Kariakoo haina umuhimu kwa uchumi wa nchi kama tunavyo aminishana Bongo lala

Kariakoo haina umuhimu kwa uchumi wa nchi kama tunavyo aminishana Bongo lala

Kariakoo haihamisishi ukuaji wa viwanda vya ndani, Kariakoo ni Dumping site ambako asilimia 100 ya products zinazo uzwa pale ni Made in nje.

Ni wajinga pekee ndio wanaoweza kuamini kwamba soko lenye asilimia 100 ya bidhaa za nje ya nchi lina umuhimu sana kwa uchumi wa nchi kuliko, Kilimo, kuliko Madini, kuliko Uvuvi na kulilo utalii.

Kariakiakoo ni makao makuu ya kituo uapnde wa Tanzania cha kupromote products za nje hasa kupromote viwanda vya China na kupelekea China kutoa ajira zaidi kwa wachina.

Huwa nashangaa sana tunapo aminishwa kwamba kariakoo ndio roho ya uchumi wa nchi, yaani sehemu inayo promote viwanda vya China inaweza vipi kuwa roho ya uchumi wa nchi?

Kariakoo ni Dumping site ya products low qualities kutoka nje ya nchi.

Kama angalau asilimia 40 ya bidhaa za kariakoo ni made in Tanzania hapo kungekuwa na logic ila asilimia 100 then wajinga sisi tunaaminishwa kwamba pale ndio uchumi wa nchi ulipo?

Vipi huko wanako enda kuchukua bishaa?

Kariakoo ni kituo moja wapo cha kuua viwanda vya ndani.

Nchi inamalizwa na siasa za kijinga sana.
Ujinga umetuzidi kama mtoa hoja alivyoeleza. Kariakoo ni muhimu kwa TRA kudai kodi sio kwamba ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi. Ni soko muhimu kwa uuzaji wa bidhaa za nje kwa hivyo ni mhali muhimu kwa taifa kutoza kodi na kodi kubwa kwa zile bidhaa zinaleta ushindani usio sawa kwa zile bidhaa tunazalisha nchini.
 
Ujinga umetuzidi kama mtoa hoja alivyoeleza. Kariakoo ni muhimu kwa TRA kudai kodi sio kwamba ni muhimu sana kwa maendeleo ya nchi. Ni soko muhimu kwa uuzaji wa bidhaa za nje kwa hivyo ni mhali muhimu kwa taifa kutoza kodi na kodi kubwa kwa zile bidhaa zinaleta ushindani usio sawa kwa zile bidhaa tunazalisha nchini.
Nchi yako haina viwanda vya kutosha. Madini, Utalii, Kilimo bidhaa za utendaji zinatoka hapo Kariakoo. Sasa jiongeze boss.
 
Kariakiakoo ni makao makuu ya kituo uapnde wa Tanzania cha kupromote products za nje hasa kupromote viwanda vya China na kupelekea China kutoa ajira zaidi kwa wachina.
Kariakoo imekuwepo hata kabla ya large scale China-made goods importation

Kariakoo imekuwepo tangu enzi za electronic devices nyingi zikiwa ni za kutoka Japan

Kariakoo ni soko la bidhaa kutoka kokote duniani ingawa asilimia kubwa ya bidhaa ni za China. Kusema Kariakoo inapromote viwanda vya China unakosea sana.

China hawaifahamu Kariakoo kinachofamika na China ni kituo cha biashara cha pale Ubungo.

Hapo Ubungo, Mchina anaanzisha exhibition trading platform, cros-border E-commerce platform, commodity procurement platform kwa
Made in China goods only

Una hoja nzuri ya kutaka kuendeleza viwanda vya ndani ili kupunguza uingizaji wa bidhaa kutoka nje hilo pekee ndilo nakuunga mkono.
 
Dunia nzima nchi zinapigana kuwa nchi za viwanda, na wanajua nguvu ta nchi yoyoe iko kwenye viwanda na si kuwa Dumping site.

Su bure meli za mizigo zinageuza tupu kurudi ziliko toka then tunashangilia, yaanu tunashangilia meli kubwa za mizigo kutua nanga kuleta products na kuondoka tupu?

Magari ya mizigo huwa yanarudi tupu Dar es salaam mengine yanaamua kubebana kwa sababu sisi ni Dumping site ya products za nje ya nchi.

Sijui SGR itabeba mizigo gani kupeleka Dar es salaam Bandarini

Sawa Mkuu, lakini tatizo ni Serikali yetu sikiveu ndiyo imetujengea uchumi wa design hiyo. Hayo unayoyasema ya uchumi wa viwanda siyo uchumi wetu labda in our dreams.
 
Uko sahihi. Pia biashara za Kariakoo hazina msaada wowote kwa vijana kuongeza maarifa yoyote kwenye fani walizosomea. Uchuuzi hauna future kabisa. Vijana wa IT, Mining, Kilimo, na fani zingine wamekuwa wachuuzi wa bidhaa zinazotengenezwa na vijana wenzao wa China.
 
Una uwezo mdogo wa kujenga hoja.

Ukisema kariakoo haina umuhimu kwa uchumi, uchumi ni nini na unajengwa na vitu gani. Kwa akili yako uchumi ni viwanda tu nani alikukaririsha uchumi ni viwanda tu.

Ilala ndio sehemu inachangia aslilimia kubwa ya makusanyo ya kodi nchi nzima hii TZ na mapato hayo ndio yanaenda kuunda pato la Taifa la ujumla. Unasemaje halina umuhimu hizi akili.

Viwanda hio ni sector nyengine kabisa initiate kujengwa kwa viwanda kama factor moja ya kiuchumi ila usi initiate factor kwa ku-undermine factor nyengine. Karikoo ni TRADING ECONOMY ni uchumi unaojitegemea na hakuna nchi isiyofanya TRADING meli haziji TZ tu daily Meli zipo baharini kupeleka bidhaa kila sehemu ya Dunia.

Kama unawaza Uchumi ni kiwanda una safari ndefu kujifunza uchumi.
 
Uko sahihi. Pia biashara za Kariakoo hazina msaada wowote kwa vijana kuongeza maarifa yoyote kwenye fani walizosomea. Uchuuzi hauna future kabisa. Vijana wa IT, Mining, Kilimo, na fani zingine wamekuwa wachuuzi wa bidhaa zinazotengenezwa na vijana wenzao wa China.
Kariakoo kuna uhusiano gani na masuala ya kusoma, you guys inabidi mounzike kila kitu kuingiza wasomi.
 
Viwanda vinakufa kwa sababu ya kodi na wanasiasa kua wafanya biashara juzi kiwanda kinauzwa watu wajenge nyumba urafiki achana na viwanda vingine vingi vimejifia mashirika mengi pia yamejifia machache yanajikongoja km Tazara na Mengine mengi.Serikali imekaa kutafuta kodi tu hawawazi kujenge uchumi kwa mwananchi kwa kuongeza thamani ya bidhaa zetu kwa kujenga viwanda.Vijana wengi wanaisgia kua machinga hata kusimamia tu kilimo basi vijana wajiajiri huko wameshindwa ila watu wakilima na kuvuna unakuta vizuizi lipa tozo mara hiki.Tanzania hatuna viongozi .
 
Wewe unaiita Kariakoo dampo una akili kweli? Hivi unajua thamani ya mitaji ya biashara waliyoiweka watu pale?

Acha dharau mdogo wangu, pale pana mzunguko sana wa fedha na hata wateja kutoka nje ya nchi kama Congo huenda kununua bidhaa Kariakoo. Bidhaa zinatoka Kariakoo zinaenda mikoani

Mpaka Kariakoo iitwe mkoa wa kikodi unafikiri TRA walikurupuka
Haiondoi neno Dampo, Kariakoo ni Dampo la products za kigeni, shida wana siasa wanawadanganya sana, mitaji haibadili ukweli, maada ngumu huwezi elewa
 
Back
Top Bottom