Kamati maalum ya TLS kuchunguza Mkataba wa uendeshaji bandari ya Dar

Kamati maalum ya TLS kuchunguza Mkataba wa uendeshaji bandari ya Dar

Huu upepo utapita maisha yataendelea

Ova



Kwamba unaichukulia poa hii taharuki ya wananchi juu ya kadhia iliyopo?

Kwamba unawatia moyo Viongozi kwenye uamuzi unaosemekana kufanyika?

Au una maana gani ?
 
Mwanasheria Mkuu nae hana taarifa kwenye huu Ujambazi hawa wazee wa Uchaguzi wa Arusha naona nao wanafuta miguu ya kutokea Nchi inauzwa ndio nao wanaamka...
 
Tunahitaji mkaba mzuri haya mambo ya uarabu, uchina na wazungu hauna tija. Tumejaribu kwa wazawa matunda yake ni kujuana na wizi tu!
Unaropoka lolote linalokuijia akilini bila kufikiri. TICTS wamekaa pale zaidi ya miaka 20, ni wazawa?
Hopeless Kabisa!
 
Kule Kenya, kuna Mwanaharakati, Okiya Omtatah, siku hizi kawa 'Senator' ingekuwa upuuzi huu umetokea huko, saa hizi tayari kesi ingekuwa ipo mahakamani.

Hawa TLS hawana lolote. Ni sehemu muhimu sana ya matatizo ya nchi hii.
 
na ni mmojawapo wa wanasheria waliokuwepo REX ATTORNEYS, waleee wa mkataba wa richmond kama mnakumbuka.
Hao ndo wamiliki wa rex mkuu ni wachagga wa old misho mama mdogo wake na shose sinare
 
Kule Kenya, kuna Mwanaharakati, Okiya Omtatah, siku hizi kawa 'Senator' ingekuwa upuuzi huu umetokea huko, saa hizi tayari kesi ingekuwa ipo mahakamani.

Hawa TLS hawana lolote. Ni sehemu muhimu sana ya matatizo ya nchi hii.
Habari zako ladyboy wa jamii forums. Tupinge mkataba sio ushabiki tu kwasababu kampuni ya nje. Tuna tabia ya kuogopa sana vitu vya nje kwasababu tuna wananchi wengi na wasomi wasio na maono kama Ladyboy huyu! tuwapuuze hawa wasomi mcharwa cha maana mkataba mkataba mkataba!
 
Habari zako ladyboy wa jamii forums. Tupinge mkataba sio ushabiki tu kwasababu kampuni ya nje. Tuna tabia ya kuogopa sana vitu vya nje kwasababu tuna wananchi wengi na wasomi wasio na maono kama Ladyboy huyu! tuwapuuze hawa wasomi mcharwa cha maana mkataba mkataba mkataba!
Yule Mbunge anayejiita Msukuma ni ndugu yako? Tabia zenu zinafanana sana! Ila najua huyo Msukuma siyo pandikizi toka nje kama ulivyo wewe!
 
Yule Mbunge anayejiita Msukuma ni ndugu yako? Tabia zenu zinafanana sana! Ila najua huyo Msukuma siyo pandikizi toka nje kama ulivyo wewe!

Tatizo la wasomi washamba mtu ukiwa international na unajua wanakuita pandikizi, beberu…. Wewe baki kujidanganya tu pandikizi kwa lipi hasa. Mr ladyboy! Wewe tukupe award 🥈
1686324703647.png
 
BARAZA la Uongozi la Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) limeunda kamati maalum ya wataalamu kuchambua makubalino yaliyoainishwa katika mkataba wa uendeshaji bandari ya Dar es Salaam kati ya serikali ya Tanzania na Kampuni ya Dubai ya DP World.

Rais wa TLS, Wakili Harold Sungusia amesema kamati hiyo itaongozwa na Makamu wa Rais wa TLS, Wakili Aisha Sinda na itakuwa na wajumbe wengine wanne

Sungusia amewataja wajumbe wengine kuwa ni

Dk. Hawa Sinare – (Makamu Mwenyekiti),

Wakili Mpale Mpoki – (Mjumbe),

Wakili Stephen Mwakibolwa – (Mjumbe) na Wakili Mackphason Mshana - Katibu“

TLS inatambua uwepo wa mijadala inayoendelea nchini kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu uendeshaji wa bandari ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai… Kamati itatoa ripoti yake na mapendekezo yake kwa Baraza la Uongozi tarehe 12/06/2023 ili TLS iweze kutoa maoni na kwa hatua zaidi,” amesema Wakili Sungusia.

====

TLS inatambua uwepo wa mijadala inayoendelea nchini kuhusu makubaliano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai kuhusu uendeshaji wa bandari ya Tanzania na kampuni ya DP World ya Falme ya Dubai. Kutokana na unyeti wa swala hili, Baraza la Uongozi la TLS likiongozwa na Rais, Wakili Harold Sungusia limeunda kamati ya wataalamu kuchambua makubaliano hayo. Baraza hili litaongozwa na Makamu wa Raisi wa TLS, Wakili Aisha Sinda, likiwa na wajumbe wafuatao.
1. Dkt Hawa Sinare – Makamu Mwenyekiti
2. Wakili Mpale Mpoki – Mjumbe
3. Wakili Stephen Mwakibolwa – Mjumbe
4. Wakili Mackphason Mshana – Katibu
Kamati itatoa ripoti yake na mapendekezo yake kwa Baraza la Uongozi tarehe 12/06/2023 ili TLS iweze kutoa maoni na kwa hatua zaidi.
🤣🤣🤣🤣 Mbwembwe tu hizo mwarabu tayari anachukua bandari chaaap!!!
 
Tatizo la wasomi washamba mtu ukiwa international na unajua wanakuita pandikizi, beberu…. Wewe baki kujidanganya tu pandikizi kwa lipi hasa. Mr ladyboy! Wewe tukupe award 🥈 View attachment 2651414
Mkikuyu uliyejifanya Mmeru wa Arusha halafu ukanunua uraia? Nchi yetu hii imepitia matatizo kwelikweli.

Kisomo huna na wala huna ujualo, bado unajifanya wewe ni mjuaji, tofauti gani kati yako na Msukuma?

Lakini najua Msukuma kajiuza kwa waarabu, wewe je? Unasubiri Tanzania imezwe na Kenya? Hilo sahau.
 
Hawa watu ni wanafki, mkataba umesainiwa tangia October, tuseme hawakujua? Mpaka makelele ya social media ndio waamke!

Kwanza hakuna watakachofanya ni kutafuta popularity ya hovyo! And this tells alot juu ya vyombo ambavyo havina meno!

Haya; TLS watuambie wamefanya nini na mkataba ndio huo umeshabarikiwa na bunge!
 
Hii issue ya DPW ilipoibuka tuliambiwa kuwa TLS wameunda taem ambayo itapitia huo mkataba na kutoa maoni au ushauri wao kwa serikali.

Mpaka sasa umekuwa na upotoshaji mwingi na Wananchi hawauelewi ukweli ni upi na uongo ni upi.

Kwa jinsi ninavyojua TLS walikuwa watupe marejesho at least week moja iliyopita.

Kwa nini TLS wameamua kukaa kimya wakati hii issue ni ya kisheria zaidi na wamewaachia Wanasiasa waendelee kutupa mawazo yao binafsi. Ni lini TLS watakuja hadharani na kuwasilisha maoni yao!!?
 
Ndio kwanza tunaanza kupata picha ya nini kinaendelea nyuma ya pazia. Makubwa yanakuja.
 
Ndio kwanza tunaanza kupata picha ya nini kinaendelea nyuma ya pazia. Makubwa yanakuja.
I wish hii issue ingekuwa wakati Dr. Nshala au Fatma Karume wakiwa madarakani. I hope Dr. Hosea hajaikalia report au hajawahi compromised.
 
Hii issue ya DPW ilipoibuka tuliambiwa kuwa TLS wameunda taem ambayo itapitia huo mkataba na kutoa maoni au ushauri wao kwa serikali.

Mpaka sasa umekuwa na upotoshaji mwingi na Wananchi hawauelewi ukweli ni upi na uongo ni upi.

Kwa jinsi ninavyojua TLS walikuwa watupe marejesho at least week moja iliyopita.

Kwa nini TLS wameamua kukaa kimya wakati hii issue ni ya kisheria zaidi na wamewaachia Wanasiasa waendelee kutupa mawazo yao binafsi. Ni lini TLS watakuja hadharani na kuwasilisha maoni yao!!?

Maji marefu wametulia kama hawapo!
 
Back
Top Bottom