Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

Kariakoo hakuna machimbo tena, kwa atakayepuuza sitaongea tena

Kuna duka niliingia hapo mkwajuni yaani jamaa hana tamaa yeye kaamua kuuza kama super market anabandika na price tag kabisa hataki kukaushana mate na wiziwizi usio na kichwa wala miguu.Hii itapendeza hapo kariakoo watu wafanye biashara kama jamii zilizostaarabika bandikeni price tag mtu ajikadirie mwenyewe hakuna mbambamba na foleni bila sababu.
 
Kariakoo wanakupokea jinsi unavyoenda, ukitaka usisumbuke kabla ya kwenda Kariakoo jaribu kusurvwy bei mtandaoni. Ukifika huko ujue kabisa lasivyo itauziwa mara mbili yake.
Nilienda kununua sabufa tena duka famous kabisa na bei yake nilikuwa naijua, hata imstagram page yake kaweka bei, kufika pale mawinga wakanipokea sabufa ya 175k wakaniambia 300k nikawaambia straight bei yake ni 175k najua bado wanabisha mwisho 270k.
Nikataka kusepa zangu ndio mwenye duka akaniambia njoo uchukue, yaani ni kero mno
 
Kuna duka niliingia hapo mkwajuni yaani jamaa hana tamaa yeye kaamua kuuza kama super market anabandika na price tag kabisa hataki kukaushana mate na wiziwizi usio na kichwa wala miguu.Hii itapendeza hapo kariakoo watu wafanye biashara kama jamii zilizostaarabika bandikeni price tag mtu ajikadirie mwenyewe hakuna mbambamba na foleni bila sababu.
System hiyo ni ya nchi zilizoendelea,kwa TZ ni mlimani city tu,bei unaikuta kwa kitu unachotaka kununua
 
Ukitaka kwenda mbali lazima uwe fala kwenye mambo flan flan. Ni kama vile unavyotaka kuuza eneo unakuwa kwa muda mbele ya madalali mambo yako yaende. Usipojifunza kunyenyekea bro sahau kufika mbali nakuhakikishia utabakia tu kumiliki nyumba mbili tatu ukienda mbali utajenga hoteli au kumiliki apartment utajidanganya we ni tajiri. Mzee jifunze walipokosea waliokutangulia utafika mbali. Mi winga ndio wananipangia cha kuweka order kiwandani na mzigo ukifika fasta unaisha nataka nini sasa.

Kuitwa boss tajiri mwenye duka cjui mkuu hizo mambo ni upuuzi umetupumbaza wengi.

We jichanganye nao nakuhakikishia utakula mema ya nchi. Mfano mdogo.

Kuna winga mimi tulifikia mahali nikawafungulia maduka tunagawana kwenye faida baada ya mtaji wangu kurudi.

Mzee the sky is your limit ni wewe tu.
Yaani wewe jamaa unatetea upuuzi bila Aibu Tena kwa kujiamini kweli....
Mimi napiga vita uwinga kabisa kwa sababu ni utapeli mtupu, uwinga hauna tija yoyote kwa wafanyabiashara au wateja.
Subiri ukutane na majitu kama huyu jamaa wa kujiita Kitali yanakwambia eti yamekuza biashara zao kupitia mawinga, yaani biashara zao zimekuwa kupitia vibaraka wao wanaowatapeli na kuwaibia wateja...

Uwinga ni Moja sababu kwanini bidhaa zetu kwa asilimia kubwa huwa tunauziana sisi wabongo tu, raia wa mataifa mengine hawataki kabisa huu ujinga, ukienda hapo Zambia hata kwenye masoko tu ya kawaida Kila bidhaa imewekewa kabisa price tag, yaani huna haja ya kuuliza bei ukifika dukani... Njoo bongo Sasa yaani muuzaji Yuko tayari akamuite winga ndio aje akuuzie hata kama umemkuta yeye dukani.. ovyo sana
 
Kwa kukusaidia ni kuwa ukiwa na hela akapita muuza ndizi na ukanunua bila kibargain haimaanishi una hela ni kuwa unataka nae apate chochote kitu kuisaidia familia yake. Na wewe unabarikiwa. Maisha unabana ukiwa hapo chini unavyotafuta mtaji ila ukishaanza uwekezaji wajali wengine nakuhakikishia hela zitakuwa zinakufuata. Maisha yangu nimefanyiwa hivyo nilivyokuwa naanza life na mimi nafanya hivyo na kiukweli naziona baraka. Kwa umri wangu wa miaka 45 ninaweza kufunga box nk lakin huwa hizo kazi unampa mtu nae apate riziki ndio maisha yalivyo we baki na mawazo yako uniite mjinga kwangu sio kitu maana kila mtu ana namna amechagua namna ya kuishi humu dunian
Sasa kama ni hivi basi haukuwa na aja ya kutoa maneno yaliyojaa fedhuri na dharau kwa mleta mada....

Kama wewe unaona ni sawa tu kununua kitu ambacho Kiko overpriced kwa lengo la kutaka na wengine wapate kwa sababu kipato chako kinaruhusu, basi wasikilize na waheshimu wale ambao Bado Wana bargain mpaka kwenye lowest price line, maana hapa duniani binadamu hatufanani kama tu ilivyo kwa vidole.

Kuhusu uwinga Bado nakwambia uwepo wao ni sumu na pigo kubwa sana kwa wateja, na ndio chanzo Cha kupunguza kwa customer base ya Eneo husika, mfano kama Mimi leo hii siwezi kabisa kwenda Karume kutokana huu ushenzi, yaani unaingia tu pale mlangoni unapokelewa na mawinga kama watano na Kila mtu anakuongelesha, haya unafika golini suruali moja ya mtumba wanakutajia bei eti 35,000/= kweliii??? Hapo unategemea Kuna mtu anarudi Tena Hilo Eneo.?

Hao mawinga wenu wanawaharibia biashara sana wewe endelea kuwatetea tu hapa
 
Usijisumbue kwenda Kariakoo kununua mzigo ukidhani Kuna bei nafuu
Kariakoo wamejaa wajanja na madalali tu
Unaweza ingia kwenye duka ukamkuta mwenye duka ukamuuliza bei akakuelekeza uongee na vijana wake wakuumize
Nyie watu situka Kariakoo hakufai kabisa, mawinga wameharibu uaminifu.

Matajiri wanauchukulia wateja kama wajinga, wanajua kuwa mtaenda tu.

Sasa naomba niwape machimbo mapya Kwa Dar

1. Kwa wale wa electronics nenda Tegeta pale Kibo complex utapata bei ambayo Kariakoo haipo

Pia nenda Mbagala rangi Tatu utapata electronics zote, kuanzia Tv, simu, cable

2. Nguo nenda Mwenge au Makumbusho

3. Mitumba
Usijaribu kwenda Karume au Ilala tena
Kwa mitumba ya bei nafuu, mabalo za rejareja nenda Tandika, Temeke, Tandale na Mwenge

Kanda ya ziwa, machimbo yapo Katoro

Kwa machimbo mengine, tujaribu ku share.

Ila chonde chonde Kariakoo utaishia kupandiliwa na kupigwa bei ya maana.

Kariakoo nilikuwepo Jana, nikahairisha kuchukua mzigo kisa mawinga
Ukitaka kuishi vizuri kariakoo tafuta winga ambaye yuko royal kwako,winga atakuumiza iwapo hamjuani wala hamjawahi kufaana kwa chochote,winga uliyewaji kumfaa jambo lake hanaga kinyongo,mimi mizigo yangu nachukua kwa mawinga wanaonipa hadi bei za kiwandani china pamoja na go dwlown zao nina access ya kuingia,ishu ni aina ya koneksheni uliyonayo.
 
Ukitaka kuishi vizuri kariakoo tafuta winga ambaye yuko royal kwako,winga atakuumiza iwapo hamjuani wala hamjawahi kufaana kwa chochote,winga uliyewaji kumfaa jambo lake hanaga kinyongo,mimi mizigo yangu nachukua kwa mawinga wanaonipa hadi bei za kiwandani china pamoja na go dwlown zao nina access ya kuingia,ishu ni aina ya koneksheni uliyonayo.
Ona Sasa ndio maisha gani haya??? Kwamba hela tuitafute kwa shida na hata jinsi ya kuitumia tuanze kutafuta connection hili itumike kwa namna sahihi?? Like serious?

Nikisema hii jamii yetu ya kibongo ni jamii ya ovyo sana muwe mnaelewa, hebu ona vitu ambavyo tumevi normalize.. yaani vitu vya oovyoo
 
Ona Sasa ndio maisha gani haya??? Kwamba hela tuitafute kwa shida na hata jinsi ya kuitumia tuanze kutafuta connection hili itumike kwa namna sahihi?? Like serious?

Nikisema hii jamii yetu ya kibongo ni jamii ya ovyo sana muwe mnaelewa, hebu ona vitu ambavyo tumevi normalize.. yaani vitu vya oovyoo
Kabisa jamii ya hovyo sana.

Yani mtu anatoa ushauri wa kipumbavu na anaona sawa tu.

Sasa kwa hali ya kawaida inawezekana vipi kila mtu awe na winga wake ambaye yupo royal.

Ni kitu kisichowezekana ni pia ni usumbufu kwa mteja.

Muhimu watu wakatae kwenda Kkoo.
 
Winga huwezi kumkwepa

Winga wapo dunia nzima

Hata Tajiri namba moja duniani Jeff Bezos ni winga.

Hata kampuni ya Nike yenyewe ni winga wa vifaa vya michezo. Ila haina kiwanda hata kimoja.

Kampuni ya Gucci ni winga
Mifano yako ni ya kiduwanzi sana na Haina mshabiano wowote wa kimantiki na hao vibaka wenu wa kiriakoo.. japo wewe unajiona umeandika bonge la point
 
Ukitaka kuishi vizuri kariakoo tafuta winga ambaye yuko royal kwako,winga atakuumiza iwapo hamjuani wala hamjawahi kufaana kwa chochote,winga uliyewaji kumfaa jambo lake hanaga kinyongo,mimi mizigo yangu nachukua kwa mawinga wanaonipa hadi bei za kiwandani china pamoja na go dwlown zao nina access ya kuingia,ishu ni aina ya koneksheni uliyonayo.
Royal--loyal

Ova
 
Ona Sasa ndio maisha gani haya??? Kwamba hela tuitafute kwa shida na hata jinsi ya kuitumia tuanze kutafuta connection hili itumike kwa namna sahihi?? Like serious?

Nikisema hii jamii yetu ya kibongo ni jamii ya ovyo sana muwe mnaelewa, hebu ona vitu ambavyo tumevi normalize.. yaani vitu vya oovyoo
Watu hununua au kuuza kitu kwako kwa sifa kuu tatu
1.Kukufahamu(Know how)
2.Kukupenda(Like)
3.Kukuamini(Trust)

Nje na hizo sababu,niamini mimi,ukiachilia mbali ubantu wa wabantu utapigwa tu kwenye bei maana utadondokea kwenye myego wa price discrimination.

Biashara ni mchezo wa supply chain na utele wa taarifa,sifa mojawapo ya mfanyabiashara ni kuficha taarifa.Tafuta kitabu cha Robert Kiyosaki kinaitwa Guide to investing kitakusaidia.

Kwenye mnyororo wa usambazaji inayegemea na;-
1.Taarifa ulizonazo
2.Nani unahusiana naye
3.Aina la soko unalotaka kulihudumia
 
Back
Top Bottom