All truth23
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 1,215
- 1,401
Yes Angesema maana ni mtu wa HAKIMfano Dpworld wangekuwa wanatokea Rome Italy..
Angeuliza haya maswali???
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yes Angesema maana ni mtu wa HAKIMfano Dpworld wangekuwa wanatokea Rome Italy..
Angeuliza haya maswali???
Usiakubalian na ujumbe WA mtu kwakuangalia nan anaongeaTatizo la Pengo ni kutokuaminika
Mkuu kuna namn nmekuelewa ILA ni kwamba s/k imeshindw kupm kiwango cha utendaji kaz kbs na kusimamia walio wapa dhamnNi muda wa kuangalia management companies au raia wa kigeni wenye sifa sahihi na kuwapa kazi za kusimamia taasisi zote za kibiashara zinazomilikiwa na serikali sio bandari tu.
Muhimu ni kuwekeana mikataba ya performance targets.
Juzi Suma JKT imezindua kituo chao mafuta kwa hakiba ya hela zao; kwa sababu hakuna ubadhirifu kama ilivyo kwenye taasisi za serikali.
Kwanini TPDC aina vituo vya mafuta kuwa mshindani ndani ya soko. Moja ya sababu ni kwamba mteja wake mkubwa wa gas hivi sasa ni TANESCO na Dangote. TANESCO toka wameanza kupewa gas na TPDC awajawahi lipa ata centi 5, gas ambayo wanatumia kufanyia biashara na juzi hilo deni la TPDC serikali wamelifuta.
Watu ambao wameshindwa kuwalipa taasisi ambayo inauwazia malighafi wanayozalishia, hapo hapo wameenda kuingia mkataba wa kununua umeme wa jua; kipindi ambacho watakuwa na uzalishaji wa ziada bwawa la Nyerere.
Nimewatolea mfano tu hao TANESCO lakini wote TTCL, ATCL, NHC, TPDC, TRC na ikiwezekana halmashauri kama kuna uwezo wa kuajiri wageni katika nafasi ya wakurugenzi iwe hivyo.
Ifike wakati tuambizane ukweli watanzania hasa wanaoteuliwa na serikali awawezi kazi; unahitajika utaratibu mwingine ukizingatia sector zingine zina multiplier effect kubwa ya uchumi kama bandari.
Serikali isiishie na bandari tu, waende mbele wenyeji awawezi kazi.
Isijekuwa uwo uhuni uko Kwa HAO viongoziHadi viongozi wa dini wanaupinga huu mkataba ujue ni wa kihuni zaid na haufai.Shauri zenu watawala msiposikia sauti za wengi maana sauti za wengi ni ya Mungu.
Dah. Acha kashfa, sauti ya Mungu NI sauti ya wanadamuHuyu mzee imekuwaje mpaka sasa hajapitishiwa bahasha mmefanya kosa kubwa
Tukiwapa wageni kila kitu maana yake tumeuza uhuru wa kiuchumi tumebakisha uhuru wa kisiasa. Kitakachofuata mbeleni huko hawa wageni ndiyo watakaoamua nani awe kiongozi, tukifika hapo (na ni jirani sana kufika hapo) tutakuwa pia tumeuza uhuru wa kisiasa na sasa itakuwa ni ukoloni mpya 1000%Nakubaliana na wewe kwamba kama Viongozi wetu wanafanya maamuzi ya kubinafsisha au kuruhusu uwekezaji wa nje, kwa imani yao kuwa nchini watu wanawaongoza hawana uwezo, waanze kubinafsisha nafasi zao za uongozi. Wanawajibika kujenga uwezo wa wanaowaongoza na si vinginevyo.
Ukushindwa kuendesha sekta ya bandari hutoweza asilani kuendesha SGR, MGR na CGR. Tujiandae kuwapa Waarabu navyo.Nakubaliana na wewe kwamba kama Viongozi wetu wanafanya maamuzi ya kubinafsisha au kuruhusu uwekezaji wa nje, kwa imani yao kuwa nchini watu wanawaongoza hawana uwezo, waanze kubinafsisha nafasi zao za uongozi. Wanawajibika kujenga uwezo wa wanaowaongoza na si vinginevyo.
Tatizo siyo wanatokea wapi, tatizo ni MoU isiyo na kikomo, kuitisha maoni ya wadau ndani ya masaa 24, kutoa mwanya wa kumilikisha bandari zote Tanzania, kutoa mkataba kwa kampuni inayomilikiwa na nchi wakati na sisi ni nchi tunamiliki kampuni ya TPA.Mfano Dpworld wangekuwa wanatokea Rome Italy..
Angeuliza haya maswali???
Ulishawahi jaribu?Kuna siku yoyote chama tofauti na ccm kimetawala Tanzania tofauti na TANU.Mafanikio ya TANU kila mtu anayajua,madhaifu ya ccm kila mtu anayajua na tatizo kubwa ni kuendekeza sera za udini ili nchi isonge.Hicho chama Cha siasa kitakodi wafanyakazi kutoka nje au?
Kama hawa watanganyika,hata kije chama gani ni kazi bure
Kumbe hana akili kiasi hicho?Ni mrija wa kupitia fungu la kumi la Mungu kupitia kwa waumini. Huku viongozi wakitoka toa cheti cha peponi (indulgence certifice) ya Mungu wao.
Siamini kama jambo kubwa kama hilo linaweza kuletwa kwa wananchi bila kupita kwanza kwenye baraza la mawaziriKwani na huyo atakayeondoka atakua hajaenda sehemu husika?
hujasoma Cuba wewe.Siamini kama jambo kubwa kama hilo linaweza kuletwa kwa wananchi bila kupita kwanza kwenye baraza la mawaziri
Kama ni hivyo waacha waipate shubiri wataeleza huko mbelehujasoma Cuba wewe.
Katika watu waliowahi kuwa viongozi wakuu Nchi hii Mzee Kikwete alikuwa na uongozi wa hovyo ever. Wizi Rushwa na kila aina ya upuuzi ulifanyika wakati wake. Mzee Pengo hana element za udini ila wewe naona unazo kwa kiwango cha juu mno. Unatetea kitu ambacho hakifai kwa namna yoyoteNilishamtoa thamani kabisa huyo jamaa, tena afadhali akae kimya tu mnafiki huyo. Maana alichagua kutofautiana na wenzake wote kwa ajili tu kumbeba mwendazake, hata pale wenzake walipodharirishwa na kutiwa misukosuko na serikali ile yeye bado aliamua kuwa upande wake.
Pengo ana elements nyingi sana za udini, alimsumbua sana Kikwete lakini kamwe hakuwahi kuinua mdomo dhidi ya Magufuli, alibaki akimsifu huku akiwapiga vijembe Maaskofu wenzake wa Katoliki walipojaribu kusimama. Akaenda mbele zaidi na kuanza kumtabiria urais Makonda.
Zee la hovyo sana Hili.
Pengo ni hovyo, alimkalia kooni Kikwete, tukamuunga mkomo. Alipoingia Magufuli, akamkumbatia Magufuli na Makonda wake. Hakuwahi hata siku moja kumkosoa Mwenda zake kwa lolote, hata Maaskofu wenzake walipojaribu kukosoa yeye alikua kunyume nao, yeye aliendelea kumuunga mkono pamoja na madubwasha aliyoyafanya.Katika watu waliowahi kuwa viongozi wakuu Nchi hii Mzee Kikwete alikuwa na uongozi wa hovyo ever. Wizi Rushwa na kila aina ya upuuzi ulifanyika wakati wake. Mzee Pengo hana element za udini ila wewe naona unazo kwa kiwango cha juu mno. Unatetea kitu ambacho hakifai kwa namna yoyote
Huyu padri mnafiki sana...anaongea hivi kwa kuwa huyu SI MWENZETU.."....huenda Serikali imeona kuna tija. Lakini najiuliza, hivi kweli sisi hatuwezi kuendesha bandari yetu wenyewe? Sielewi viongozi wetu ama wanajitafutia pesa na kuwaacha Watanzania wakididimia ama...yaani hata sielewi maana nashindwa kuelewa!
"....je, pesa ni muhimu kuliko kuwajengea uwezo Watanzania ili wao waweze kuiendesha bandari yao?! Kila mmoja wetu ajiulize hilo."
"....mwenyezi Mungu alimweka binadamu ili aweze kutawala mali na hata pesa. Hilo ndilo jawabu langu la ki maadili."
"Huwezi kumtweza mwanadamu mwenzako kwa sababu ya hela. Ni hilo tu naomba nijizuie kusema zaidi," Pengo.
Kanisa Katoliki TV.
Wakatoliki walitoa Waraka wa Kwaresima na Waluteri wakatoa Waraka wa Pasaka. JPM alitaka kupata wazimu na kuanzisha vita vya kuvuruga na kukagawa makanisa kwa kutumia wanasiasa, vyombo vya dola na fedha!Ukiwa kiziwi utasikiaje? Wenye masikio na macho tunaukumbuka ule waraka mkali wa pasaka uliotolewa na TEC, uliomkera sana JPM kiasi cha kufikia kuamrisha makanisa yalipe kodi hata kwa vitu ambavyo ni kwaajili ya huduma.
Suluhu ilipatikana baadaye sana, ndipo misamaha ya kodi kwa vifaa vya huduma zinazotolewa na taasisi za dini, ikarudishwa tena.
Lakini pua tuulizane, JPM pamoja na ubabe wake dhidi ya demokrasia na utii wa katiba, aliwahi kuuza rasilimali gani ya nchi?