Kanisa Katoliki mnazingua, michango imekuwa kero

Kanisa Katoliki mnazingua, michango imekuwa kero

Me catholics wanachonikwaza ni pale tunapochanga kwenye jumuia kujenga buildings for social welfares kama Dispensary, ukumbi or whatever alau ukishakamilika hawa wanajumuia wa chini kabisa huku, waliojinyima kujenga hivyo vitega uchumi, hawapati incentives yeyote kwenye matumizi ya vitu walivyojenga kwa gharama zao. Inaumiza sana maana hatuombi iwe for free lakini unaweza sema kwa mwaka kila mwana jumuia hai apewe angalau discount charges ya hata 15% kila mara anapoenda ku seek huduma ambayo alichangia kwenye uanzishaji wake.
Unachofeel ni kweli, umefeel kitakatifu sana

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
As i said before! Kanisa ni mali yetu waumini. Kwa hiyo ni sisi wenyewe ndiyo tutakao lijenga.

Kuhusu kutoa sadaka kwa kunyanyuka benchi moja baada ya jingine; kwa upande wangu sioni kama kuna shida! Tena Parokiani kwangu huwa wanasema kama huna hiyo sadaka, unaenda pia kule mbele na waumini wenzako kumshukuru Mungu ili wiki ijayo akupatie kipato cha kutoa kama wengine.
Lengo la kwenda mbele Kwa asiye na sadaka siyo Kumshukuru Mungu, kwani Mungu yupo kule mbele? Lengo la kupita mstari Kwa mstari ninkuakikikisha Kila mtu anatoa, na kusema Kila mtu apite mbele ni kumfanya mtu aone aibu kupita bila kutoa sadaka
 
Wakatoriki siku hz wanashindana na lutheran, Pentecost kwa wingi wa michsngo,
Makanisa ya Afrika, wachungaji wake huduma pekee wana kupa, ni "kukuombea kwa Mungu" Na maneno ya faraja tu,
Hawakujengi kisaikolojia ili upambsne zaidi, uwe tajiri,
 
Mnashindwa wapi kusoma saikolojia za watu.Yani kunapokuwa na matukio ya komunyo ya kwanza au kupaimara mnawakamua waumini michango hadi wanachukia dini.

Halafu siku ya tukio la komunyo bado tena wanakamuliwa wazazi kupitia harambee tena siyo tu kuwahusisha wanaume katoliki na wanawake katoliki bali wanaitwa watoto wanapangwa mbele na kuitwa kila mzazi aje kumgombowa mtoto, halitoshi mama aliyesuka vizuri anapelekewa kikapu.

Acheni kuwadhalilisha wazazi kama alibakiwa na buku 2 hatimaye anashindwa hata kukodi boda. Michango ya ujenzi ina utaratibu wake haya mengine ni unyanyasaji.
Kuna Uzi niliuanzisha hapa miaka kama Minne au Mitano iliyopita Kulalamikia hili hili na kusema kuwa ndiyo limechangia si tu Kusuasua Kwangu kwenda Kanisani au hata Kuhudhuria Jumuiya ( ambako nako huko muda mwingi Watu wanaacha Kusali wanaanza Kutetana na Kupigana Majungu ) na kuamua tu Kusali kipeke yangu peke yangu Nyumbani / Chumbani Kwangu.
 
Kuna Uzi niliuanzisha hapa miaka kama Minne au Mitano iliyopita Kulalamikia hili hili na kusema kuwa ndiyo limechangia si tu Kusuasua Kwangu kwenda Kanisani au hata Kuhudhuria Jumuiya ( ambako nako huko muda mwingi Watu wanaacha Kusali wanaanza Kutetana na Kupigana Majungu ) na kuamua tu Kusali kipeke yangu peke yangu Nyumbani / Chumbani Kwangu.
mkuu njoo jumuiyani usijitenge
 
mkuu njoo jumuiyani usijitenge
Nipo Msituni huku Porini naitengenezea Jina na Sifa Tanzania yako / yetu huko Jumuiyani Kwako nitaenda muda gani? Ninachoweza ni kila Jumapili kuhudhuria Maombi Mjini Kampala kwakuwa kila Ijumaa huwa nakuwa huko Kwangu kwa ajili ya Kupumzika ( Refreshing ) na Jumapili nageuka kuja katika Kituo changu Tukuka cha Majukumu ya kuiletea Heshima Tanzania ndani ya Uganda lakini pia Kuisaidia Uganda kwa Kazi ambayo nawafanyia ambayo nimepewa Heshima Kubwa ambayo itabakia kuwa Historia katika Maisha yangu yote.
 
Haya mambo usizungumze tu kama muumini wa Mwamposa au nabii wanaoota kama uyoga siku hizi.

Katoliki ni moja, kanisa la kimapokeo. Ukisema ni Parokia yake n.k unakuwa unamaanisha?
- Ina maana kwenye umri ulionao umekuwa kwenye Parokia moja tu?

Umeshasikia kuwa Chota baraka kwa kuchangia Radio Tumaini, Radio Maria etc?
  • Mipango ya ujenzi wa Kanisa Gezaulole, kuna haja ya kuwakamua waumini? Sadaka, zaka, miradi ya shule, kumbi na hospitali za Jimbo kama la DSM inafanya kazi gani?
  • Unajua Parokiani huko, watu wanakamuliwa kuanzia ngazi ya Familia, Jumuiya, Kanda hadi Parokia, kisha wanaanza tena kwenye vyama vya kitume, na ukiangalia michango ni ile ile ila majina tofauti?
  • Unazungumzia viongozi waliochaguliwa? Fikiria sasa hao viongozi ndo wawe mfano wa wewe, unadhani nini kitabadilika?

Unayafahamu maisha ya kifahari wanayoishi hawa watawa wetu walioapa kutoa maisha yao sadaka?

Katoliki inachochora kwenye mipesa!
Umesema vema
 
Huku kwetu Paroko alianza kutupagia kiwango kila jumuiya, tukamuitikia tu. Ikifika ktk utekelezaji tunapeleka tulichokipata kata kama 70,000. Basi anakasirika

Akaanza kufoka na kututishia kwa maandiko. Tukamwambia yeye hana majukumu, pia asitupangie ktk utoaji. Maisha ya waamini n magumu sana. Wapo wanakula milo miwili tu. Yeye hajawahi kugawa hata mche wa sabuni kwa kaya maskini.

Sisi tumeamua kutoa sadaka, zaka na mavuno basi. Tena kila mmoja kuamua si kumpangia ktk utoaji.

Katika kikao cha halmashauri Paroko alipewa ukweli tu, ajue pia hali ya kiimani ya waamini wake kama anavyojua kaya zisizotoa michango.

Wakatoliki ifike wakati tauche unafiki wa kufukia makosa. Tuache yasemwe turekebishe. Jamaa amesema baadhi wanamwandama kwa maneno makali. Sio namna nzuri ya kutatua ama kutetea taasisi.
 
Jombaa hivi ukipiga mahesabu ya matumizi yako ya mwaka mzima na sadaka ulizo mtolea Mungu Mzani wako Unaelemea wapi?

Sasa Kama mzani wako unaelemea kwenye matumizi basi kwa Mungu wewe ni Mwizi Na huna faida kwenye Ufalme wa Mungu Mjomba.

Hivi kama Unaakili timamu Mungu Anakupa Uzima, anakulinda, anakupa BARAKA za kupata hiyo fedha unayo bwabwaja unapata uchungu kumtolea?

Jitafakarini sana kama sadaka zako kwa mwaka hazifiki 1M Na Unakipato kizuri jitafakari Na Utubu kwa Mungu Mjomba.
 
Mnashindwa wapi kusoma saikolojia za watu.Yani kunapokuwa na matukio ya komunyo ya kwanza au kupaimara mnawakamua waumini michango hadi wanachukia dini.

Halafu siku ya tukio la komunyo bado tena wanakamuliwa wazazi kupitia harambee tena siyo tu kuwahusisha wanaume katoliki na wanawake katoliki bali wanaitwa watoto wanapangwa mbele na kuitwa kila mzazi aje kumgombowa mtoto, halitoshi mama aliyesuka vizuri anapelekewa kikapu.

Acheni kuwadhalilisha wazazi kama alibakiwa na buku 2 hatimaye anashindwa hata kukodi boda. Michango ya ujenzi ina utaratibu wake haya mengine ni unyanyasaji.
It's as simple as this. Unacho, toa "kadiri unavyoweza". Huna, huko kukosa ndiyo matoleo yako na Mungu anayapokea pia kwa sababu "anaona hadi moyoni mwako." Kwa hiyo, shida iko wapi, kwako au kwa kanisa?
 
Back
Top Bottom