Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huna uwezo wa kupima brain ya Kabudi, uwezo ulionao ni kutoa maoni kwa mihemuko kupoza mkwamo ulio nao.Palamagamba hana uwezo wa kuona hayo, yule jamaa brain yake ilishakua contaminated, ni mtu wa kujipendekeza zaidi kuliko kawaida.
Kitaka kumjua mtu mpe Mali au madaraka! Hata huyo mtu wenu najuta siku za nyuma nilikuwa"Mjinga" Kwa kuamini zile hotuba alizokuwa akitaja kilometres kumbe zilikuwa fix!Kwa elimu yetu ilivyo Tanzania na jinsi nnavyomuona anapoongea kwa mikogo, hilo silishangai. He is more of an actor rather than academic.
Hawa wawekezaji wanadai nini?Palamagamba alibadili Mikataba? Au alibadili Sheria?
-Kaveli-
Sikiliza ndg yangu hapa lilikua ni swala la busara kutumika. Nikweli huwezi kuendelea kwa kulegeza mambo lkn tayari mamlaka ilisha ingia mikataba Hivyo hata sheria zetu tulipaswa tuzibadili taratibu Sana na kushirikisha sehemu kubwa Sana ya wahusika yaani wawekezajiKama kawaida yetu tuanze na zomea zomea ambayo haisaidii maisha yetu na ugumu wake. Muhimu tusikilize na kufahamishwa udhaifu uko wapi! Kinachofahamika ni upigaji wa awamu zilizopita bila kujali nini kinapatikana kwa wa-TZ wengine.
Kulikuwa na upuuzi kwa nchi za afrika ambao unarudiwa kwenye barua ya huyo mtu wa kampuni. Eti, foreign investment. Nchi gani imeendelea kutokana na kulegeza ili foreign investment ziingie? Foreign investment hufuata palipo pazuri basi! Sasa kama wao wanaona mazingira ni mabaya. waombe chao waondoke. Lakini nikionacho wanahangaika ili wabaki nchini kwa nguvu ya kisheria ya investments. Wabaki halafu tuwaone wataishije na usalama wao.
Hawa wawekezaji wanadai nini?
Tunawajua Zitto na Tundu wanawahujumu Watanzania ili tutoke kwenye Malengo ya kitaifa
Hawa wawekezaji wanadai nini?
Mtindo wetu wa maamuzi na utunzi wa sheria ulikuwa umeharibika. Tunamzoza rais bila kumbukumbu ya mambo ya nchi hii. Huwezi kurekebisha sheria kwa msaada wa wawekezaji, ukawaita wadau. Wao lengo lao ni moja wanapokuwa Afrika, kupora! Isingewezekana kuwa na sheria nzuri kwa mijadala ya bungeni na hata baadhi ya watendaji wa serikali.Sikiliza ndg yangu hapa lilikua ni swala LA busara kutumika. Nikweli huwezi kuendelea kwa kulegeza mambo lkn tayari mamlaka ilisha ingia mikataba Hivyo hata sheria zetu tulipaswa tuzibadili taratibu Sana na kushirikisha sehemu kubwa Sana ya wahusika yaani wawekezaji.
yaani ni sawa unakuta gari lipi ktk speed ya kasi ya gia ya namba tano halafu ghafla unaweza rivas bila ya kupunguza mwendo na kuzima breki Hivyo lazima gari lipinduke tu. Ndicho hicho kinachotokea Tanzania
Hawa hawana raha na Afrika hata siku moja! Magufuli akiwatia adabu wezi, ni sisi hawa tunaolalama kusema eti dikteta. Huyo Lissu wa uhamishoni wa kwanza kujua kila kitu cha nchi hii na kuona makampuni yatakavyoshitaki.Uko sahihi ni hatua gani tumewachukulia hao wapigaji wa hapa kwetu? Au ni yale yale ya kulindana huku tukishindwa kuwajibishana? Ilitakiwa wakati tunasumbua hiyo mikataba, watu wetu waliokuwa wameingia hiyo mikataba wawe ndani, ili hata hayo makampuni yaliyovunjiwa mikataba yao wajue kweli tuko serious. Sasa muwekezaji kaingia mkataba hata kama ni wa kinyonyaji aone basi hata viongozi aliongia nao mikataba wako jela, na sio kuwaona wakitanua kwa pesa walizowahonga, na nyingine zikiwa katika mabenki ya ughaibuni. Hamna mzungu mjinga wa hivyo.
Wakati wanakagua vyeti feki, kuna neno lilitumika kwa wale wenye vyeti hivyo. Walisema ni watu wenye vyeti bila elimu.Haya ndio matatizo ya kutokutumia akili na elimu ndogo. Nchi zote Duniani zinalilia uwekezaji wewe unasema hakuna nchi inaendelea sababu ya uwekezaji, una akili kweli? China imeendelea kwa kuuza korosho? Au unadhani Tanzania tunaweza kuendelea kwa kuuza utumbo wa kuku?
Hawa hawana raha na Afrika hata siku moja! Magufuli akiwatia adabu wezi, ni sisi hawa tunaolalama kusema eti dikteta. Huyo Lissu wa uhamishoni wa kwanza kujua kila kitu cha nchi hii na kuona amakampuni yatakavyoshitaki.
Toa mfano mmoja tu wa dictatorship unayoionaTunaposema ni dictator hatukosei, usitake kuleta utetezi mwepesi kwa kuchomeka mifano tofauti. Tunajua wapi ni hatua stahiki na wapi ni uonevu. Mvua ni nzuri lakini ikizidi inaleta mafuriko, uharibifu wa mazao na miundombinu, itakuwa wendawazimu watu wakijadili madhara ya mvua iliyozidi, halafu ww useme nyie si ndio mnalalamikia ukame!