Kanda ya Ziwa tusikilizwe kuhusu uwanja wa ndege. Haivumiliki tena

Kanda ya Ziwa tusikilizwe kuhusu uwanja wa ndege. Haivumiliki tena

Hivi kwa uelewa wako unadhani ni kanda ipi nyingine ina uwanja wa kimataifa ambao jengo lake ni zuri labda mithili ya JKNIA?

Tafadhali kama hujawahi kufika Songwe usiutaje maana jengo lake ni kama jengo la sekondari, wala usitaje KIA sababu hata haifikii ule uwanja Terminal 2...
lakini afadhali hao kuliko banda la kuku la Mwanza airport
 
Mama akitupatia daraja la kigongo na uwanja wa kimataifa, mwanza kazi atakuwa amemaliza aje kula samaki tu, wasukuma wanasema "mayu wa mbasa"
 
Hivi kwa uelewa wako unadhani ni kanda ipi nyingine ina uwanja wa kimataifa ambao jengo lake ni zuri labda mithili ya JKNIA?

Tafadhali kama hujawahi kufika Songwe usiutaje maana jengo lake ni kama jengo la sekondari, wala usitaje KIA sababu hata haifikii ule uwanja Terminal 2...
Kwa kutumia akili ya kawaida tu, ili kuilaumu serikali kwa haki, tujiulize;
Ni ndege ngapi za safari za kimataifa zinatua na kuruka kwenye viwanja vya Mwanza na Songwe?
Idadi ya ndege kwa ujumla kwa siku?
Baba wa taifa, pamoja na kuwa Rais kwa miaka zaidi ya ishirini, hakujenga barabara ya lami Butiama kwa sababu ya idadi ya magari ya kuwa ndogo.
Tunahitaji kuwa na fikra za kitaifa zaidi (statesmen) badala ya ubinafsi wa kikinga.
Hawa watu wenye fikra kama hizo wahitaji elimu ya ubinadamu kwanza.
 
Maadam baadhi yetu tuliutetea uwanja wa Chato, Naunga mkono Uwanja wa Ndege wa Chato. Una justification, utakuwa kama Ggabolite au Yamoussoukro. Watalii watamiminika! by that time, hakuna aliyejua kuwa rais anaweza kufa madarakani!. Hata kama Magufuli hayupo, tunaweza kuindeleza ile mipango yake na uwanja ukawa busy!.
P
Na haya ndiyo mawazo tunayotaka, kwamba ule uwanja ingawa ulijengwa na Marehemu Magufuli, siyo mali ya marehemu. Uwanja ni mali ya umma na uendelezwe, ufunguliwe utumike kama ulivyokusudiwa.
Tatizo ni kuhusisha maendeleo na siasa, hapo ndio tunakwama, anapokuja kiongozi mwingine anaanza kusema au kudhani mtangulizi wake alikuwa na mawazo au nia tofauti ya vitu alivyoviweka. Vision ya Taifa inakosekana, Uwanja wa ndege unajulikana na matumizi yake yanajulikana , sasa tunakwama wapi?
 
Na haya ndiyo mawazo tunayotaka, kwamba ule uwanja ingawa ulijengwa na Marehemu Magufuli, siyo mali ya marehemu. Uwanja ni mali ya umma na uendelezwe, ufunguliwe utumike kama ulivyokusudiwa.
Tatizo ni kuhusisha maendeleo na siasa, hapo ndio tunakwama, anapokuja kiongozi mwingine anaanza kusema au kudhani mtangulizi wake alikuwa na mawazo au nia tofauti ya vitu alivyoviweka. Vision ya Taifa inakosekana, Uwanja wa ndege unajulikana na matumizi yake yanajulikana , sasa tunakwama wapi?
Naunga mkono hoja, ilitakiwa kila Tarehe 12- 17 March iwe ni wiki ya JPM, kufanyike Tamasha kubwa Chato, mikutano, Marsha, semina, makongamano, hata maandamano yafanyike Chato kwa wiki nzima, Tuanzishe Tamasha la Utalii wa Makaburi, ndege zitafurika, Chato itajaa, Itachangamka na Magufuli mwenyewe huko aliko atafurahi!. Ile GS Hotel itakuwa Fully Booked mwezi mzima.

Tamasha hilo litafuatiwa na , Wiki ya Maadhimisho ya Miaka Mitatu ya awamu ya 6 Madarakani.

Hili Mnalionaje?.

P
 
Leo nimemsikiliza Musukuma akizungumzia kuchelewesha kuhusu jengo la uwanja wa ndege wa Mwanza na miundo mbinu yake kuufanya uwe wa kimataifa.

Hali hii kwa sasa inatoa picha kama alivyosema Msukuma dharau kwa kanda ya ziwa haijalishi Makonda ni Mwenezi au Dotto ni Naibu Waziri Mkuu,kisiasa haitatosha kuwashawishi wananchi ambao ni wazi wanaonekana kutengwa kupitia uwanja huu, Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma lakini kwenye mpango wa sasa uwanja huu haumo.

Ni nani anayeupiga vita. Rais kwa hili tunaomba uingilie kati kwa jinsi utakavyoona inafaa. Aidha barabara njia nne za kuingia jijini zimetupiliwa mbali hakuna anayezungumzia kwenye Mpango. Nadhani miji kama Mwanza Mbeya ni wakati wa kujenga njia nne kama ilivyo kwa Dar.

Kura ziko nyingi sana kwenye maeneo haya siyo ya kufanyia mzaha. Makonda pata maelezo ya miradi hii uondoe lawama.
Kwani chattle international airport umekuwaje?
 
Naunga mkono hoja, ilitakiwa kila Tarehe 12- 17 March iwe ni wiki ya JPM, kufanyike Tamasha kubwa Chato, mikutano, Marsha, semina, makongamano, hata maandamano yafanyike Chato kwa wiki nzima, Tuanzishe Tamasha la Utalii wa Makaburi, ndege zitafurika, Chato itajaa, Itachangamka na Magufuli mwenyewe huko aliko atafurahi!. Ile GS Hotel itakuwa Fully Booked mwezi mzima.

Tamasha hilo litafuatiwa na , Wiki ya Maadhimisho ya Miaka Mitatu ya awamu ya 6 Madarakani.

Hili Mnalionaje?.

P
Naunga mkono hoja ijumaa nitakuwa tayari chattle.
 
Kwa kutumia akili ya kawaida tu, ili kuilaumu serikali kwa haki, tujiulize;
Ni ndege ngapi za safari za kimataifa zinatua na kuruka kwenye viwanja vya Mwanza na Songwe?
Idadi ya ndege kwa ujumla kwa siku?
Baba wa taifa, pamoja na kuwa Rais kwa miaka zaidi ya ishirini, hakujenga barabara ya lami Butiama kwa sababu ya idadi ya magari ya kuwa ndogo.
Tunahitaji kuwa na fikra za kitaifa zaidi (statesmen) badala ya ubinafsi wa kikinga.
Hawa watu wenye fikra kama hizo wahitaji elimu ya ubinadamu kwanza.
kipi kinaanza kujenga uwanja kwanza au ndege za kimataifa kutua tuzione ndipo tujenge uwanja,uwanja ndiyo unaoleta ndege. uwanja wa Mwanza ni strategic mno kwa maziwa makuu na Afrika ya Kati na magharibi mama hili usiliache jenga jengo la kisasa pale,ingawa vita ni kubwa kuanzia TAA na Wizara yenyewe.
 
Na haya ndiyo mawazo tunayotaka, kwamba ule uwanja ingawa ulijengwa na Marehemu Magufuli, siyo mali ya marehemu. Uwanja ni mali ya umma na uendelezwe, ufunguliwe utumike kama ulivyokusudiwa.
Tatizo ni kuhusisha maendeleo na siasa, hapo ndio tunakwama, anapokuja kiongozi mwingine anaanza kusema au kudhani mtangulizi wake alikuwa na mawazo au nia tofauti ya vitu alivyoviweka. Vision ya Taifa inakosekana, Uwanja wa ndege unajulikana na matumizi yake yanajulikana , sasa tunakwama wapi?
Chato Airport ibakie hivyo hivyo ili kizazi kijacho kitambue kuwa Tanzania iliwahi kutawaliwa na kiongozi mwongo na mbinafsi. Sisi Chato ndiyo kama Gbadolite ya Mobutu see seko.
 
Chato Airport ibakie hivyo hivyo ili kizazi kijacho kitambue kuwa Tanzania iliwahi kutawaliwa na kiongozi mwongo na mbinafsi. Sisi Chato ndiyo kama Gbadolite ya Mobutu see seko.
Tukiiacha inakuwa siyo sawa, Chato ni Tanzania, Na tunahitaji kuuendeleza ili vizazi vijavyo visituone wapuuzi/Wajinga, kwamba uwanja upo badala ya kuuendeleza na tuutumie tukauacha kwa sababu za kisiasa, ambazo hazina tija yoyote.

Pesa za wananchi zilitumika hivyo tunahitaji tija kwenye matumizi hayo.

Tutenganishe siasa zetu na maendeleo ya nchi yetu. Viongozi wafanye maswala ya policies na usimamizi bora wa rasilimali zetu, uongo wao wabaki nao wenyewe.
 
Naunga mkono hoja, ilitakiwa kila Tarehe 12- 17 March iwe ni wiki ya JPM, kufanyike Tamasha kubwa Chato, mikutano, Marsha, semina, makongamano, hata maandamano yafanyike Chato kwa wiki nzima, Tuanzishe Tamasha la Utalii wa Makaburi, ndege zitafurika, Chato itajaa, Itachangamka na Magufuli mwenyewe huko aliko atafurahi!. Ile GS Hotel itakuwa Fully Booked mwezi mzima.

Tamasha hilo litafuatiwa na , Wiki ya Maadhimisho ya Miaka Mitatu ya awamu ya 6 Madarakani.

Hili Mnalionaje?.

P
HAPANA, Matamasha ni uharibifu wa pesa za umma. Nchi yetu inahitaji kila senti iliyoko mfukoni au draw zetu popote zilipo, yani tunamatatizo mengi sana na mengi kama siyo yote yanahitaji pesa. Hii michezo ya Mgeni rasmi, sijui kongamano, mikutano isiyo isha na isiyo na tija huikuti nchi zilizoendelea.

Hapa kwetu tumezidi, kuwasha mwenge ni shughuli ya mabilioni na itifaki za kijinga, kuuzima vile vile. Umeona juzi Arusha shughuli ya kuuwasha Mwenge, kauwasha MAJALIWA, hahaha we acha tu. Semina, makongano, na warsha ndio usiseme pesa zinaliwa kinachojadiliwa hakipo.

Nchi za wenzetu maeneo ya utalii yanajiendesha, pesa zinakusanywa zinahudumia eneo husika, zikizidi maboresho yanafanyika kuongeza haiba ya eneo husika. Nchi yetu pesa za utalii tunazisikia kwenye hotuba tu, hatufahamu zinakwenda wapi.

Tukiyaendeleza maeneo ya kumbukumbu na kuyaweka vizuri watalii watakuja kuyaangalia, na pesa zitaingia na tutafanya maboresho, sioni haja ya maandamano na warsha.

Na nchi za wenzetu hata huo utalii hautangazwi kiivyo, maeneo yanajulikana yako kwenye mitandao, na hayabadiriki.

Mfano nimewahi kuishi marekani, lakini sijawahi kuona popote LAS VEGAS inatangazwa, Lakini ukifika LAS VEGAS hutoamini, ndege zinavyopishana kuleta watalii wa nje na wa ndani, Mahoteli na kasino zimejaa, mitaani ndio usiseme, na Washington DC vile vile, na miji mingine.

Tofauti na kule hapa kwetu pesa nyingi huishia mifukoni na matumboni mwa wasimamizi. Utaona mara sare za vitenge kila siku, kila mkutano na sare yake na hiyo ni budget ya wizara.

Tuache haya mambo tuwe wazalendo wa kweli, pesa zitumike kwenye vitu halisi vyenye kuleta tija na thamani ya pesa ionekane, tuache ujanja ujanja, hatutaendelea kamwe.

Tuyatambulishe maeneo ya utalii, tuyaweke kwenye mazingira mazuri, kisha tuyahudumie ili yaendelee kutuingizia pesa, tulinde maliasili zetu, Huko Marekani Zoo kibao na ukiangalia wanyama 90% wametoka Tanzania, sasa jiulize mapato ya zoo Tanzania tunapa asilimia ngapi au kuna mfumo gani unatumika kulinda wanyama wetu walioko huko kwenye hizo zoo nje ya Tanzania.

Wanazaliana, je?tiunajua ni wangapi sasa na tunampango gani kuwarudisha au ndio tumetoa sadaka? Tuanachezea rasilimali ambazo walipaswa waje hapa kuziona tuanwapelekea huko nje, halafu mbuga zetu tuna kata vitalu tena tunawakabidhi wao ndio waendeshe sisis tunapewa asilimia kadhaa yani kodi, kwanini?

Uzalendo tunamuachia nani?

Kaka ni mengi ya kuzungumza lakini tuishie hapo, nimesema HAPANA kwa wazo lako.
 
"Songwe umejengwa, Arusha, Tanga,Dodoma,Tabora, Kigoma"

Ukiacha Msalato, viwanja vya:

  • Tanga
  • Tabora
  • Kigoma
  • Arusha

Sio vizuri na havina facilities nzuri kama uwanja wa Mwanza, and none of them are international.

Sasa sijui argument yako ni nini? Kiwanja pekee ambacho recently kimejengwa international ni Msalato.

Hivi unajua Tanzania kuna viwanja vi 3 tu internafional?

  • Dar es salaam
  • Kilimanjaro
  • Zanzibar

?????????????????

Halafu mlivyo wajinga mnasema kabisa, eti Makonda kupewa cheo na waziri Mkuu msaidizi ambao wanatoka kanda ya ziwa, haitoshi?

Kwani kanda ya ziwa wanapewa vyeo kwa sababu labda wanabembelezwa kitu gani? Wanaombwa nini hao watu wa kanda ya ziwa?

Si muende mkakichomoe cha chato mkllete Mwanza kama. Mna uitaji. Kwa nini mlikipeleka huko chato kikaanikie Mahindi na mbaazi?
kwani chato ni Mwanza hiyo ni Geita fahamu mipango ya serikali ilivyo.Dont shout.Msijifiche kwenye kichaka cha uwepo wa uwanja wa Chatto.Kiwanja cha Mwanza kinatumika na wote ukiwemo wewe mwenyewe mpinga maendeleo.
 
Uwanja wa kimataifa si ulishajengwa chato..
Pale kitobuni mwa utalii kanda ya ziwa?!
Muulize Ndumbaro
 
Kamati za Bunge zilizotembelea Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa nini hazipitii au kuzungumzia mradi wa ujenzi wa jengo la abiria La Airport Mwanza wakati kuna pesa za walipa kodi zimeingia hapo? kupitia halmashauri na serikali kuu kulikoni?
 
Mkataba umesainiwa leo ujenzi wa jengo uanze hofu yangu ni capacity ndogo ya kubeba watu. ingeongezwa kutoka 200 hadi 300.
 
Back
Top Bottom