Kampuni ya uchimbaji madini ya Uingereza, Resources Indiana kuishitaki Serikali ya Tanzania kwa ukiukwaji wa mikataba

Kampuni ya uchimbaji madini ya Uingereza, Resources Indiana kuishitaki Serikali ya Tanzania kwa ukiukwaji wa mikataba

Kama unahitaji Urais umepata,tuone huko kulala majalalani vip,jalalani ulimuona vipi kama hamkuwa wote mnaokotaokota?
Watahangaika sana walitaka waendelee kutunyonya na madini yetu sasa wanaona wanakuwa masikini wanatafta lingine,ila yote yatapita salama mbele ya jembe letu MAGUFULI
 
Mimi nadhani kama nchi tumekwishaingia kichakani, lililopo ni kutafuta njia ya kutoka huko.

Tusipoweka tahadhari na kuelewa haya yanayoendelea, tutajikuta ndio tunaingia kwenye msitu wenyewe na sio kichaka tena.
Maana yangu hapa ni hii; hizi kesi zinazoibuka sasa hivi ndizo zinazoweza kuvuruga hata uongozi tutakaotaka tuwe nao baada ya uchaguzi mkuu ujao kwa pande zote mbili, kwa ubaya au kwa uzuri.

Ni rahisi sana kwa Magufuli kuzitumia kesi hizi na kuwahadaa wananchi aendelee kubaki madarakani, kwa huruma za wananchi, au kwa ujinga wao wa kutoelewa mambo yalivyo.

Sijui kama upinzani wanao uwezo wa kuzitumia kesi hizi kuonyesha ubovu alioufanya Magufuli, na wananchi hao wakawa na upeo wa kuelewa wanayoelezwa na kumwadhibu aliyevuruga mambo.

Swali ni je, wapinzani wakichukua uongozi wa nchi, watazifuta hizo sheria zinazolalamikiwa na hao wawekezaji? Watakuwa na ujasiri wa kuwaeleza wananchi juu ya hilo?

Pendekezo ambalo naweza kulitoa kuhusu kesi hizi - ili tusiendelee kuzongwazongwa na hawa wawekezaji, tukubali kwenda kwenye usuluhishi, na huko ndiko tutafute njia za kuwabana hawa.

Mengi ya makampuni haya hayajagundua chochote. Hayachimbi madini sehemu yoyote hapa nchini. Mikataba hii ina masharti yake na ukomo wake. Tuyaangalie masharti hayo na tujikite huko katika kuwabana wasituletee rabsha na kutupa sifa mbaya kama taifa zima.
Hapo ndio unabugi,Serikali itabakia palepale hakuna cha huruma wala furaha,Jembe litapeta tu hata walete kesi gani,walitaka waendelee kutunyonya na kubeba madini burebure,wao wafungue tu kesi
 
Watahangaika sana walitaka waendelee kutunyonya na madini yetu sasa wanaona wanakuwa masikini wanatafta lingine,ila yote yatapita salama mbele ya jembe letu MAGUFULI
Sasa kama huwezi kuchimba mwenyewe hayo madini,utabaki nayo hadi mwaka gani ili unufaike nayo?
Afrika ni shamba la bibi tuu ,tukipenda tusipende,akili zetu ni finyu mno kwenye mambo haya makubwa ya kiuchumi wa kidunia.
Wazungu wamesha tu over lap, Hata ukifanikiwa kuchiomba mwenyewe ,utamuuzia nani? wakati mnunuzi mkuu ndo huyo huyo beberu,utabaki na dhahabu zako stoor na mwisho utafilisika,
Kubali uliwe na wewe ule angalau siku zisogee.
 
Kuna mambo tunajitakia wenyewe. Hata kama mikataba yetu huko nyuma ilikuwa ya hovyo, bado ni serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndio iliingia makubaliano na hawa watu. Ni ujinga wetu tu. Sasa tumepevuka hivyo tusizidi kufanya ujinga mwingine, ambao ni pamoja pia na kuvunja pasipo tahadhari mikataba iliyoongozwa na sheria zetu za kijinga.
 
Hapo ndio unabugi,Serikali itabakia palepale hakuna cha huruma wala furaha,Jembe litapeta tu hata walete kesi gani,walitaka waendelee kutunyonya na kubeba madini burebure,wao wafungue tu kesi
Of course, "kupeta kwa jembe" unakokusema kunafahamika kwa kuwatumia polisi na tume ya uchaguzi. Ni nani anahoji hilo kwa sasa?
Usijifanye kama umevumbua jambo lisilofahamika hapa.

Lakini usome vizuri tena huo mstari ulioandika wewe: "Jembe litapeta tu hata walete kesi gani walitaka waendelee kutunyonya na kubeba madini burebure wao wafungue tu kesi." Unaelewa kweli maana ya hiki ulichoandika hapa?

Mradi umejisikia tu 'kujivimbisha' unadhani dunia nayo itaogopa huko kujivimbisha kwako?
 
Nakumbuka Tundu Lissu alishauri njia sahihi za kuvunja mikataba zifuatwe; aliongelea sana hii kitu na akatahadharisha utaratibu sahihi usipozingatiwa nchi itashtakiwa. Naona yale yote aliyoongea yanaanza kutimia moja baada ya jingine. Kuna watu huko mbele ya safari watatakiwa kunyongwa ili iwe fundisho kwa wengine maana hasara waliyoliingiza taifa haina mfano. Yetu macho!
Tundu Lisu alionya wakaishia kumnunulia bunduki na lisasi zaidi viungo vyake, wakamiminia lisasi lakini mungu alimkingia kifua akasema uatishi ungalie majibu ya maneno yake lisu.
 
Hao wanaotaka kuitangaza Nchi yao vibaya wakiwa wakimbizi katika nchi za watu na ombaomba wataisoma namba,watafukuzwa hata uongozi wengine wamepewa huku ni wakimbizi
Hahaha yani wawakilishi wa makampuni ya nje, kule kwao ni omba omba, au wakimbizi au sijakuelewa?
 
Hakimu Mfawidhi,
JAMANI HIZI CASES NINYI MNAZIPATA WAPI? MIE NIMEZITAFUTA ATA KWENYE GOOGLE LAKINI NAZIKOSA NAKUJA KUZIPATA BAADA YA YALE MADUBWASHA YAMESHAKAMATWA KULE CANADA
Mkuu zinapatikana mitandaoni. Kwenye websites za hayo makampuni au kwenye mahakama. Mahakama za huko hua zina websites na huweka kumbukumbu ya kila shitaka linalopelekwa huko kimtandao hivyo rahisi kupatikana na kusomwa.
 
Tutapambana nawo wezi na waporaji wakubwa, hawana maana hata kidogo...
Kama mbwai iwe mbwai...
 
Kampuni ziko nyingi tu zinafuata. Kuna mahala tulikosea, kubadili sheria na kufuta mikataba tuliyoingia huko nyuma bila kufuata utaratibu. Mikataba tuliingia wenyewe tena kwa kushangilia, wazee wa ndiyooo kila siku, sasa tumehsingia mkenge ndio tunashtuka kuivunja bila kufuata utaratibu.

Baadae tunaweza kuja kujikuta tuna mashitaka mengi sana kwenye mabaraza ya usuluhishi.
Sawa tu kwani Kesi Kitu Gani bwana. Tutapambana tu. Ni bora kesi kuliko madini yaliyokuwa yakiibiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio matokeo ya watu kutenda bila ya kufikiria. Tundu Lissu alisema haya lakini watu toka mtaa wa Lumumba wakamkejeli vilivyo. Ndio maana Mchungaji Peter Msigwa aliwaambia kuwa ccm wanachukua muda mrefu sana kuelewa vitu wanavyoambiwa kwa muda huo.
Asipobadilisha hizo sheria na akakaidi hukumu za arbitrators tusubiri vikwazo vya uchumi.
Mhhh, vikwazo kwa ajili ya nini. Kuinuka kiuchumi ni mapambano

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom