Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

Kamati Kuu ya CHADEMA yawavua nyadhifa na uanachama Halima Mdee na wenzake 18 walioapishwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum

Nyumbu ni CCM kwani acha ufala ulizani ukiipakazia chadema unyumbu kienyeji unakwepa kuwa nyumbu, kutengeneza sinema za kuidhoofisha chadema ni unyumbu hata kuubaka kuunajisi kuulawiti uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani ni unyumbu huo, nyumbu ni CCM hata Ndungai kuwanunua covid 19 ni unyumbu huo
Nyumbuuuuu, hahahaha, labda wewe ni nyumbu mwenye akili. Naomba niulize, kuazimia na kuamua ni kitu kimoja? Nisaidie jibu angalau na wewe uniite nyumbu mara moja japo dunia nzima nyumbu wanajulikana ni akina nani
 
hii inaonyesha level ya education yako!

Tunasubiri kwa hamu sana.Hata Jiwe ataukuwa ametega sikio huku pressure inapanda na kushuka.

Mpaka sasa dalili zinanionyesha kuwa Kamati Kuu imelamba vichwa vya wasaliti wote.

Alafu Ili kuthibitisha kuwa CHADEMA hawahusiki na huo uteuzi wa hao wasaliti, moja ya maamuzi ya kikao iwe ni kulitaka Jeshi la Polisi, tena kwa kuwaandikia barua rasimi, wachunguze sakata hili(tuhuma za kugushi na nyinginezo) bila kujali Polisi watachukua hatua au laa na CHADEMA waahidi ushirikiano alafu tuone kama kunakitachofanyika.

Hii Press inasubiriwa na kufuatiliwa kama fainali ya World Cup!
Subir uone ww polisi wataenda kumkamata mbowe kwa kosa la kuliita bunge geriji

Siasa za hii nch hapana alieshika dola ndio kila kitu
 
Jtatu wanakwemda mahakamani na DPP wakidai kwamba hawakupata nafasi ya kusikilizwa...


...
 
Magufuli na CCM yao wanaweza kufanya lolote ili mradi wapate wakitakacho kujipatia;

å Amani ya muda
å Raha ya muda
å Furaha ya muda
å Madaraka na nguvu za kimamlaka za muda..

Kanuni na sheria na katiba hazina haja kwao...

Kubwa lao Jiwe alishasema zinawashelewesha kupeleka mandeleo kwa wananchi...!!

We are living like animals like those lived in nation called ANIMAL FARM..

Tanzania kwa kasi kubwa tunaanza kugeuka kama ANIMAL FARM.
 
ha
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe atazungumza na Umma wa Watanzania kupitia mkutano na waandishi wa habari, leo Novemba 27, 2020, kuanzia saa 3.00 (usiku huu), kuhusu maamuzi ya Kikao cha Kamati Kuu ya Chama

Vyombo vya habari vya Kitaifa na Kimataifa vimealikwa.

Stay Tuned for Updates

======================
Waandishi wanaanza kuwasili ukumbini wanaoingia wanatakiwa kuwa vitambulisho.
Muda wowote kuanzia Viongozi wa Chadema wataingia ukumbini kuongea na waandishi wa habari.
22:08
Bado Viongozi wa Chadema hawajafika ukumbini
Mkutano huo utakuwa live kupitia
Tayari Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe ameshafika ukumbini
Tunawashukuru Watanzania wengi ambao wanafuatilia kikao maalum cha ajenda moja ya kujadili, kushauriana na kutafakari juu ya wanachama wetu 19 waliokwenda kuapa kuwa wabunge wa viti maalum- Freeman Mbowe
"Sisi kama kamati kuu ya chama kikuu cha upinzani, tumeona na kuridhishwa kuna ukiukwaji mkubwa umekiukwa katika mchakato mzima wa uchaguzi na huu wa viti maalum. Tumejiridhisha ndani ya chama kuhusu mapungufu kadhaa yaliyofanyika-; Mbowe
“Chama chetu hakijateuwa Wabunge wa Viti Maalum lakini tunaona wapo Bungeni wanaapishwa”Mbowe
Tangu nchi hii ipate uhuru hatujawai kuona Mbunge/Wabunge wakiapishwa garage, mambo ya kihuni kabisa haya..." Mbowe
“Hiki chama kinaongozwa na principles bila kujali maumivu makubwa tuliyopitia chama chetu kitafuata utaratibu siku zote, kwahiyo kamati kuu imewavua nafasi zao za uongozi viongozi wote waliokua na nafasi katika mabaraza ya chama.”
@freemanmbowetz

“Kamati Kuu imewavua Uongozi wale wote ambao walikuwa Viongozi kwenye Mabaraza kati ya hao Dada zetu 19 sitaki kupoteza muda kuwataja majina, kwahiyo kuanzia sasa hawapaswi kushughulika na lolote kama Viongozi na tumeelekeza nafasi zao zizibwe haraka” -MBOWE

"Ili kanuni ambayo Spika ametumia iweze kufanya kazi kuapisha wabunge wetu. Kwanza wangestahili kubadilisha Katiba iruhusu wabunge kuapishwa nje ya utaratibu ambao ni ndani ya Bunge" -


Nusrate Hanje Katibu wa Bavicha amefungwa jela siku 133 kwa makosa yenye dhamana, hawa Watesi wetu wanakwenda kumtoa saa moja usiku akaape.”


”Chama chetu hakijateua Wabunge wa Viti Maalum tunaona tu Watu wetu wanaapishwa na hatuna taarifa, hatujapeleka majina, fomu za Tume zipo ofisini Mama zetu hawa Dada zetu hawajajaza fomu, ila tunaona tu wanaaapishwa”-

"Sisi kama chama cha siasa, hii 'process' yote hatuijui, tunaona tu wabunge wetu wanaapishwa. Chama chetu hakijateua wabunge wa viti maalum" -

"Wabunge hawa 19, mama zangu na dada zangu wameapishwa kiapo batili kwani Katiba inasema waapishwe mbele ya Bunge. Sasa kanuni zimebadilishwa ili kumruhusu Spika kumwapisha popote hata eneo la gereji-

“Tangu Nchi yetu imeanza hatujawahi kuona Wabunge wanaapishwa Gereji, lakini Dada zetu na Mama zetu hawa wameapishwa nje ya Bunge, wakati Katiba inataka waapishwe ndani ya Bunge, kwahiyo wamekula kiapo batili”
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amesema Kamati Kuu ya Chama hicho iliyoketi leo Nov 27,2020 imeazimia kuwavua uanachama Halima Mdee na wenzake 18 waliopishwa juzi kuwa Wabunge Viti Maalum “wamekinajisi Chama na wamekataa kuja kwenye Kamati Kuu”

”Chama chetu hakijateua Wabunge wa Viti Maalum tunaona tu Watu wetu wanaapishwa na hatuna taarifa, hatujapeleka majina, fomu za Tume zipo ofisini Mama zetu hawa Dada zetu hawajajaza fomu, ila tunaona tu wanaapishwa”

“Kamati Kuu imewavua Uongozi wale wote ambao walikuwa Viongozi kwenye Mabaraza kati ya hao Dada zetu 19 sitaki kupoteza muda kuwataja majina, kwahiyo kuanzia sasa hawapaswi kushughulika na lolote kama Viongozi na tumeelekeza nafasi zao zizibwe haraka”
"Kamati Kuu imeazimia kuwavua uanachama wake wote 19 wakiongozwa na Halima Mdee , walioapa kule Dodoma.-Mbowe

haya ndo maamuzi sasa ya Chama na hiki sasa ndiyo chama cha Siasa kilichokomaa kisiasa na si kidola. ni heri kukabiliana na matokeo ya mbinu chafu zozote zitakazochukuliwa na dola sababu ya uamuzi huu kuliko kuendelea kubakia na hawa wanawake. chadema mngefanya kosa kuwasamehe mngejipoteza. mmecheza karata vizur hata kama mtateseka kwa muda fulani kukosa ruzuku kidiketa ni heri mara alfu moja, kumbukeni kuwa kuliko kuwa huru ndani ya ubaguzi wa rangi na uonevu wa wachache dhidi ya wengi, mandela nelson madiba alichagua kukaa gerezani miaka 27 na alipotoka akalikomboa Taifa lake. wananchi tumewaelewa cdm na dunia imewaelewa. Hongereni Sana!! hongera sana Mhe Mwenyekiti wa Chama. Mbowe una kipaji sana vizazi vijavyo vitakukumbuka
 
Mnyika yupo kwenye wakati mgumu kwa kujaribu kupingana na mwenye kigoda ambae ndio mwenye maamuzi ya mwisho ndan ya chama. Maamuzi yake yawe ya faida au hasara, hakuna anaeruhusiwa kumpinga wazi wazi wala mafichoni

Ulijiunga hapa jukwaani mwezi wa tisa ili uwe unaoongea huu uzushi?
 
Back
Top Bottom