Kamati ya Amani yapiga marufuku Magufuli kuitwa "Mwendazake", Wametumia sheria gani?

Kamati ya Amani yapiga marufuku Magufuli kuitwa "Mwendazake", Wametumia sheria gani?

Lakini kwa mujibu wa Kamusi kuu ya Kiswahili ya baraza la Kiswahili nchini (BAKITA) toleo no.2 la mwaka 2017, neno mwendazake linamaanisha "mtu aliyekufa hivi karibuni na anaelekea kuzikwa au mipango ya mazishi yake inaendelea." Mwendazake ni kisawe cha neno marehemu ama hayati.
Waache upumbavu, kwani Magufuli si bado anaishi mioyoni mwa baadhi ya watanzania? Kwani neno hilo likitumiwa linawadhuru nini wao? Si neno la kiswahili? Hawa ndiyo maana wakati mwingine wanatafsiriwa ni waganga njaa, wamekosa mambo ya msingi ya kujadili wanashikashika vitu very minute, tulitegemea wazungumzie katiba mpya na siyo vineno vidogo kama Mwendazake
 
Ukiisikiliza hii kamati mara nyingine unaweza kupata hasira kiasi ambacho ukatoa maneno ukajikuta umeingia matatizoni kwa kumkufuru mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi pamoja na vyote vilivyomo. Hii kamati si ndio ile ile yupo yule shehe aliyemfananisha mwendazake na Yesu akaona haitoshi akamfananisha na Mtume Muhamad SAW bado hakuridhika akamfananisha na Mungu kabisa. Ngoja niishie hapa hapa nibaki nasoma tu maoni maana naona nikiendelea hii kamati itanichonganisha na muumba.
 
Waache kiherehere hao Maaskofu uchwa walio ufyata kwa Dikteta uchwara mwende zake.
Kumbe hata wao maaskofu uchwara wanajua kuwa mwenda Zake ni Magu basi kwa mamlaka niliyopewa natamka shujaa Wa waganga wa gamboshi na uuaji ataitwa Mwenda zake milele hapa duniani na huko kuzimu alipo

Sent from my TECNO-W3LTE using JamiiForums mobile app
Nayo ni majizi tu kama majizi wengine
 
Hii kamati si ndio ile ile yupo yule shehe aliyemfananisha mwendazake na Yesu akaona haitoshi akamfananisha na Mtume Muhamad SAW bado hakuridhika akamfananisha na Mungu kabisa
Ni kweli Mkuu wakati mwingine bora kuwasamehe maana hatujui hata huo uongozi waliupataje
 
Kamati ya amani ya viongozi wa dini nchini imepiga marufuku, John Pombe Magufuli kuitwa "mwendazake". Mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT), Askofu Peter Konki amesema neno "mwendazake" ni matusi makubwa kwa Magufuli na ametaka wanaotumia neno hilo washtakiwe kwani wanahatarisha amani.

Lakini kwa mujibu wa Kamusi kuu ya Kiswahili ya baraza la Kiswahili nchini (BAKITA) toleo no.2 la mwaka 2017, neno mwendazake linamaanisha "mtu aliyekufa hivi karibuni na anaelekea kuzikwa au mipango ya mazishi yake inaendelea." Mwendazake ni kisawe cha neno marehemu ama hayati.

Je unaamini neno mwendazake ni matusi? Je wanaomuita JPM mwendazake washtakiwe kama alivyoshauri Askofu Konki? Je Askofu apuuzwe, au anunuliwe Kamusi ajifunze Kiswahili?

Credit Malisa GJ

Hawa wazee kazi yao ni kupiga marufuku,au kuhamaisha amani
😆😆😆
 
Kwanza watueleze na watuthibitshie pasipo shaka kuwa wamejuaje kuwa huyo mheshimiwa waliyemtaja ndio watu wanamwita mwendazake. Pili hawaoni kufanya kwao mkutano na kutangaza kupiga marufuku ndio watakuwa wanatangaza kabisa na kuwajuza hata wale ambao walikuwa hawajui kuwa mwendazake ni nani sasa watamjua.

Mimi nafikiri viongozi wetu wa dini wana wajibu mkubwa sana katika maisha ya mwanadamu ya kila siku. Lakini kujiingiza huku kwenye hayo mambo ya kutoa matamko sijui watu wasimwite fulani mwendazake kunawashushi hadhi waliyo nayo kwenye jamii kwani haya majina/maneno mengine huzuka ghafla kutokana na msimu na mazingira yalipotokea tukio fulani kwa hiyo hata mwisho wa hayo majina/maneno nao huwa ni ghafla tu bila hata matamko.
 
Yeye aliyebaki ndio tutamwita mwendazake maana analitaka hilo jina “ mwendazake askofu konki “
 
Kwa kufanya hivo ni kutuonyesha jinsi wanapingana na kamusi ya TUKI
 
Kamati ya amani ya viongozi wa dini nchini imepiga marufuku, John Pombe Magufuli kuitwa "mwendazake". Mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT), Askofu Peter Konki amesema neno "mwendazake" ni matusi makubwa kwa Magufuli na ametaka wanaotumia neno hilo washtakiwe kwani wanahatarisha amani.

Lakini kwa mujibu wa Kamusi kuu ya Kiswahili ya baraza la Kiswahili nchini (BAKITA) toleo no.2 la mwaka 2017, neno mwendazake linamaanisha "mtu aliyekufa hivi karibuni na anaelekea kuzikwa au mipango ya mazishi yake inaendelea." Mwendazake ni kisawe cha neno marehemu ama hayati.

Je unaamini neno mwendazake ni matusi? Je wanaomuita JPM mwendazake washtakiwe kama alivyoshauri Askofu Konki? Je Askofu apuuzwe, au anunuliwe Kamusi ajifunze Kiswahili?

Credit Malisa GJ

Hawa wazee kazi yao ni kupiga marufuku,au kuhamaisha amani
Hatuachi kama wanaona vipi wanywe sumu wamfuate. Viongozi wa dini sampuli hii ni wa kuwasusia kabisa kwenye nyumba za ibada wanakohudumu
 
Kamati ya amani ya viongozi wa dini nchini imepiga marufuku, John Pombe Magufuli kuitwa "mwendazake". Mwenyekiti mwenza wa kamati hiyo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la maaskofu wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT), Askofu Peter Konki amesema neno "mwendazake" ni matusi makubwa kwa Magufuli na ametaka wanaotumia neno hilo washtakiwe kwani wanahatarisha amani.

Lakini kwa mujibu wa Kamusi kuu ya Kiswahili ya baraza la Kiswahili nchini (BAKITA) toleo no.2 la mwaka 2017, neno mwendazake linamaanisha "mtu aliyekufa hivi karibuni na anaelekea kuzikwa au mipango ya mazishi yake inaendelea." Mwendazake ni kisawe cha neno marehemu ama hayati.

Je unaamini neno mwendazake ni matusi? Je wanaomuita JPM mwendazake washtakiwe kama alivyoshauri Askofu Konki? Je Askofu apuuzwe, au anunuliwe Kamusi ajifunze Kiswahili?

Credit Malisa GJ

Hawa wazee kazi yao ni kupiga marufuku,au kuhamaisha amani
Akumbushwe Amani haiji kwa marufuku.
 
Back
Top Bottom