Kanisa Kuu mbadala wa St. Joseph kujengwa Gezaulole, Jimbo Kuu - Dar es Salaam

Kanisa Kuu mbadala wa St. Joseph kujengwa Gezaulole, Jimbo Kuu - Dar es Salaam

Hili jengo linaweza kuwachukua miaka 20 mpaka kukamilika kwa viwango hivi, huku gharama yake ikiwa kati ya Bil 30 - 50.
Kwa wakatoliki bilioni 50 ndogo sana wakianza michango hasa ndani Jimbo kuu la DSM.
Itachukua muda miaka 4 - 5 tu.
 
Jimbo la Dar es Salaam Lina parokia zaidi ya 20,michango itapita hapa miaka 3 Hadi 4 litakuwa limekwisha.
Ni zaidi ya 20 ndugu. Dekania ya mbezi tu ina parokia 10,iweje dsm nzima ziwe 20.
 
Jina la Kanisa: Bikira Maria Mama wa Mungu Cathedral Umbo: Msalaba Ukubwa: 13,000sqm Idadi ya waumini 9,816 Minara mikubwa 4.

Milango 19 Altre ya walei na ya makrelo Kisima cha ubatizo Vituo vya njia ya msalaba Minara midogo 12 Sakastia 3 Maaskofu 1 Mapadre 2 Waministranti 3 Box maungamo 6 Sacrarium

Lift ya kwenda juu na basement Cathedral square ipo nje Ghorofani Waiting lounge watu 120-150 Ofisi 4 Store 4 Archive Makanisa madogo 2; Watu 200 Basement


Makaburi 12 ya chini Makaburi ya ukutani Vituo 14 njia ya msalaba Kanisa la kuabudia watu 220 Strong room Handaki.
View attachment 2752329
Linastahili!
 
Mnaona msivyo na akiri. Hizo hela kwa Mungu ni za nini? Uko mbinguni ananunua nini? Huwa anashuka kuja kuzichukua? Dini ni scam.
viongozi wa dini ni watumishi wa Mungu, wanapokea sadaka kwa niaba ya Mungu. Mungu ana wawakilishi wake, ana mabalozi wa siri zake. Makuhani, manabii na mitume ndio wawakilishi wake duniani. Pia ana wajumbe wake huko mbinguni wanaitwa malaika. Malaika ni kama kikosi maalumu kwa kazi maalumu kama ilivyo kwa vikosi maalumu vya kijeshi yaani special forces for invisible operation. Mungu ni mkubwa na mawazo yake hayachunguziki utaumiza kichwa bure kutaka kuchunguza ukubwa wake
 
Wasabato mmekaririshwa! Nani alikwambia Wakatoliki wanasujudia hizo sanamu humo Kanisani? Hizo zinatumika katika kutafakarisha! Umewahi kusoma ile habari ya nyoka wa shaba aliyetengenezwa mbele ya wana wa Israeli? Mbona hiyo hukulalamika kwamba ni sanamu?
Issue sio kukaririshwa! Issue ni kujifanya hujui wakati unajua kuwa haya ni maneno kutoka kwa Mungu mwenyewe na hayajawahi kubadilika, na suala la sanamu mnajifanyia (hamkuagizwa popote mfanye!), mnalisujudu, mnatoa sadaka, mnatubu mbele yake, na mnalibeba na kulitembeza barabarani wakati hiyo ni ibada ya kipagani

Unaongelea suala la sanamu ya Nyoka, kwani hujui ilikuwaje mpaka ikafanyika hivyo?? Na kama ndivyo ilivyoagizwa soma wafalme ntanukuu

2 Wafalme 18:3-4
[3]Akafanya yaliyo mema machoni pa BWANA, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.

[4]Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; akaivunja vipande vipande ile nyoka ya shaba aliyoifanya Musa; maana hata siku zile wana wa Israeli walikuwa wakiifukizia uvumba; naye akaiita jina lake Nehushtani

Mbona hakuadhibiwa kwa kufanya hiko?
Ndio ujue kuwa Mungu akikuagiza unatenda hata kama machoni pako utaona sio sahihi, ndio maana Ibrahimu aliambiwa amtoe mwanae Sadaka lakini haijahalalisha mpaka leo tutoe wanetu sadaka

Alimwamrisha Musa aitupe fimbo iwe nyoka, lakini leo tunapinga masuala ya miujiza sababu hatuamini katika hivyo mwisho kabisa, baada ya Muda ni nani ambae alijifanyia sanamu ya kuchonga?
 
Maskini waafrika, hela zote hizo za kujenga kanisa si wajenge kiwanda kiajiri maelfu ya vijana wapate ajira na kipato. Makanisa na misikiti ni mawakala wa umaskini kwanza yanadumaza akili pili yanachukua hata kidogo walichonacho masikini eti ni sadaka na fungu la kumi.

Huu utumwa sijui utaisha lini maana yatupasa kujenga vitega uchumi vyetu kama viwanda badala ya misikiti na makanisa ambavyo ni vitega uchumi wa mwarabu na mzungu.
Kanisa katoliki Lina viwanda,vyuo vya ufundi,vyuo vya uuguzi,vyuo vikuu,shule zote,mashamba ya kilimo,Apartments,Benki TV,Redio nk..sasa unataka lifanye kipi ikupendeze Mzee.Acha mengine yapite.Kila watu wanapopost Dar es Salaam hawaachi kutumia picha ya st.Joseph Cathedral bila kujali dini ya anayepost kizuri hupendwa na Kila mtu.Mimi mwenye nikionaga miskiti mizuri navutiwa sio kwa mambo yake bali usanifu wake
 
Maskini waafrika, hela zote hizo za kujenga kanisa si wajenge kiwanda kiajiri maelfu ya vijana wapate ajira na kipato. Makanisa na misikiti ni mawakala wa umaskini kwanza yanadumaza akili pili yanachukua hata kidogo walichonacho masikini eti ni sadaka na fungu la kumi.

Huu utumwa sijui utaisha lini maana yatupasa kujenga vitega uchumi vyetu kama viwanda badala ya misikiti na makanisa ambavyo ni vitega uchumi wa mwarabu na mzungu.
Wivu wa mama mjamzito
 
Back
Top Bottom