Kardinali Pengo: Ni kweli Watanzania hatuwezi kuendesha bandari yetu?

Kardinali Pengo: Ni kweli Watanzania hatuwezi kuendesha bandari yetu?

Mfano Dpworld wangekuwa wanatokea Rome Italy..
Angeuliza haya maswali???
Bahati nzuri umeelekeza hilo kwa Pengo mwenyewe, kutokana na anakojulikana kuwepo kwa imani yake ya kiroho; lakini na hawa wengine wanaohoji huo mkataba na wao unawahusisha na swala hilo?
Je, sababu za baadhi ya watu kuhoji ni kwa vile ni DP World na anakotokea, au wanahoji mikataba iliyoingiwa bila kujali ni nani anayehusika na mahali anakotokea?

Kidogo inashangaza kwa mtu kama wewe kuhoji kama ulivyofanya; lakini inaweza kueleweka kwa vile mtu unayehoji anaeleweka ni nani.
 
It's proven beyond doubt hatuwezi. Tumeendesha zaidi ya miaka 50 bila tija yeyote, majirani wote wamehamia Mombasa na Beira. Bandari yenye potential ya kuchangia zaidi ya 70% ya bajeti ya nchi inachangia 30% tu, mnataka uthibitisho gani zaidi?
Watu zaidi ya arobaini wamelike!

Familia ya watu kumi hawawezi kuendesha mradi wa familia!
Mtu anatoa conclusion hio kwa kuwa mmoja wa familia amekabidhiwa kuendesha mradi na ameshindwa!

Tanzania Ina watu zaidi ya million 60!
Ni watu wangapi wamepewa dhamana ya kuendesha bandari? Watu Hawa waliteuliwa kwa vigezo gani? Walipewa masharti gani? Walisimamiwa kwa viwango gani? Waliwajibishwa kwa viwango gani? Waliwezeshwa kwa kiwango gani?

Umetafiti haya yote ukaja na conclusion kuwa hatuwezi?
 
Watu zaidi ya arobaini wamelike!

Familia ya watu kumi hawawezi kuendesha mradi wa familia!
Mtu anatoa conclusion hio kwa kuwa mmoja wa familia amekabidhiwa kuendesha mradi na ameshindwa!

Tanzania Ina watu zaidi ya million 60!
Ni watu wangapi wamepewa dhamana ya kuendesha bandari? Watu Hawa waliteuliwa kwa vigezo gani? Walipewa masharti gani? Walisimamiwa kwa viwango gani? Waliwajibishwa kwa viwango gani? Waliwezeshwa kwa kiwango gani?

Umetafiti haya yote ukaja na conclusion kuwa hatuwezi?

Bandari sio watu tu, Kuna gharama za uwekezaji, technology nk ambapo bongo imethibitika pasi na shaka kwa miaka zaidi ya 50 hatuwezi. Apewe muwekezaji.
 
Sisi tunaweza kuendesha bandari ila shida inakuja je unaweza kumbishia riziwani asitoe makontena Je unaweza kumbishia mtoto wa samia mtoto wa mpango mtoto wamajaliwa au hamjui wakati wa mzee wa msoga mtoto alivyokuwa anapitisha mali bila kodi au ushuru
 
"....huenda Serikali imeona kuna tija. Lakini najiuliza, hivi kweli sisi hatuwezi kuendesha bandari yetu wenyewe? Sielewi viongozi wetu ama wanajitafutia pesa na kuwaacha Watanzania wakididimia ama...yaani hata sielewi maana nashindwa kuelewa!

"....je, pesa ni muhimu kuliko kuwajengea uwezo Watanzania ili wao waweze kuiendesha bandari yao?! Kila mmoja wetu ajiulize hilo."

"....mwenyezi Mungu alimweka binadamu ili aweze kutawala mali na hata pesa. Hilo ndilo jawabu langu la ki maadili."

"Huwezi kumtweza mwanadamu mwenzako kwa sababu ya hela. Ni hilo tu naomba nijizuie kusema zaidi," Pengo.

Kanisa Katoliki TV.
Ana hoja ila anakosa uhalali mbele ya watanzania. Kipindi cha jiwe alisifia kila uovu aliyofanya hata kama ulioondoa mpaka haki watu ya kuishi. Walimpigia makofi na kumpelekea zawadi. Kwa sasa anasema kwa sababu kuna alicholosa na sio kwa sababu yuko objective.
 
"....huenda Serikali imeona kuna tija. Lakini najiuliza, hivi kweli sisi hatuwezi kuendesha bandari yetu wenyewe? Sielewi viongozi wetu ama wanajitafutia pesa na kuwaacha Watanzania wakididimia ama...yaani hata sielewi maana nashindwa kuelewa!

"....je, pesa ni muhimu kuliko kuwajengea uwezo Watanzania ili wao waweze kuiendesha bandari yao?! Kila mmoja wetu ajiulize hilo."

"....mwenyezi Mungu alimweka binadamu ili aweze kutawala mali na hata pesa. Hilo ndilo jawabu langu la ki maadili."

"Huwezi kumtweza mwanadamu mwenzako kwa sababu ya hela. Ni hilo tu naomba nijizuie kusema zaidi," Pengo.

Kanisa Katoliki TV.

Tatizo la nchi yetu siyo kutokuwa na watu wenye uwezo na haiba ya kusimamia Sera, Sheria na kanuni zinazoongoza nchi, Wala hatuna shida ya wasomi wanaoweza kutunga mitaala ya elimu ya kufaa kwa maendeleo ya taifa. Tatizo nchi Ina wachache wanaotupangia Nani awe Nani, hata Kama Hana maadili kuanzia nyumbani kwake, hana "record" ya ubobevu wa kivitendo popote.

Mtu hawezi kuwa na mapenzi ya kweli kumsaidia jirani wakati watu wa nyumbani kwake Wana hitaji hilohilo. Ukiona imetokea hivyo, ujue Kuna agenda isiyojulikana.

Mimi nafikiri usimamizi Makini na wenye viwango vya uadilifu ndio hitaji kuu katika nchi yetu. Kuwajibisha wanaotumia vibaya madaraka yao kwa Uma bila huruma ni nidhamu muhimu tunayokosa.

Kama haya yangekuwa yako katika mstari wake, hakika tusingehitaji mwekezaji katika maeneo nyeti kiusalama. Naomba serikali usimpe nafasi spika mstaafu kuwa nabii wa kweli.

Hata Katiba iliyopo na udhaifu wake, ikiwa mikononi mwa waungwana ingeweza kutupeleka mbali Sana. Kiongozi yeyote asiyetosheka atatumia nafasi yake kuleta mengi yasiyofaa.

Hapa sijamhusisha raisi wangu. Binafsi siamini kinachoendelea ni Haiba ya raisi wetu, Ila ikithibitika kuwa Kuna udhaifu unaopigiwa kelele leo, atakuwa ameingizwa kimtego kuharibu sifa yake njema kwetu sisi tusiojua kuchambua Mambo kwa kina, ambao ndiyo wengi.

Haishangazi kuwa tunajiandaa kimrudisha madarakani kwa Kura zetu 2025. Lakini kwa habari ya bandari zetu na usalama wa Maisha yetu na vizazi vijavyo, tunasukumwa nyuma maili nyingi. Kubinafsisha bandari (eneo nyeti kimaslahi na kiusalama) kwa mtindo huo kumetuingiza kwenye Mashaka makubwa.

Hata hivyo, katika Hali ya kumaanisha, binafsi na kwa kuhamasisha watu wengine tunamuombea raisi na serikali yake (hasa rais) wafungue macho sawasawa ili waweze kuona hila za watu wa nje wenye Nia mbaya na taifa hili tangu zamani. Jambo hili kwa wale wenye ufahamu wa kadri, wametiwa hofu kubwa, naomba serikali isipuuze hofu hii.

Wala isijisikie vibaya wananchi wakihoji Jambo hili kwa nguvu, Wala isilazimishe hata Kama Lina maslahi - hiyo siyo njia pekee ya maendeleo.

Amani usalama na ustawi wenye uwiano vipewe vifikiriwe kwa kina na kwa nguvu zote. Hiyo itatoa ushawishi kuwa Kuna Nia njema Ila ni kasoro za kiutendaji zilizojitokeza.

Ambazo pia zinaweza kuwa kiashirio Cha uwezo duni wa washauri na watendaji waliohusika katika swala hili.
 
Mfano Dpworld wangekuwa wanatokea Rome Italy..
Angeuliza haya maswali???

Hili la bandari halitaisha leo Wala kesho
Hapa CCM wamelikoroga Bora hata issue za migodi na gesi ambapo wawekezaji ndio wenye technology ila hili la bandari tunauwezo wa Kununua mitambo na tukaendesha wenyewe
Hivi kile chuo cha bandari kilikufa au bado kipo? Na kama kipo, kinafanya nini? Nini ilikuwa malengo ya kuanzishwa kwake? Nasikia wanasemaga kuanzishwa kwa chuo cha taifa cha usafirishaji, ilikuwa kukabiliana na changamoto zote za usafirishaji na kumaliza kabisa matatizo katika nyanja ya usafiri, vipi chuo cha bandari hakikuwa na lengo lolote?
 
Wewe na pengo mmeona tunaweza!?.. uingereza na marekani wamewapa waarabu hao waendeshe bandari zao...mnadhani wakihitaji nini bandarini!?
Unadhani the crown his majesty's government ya uingereza au marekani wanaweza kupewa masharti ya kipuuzi kama haya wanatupa sisi? Eti bandari zote uingereza au marekani ziwe chini ya udhibiti wao kama vile mali yao au nchi eti ifute sheria wao hawataki na kuweka sheria za kuwaruhusu kufanya yale wao wanataka? Hao waarabu wana package za aina ya kupewa kila watu. Na usidhani DP World wanaokuja tz ndio hao hao wataenda uingereza.
 
Unadhani the crown his majesty's government ya uingereza au marekani wanaweza kupewa masharti ya kipuuzi kama haya wanatupa sisi? Eti bandari zote uingereza au marekani ziwe chini ya udhibiti wao kama vile mali yao au nchi eti ifute sheria wao hawataki na kuweka sheria za kuwaruhusu kufanya yale wao wanataka? Hao waarabu wana package za aina ya kupewa kila watu. Na usidhani DP World wanaokuja tz ndio hao hao wataenda uingereza.
Excuse za kijinga,umeuona mkataba wa uingereza na dp world
 
nadhani ccm ndio hawawezi. ila kuna siku tukipata chama kingine kikashika nchi, hao waarabu wataondoka wenyewe. sisi ndio wenye jeshi, wenye polisi na kila kitu, tukiamua kuwafanyia fitna hawatafanya chochote na wataondoka tu, na sisi wenyewe tutashika usukani. binafsi ningekuwa rais nisingeshindwa kuendesha bandari.
 
"....huenda Serikali imeona kuna tija. Lakini najiuliza, hivi kweli sisi hatuwezi kuendesha bandari yetu wenyewe? Sielewi viongozi wetu ama wanajitafutia pesa na kuwaacha Watanzania wakididimia ama...yaani hata sielewi maana nashindwa kuelewa!

"....je, pesa ni muhimu kuliko kuwajengea uwezo Watanzania ili wao waweze kuiendesha bandari yao?! Kila mmoja wetu ajiulize hilo."

"....mwenyezi Mungu alimweka binadamu ili aweze kutawala mali na hata pesa. Hilo ndilo jawabu langu la ki maadili."

"Huwezi kumtweza mwanadamu mwenzako kwa sababu ya hela. Ni hilo tu naomba nijizuie kusema zaidi," Pengo.

Kanisa Katoliki TV.
Nadhani hilo la kuwajengea uwezo waTz ni muhimu sana. Actually sio itasaidia kuendesha Bandari tu, lakini pia katika mambo mbalimbali ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.
 
Nje ya siasa mkataba huu ni wazi unaungwa mkono na watu wachache sana.
 
Back
Top Bottom