule wimbo wao pendwa kuwa - CCM ni Ile Ile?

"Au kwenu nyie yenu ni ya zambarau?"

Hapa nilikuwa sikuelewa umeandika nini. Mimi najadili kitu kichoandikwa kwa ufasaha na sio kukurupuka tu. Jitahidi kuandika kwa ufasaha ili tujadili kwa ufasaha.


Hapa nilikuwa wazi kuhusu tume jinai nikaenda na kukupa link yenye kutambua mchango wa tume hiyo ya rais.

IMG_20230818_131015.jpg


Nilikuwekea ikiwamo kiunganishi husika Kwa taarifa zaidi.

Ufasaha upi zaidi ya huo unaouhitaji wewe ndugu zaidi ya huu wa Jaji mkuu?

Baada ya hayo nakushukuru na nakutakia majadiliano mema yenye heshima na busara.

Pasi na shaka niya nukuu nami kwako maneno yako ya hekima sana hapa:

"Nikushukuru pia na nakutakia majadiliano mema yenye heshima na busara."

Mwisho wa kukunukuu.
 
Hivi ni sahihi kwa mkuu wa mkoa wa Dar kuwatishia wanaopinga mkataba tata wa bandari?

Hivi ni maadili mema ya kiongozi kama mkuu wa mkoa wa Dar aliyepo sasa hivi kuwaonesha jeuri wananchi kwamba hakuna mtu anayeweza kumpanda juu ya kipara chake? Kwamba wakome kama walivyokoma kunyonya maziwa ya mama zao? Mamlaka ya uteuzi bado tu inamfuga akijikweza kwa mshahara wa kodi zao?

Watawala wamejisahau. Zawadini anataka tuwaheshimu na tusiwachukulie hatua zozote isipokuwa tu zile wanazotuchagulia wao.
 
Hata mkoloni sheria alikuwa nazo. Ndiyo maana kutwa kucha tunapogania katiba mpya Ili kuwa na sheria za haki Enye kukubaliwa Kwa haki na sote.
Ni kweli mkoloni sheria alikuwa nazi na waliozvunja sheria hizo walchukuliwa hatua.

Hili la kupigania katiba tunapigania sote, ila nikumbushe tu hata baada ya hiyo katiba mpya kutatungwa sheria na wataozivunja watachukuliwa hatua kwa mujibu wa hizo sheria zitazotungwa. Hizi zilizopo sasa zilitungwa na wawakilishi wetu mimi na wewe.
Hawa ndugu wanashikiliwa kinyume cha sheria. Hakuna shaka kuwa unajua mtu akikamatwa ndani ya masaa 24 inabidi awe kafikishwa mahakamani.
Katika hili kwa sasa umesema kweli.
Asante Kwa kutambua ni Kwanini ninalazimika kuwaita unprincipled na kwamba si from nowhere!
Penye ukweli huwa tunasema.
Mimi ninasimama na ndugu huyu ambao ndiyo ulio ukweli mchungu:
Kusema ni kitu kimoja na kutenda unayoyasema ni kitu kingine. Kwa bahati mbaya umesema yale usiyoyatenda na huo ndo unafiki.
Kwa hiyo kwako wewe haipo tofauti ya kutamka mapinduzi na kupanga mapinduzi? Kwamba kumbe hawa wanashtakiwa Kwa kutamka mapinduzi Wala si kupanga mapinduzi?
Hawa wanashitakiwa kwa kutangaza hadharani kwamba kuiondoa serikali - kufanya mapinduzi.
Uhalali wa serikali unakoma unapojinyakulia haki za raia na uka geuka kuwa wabakaji. Jiridhishe kuhusiana na kadhia ya bandari za bara kukabidhiwa dp world lakini Siyo za Zenji. Hiyo ikiwa bila ya ridhaa ya wabara.
Ikiwa uhalali wa serikali unakoma kwa kujichukulia haki za raia basi nawe jiunge nao.

Swala la bandari kukabidhiwa DPW lkn sio za Zenj ni uamuzi uliofanywa na serikali. Ungekuwa na hoja ikiwa ungesemea haki ya hiyo Zanzibar siku moja. Vinginevyo haya ni malalamiko yanayobagua kwa utaratibu uleule kwamba ya kwao hayatuhusu na hivi hatuendi sawasawa.
Ninakukumbusha Tena kuyarejea maandiko ya brazaj tokea 26 Nov 2016 kuhusu haki. Bila
kusahau kuihusu Zanzibar, Maalim Seif na wote uliowataja wakiwamo masheikh wa uamsho. Ya nini kuandika mate?

Nipende kukutaarifu brazaj hakuwahi kukaa kimya au kuacha kukerwa na ubaguzi wowote na hata kama mbaguzi huyo alitaka kuwa zawadini ambaye mapema nikimtambua kama mshirika mwaminifu wa siku zote kabla ya maandiko yako haya.

Lini nimewahi kuwa na simile na wabaguzi tokea kokote watokako hata kama ingekuwa mbinguni? Kama wao kama wewe sitakufumbia macho kwenye hili!

Kwenye hili nitakuwa mchoyo wa fadhila kutokuwafahamisha kuwa: "mme boogie
Swala hapa sio kusema tu ila tunachotaka ni kuona.

Huenda tumebuggie kama mawazo yako yalivyo lkn pia huenda umebuggie wewe.
Hayupo anayetaka Shari. Hata hivyo waliotambua amani kutopatikana ila kwa ncha ya upanga hawakukosea.

Kwamba tunataka haki? Kwamba iwe kwa vipi? Hayo hayawezi kuwa Kwa utashi au uchaguzi wa maadui zetu.

Huo ndiyo ulio ukweli mchungu kwa huyu ndugu yenu na hasa kama mwampenda.
Sawa. Mimi nangoja kuona kwa vitendo haya unayodai leo. Kule waswahili husema "tusiandikie mate na wino upo"
Atatawala si kwa matakwa yake, bali Kwa mujibu wa Katiba!
Sio kwamba atatawala kwa mujibu wa katiba, bali hivi sasa anatawala kwa mujibu wa katiba. Akienda kinyume na katiba bunge litamwodoa kwa mujibu wa katiba yenyewe.
 
Ni kweli mkoloni sheria alikuwa nazi na waliozvunja sheria hizo walchukuliwa hatua.

Kuchukuliwa hatua kutokana na kuwapo kwa sheria batili huwafanya watu kuwa mashujaa. Huku si ndiko walikopatikana kina Mandela?

Kiuhalisia ni heri kufa shujaa kuliko kuishi kama mtumwa katika nchi yako.

Hili la kupigania katiba tunapigania sote, ila nikumbushe tu hata baada ya hiyo katiba mpya kutatungwa sheria na wataozivunja watachukuliwa hatua kwa mujibu wa hizo sheria zitazotungwa. Hizi zilizopo sasa zilitungwa na wawakilishi wetu mimi na wewe.

Hatuna tatizo kuhukumiwa Kwa mujibu wa sheria tulizo muafaka nazo. Siyo hizi za ma CCM.

Katika hili kwa sasa umesema kweli.

SI Sasa maana hakuna ulipobadilika msimamo wangu. Kwamba tunapiga hatua hIyo ni dalili njema kuwa tunasonga mbele
polepole, tutafika.

Penye ukweli huwa tunasema.

Kwa hakika hatutanyamaa!

Kusema ni kitu kimoja na kutenda unayoyasema ni kitu kingine. Kwa bahati mbaya umesema yale usiyoyatenda na huo ndo unafiki.

Sina hakika unalenga nini kwenye hili. Utende vipi bila kunena ndugu? Kwani umekuwa bubu?

Nikutaarifu pasipo na shaka yoyote. Kama ilivyokuwa kwa timu ya ushindi hii:



Tumedhamiria kweli kweli na bi mkubwa analijua hilo.

Hawa wanashitakiwa kwa kutangaza hadharani kwamba kuiondoa serikali - kufanya mapinduzi.

Bila shaka unayo habari kuwa dhamana zinatoka? Vipi unao mpango wa kumwuliza bi mkubwa, kulikoni?

Mapinduzi gani ya kimchongo hayo? Kaulize wanaume wa Niger wakwambie mapinduzi ni kitu gani .. au ECOWAS wanasema je kuhusu mapinduzi?

Ikiwa uhalali wa serikali unakoma kwa kujichukulia haki za raia basi nawe jiunge nao.

Labda kama una nia ya kunambia nijitoe? Kwamba ninyi kumbe hammo? Hivyo kumbe wenzetu mko wapi?

You are either with us, or against us - Wikipedia

Kwa hakika kwenye hilo George Bush atakuwa ana ujumbe mahsusi kwako na hata kwa ujumla wenu.

Swala la bandari kukabidhiwa DPW lkn sio za Zenj ni uamuzi uliofanywa na serikali. Ungekuwa na hoja ikiwa ungesemea haki ya hiyo Zanzibar siku moja. Vinginevyo haya ni malalamiko yanayobagua kwa utaratibu uleule kwamba ya kwao hayatuhusu na hivi hatuendi sawasawa.

Serikali haiwezi kuwa na uamuzi wake uliokuwa tofauti na wa wananchi katika lolote. Kwani serikali ni nini ndugu?

"Uamuzi wa serikali usiokuwa wa wananchi huo ni batili."

Ndipo hapa ambapo huyu mama na awache mara moja kushupaza shingo.

"Kibri si maungwana!"


Swala hapa sio kusema tu ila tunachotaka ni kuona.

Kwa hakika kusema ni suala!

Hilo ndilo suala lenyewe haswa kama hatuoni tunachokitaka. Kwa hakika kama ndivyo tutaruka naye.

Kuliko Koni kutaka kutubaka mchana mchana kweupe?

Huenda tumebuggie kama mawazo yako yalivyo lkn pia huenda umebuggie wewe.

Kwamba mko kimya ati mwaona hawa wenzetu ni mahaini? Kwani hata ipo siri basi? Kwani vipi dhamana hizi? Mbona hata bi mkubwa anajua ka boogie? Sembuse nyie?

Kauli ya wengi ni kauli ya Mungu. Mola hajawacha kusema ole kwao wenye kuikaidi kauli yake.

Mbona ni suala la muda tu?
Sawa. Mimi nangoja kuona kwa vitendo haya unayodai leo. Kule waswahili husema "tusiandikie mate na wino upo"

Waulize kule kama twaandikia mate. Kwani dar - Mbeya - Dar nauli nani kalipa? Slaa aliwaomba safari hIyo au tuseme ilikuwa ni royal tour?

Sio kwamba atatawala kwa mujibu wa katiba, bali hivi sasa anatawala kwa mujibu wa katiba. Akienda kinyume na katiba bunge litamwodoa kwa mujibu wa katiba yenyewe.

Atake asitake atatawala Kwa mujibu wa Katiba. Skooner kwenye katiba? Aah aah!

"Kama kwenu hiyo ni sawa huko huko, ila si kwetu:

FuOaIYLXgAAoFSO.jpeg


Habari ndiyo hiyo.
 
Kama kumbukumbu huna huwa unaweza hata uka google kujiridhisha:
Nimeiona. Waliokamatwa kwa uhaini walikuwa ni babu Duni.
Kumbe wajua wajadiliana na brazaj? Basi mrejee brazaj tokea 26 Nov 2016 si kabla ya hapo.
Wewe ulidhani sijui? Hapa hujatumia ID fiche, hivyo nakuona na nakutambua na hilo halitaki tochi.
Hadi hapo utakuwa umetambua uzoefu wako wa ki analogu haufui dafu kwenye wa mamboleo almaarufu - kidijitali.

Aghalabu ni kuwa waungwana husema 1+1 = 2 haijali ni wazoefu wa wajinga wangapi wanasema ni 5.
Uzoefu sio lazima wa kidijitali, hata huo wa analog ni uzoefu na ndo ulotupeleka hapa kwenye dijitali.

Ni kweli hesabu ya moja na moja ni mbili kianalogi lkn onaweza kuwa tatu au nne. Hii huijui na dijitali yako? Waswahili husema ukimnyooshea mwenzio kidole kimoja, vitatu vinaelekea kwako. Na hili nalo unapaswa kulijua.
Wapi na lini, au mimi na nani tulisema zi tofauti?
Tunazungumzia JF na sio mahala pingine.
Lini tumeacha kuwanyooeshea vidole hao ndugu? Au wewe hujausikia ule wimbo wao pendwa kuwa - CCM ni Ile Ile?

"Au kwenu nyie yenu ni ya zambarau?"
Hili la CCM tunasema sote.

Kwetu ni mchanganyiko wa zambarau na CCM. Si izi nchi ni tofauti?
 
Ama kweli dunia inakwenda kasi sana.

Kwamba Dkt. Slaa, balozi wa Hayati Magufuli leo yuko korokoloni tena chini ya awamu ya 6?

Ikumbukwe hata kina Mbowe hayakuwakuta ya kuwakuta kwenye awamu ile.

View attachment 2717325

Kwa hakika Mh. Kikwette, hata asipoyasemea kwa mara nyingine tena.

Chonde chonde enyi mlioko madarakani:

Kikwette na asikilizwe!
Ndiyo maana issue hii itaondoka na watu. Walifanya jambo la ajabu sana. Mungu ambariki sana Dkt Samia, ninyeye tu mpaka 2035!
 
Back
Top Bottom