Tetesi: Kampuni ya Yapi Merkezi kuchunguzwa kwa rushwa na kuingilia mambo ya ndani Tanzania

Tetesi: Kampuni ya Yapi Merkezi kuchunguzwa kwa rushwa na kuingilia mambo ya ndani Tanzania

Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Tanzania vyadaiwa vimeanza uchunguzi dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Kampuni ya Ujenzi ya Yapı Merkezi Bwana Erdem Arioglu.Vyanzo mbalimbali vinaeleza kuwa Arioglu anatuhumiwa kuwa sababu kubwa ya kuchelewa kukamilika kwa mradi wa SGR huku akiwatendea visivyo makandarasi wa Kitanzania kwa kuwacheleweshea malipo yao.

Raia huyo wa Uturuki pia anatuhumiwa kuingilia siasa za ndani za Tanzania kwa kutoa rushwa kwa Wabunge mbalimbali kukwamisha miradi mbalimbali ya maendeleo kupitia michango yao Bungeni.Bunge la Tanzania linatarajiwa kutoa taarifa baada ya uchunguzi huku baadhi ya Wabunge wakitaka raia huyo wa Uturuki kuondolewa nchini mara moja.

Mbali na tuhuma hizo kampuni hiyo pia inatajwa kuendelea kuipa Tanzania hasara ya mabilioni kutokana na ujenzi wa chini ya viwango katika baadhi ya maeneo.Eneo mojawapo ni kipande cha daraja la Nkurumah eneo la Kamata jijini Dar es Salaam ambapo kampuni hiyo iliamuriwa kuvunja na kuanza ujenzi upya baada ya kuonekana liko chini ya kiwango ikiwemo muonekana wa wazi wa nyufa kama inavyoonekana pichani!.

Katika baadhi ya maeneo ya mradi huo usanifu umekiuka angalizo kwenye njia za maji na kuzifunga jambo ambalo linahatarisha usalama wa matumizi ya mradi huo pale utakapokamilika.Athari za jambo hili zinaelezwa kuwa zitailetea nchi maafa makubwa zaidi kama ajali na hasara za ukarabati wa mabilioni pale ambapo mradi huo utakamilika.

Katika tuhumu hizo imeelezwa kwamba serikali imeunda timu ya uchunguzi huku timu nyingine ya siri ikihakiki shughuli na rushwa katika mradi huo kabla ya kutoa ripoti rasmi.

View attachment 2313893
Mwacheni JPM apumzike jamani, mkichunguza, mnamuumbua
 
Shame kabisa, kwenye huo Mradi Jiwe alijaza Maaskari wengi, walishindwa Kujua hizo hujuma na kuzizuia wakiwa on ground?
 
Ukute wanataka aondoke Yapi Merkezi,wamtafute ambaye atawapa wao ten percent.
Na atakayepewa ni yule mchina wa rais wa mawe! Firina zote hizi anazileta yeye ili mchina aweke mzigo mezani wa kumsaidia kwenye kampeni za kugombania kijiti ma maadam! Mama hajamshtukia huyo mvaa bendera Hadi Sasa.
 
..mturuki amechelewesha sana huu mradi.

..haiwezekani dar to moro ichukue miaka 5 na bado mradi haujakabidhiwa.

..mchina alijenga reli ya tazara, dsm to kapirimposhi, na akakabidhi mradi ndani ya miaka 5.

cc Proved
Jee munampa fedha za kufanyia kazi kwa wakati?

Halafu unalinganisha mchina wa enzi ya Mao Zedong na leo hii wapi kwa wapi? Miaka 50+ nyuma!
 
Acha hizo, ingekuwa enzi za mwendazake ningekutaka uvae jezi ya Chadema kisha upite barabara ya stesheni, huko ungejua kuwa CCM na vyombo vya usalama ni mapacha.
Hahahaa au wakuone mko watu kama kumi tu mna jambo lenu. Ilifika mahali hata vikundi vya Saccos vikawa vinazuiwa wakidhani wanajadili mambo ya Chadema.
 
Shame kabisa, kwenye huo Mradi Jiwe alijaza Maaskari wengi, walishindwa Kujua hizo hujuma na kuzizuia wakiwa on ground ?
Tunaambiwa vyomba vya usalama( vipenyo) viko kila mahali sasa mbona kila kona tunapigwa vyenyewe huwa vina kazi gani?
 
Huyu Bimkubwa kuna mambo mazito kama SGR na Nyerere Dam hayatilii maanani yeye kakazana na COVID 19 tu na mikopo sijui anachukua ya kazi gani.

Hivi wachina si wapo? Si muwape hiyo miradi ya kimkakati? au kuna maelekezo ya Msoga?
 
..mturuki amechelewesha sana huu mradi.

..haiwezekani dar to moro ichukue miaka 5 na bado mradi haujakabidhiwa.

..mchina alijenga reli ya tazara, dsm to kapirimposhi, na akakabidhi mradi ndani ya miaka 5.

cc Proved
Akina Majaliwa Kassimu walikuwa wanashinda mitandaoni kutwambia tangu 2019 mradi umefika asilimia 75%😀😀
 
Jee munampa fedha za kufanyia kazi kwa wakati?

Halafu unalinganisha mchina wa enzi ya Mao Zedong na leo hii wapi kwa wapi? Miaka 50+ nyuma!

Kipande cha Dar to Moro serikali ilisema tunatumia fedha za ndani, na tulihakikishiwa kwamba fedha hizo zipo.

Binafsi nilitegemea miaka hii ujenzi utakamilika kwa haraka kuzidi wakati wa Tazara kwasababu ya maendeleo ya kiteknolojia na uwepo wa vifaa na mitambo ya ujenzi bora zaidi.

Nimelinganisha Dar to Moro vs Dar to Kapirimposhi. Sioni mantiki ya mkandarasi wa Sgr kuchelewa kukamilisha kipande kidogo hicho kwa wakati.
 
Nilikuwa namjibu huyo aliyesema mchina ana Bei nafuu, ikiwa hajui mchina ndio ana Bei kubwa

Kuna sababu za kuchelewa, huu mradi unategemea donors. Sio kwamba pesa ipo tu bank. Hata bwawa linachelewa Kuna sababu zipo.

Aalafu huyo mchina nimekuambia kapewa kipande cha Isaka Mwanza. Kaangalie kinachoendelea.

Na hata hivyo kishapewa tena kipande kingine cha Tabora kigoma. Hivyo Kama unawapenda wachina Subiri watajenga tu wana vipande vingi na vikubwa tu

..kipande nilichohoji ucheleweshaji wake ni Dar to Morogoro.

..maelezo ya serikali yalikuwa kipande hicho kinajengwa kwa kutumia fedha za ndani, sio mkopo, donors / wafadhili.

..sijahoji kuhusu Moro Dom Makutupora. Lakini pia ninavyokumbuka fedha za kipande hicho ni mkopo toka kwa mabenki ya ulaya / mabeberu.

..mimi nilikuwa mmoja wa wanaJF waliotetea Yapi Merkez waliposhinda tender. Niliangalia rekodi yao ya ujenzi Dubai, Qatar, etc nikaamini wako vizuri. Sijui ni kwanini wamechelewesha mradi huu kwa kiwango hiki.

..hata Wachina wakichelewesha kazi tutahoji kulikoni. Tunatakiwa tu-demand kazi zenye kiwango zinazokamilika kwa wakati.
 
..kipande nilichohoji ucheleweshaji wake ni Dar to Morogoro.

..maelezo ya serikali yalikuwa kipande hicho kinajengwa kwa kutumia fedha za ndani, sio mkopo, donors / wafadhili.

..sijahoji kuhusu Moro Dom Makutupora. Lakini pia ninavyokumbuka fedha za kipande hicho ni mkopo toka kwa mabenki ya ulaya / mabeberu.

..mimi nilikuwa mmoja wa wanaJF waliotetea Yapi Merkez waliposhinda tender. Niliangalia rekodi yao ya ujenzi Dubai, Qatar, etc nikaamini wako vizuri. Sijui ni kwanini wamechelewesha mradi huu kwa kiwango hiki.

..hata Wachina wakichelewesha kazi tutahoji kulikoni. Tunatakiwa tu-demand kazi zenye kiwango zinazokamilika kwa wakati.
Ujenzi wa dar Moro ni fedha za ndani na mkopo kutoka AFDB. Na huu mkopo wa AFDB mbona ulikuwa wazi tu. ni Kama ilivyokuwa Daraja la tanzanite ambalo limejengwa kwa mkopo na pesa za ndani. Yote haya yalikuwa reported kwa umma.

Sasa ikiwa pesa za mkopo zinachelewa na hata za ndani haziendi kwa wakati unataka ujenzi ufikie wapi?
 
Wewee wa ajabu! Hii kampuni si ililetwa na JPM? Kwa hiyo ndiye aliyehongwa?
Wakati wa JPM, kazi ilipigwa kwelikweli na hii hii kampuni.

Kwa ufupi Hawa wakandarasi ni wakandarasi wa kimataifa, sio wakuokota , wanefanya ujenzi nchi mbalimbali.

Kwa Sasa wameamua kua hivo ili kuendana na Serikali ya Sasa ya Samia ilojaa upigaji na kutowajibika .

Lini Samia amewah fanya angalau ziara yenye lengo la kufatilia utendaji kazi ??.( Ukinielewa hapo, Utajijua wee ni Mpumbavu namba Moja).
 
Wewee wa ajabu! Hii kampuni si ililetwa na JPM? Kwa hiyo ndiye aliyehongwa?
Hakuna kampuni inaletwa na raisi, utaratibu unaotumika ni single source. Ndio maana unaona hata kipande cha Tabora kwenda kigoma kapewa mchina.

Leo Tanesco wamesaini mkataba na kampuni ya uarabuni Masdar kuzalisha umeme mg 2000. Unataka kusema mama Samia ndio kawaleta hao Masdar?

Acheni kukariri
 
Back
Top Bottom