Kamati ya Amani yapiga marufuku Magufuli kuitwa "Mwendazake", Wametumia sheria gani?

Na mimi nitawashataki kwa kutumia jina langu vibaya...
 
Kama kuna watu wamepigwa na njaa hizi siku 100 za kwanza za Mother ni viongozi wa dini feki, wasanii feki, wamiliki wa vyombo vya habari vya hovyo (Musiba na wenzake) na watoto pendwa wa jpm wasiokuwa na maadili (Sabaya and co). Kwa sasa wataropoka lolote ili nao waonekane, but the good thing is Mama hana shobo na wanafiki na waganga njaa. Jana kuna msanii kamsifu mother then kamwambia Mama simama watu wakuone akamgomea tena kwa kutikisa kichwa
 
Huyo Askofu wa Kilokole ndiyo wale walimpa Nishani ya kuishinda Covid
 
Hahah ila hilo neno limekaa kikuda...lakini sasa ndio lishakuwa maarufu
 
Hivi hii "Kamati" inafanya kazi kutokana na sheria gani?
 
Wana mapepo hawa sio bure
 
Mwendazake neno la kistaarabu tu. Naona shida chimbuko lake Kenya. Tanzania hatuna hati miliki ya kiswahili ,plain stupid to brew controversy on non issue.
 
Sasa kwani hajaenda? Si amekwendazake au nasema uongo ndugu zangu?
 
Wachache walijiundia kakikundi fulani, wakakaita kamati ya Amani, eneo lisilo na machafuko😆😆😆kisha wanaamini wao wana nguvu na mamlaka ya kutoa matamko ya kupiga marufuku.

Wanatafuta kuchochea ili tumuite mwendazake, ili wapate kukaa vikao vya kujadili kupiga hatua za kuchukua kwa wale watakaomuita mwendazake, mwendazake. Are we together?

Siyo vibaya kuunda pia kamati ya uzalendo.
Tunahitaji kamati ya upendo.
Nafikiria hata kamati ya uvumilivu.

Everyday is Saturday................................😎
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…