Uchaguzi 2020 Kampeni za uchaguzi huu zimetufundisha mengi kuhusu CCM, hata wakishinda uchaguzi kwa hila siku zao madarakani si nyingi

Acheni kujidanganya hakuna Mwananchi anyeweza kuamua chochote, Mapinduzi yote Dunaini yana Viongozi nyuma yake, Wanananchi kama Wananchi hawajawahi kufanya mapinduzi popote pale tangia kuanza kwa Dunia hii, ...
Huwajui viongozi wetu au unajitia wendawazimu!
 
😂😂😂😂😂😂😂
 
Umeandika kinyonge, huna matumaini tena kuwa Lissu atashinda?
 
Tanzania ilikuwa na watu wajinga wajinga! Ukiwa huna exposure nje ya Tz unaweza ona Tanzania ina watu smart, Mpaka nilipopata kwenda ughaibuni ndio nilifahamu Tz idadi kubwa ni wajinga.

Lakini muamko upo, hasa kipindi hichi ambacho mchangamano wa watu unapoongezeka.

Ukitaka kujua hili angalia sehemu kubwa ya majimbo ya mijini ndio mwamko ulipoanza wa mabadiliko.

Mbeya mjini, Iringa mjini, kigoma mjini, Arusha mjini, Moshi mjini, Bukoba mjini, Tanga mjini, Mwanza

Hapo mchanganyiko ni Mkubwa, Vijijini muamko utakuja hivi punde tuu.

Ngome Kuu ya CCM kwa sasa ni Dodoma, Singida tuu hata kanda wa ziwa kwa sasa si sanaa. Na Dodoma walikuwa wazembe kwasababu hakuchangamana sana wagogo, na hali ya ukame wengi hawakupapenda, sasa ndani ya awamu 2 zijazo changes zitakuja tuu, sasa ivi wagogo wana exposure ya makabila mengi;

Nilipata kwenda Mtera na Kongwa 2013 aisee Nafsi yangu iliumia sana, sikuwahi kufikiri kama kuna watanzania wenzagu wanaishi mazingira mbaya namna ile.
 
Huwajui viongozi wetu au unajitia wendawazimu!

CHADEMA &Co. wanashindwa na hawawezi kufanya mapinduzi au hata tu kuilazimisha CCM ikae meza moja nao na kuongea kwa sababu hawana hela, kufanya Mapinduzi siyo kazi ya kitoto, unahitaji mkwanja wa kuwalipa hao watakao hatarisha maisha yao na kuingia barabarani, kama hauna hela utabakia mikwara ya mitandaoni tu kama sasa hivi, ...
 
Haya ndiyo mawazo yanayowapa viburi. Kumbuka watakao jitoa mhanga ni wale ambao ndugu zao wa karibu walionja mateso ya Jiwe.
 
Utawala wowote huwa hauzidi miaka 40,soma historia, ccm ilikufa 2015 ikabebwa na dola na sio mioyoni mwa watz. Kila Jambo lina maana yake kinabii ujio wa corona umepelekea kukiukwa kwa zindiko la mwenge hapa masharti yamekiukwa, waliambiwa wautembeze mwenge kila mwaka ili kupumbazia akili za watz sababu wamekiuka masharti ni lzm ccm ife.
 
Haya ndiyo mawazo yanayowapa viburi. Kumbuka watakao jitoa mhanga ni wale ambao ndugu zao wa karibu walionja mateso ya Jiwe.

Hakuna kitu kama kujitoa mhanga Dunia hii, kila kitu huwa kinapangwa na huwa kuna watu nyuma ya wajitoaji mhanga, na ili uweze kufanya hilo unahitaji mkwanja mrefu, bila mkwanja hakuna kitu, na chadema hawana hela, ...
 
Hakuna kitu kama kujitoa mhanga Dunia hii, kila kitu huwa kinapangwa na huwa kuna watu nyuma ya wajitoaji mhanga, na ili uweza kufanya hilo unahitaji mkwanja mrefu, bila mkwanja hakuna kitu, ...
Jana si leo, ni hayo tu.
 

Wewe jidanganye hivo sababu hujuwi wananchi wana hasira kiasi gani kwa haya yankukusanya wandunzi na wafanyakazi kwa nguvu wakati watu wamezidi kuwa masikini katika awamu hii subiri utaona na moto utaanzia Zanzibar Kesho
 
Mradi sasa ni hakika kuwa NEC ipo upande wa ccm, sioni njia nyingine ya kutokea zaidi ya nguvu ya umma!
 
Wewe jidanganye hivo sababu hujuwi wananchi wana hasira kiasi gani kwa haya yankukusanya wandunzi na wafanyakazi kwa nguvu wakati watu wamezidi kuwa masikini katika awamu hii subiri utaona na moto utaanzia Zanzibar Kesho

Mimi nakwambia uhalisia jinsi ulivyo, wananchi kuwa hasira hilo linajulikana Dunia nzima kuna Wananchi wana hasira, lkn kuwa na hasira na kufanya Mapinduzi ni vitu viwili tofauti, Wananchi kama wananchi wanahitaji Kiongozi ili waweze kufanya chochote, na kufanya chochote unahitaji mkwanja, hakuna atajayeingia barabarani huku tumbo ni tupu watoto hawajakula nyumbani, utamwambia machinga au boda boda aingie barabarani bila ya kumpa hela atakuelewa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…