Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume

Kanisa Takatifu Katoliki la Mitume

Umechannganya ukweli mdogo na mengi yasiyo ya kweli.

Nikupeleke shule kidogo.

1) Kristo alianzisha Kanisa na akamteua Simon (akambadilisha jina na kumwita Petera, yaani Mwamba) kuwa kiongozi mkuu wa Kanisa hilo. Math 16:18

2) Kwa njia ya maono, Yesu alimteua Paulo kuwa mtume wa mataifa.

3) Wote wawili, Petro na Paulo walifika Rumi kwa namna ambayo hawakuipanga. Japo walienda kwa sababu ya mashtaka, lakini ikawa ndiyo njia ya kuifikisha injili Rumi ambako ilikuwa ndiyo makao makuu ya dola kuu Duniani iliyoongozwa na wapagani.

4) Siku ya kuiabudu Miungu mbalimbali, Paulo alifika kwa watu waliokuwa wanasali kwa, "Unknown God", anaanza kuwahubiria ni yupi huyo wasiyemjua. Na watu wengi wanakuja kumsikikiza, wengi wanastaajabu, habari zinamfikia mfalme, naye anagiza Paulo apelekwe kwakwe akamhubirie. Mfalme baada ya kusikikiza mahubiri, anatoa kibali cha Paulo kuendelea kueneza imani hiyo mpya, lakini mfalme anabakia na upagani wake.

5) Petro ndiye alijenga kikanisa kidogo Roma. Petro na Paulo, wote waliuawa Roma lakini wakiwa wamejipatia waamini wengi wa Kristo. Baada ya vifo vyao, ukristo unapata nguvu zaidi baada ya mfalme Costantin, yeye binafsi kumkiri Kristo. Na hivyo wakristo kusali na kuhubiri kwa uhuru.

6) Kanisa lilianza kuitwa Katoliki baada ya kikao cha kwanza cha mitume, ikimaanisha kanisa lililoenea Duniani kote. Hivyo walioifuata imani hii iliyoenea Duniani kote waliitwa wakatoliki.

7) Mgawanyiko wa kwanza wa Kanisa Katoliki ulifanywa na aliyekuwa Katibu wa papa. Alipojitenga hakuwahi kusema kuwa ananzisha kanisa jingine bali alijitenga tu na mamlaka ya Papa. Imani aliyoendelea kuihubiri ilibakia ile ile ya Katoliki. Ili kutofautisha wakatoliki wanaofuata huyu aliyejitenga na wale waliobakia chini ya mamlaka ya Papa, ndipo likazaliwa neno hilo la Wakatoliki walio chini ya Rumi, walioitwa Waktoliki wa Rumi (Roman Catholics) na wakatoliki wa kanisa la mashariki walioitwa Orthodox.

Lakini ni uwongo mkubwa kudai kuwa eti mfalme Costantin alibadilisha mambo mengi ya kiimani au ndiye aliyehamisha makao makuu ya Kanisa toka Jerusalem kwenda Rumi.

Mfalme Costantin alichosaidia ni kulipa uhuru Kanisa. Na hivyo kanisa likastawi na kupata waamini wengi Rumi kuliko kwenye mataifa mengi ambayo watawala wao hawakuwa wameupokea ukristo. Hivyo kanisa la Rumi likawa taasisi imara na kubwa kuliko mahali pengine popote.
Mkuu nakushukuru kwa kunipa shule, ijapokuwa imejaa simulizi za mapokeo ya kibinadamu na mantiki zake. Naomba ukumbuke Neno la Mungu halihitaji kutetewa na falsafa za kibinadamu, kwa kuwa ni kamilifu sana na tena linajitetea lenyewe.

Naomba uitafakali nukuu kutoka katika aya ya Neno hilo hilo,

MATHAYO 23
9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.
10 Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.

WAKOLOSAI 1:18
Yeye ni kichwa cha mwili wake, yaani kanisa; yeye ni chanzo cha uhai wa huo mwili. Yeye ndiye mwanzo, mzaliwa wa kwanza aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, ili awe na nafasi ya kwanza katika vitu vyote.

Lazima tujifinze siri iliyopo nyuma ya kifo na kufufuka kwake Bwana Yesu Kristo. Kwa kufanya Agano Jipya amekuwa ndiye Kuhani Mkuu, na ndiye kichwa cha kanisa lake la kweli. Kanisa hili ni jumuiya ya waongofu wanaolitii Neno lake la kweli.

Kristo kupitia kauli kutoka katika kinywa chake mwenyewe kama alikataza mtu ndani ya mwili wa kanisa lake kutambulika kwa cheo cha "ubaba" ama "upapa" ama kiongozi mkuu, sasa inakuwaje cheo hiki kinakuja kuibukia kanisani kule Rumi badala ya Yerusalemu, na pia tunaona cheo hiki hakipo katika kitabu cha Matendo ya Mitume!?

Kanisa Katoliki la Rumi ndilo mama wa dini ya Kikristo na utitiri wa madhehebu ndani yake. Kwa kufanya hivyo ndiyo ili "cement" rasmi matendo ya Unikolai.

“Nikolai” ni neno la kigiriki lenye maana ya “Kuteka madhabahu”.

Ijapo kuwa Unikolai ulianza toka siku za awali za uwepo wa Kanisa.. Lakini mfumo rasmi ulisimamishwa na upapa wa Rumi ambapo uliondoa nafasi ya uongozi wa Roho Mtakatifu ndani ya kanisa, na badala yake kusimamisha uongozi wa wanadamu.
 
Hakuna mtume amewahi kuwa mkatoliki
Kama unamfaham mtaje mmoja
Petro hakuanzisha kanisa katoliku wala kukanyaga rumi maisha yake yote
Aliendeleza kanisa la mitume Jerusalem

Kanisa la kwanza sio katoliki
Kanisa kwanza ni la mitume la Jerusalem
Na halijawahi kuwa na oadri wala sister wala sala za bikira maria, na kubusu masanamu.

Katoliki ni dhehebu la kwanza (sio kanisa la kwanza)
 
Back
Top Bottom