Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

Kamati Kuu ya CHADEMA, mkiteua wabunge wa Viti Maalumu kuingia Bungeni, mtakuwa mmefanya kosa kubwa sana

Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Katika vitu ambavyo CCM kwa sasa wanatamani vitokee, ni kupata wabunge wa upinzani japo wachache ili kuondoa dhana ya Bunge kuitwa Bunge la CCM-Bunge la chama kimoja...
Jambo la kwanza litakalofanyika,
Ni kubadili sheria ili mbunge akivuliwa uanachama na chama chake aendelee kuwa mbunge. Ili wale watano waendelee kuwepo bungeni hata kama vyama vyao vitaamua vinginevyo

Sent from my vivo 1611 using JamiiForums mobile app
 
Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Katika vitu ambavyo CCM kwa sasa wanatamani vitokee, ni kupata wabunge wa upinzani japo wachache ili kuondoa dhana ya Bunge kuitwa Bunge la CCM-Bunge la chama kimoja...
Tuangalie na upande mwingine wa kiuchumi! Hivi wakiingia bungeni wakawa wanavuna mpunga tu kuna ubaya gani? Mimi nashauri tupotezee wabunge waingie bungeni wakae kimya kabisa wasiseme lolote! Maana hizi ruzuku zitatusaidia pia kuimarusha chama!
 
Ni hivi. Hakuna mbunge wa cdema kuingia bungeni. Yani wawe wenyewe waone wafanye movie zao walizozoea
 
Naunga mkono hoja, kwa namna uchaguzi ulivyoendeshwa na hatimaye matokeo yake...ni sahihi kbs kwa chadema kususia takataka yoyote inayohusiana na ma ccm.

Wasishiri haramu hata kidogo.
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekitaarifu CHADEMA kupeleka majina 22 ya viti maalumu.

Inasemekana uongozi mkuu wa CHADEMA umeketi leo kujadili kuhusu hili swala. Kikubwa ni wapeleke majina au wasusie...
Majina hupelekwa NEC katika hatua ya uteuzi wa wagombea
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekitaarifu CHADEMA kupeleka majina 22 ya viti maalumu.

Inasemekana uongozi mkuu wa CHADEMA umeketi leo kujadili kuhusu hili swala. Kikubwa ni wapeleke majina au wasusie...

Mwambie mwenyekiti wako Freeman za kuambiwa achanganye na zake; maana Tundu hayupo kwa maslahi ya chama wala nchi ila yupo kimaslahi binafsi. Kwa maana hiyo mwenyekiti afanye maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi na chama chake

Wakisusia hizo nafasi 22 wenzao watakuja kuzijaza kwa kasi ya 5G, na wajue pia kujenga upya chama bila kuwa na wawakilishi bungeni ni kazi kubwa zaidi.

Halafu waambie hapo kijiweni kwako rais John Pombe Magufuli amesema Tanzania ni tajiri, najua wanajua kabisa wao kakatisha au kupunguza hiyo misaada kunaweza kuwapotezea maslahi yao mengi sana Tanzania pia.

Hii ni Tanzania ya sasa rais ni John Pombe Joseph Magufuli
 
Yaani wafanyiwe kila aina ya uharamia halafu waingie bungeni kwa njia ya asante NEC?.

Huu siyo muda wa kugawana nafasi za kula, kuingia bungeni ni kulegitimise mchakato haramu...
Shida ndiyo hiyo. Kwa sababu uliwapigia kura basi mtu mwingine yeyote ambae aliwapigia kura lakini ana mawazo tofauti na wewe amekuwa influencer aliyetumwa na CCM n.k.

Kwa upande wangu, unachokipendekeza ndicho wanachotaka CCM. Wanajua kabisa kuwa uwezo na nia wa kuichangia CHADEMA ili ijiendeshe hamna. Kama vile wanavyojua kuwa uwezo na moyo wa kuingia mtaani kudai hiyo Tume Huru hamna. Viongozi wenu wamekuwa wakikamatwa, lakini ni wachache sana mlioweza kuonyesha sura zenu kwenda kwenye vituo waliko wekwa na kudai waachiwe.

Kuna viongozi wa Bavicha wako ndani zaidi ya miezi minne lakini hatujasikia wala kuwaona mkishinikiza kwa vitendo wapewe dhamana. Kuna vijana wengi wako ndani kwa kukosa dhamana na wala hatujawasikia mkijikusanya kuwatolea dhamana. Ni kweli mliwalipia faini viongozi wenu lakini hamkuonekana wakati wakina Halima wanapata kipigo. Wametangaza maandamano hamkuonekana. Mkiulizwa mnasema mlitaka wao watangulie!

Mnajazana humu kuwatishia wakina Mbowe na viongozi wenzake kuwa wasithubutu kuwaangusha wakati hamjapitia theluthi moja ya mateso ambayo wao wamepitia kukitetea chama chao na taifa lao. Unawaambia watafute namna nyingine ya kusurvive nje ya ruzuku na michango ya wabunge wao ukisahau kuwa wengi wao biashara zao zimeathirika sana, wana kesi mahakamani ambazo inabidi wagharamie na kuwa biashara zote zinaratibiwa na serikali. Aidha, taratibu za kupata michango na misaada kutoka nje ya nchi zinawabana vilivyo.

Hapana msiokitakia mema chama mnachojifanya kushabikia ni nyinyi, sio sisi. Kama nchi itaingia kwenye hilo giza unalodai,wa kulaumiwa watakuwa ni wananchi ambao wameshindwa kusimama na wapinzani wakati wana wapigania na sio viongozi wa vyama hivyo.



Amandla...
 
Walioshinda ubunge kama yule dada wa Nkasi aende bungeni (japo namtilia shaka nyendo zake), viti maalum nao waende bungeni, na wale wanaoona wameonewa kwenye majimbo yao hawakushindwa kihalali waende mahakamani...

Bila fisi kumsusia butcher hakiwezi kueleweka.

Mbona Zanzibar kimeeleweka?

CDM wajichunge sana na mawazo uchwara haya ya kigamba gamba.
 
Mwambie mwenyekiti wako Freeman za kuambiwa achanganye na zake; maana Tundu hayupo kwa maslahi ya chama wala nchi ila yupo kimaslahi binafsi. Kwa maana hiyo mwenyekiti afanye maamuzi sahihi kwa maslahi ya nchi na chama chake...
Gamba kazini.
 
Bila fisi kumsusia butcher hakiwezi kueleweka.

Mbona Zanzibar kimeeleweka?

CDM wajichunge sana na mawazo uchwara haya ya kigamba gamba.
Zanzibar kimeeleweka kitu gani?
 
Shida ndiyo hiyo. Kwa sababu uliwapigia kura basi mtu mwingine yeyote ambae aliwapigia kura lakini ana mawazo tofauti na wewe amekuwa influencer aliyetumwa na CCM n.k...
Sisi ndo wananchi ambao ni mitaji ya wanasiasa huu ndio msimamo wetu wakikubali kupeleka wabunge wa viti maalum bungeni itawaghalimu zaidi
 
Sisi ndo wananchi ambao ni mitaji ya wanasiasa huu ndio msimamo wetu wakikubali kupeleka wabunge wa viti maalum bungeni itawaghalimu zaidi
Itawagharimu nini? Kama kweli kura zenu ziliporwa mbona hamuonekani kuzidai? Uchaguzi huu umedhihirisha kabisa kura zenu hazina thamani na nyinyi si lolote si chochote.

Amandla...
 
Kuna mnyukano huko wa hatari kina Matiko, Mdee, Bulaya, Magelesi and the likes wameunda women wing kushinikiza kamati kuu kuwaruhusu wateuliwe na kushiriki bingeni kama viti maalum, vinginevo wakiwahama wasilalamike.
Kama ni viti mahalum wahame tu, mtoa mada katoa hoja nzito na fikilishi wananchi hasa wafuasi wa chadema hawategemei eti chadema kutoa viti mahalum,
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekitaarifu CHADEMA kupeleka majina 22 ya viti maalumu.

Inasemekana uongozi mkuu wa CHADEMA umeketi leo kujadili kuhusu hili swala. Kikubwa ni wapeleke majina au wasusie...
Kama huo ubalozi wako unataka kutoa pesa kwa ajili ya kukuza demokrasia Tanzania, hiyo pesa itasaidia nini kuwafidia waliodhulumiwa haki zao kwenye uchaguzi uliopita?

Hiyo pesa itapewa serikali ya CCM, na wanaweza wakaipeleka kwenye kufanya mambo mengine kabisa, bado sijamuona mwenye best alternative ya kususia kwenda bungeni.
 
Shida ndiyo hiyo. Kwa sababu uliwapigia kura basi mtu mwingine yeyote ambae aliwapigia kura lakini ana mawazo tofauti na wewe amekuwa influencer aliyetumwa na CCM n.k...

Kuliko kuhalalisha haramu ni heri wao wote wakaunga mkono juhudi wakachukua kadi za CCM lakini siyo kukubali ujinga, Road to freedom has never been easy. Unataka akina Lissu wawe kama Chief Buthelezi kuungana na Makaburu kwenye udhalimu wao?
 
Walioshinda ubunge kama yule dada wa Nkasi aende bungeni (japo namtilia shaka nyendo zake), viti maalum nao waende bungeni, na wale wanaoona wameonewa kwenye majimbo yao hawakushindwa kihalali waende mahakamani...
Wewe sema waende wakawakilishe wananchi kuwaletea maendeleo swala la katiba mpya sahau swala la katiba mpya.Nafasi ya katiba mpya mlipewa na kikwete bado mkasusa, ccm hawako tayari. Mkiingia labda mbebe hoja ya maji salama kwa kila mtanzania, hata watanzania watawaona mko serious.Hii agenda yenu ya kutaka ccm ichafuke haitawapeleka mahali.

Mkichukua hoja ya maji mtaeleweka, mfano mkudai maji salama kwa kila kijiji kama ilivyo kwa umeme vijijini.Wananchi wanataka maendeleo na Magufuli kawafungua macho, wameonja maendeleo wameyaona matamu, wameonja uzuri wa kufanya kazi kwa slogans ya HAPA KAZI TU, matokeo yake kwa sasa hakuna tena njaa Tanzania.

Mkienda na ajenga zenu za katiba mpya hakuna atayewaelewa.Magufuli anao mkataba na wananchi wenye kurasa 303, amewasomea wananch
 
Itawagharimu nini? Kama kweli kura zenu ziliporwa mbona hamuonekani kuzidai? Uchaguzi huu umedhihirisha kabisa kura zenu hazina thamani na nyinyi si lolote si chochote.

Amandla...
Soma comment hizo za raia watu wanamachungu wamechukizwa na hoja hiyo
 
Soma comment hizo za raia watu wanamachungu wamechukizwa na hoja hiyo


Kigogo kama wewe ana haki ya kuwa na mawazo yake. Yeye hawakilishi mawazo ya raia wote. Kama vile ambavyo mimi siwakilishi mawazo ya raia wote. Huu ni wakati wa kuwaachia viongozi wa Chadema waangalie na kutafakari hatma ya chama chao. Wajibu wao ni kwa chama chao na sio kwetu sisi tunaojimwambafai Twita na JF.

Amandla...
 
Back
Top Bottom