#COVID19 Kamati ya Corona: Serikali itoe taarifa uwepo wa Ugonjwa wa COVID-19 na kuruhusu matumizi huru ya chanjo

#COVID19 Kamati ya Corona: Serikali itoe taarifa uwepo wa Ugonjwa wa COVID-19 na kuruhusu matumizi huru ya chanjo

Hilo la kutoa takwimu za corona litakuwa jambo gumu kweli kweli... yani itakuwa ni kulamba matapishi.... mzee meko aliharibu mambo sana
 
Mtego upo kwenye lockdown.
Wasije tu wakamshauri mama yetu mambo ya lockdown mana watu watapandwa na hasira za ghafla.
 
Mwaka wa pili huu tangu wimbo wa corona, Watu tunaishi vizuri tu,hapo Kenya alipokwenda kujifunza walijifungia mpaka wakachoka mpaka sasa wameamua kuishi nao na kuchapa kazi, sasahivi mashule yamefunguliwa,eti Sisi huku ndio tunatangaza corona,ni njinga tu anayeweza kuamini hii ripoti,kisa eti awafuraishe wazungu wampe misaada

Wenzenu wanapata chanjo wanatoka ndani unafikir wanatoka kwa kuwa wamechoka hii nchi ina wapumbavu sana
 
Corona ilimng'oa Trampol, kiongozi mwenye kucheza ovyo na suala hili, Kwenye kura atapata Hasira za wananchi wake,

Kwa sasa itakuwa kama tuko pamoja
 
Kamati inasema nini?
Inataka kuibua hofu na taharuki kwa wananchi,wananchi wote wanajua kama corona ipo....ya nini kutishana bwana,wakati mwingine anco alikuwa sahihi...wazungu hawatutakii mema kabisa na haya mavibaraka yao.
 
Matumizi mabaya ya kodi za wananchi tu taarifa gani watazitoa zaidi ya porojo tu Dunia nzima inajua covid ipo. Tanzania tulisema Covid hakuna kwetu na mazingira tunavyoishi mtaani kama ingekuwepo kweli kila siku tungekuwa tunazika watu .

Waje na porojo zao but swala la lockdown na chanjo hatutaki ..maana chanjo imekuwa ni biashara kubwa na inampaka madalali na nina imani hata watu wa tume madalali wameshawafata

Naona kuna mtu anataka kufungua duka saa 2 usk wakat wenzie wanakaribia kufunga biashara .
Keyboard warrior una jeuri gani yakukataa kitu ikiwa jiwe aliwaburuta kama Ng'ombe

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Kilio cha wanachadema kimesikiwa, nadhani wakiongeza kelele kidogo tu kuhusu lockdown, Napo watasikiwa na baada ya hapo chanjo itafuata

Sasa nyinyi CCM kaeni na agenda yenu ya kutoyatambua hayo Ila nchi inaenda kuambiwa Corona ipo hata kama tulifahamu hivyo
Nafikiri tunaenda kutangaza lockdown, sijui familia kama zina chakula cha kutosha majumbani. Nahisi vifo vya njaa vinakaribia hongereni CHADEMA naona Sera zenu zinatekelezeka.
 
Kamati inasema nini?
Inataka kuibua hofu na taharuki kwa wananchi,wananchi wote wanajua kama corona ipo....ya nini kutishana bwana,wakati mwingine anco alikuwa sahihi...wazungu hawatutakii mema kabisa na haya mavibaraka yao.

Watakuwa wajinga sana hao wenye hofu ilikiwepo tb na watu walienda sawa had kumetulia waje kuogopa corona? Hizi porojo za mwendazake hazina nafasi
 
Mara paap jamaa kaibuka toka kwenye kibanda cha mabati.
 
Watu huku mtaani tunaishi vizuri sana, hatuna hofu wala mashaka ya kifo, naona sasa yanaletwa. Naendelea kusema hakika mwanasiasa ndiye Mungu wa dunia hii. Maana akiamua ameamua akisema amesema lazima wote tuseme amina. Baada kufa mwanasiasa mmoja anakuja mwasiasa mwingine na mambo yanabadirika, kweli mwanasiasa ndiye Mungu wa sunia hii.
 
kinachotafutwa ni justifications... ili maamuzi atakayofanya mama ambayo tayari anayo tudhani yametokana na hii tume.. ni technique moja ya ufanyaji kazi.
Mkuu Covid ipo toka 2019 imepiga waves zote kwa nguvu nchi ambayo kwa sasa covid inaitesa ni INDIA ,Tanzania tuliamua kuchukua uamuzi wa wachache yani No Lockdown kuvaa mask ni utashi wako na kutozuia mikusanyiko na Mungu alikuwa upande wetu kwa maana hatuna athari kubwa sana za covid mpk sasa

Dunia inakwenda kufunguliwa kwa maana nchi nying zimeshaachana na masharti yale makubwa kuhusu covid (Lockdown,Mask On , Social Dis nk)na maisha yanaendelea kurudi kawaida tu.. sasa nitashangaa sana huyu mama kuturudisha nyuma yani mtoto anatembea kisa hakupitia stage ya kutambaa unamwambia arudie step ya kutambaa by the way Covid Funds wazungu hawatoi siku hz... coz trend ya Ugonjwa inakwisha Kenya wamekula sana hii hela sisi tukasema watusamehe madeni hatukuchukua sasa sijui huyu anataka nini

Hakuna Sehemu ambayo Mtanzania amepigwa Burn kuwa tusiende kote tunaenda ni kupima tu covid test then unajichanganya .. Ngoja tuone kilichokuwa nyuma ya yale mabarakoa waliokuwa wanavaa
 
Back
Top Bottom