DOKEZO Kashfa kubwa kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani. Kanisa latumika kuwauzia mashamba hewa waumini wake. Ekari feki 15,000 ziliuzwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Viongozi makanisa wanapend hela kuliko chochote na hiyo ndio tabia ya wakirito wote waliomo serikalini kazi ufisadi tu
 
Nimeziona na namm nimezungumza kile ninachokijua na kukishuhudia, siwezi kuthibitisha hayo ya wengine
Niliwahi kuipenda sana KKKT sana tuu. Ila malasusa na Genge lake kwanza walianzisha sadaka zisizo na mpangilio then wakaja kupora kiti cha mtu huku konde nimejiunga na warutheli wa africa mashariki na naendelea kumuabudu Mungu kwa furaha na uhuru
 
usitetee upuuzi, KKKT miaka ya hivi karibuni limekua kanisa la ovyo sana. Mbey washaivuruga vipande vipande
 
Kwa kawaida taasisi kama KKKT huwa inafanya mambo yake kwa usahihi kulinda heshima yake. Yawezekana mpango wa kanisa ni mzuri ila watekelezaji wameenda kinyume na maadili.
Hakuna cha usahii walijua kuwa haya maeneo sio yao tu wachungaji kwa hela ni zaidi ya hatari
 
Hakuna Kanisa linafanya haya, atakuwa ni muhuni Mmoja wa Kanisan, muwage mnaheshimu watu na kutosema vitu ambavyo hamna ushahidi navyo
Mchungaji gani asie penda hela tena za Magumashi mpaka wamepandikiza watu wao serikalini hili wapige hela
 
Nidhani nimepigwa peke yangu mkazi wa hapa JF. Jamaa walinikomba 10,200,000/-
Kufanya biashara na kanisa ni kujitafutia kutapeliwa
 
Kinachofanyika sasa hivi ni wajanja wachache wanaenda ardhi wanaangalia maeneo yote yaliyotelekezwa na mashirika na taasisi mbalimbali za serikali hata kama ni miaka 40 lakini hati zao hazijafutwa kamailivyotokea Mabwepande kwenye eneo la DDC. Basi zinaundwa "syndicate" kwa kupitia viongozi wachache wa chama na serikali wasiokuwa waaminifu basi kazi inaanza. Kitachofuata hapo utaandaliwa muhtsari feki kuwa wanachi wamekubali kulipa sqm 1 TZS 4,000 jamaa watakusanya pesa watagawana. Haiingii akilini kabisa eti leo Bagamoyo na hususani Fukayosi ilivyojengeka eti leo wakafufue ranchi wakati ranchi kibao serikali imeshindwa kuziendesha.
 
usitetee upuuzi, KKKT miaka ya hivi karibuni limekua kanisa la ovyo sana. Mbey washaivuruga vipande vipande
Mkuu una hasira sana na KKKT. Mimi si mmoja wao ila huoni wapuuzi ni wale wanaovumilia uhovyo wake? Angalia vizuri nilichoandika
 
Wewe unaonekana una CHUKI KUBWA na KKKT

KKKT kwa ninavyowajua hawawezi kufanya uzembe kama huo, labda waliouziwa kuna terms hawakuzifuata vizuri
 
Mbona mi nshapewa mpaka hati yangu ya eka 5 sa itakuwaje ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…