Kampuni inayomiliki Tigo yabadili jina, sasa ni Honora Tanzania

Kampuni inayomiliki Tigo yabadili jina, sasa ni Honora Tanzania

Kuna wapumbavu humu wala hawastahili hata kujibibiwa.

TRA wana Chuo kabisa cha Taxation, Nina rafiki yangu ni Advocate huwa nikimpelekea kazi kwa sababu tunaheshimiana huwa ananitafutia Wakili aliyejikita kwenye angle hiyo mawakili wanajuwana vizuri sana nani bora kwenye case zipi, kwa sababu yeye anadeal na corporate, huwezi kumpelekea criminal case akaingia tamaa, haendi mahakamani kusimamia criminal case hata siku moja.

Kuna mawakili wa mirathi na ndoa wamejikita hapo, kuna mshuwa wangu alikuwa ni Mwalimu wa Chuo cha Ardhi wakati huo wao ndio waanzilishi wa savey na sasa ni advocate, huyo ukipambana naye kesi ya Ardhi lazima akukalishe.

Tundu Lisu licha ya kuwa ni Wakili bora lakini inasemekama angle yake ni upande wa mazingira.

Sasa JF imevamiwa na vichaa inabidi tuwavumilie.

Yani sasa kila msomi analazimika kujuwa mambo ya Taxation, hizi sijui ni akili za wapi?
Uko sahihi Dr mwenzetu
Wasikubabaishe hao vijana vijinga jinga
 
Home shopping center siyo GSM ingawaje wamiliki ni wale wale.

Home shopping center ilifungwa kisheria kwa kufuata taratibu zote za kisheria.

Wengi hawajaelewa swali langu la msingi hapo juu, Mimi ni mnufaika wa kampuni moja kubwa sana ambayo makao makuu yake hapo ulaya, tuliingia mgogoro mkubwa sana wa kikodi mpaka kufikia kufunga kampuni lakini taratibu zote za kulipa kodi ya serikali zilifuatwa na serikali ikalipwa kodi yake na kuifunga kampuni.

Zipo some cases kampuni inanunuliwa na kampuni nyingine, mfano ni SDV NOTCO imenunuliwa na Bollore ya Ufaransa na sasa inaitwa Bollore hapa unakwepaje kodi?

DAHACO imenunuliwa na Swiss port na sasa inaitwa Swissport hapa unakwepaje kodi?

Ndio sababu nikaomba kuelimishwa, kwa sababu hii ni issue tofauti kabisa na hiyo Tax holiday otherwise Wahindi wangekuwa wanabadilisha majina tu kama ni kitu rahisi hivyo.
Uko vyema sna Dr

Naoomba unipe abcd za bollore logistics

Kuna faili langu hapo ofcn kwao Hadi Sasa sijajibiwa tabata mwananchi
 
MIC TANZANIA imefanya kazi kwa hasara kwa miaka mitatu mfululizo hivyo imeamua kuuza shares zake zote kwa kampuni ya HONORA ili nayo ijaribu na kama nayo itapata hasara ndani ya miaka mitatu itauza shares zake!

Hivi ndivyo Tanganyika inavyoliwa na wajanja kupitia sheria zetu mbovu za uwekezaji[emoji24]
I was asking my self ,what the reason behind kumbe sio kubadili kuna ni wamehamisha umiliki kwa kuuza share
 
Lakini Kwa hapo nilivyosoma taarifa yao naona si mwekezaji mpya ni Jina Tu limebadilika ,tin inabaki ileile,faili Lao brela inabaki hilohilo sababu kubadili Jina hakubadili incorporation no ,sasa Kwa hapo tax exemption inakuaje
NB :Nimefanya kazi ya kubadili majina ya makampuni Kwa miaka isiyopungua 10
Na ikiwa kwamba former kampuni ilipata hasara.
 
Unaweza kuwa na PhD ikawa sio ya hiyo fani na usijue Mkuu au nakosea ukiwa na PhD ya vitunguu lazima ujue mambo ya upasuaji kwa kuwa una PhD tuu..
Upewe maua yako, hili sakata la kila mtu mjuzi kwa kila jambo linafanya wajuzi wanyamaze kutotumia nguvu nyingi kuelimisha mtu anaejua kila kitu lakini hajui
 
Nilihamishia biashara yangu kwa mtu mwingine. Nikaenda TRA kubadili umiliki. Meneja akasema bora umekuja. Maana ungesema unafunga tungekosa mapato. Nafikiri kunatechnicalities za kikodi ambazo zinacheza kwenye kuuza, kufunga au kuhamisha umiliki wa biashara.
Mm nafahamu japo kidg kuwa kufunga biashara ni hasra kwa serekali ila kusimamisha Ina ruhusiwa na makadirio yako yatasimama. Hadi uanze upya Tena

Marka nyingi ssi wamiliki wa magri ya biashra tunacheza sna michezo hyo gari ikiaribika kidg tu tuna kimboa tra kiwaataarifu kwa barua
 
Lakini Kwa hapo nilivyosoma taarifa yao naona si mwekezaji mpya ni Jina Tu limebadilika ,tin inabaki ileile,faili Lao brela inabaki hilohilo sababu kubadili Jina hakubadili incorporation no ,sasa Kwa hapo tax exemption inakuaje
NB :Nimefanya kazi ya kubadili majina ya makampuni Kwa miaka isiyopungua 10

Bwana Singo,Ulishawai kufanya kazi na Sirjeff Dennis..kama niwewe basi jibu lako ni sahihi kwa kuwa nakufahamu very well..
 
Kampuni mpya ya Honora Tanzania imetoa taarifa kwa wadau wake katika biashara kubadili jina kutoka MIC Tanzania kwenda Honora Tanzania. Pamoja na kubadili jina la kampuni, Honora wataendelea kutumia 'Brand name' ya Tigo na huduma zote zitabaki kama zilivyo.

Honora Holdings Limited imesajiliwa Mauritius.

View attachment 2725843
Mauritius 🇲🇺 ni tax haven
 
sikiliza, kuna relief ya kodi. Unaendsha kwa miaka 3 kama hakuna faida unaacha. Ujanja, unamsukumia dada yako maisha ya wizi yanaendelea

SHERIA ZETU MBOVU
Mic wapo toka 1993 Miaka 30 iliopita Kabla ya Rostam kununua Tigo alikua na Hisa voda huko nako alikaa miaka kibao kabla ya kumaliza kuuza hisa zake 2021.
 
MIC TANZANIA imefanya kazi kwa hasara kwa miaka mitatu mfululizo hivyo imeamua kuuza shares zake zote kwa kampuni ya HONORA ili nayo ijaribu na kama nayo itapata hasara ndani ya miaka mitatu itauza shares zake!

Hivi ndivyo Tanganyika inavyoliwa na wajanja kupitia sheria zetu mbovu za uwekezaji[emoji24]
sheria za kima trako za kuumiza Wananchi na kuwapendelea mabwenyenye,..
 
Sasa mweleze rais wa mawe kuwa tushushe kodi na kuboresha ulinzi wa mifumo ya fedha kama atqacha kkukunanga.

Au nasema uongo ndugu yangu ChoiceVariable ?
Sisi hatuwezi fanya hivyo, maybe Zanzibar wanaweza. Nchi zisizo na kodi ama zenye kodi ndogo kama Dubai, Panama, Monaco zina population ndogo, ni Rahisi kupata mapato kupitia njia nyengine kwa kuvutia Uwekezaji, na sababu wana raia wachache mapato madogo tu yanaweza kui transform nchi kuwa na maisha mazuri.

Ukiwa na population ya watu milioni 60 inabidi kila sehemu utafute ili kuhudumia watu wote. Sidhani kama Kuna Nchi kubwa yenye kodi ndogo.
 
Back
Top Bottom