Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Kansa ya matiti inammaliza mke wangu nikiwa nashuhudia, sina la kufanya. Sijui kama naweza kusahau hili

Yapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.

Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.

Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.

Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.

Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.

KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.

KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.

Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu

Ushauri wowote pia napokea.
Yapata miaka miwili imepita tangu mke wangu alipogundulika ana saratani ya matiti, tulianza dozi ya CHEMOTHERAPY pale GOOD SAMARITAN CANCER HOSPITAL Ifakara, tulipatiwa jumla ya mizunguko 8 ya CHEMO, hali ilionekana kuwa nzuri ila ndani ya muda mfupi sana uvimbe ulianza tena.

Baada ya kuona uvimbe umeanza upya tulihamia Dodoma BENJAMIN MKAPA napo tulipatiwa chemo 4 kisha ukafanyika upasuaji ili kuondoa titi lililoathirika na saratani, upasuaji amefanya mwezi wa 4 mwaka huu.

Baada ya upasuaji hali ilionekana kama ipo vizuri, ila baada ya miezi ipatayo mi3 mgonjwa ameanza kusumbuliwa tena.

Anasumbuliwa na; MAUMIVU MAKALI SANA MAHALA ALIPOFANYIWA UPASUAJI
KIDONDA KISICHOPONA (kilianza kidogo sana, kama kiji upele, hatimae kikakua. Hakionyeshi dalili ya kupona.

Najua yote ni mipango ya Mungu, ila sina matumaini kama mke wangu anaweza kupona kwa sasa.

KUNA MTU ASHAWAHI KUUGUZA MGONJWA WA SARATANI naomba ushuhuda ambao unaweza nisaidia cha kufanya.

KAMA KUNA DAWA ZA TIBA MBADALA ULITUMIA ZIKASAIDIA, NAOMBA MSAADA PIA.

Kwa sasa mgonjwa yupo tu nyumbani tunasubiri neema ya Mungu

Ushauri wowote pia napokea.
Mkuu hiyo kitu inayoitwa cancer ni hatari sana, mwezi may nimeishuhudia ikimuondoa dada yangu. Ilikuwa cancer ya titi yaani unaoza polepole huku unaongea Hadi dk ya mwisho
 
Pole sana mkuu
Chukua huu ishauri utanishukuru
Chukua majana ya stafeli changanya na maji masafi lita5 na majani yajae ndoo ndogo ya lita 10. Maji yachemshe hadi yawe ya moto then chukua hayo maji nusu lita saga na majani yamejaa chupa ya blender hadi majani na maji yaishe. Yaache yapoe mdogo mdogo masaa 12. Xhuja them mgonjwa yawe ndo maji yake ya kunywa. Unaweza kuongeza limao kuweka ladha na kamwe usiongeze kitu kingine ila kama ladha itakushinda basi ongeza tunda lenyewe ondoa tu mbegu blend ba maganda yake
Tumia hadi utakapopata nafuu
Mkuu fata huu ushauri huyu ni mtu wa tatu nasikia akizungumzia issue ya majani ya mstafeli kutibu cancer usipuuze please. Pole sana Mungu awasimamie.
 
Pole sana ndugu ,pole mno.
Mwenyezi Mungu ampe nguvu ya kuvumilia maumivu, ampe subira na tumaini.
Kuna wakati mwanadamu anafika kikomo kwa namna ya ubinadamu na hapo ndipo Mungu hushika nafasi ,Mungu yupo na yupo kwa wote, wote wenye heri na wenye Shari.
Yupo kwa kila mwenye haja nae, hajifichi wala hayupo mbali sana kwa yoyote aliweka nia ya dhati kumhitaji.

Wakati huu mkiwa mnapitia changamoto hio na maumivu hayo makali na kukata tamaa ndio Mungu hushika nafasi yake.

Ili kukutana na Mungu kwanza kuweni na amani, msilitazame sana hilo tatizo bali muoneni Mungu katika hilo tatizo, mshuhudieni Mungu kwenye hilo tatizo.

Jitahidini sana mfanya ibada na matendo mema na kuwasaidia wengine wenye hali kama ya kwenu, wapeni moyo wenye hali mfano wa ya kwenu, waombeeni wengine walio kama nyie, toeni sadaka za shukurani kwa wenye mahitaji maalumu, tembeleeni wagonjwa, tembeleeni wafungwa tembeleeni wazee na wenye namna yoyote ya udhaifu wanahitaji faraja na tumaini.
Ikiwa mtajaliwa kufanya hivyo itawajieni amani, itawajieni furaha na tumaini, hamtayazama tena tatizo la mke wako kama hapo awali.

Amini kaka nakushuhudia mke wako atapona , kupona kusikotazamiwa wala kudhaniwa .

Binafsi nakuombeeni katika nia zangu hakika nitawaweka nanyi, mwenyezi Mungu yupo na ataonekana kweli katika maisha yenu.
Comments nyingine za ajabu aise. Huyo Mungu amemsahau mja wake? Kwamba walikuwa hawaombi? Hata kama,baada ya maumivu makali hakuomba? Mungu gani wa kumuacha mtu ateseke kiasi hicho? Mungu wako hana msaada wowote kwa hilo,mleta mada angekuwa na shida hiyo,makanisa anajua yalipo. Hapa si pa kuleta hizo abc
 
CHEMOTHERAPY haiwezi kukuponya KANSA, inakuongezea KANSA. Ni kama unajibanika kwenye TANURU LA MOTO.

Achana na CHEMOTHERAPY, angalia chakula chake cha kila siku ni chakula gani?

Kama una akili timamu, ungelima hapo bustani upande mchicha mwingi ambao hauna MAKEMIKALI, pamoja na KAROTI, hiyo iwe FIRST AID yake.

MAUCHAFU kwenye damu yake pia, SUMUU, UTANDO, MUCUS, afanye namna ya kuondoa yote hayo. DAMU CHAFU.

PAMBANA SANA, ATAPONA KAMA UNA AKILI TIMAMU.

Ukiendelea na MAKEMIKALI na hizo CHEMOTHERAPY utamuangamiza.
Aisee hii Dunia ina viumbe vya hovyo kama BICHWA KOMWE
 
Pole, lakini lazima NIKUAMBIE UKWELII.

Hiyo unayoiita TIBA MBADALA ndio TIBA HALISI, Mimea ya asili yenye nguvu ya kukuponya na kuhuisha mwili dhidi ya maradhi ya aina yoyote.

Hayo MAKEMIKALI ndio yalipaswa kuwa TIBA MBADALA. Ukishafeli kutumia MIMEA SAFI (kitu ambacho hakiwezekani) sasa ndio ukajijaze MAKEMIKALI MACHAFU na MIONZI.

Mkiambiwa MNABEZA, ooohh MIMEA NI UCHAWI! Haya sasa!!!!! Umerudi kule kule!!!

Oooohh, wewe hujui sayansi, wewe mchawiii!! Sayansi yenyewe ndio hiyo, umelipa MAMILIONI ukajazwa MIONZI LUKUKI mpaka mwili ukaharibika zaidi na zaidi.

Najua kuna MAKANJANJA watanivamia hapa, lakini sijali. MIMI NAPASUA UKWELI TU, tukana, bwata, lakini HABARI IMEFIKA.
Ungemfariji tu jamaa yupo kwnye hali ngumu sana.
Hayo mamimea unayoyasifu ndio chanzo cha magonjwa ya figo sbbu watu wanakunywa bila kipimo.
Trend ya wagonjwa wa Figo kuongezeka vijijiñi sio nzuri
 
Apumzike kwa amani brother, alikumbwa na kansa ya eneo gani?
Ukikubali kudanganywa na hao MAROBOTI wanaoamini kwamba MAKEMIKALI YANAPONYA au MIONZI INAPONYA, utampoteza mkeo mapema sana.

Kama MIONZI inaponya, mkeo angepona. PAMBANA na Hizi TIBA umeelekezwa na watu pale juu. Usiwachukulie poa, hao ndo MALAIKA wanamuokoa mkeo.
 
Ungemfariji tu jamaa yupo kwnye hali ngumu sana.
Hayo mamimea unayoyasifu ndio chanzo cha magonjwa ya figo sbbu watu wanakunywa bila kipimo.
Trend ya wagonjwa wa Figo kuongezeka vijijiñi sio nzuri
Huna lolote we DALALI WA MACHANJO.

Tangu lini mchicha ukaharibu FIGO bwana wewe!? 🤣

MAKEMIKALI yale mnayowalisha watu ndo yanawamaliza. Na MIONZI mtu anabanikwa kwenye TANURU LA MIONZI kama ndafu.

Wauaji wakubwa!
 
Mgonjwa aligoma kufanya upasuaji. Hali yake sio nzuri sana Wala mbaya sana, Kwa Sasa anasumbuliwa na kifua kubana maana Kuna dalili Kansa inasambaa kwenye mapafu hii kutokana na vipimo vya hospital.
Anapata maumivu ya mifupa na ganzi.

Miozi ilienda kutonesha kidonda kikazidi kuwa kikubwa ila baada ya kumaliza ndio kikaanza kufunga taratibu.
Pia nilikua nawaza kurudi hospital kwaajili ya mionzi. Pia nikawa nawza ambavyo wengine wanasema mionzi ndo inaumiza zaidi daah, angalau kwa uzoefu wako unashaurije ndugu
 
Pole, lakini lazima NIKUAMBIE UKWELII.

Hiyo unayoiita TIBA MBADALA ndio TIBA HALISI, Mimea ya asili yenye nguvu ya kukuponya na kuhuisha mwili dhidi ya maradhi ya aina yoyote.

Hayo MAKEMIKALI ndio yalipaswa kuwa TIBA MBADALA. Ukishafeli kutumia MIMEA SAFI (kitu ambacho hakiwezekani) sasa ndio ukajijaze MAKEMIKALI MACHAFU na MIONZI.

Mkiambiwa MNABEZA, ooohh MIMEA NI UCHAWI! Haya sasa!!!!! Umerudi kule kule!!!

Oooohh, wewe hujui sayansi, wewe mchawiii!! Sayansi yenyewe ndio hiyo, umelipa MAMILIONI ukajazwa MIONZI LUKUKI mpaka mwili ukaharibika zaidi na zaidi.

Najua kuna MAKANJANJA watanivamia hapa, lakini sijali. MIMI NAPASUA UKWELI TU, tukana, bwata, lakini HABARI IMEFIKA.
Sawa umepasua ukweli ila mbona hujasema ni mmea upi huo atumie ila aimarike?, badala ya kusema leta kwanza ufumbuzi wa tatizo, akipona ndiyo tutarudi kupasua huo ukweli mkuu
 
Pole Sana uchungu unao pata ni mkubwa mno

Ila Acha nikushaur kitu

Mpe furaha mkeo muda wote na mwambie Kila muda kuwa unampenda na umeridhika na Hali yake usimbeze ,usimkaripie wala kumdhihaki kivyovyote vile..

Usiache kumwambia kwamba haya yote ni majaribio ya Mungu na baada ya dhiki faraja

Usionyeshe Una huzuni Sana kwa Hali yake

Vivyo hivyo muombeni Mungu katika Kila Hali

Nimeumia mno pole Sana mkuu

Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
Ahsante sana mkuu, ila kutoonyesha huzun ni ngumu sana mkuu, kuna wakati mpaka nalia kwakweli
 
Back
Top Bottom