Kasi ya wanandoa kutoka nje ya ndoa zao inatisha na kutishia uhai wa taasisi ya "NDOA"

Kasi ya wanandoa kutoka nje ya ndoa zao inatisha na kutishia uhai wa taasisi ya "NDOA"

UKISHAJUA VITU VIWILI BASI HUNA HAJA YA KUOA.

1.KUKINAI HASA KWA WANAUME( MWANADAMU AMEUMBWA KUKINAI)

2.MWANAMKE AMEUMBWA NA TAMAA YA KUTAKA VILIVYO BORA ZAIDI ( HYPERGAMY)

Kuchepuka haijaanza jana wala juzi ni swala kongwe kama ilivyo UKAHABA( UMALAYA).Acheni kujitesa huwezi kumlinda/ kumfuga huyo kiumbe mwenye akili zake timamu mliyekutana ukubwani.Furahia maisha acha masononeko.

TAFTENI HELA!!!TAFTENI HELA!!!Mwanaume kamili huwezi kumlinda mwanamke yeye ndo anatakiwa akulinde wewe dhidi ya vitoto vya elfu mbili, maana wewe unahela. Maskini na SIMPS ndo wanalinda wanawake zao!!

📌Kataa ndoa,ndoa ni utapeli!!
Upo sahihi kwa mtazamo wako. Nakubaliana na wewe baadhi ya mambo. Lakini nikwambie tu ukishakuwa mtu mzima kuelekea uzeeni unahitaji mwenza. Hasa kwa mwanaume...wanaume wengi wazee wanaoishi wenyewe wanatia huruma kwa kweli.
 
Upo sahihi kwa mtazamo wako. Nakubaliana na wewe baadhi ya mambo. Lakini nikwambie tu ukishakuwa mtu mzima kuelekea uzeeni unahitaji mwenza. Hasa kwa mwanaume...wanaume wengi wazee wanaoishi wenyewe wanatia huruma kwa kweli.
Kuhitaji mwenza maana yake ni kuwa muishi wawili kwa furaha,amani na maelewano....kuishi wawili kwa maudhi, kero na makasiriko ni jambo baya linaloweza kufupisha maisha yako.......

Takwimu zinaonyesha kuwa wanaume walio kwenye ndoa wana lifespan ndogo ukilinganisha na wale waliochagua kuwa single....na ufupi huo wa maisha unaletwa maradhi yasioambukizwa yanayosababishwa na wanawake.....

Ingawa sio jambo zuri kimaadili lakini vijana wameona unafuu ni kutafuta watoto na kutunza watoto wako huku kila mmoja akiangalia maisha yake.....

Yanini kutesana....
 
Kuhitaji mwenza maana yake ni kuwa muishi wawili kwa furaha,amani na maelewano....kuishi wawili kwa maudhi, kero na makasiriko ni jambo baya linaloweza kufupisha maisha yako.......

Takwimu zinaonyesha kuwa wanaume walio kwenye ndoa wana lifespan ndogo ukilinganisha na wale waliochagua kuwa single....na ufupi huo wa maisha unaletwa maradhi yasioambukizwa yanayosababishwa na wanawake.....

Ingawa sio jambo zuri kimaadili lakini vijana wameona unafuu ni kutafuta watoto na kutunza watoto wako huku kila mmoja akiangalia maisha yake.....

Yanini kutesana....
Hizo takwimu hazipo sahihi. Life span ya mwanaume ni ndogo awe ameoa au yupo single ni yale yake. Ukitaka kujua angalia wanaume waliofiwa na wake zao hawachukui muda wanakufa. Sio kama mwanamke anaweza akadumu miaka mingi zaidi.
 
Thamani ya ndoa imeshuka sana miongoni mwa wanandoa wenyewe licha ya kuwa ndoa bado zinafungwa sana tu ila hazidumu. Wanandoa wanatoka nje ya ndoa huku mtu anajua ana mwenza wake. Mke wa mtu akitongozwa anatoa uroda tu bila kukataa, mume wa mtu naye anatongoza nje ya ndoa huku ana mke nyumbani
 
Hizo takwimu hazipo sahihi. Life span ya mwanaume ni ndogo awe ameoa au yupo single ni yale yake. Ukitaka kujua angalia wanaume waliofiwa na wake zao hawachukui muda wanakufa. Sio kama mwanamke anaweza akadumu miaka mingi zaidi.
Sawa
 
Habari za muda huu waungwana wa hapa jukwaani.

Sijui ni mimi peke yangu tu ama ni macho ya wengi pia yanatazama kama nitazamavo mimi....

Nimekuwa nikishuhudia matukio kadhaa ya kustaajabisha, kushangaa lakini pia yana hudhunisha kuhusu matukio ya wanandoa kutoka nje ya na vile vile namna ambavyo walengwa wanavyochukulia kuwa ni hali ya kawaida kabisa..

Katika mikusanyiko ya watu na vijiwe vya kahawa nasikia baadhi ya watu wakitoa mitazamo yao kuhusu jambo hilo yenye kushangaza kuogofya kwenye masikio ya waungwana..

Jamaa anasema..." siku hizi hakuna mwanamke wa peke yako kaka, kikubwa kuheshimiana tu afanye nisije Tu"

Dada mmoja naye anasema kuwa.."Hakuna mwanaume asiyetoka na mwanamke nje ya mkewe... kikubwa heshima tu akafanyie huko uchafu wake"

Yaani imefikia hatua mpaka wanandoa wanajua kabisa kuwa kwenye muunganiko huu kuna wengine wa ziada na nafsi zao zimeridhika na hilo

Thamani ya muunganiko mtakatifu wa ndoa iko wapi?

Dhumuni hasa la ndoa liko wapi ikiwa mtu anaweza kuyafanya machafu yaliyomsukuma kufunga ndoa ili apate stara?

Ni heshima ipi inayozungumziwa na hawa wanandoa Hali ya kuwa unajua fika kuwa unafanya lile lisilompendeza mwenzi wako?

Muendelezo wa matendo machafu haya yanapelekea vijana kutoona umuhimu wa kuoa ikiwa anawaona wanandoa wanafanya yale wanayoyafanya wao.

Tumefikaje huku..?
Changamoto za ndoa sio jambo jipya humu duniani! Tena changamoto hazizuii watu kuendelea ku-enjoy kwenye ndoa zao. Ndiposa wanasema, tamu ya peremende Ni mate yako.

Nionavyo, mambo yote yanayohusisha mwanadamu yanafanana Na coin. Kwamba Kuna kichwa na mkia, yaani kuna raha na karaha ya kila jambo.
 
Mimi mke wangu sijawahi kumuhisi anatoka nje ya ndoa wala mimi sitoki nje ya ndoa yangu naishi kiapo changu.

Hiyo nadhani ni hulka ya mtu na mtu hasa wale wasiozipa akili zao tuition ya kuwaza mazuri na mabaya yatakayotokea baada ya matendo hayo
Wachepukaji watakubishia mpaka jasho la meno liwatoke
 
Umuhimu wa “Ndoa” unazidi kupoteza ladha😜. Hasa ukizingatia Michepuko ina Nguvu za kimataifa,ina Silaha kama zote marekani ikalale 😅😜
 
Hakuna kipya,Tangy enzi za pharao watu walikuwa wanapiga shoo za ugenini...case study mke wa Potifa na Yusuf
 
Umuhimu wa “Ndoa” unazidi kupoteza ladha😜. Hasa ukizingatia Michepuko ina Nguvu za kimataifa,ina Silaha kama zote marekani ikalale 😅😜
Umei-over rate sana michepuko madam!michepuko haina nguvu hizo ndio maana inafichwa kama bangi🥲
 
Ni kawaida ya wazinzi kudhani kila mtu anawaza kama wao anatenda kama wao.
Ndugu yangu
Kumpata mwenza aliyetulizana kwa nyakati hizi ni BARAKA, NEEMA na BAHATI kubwa.....hivyo unapaswa kumshukuru mola wako kwa hiyo lakini usiongee hadharani kwa watu Kwa kuvimba kwani mwanadamu hajakamilisha na anaweza kuteleza muda wowote ukaingia aibu kwa maneno yako......

Pengine watu wanayajua ya mkeo ambayo wewe huyajui na kwa heshima yako wameamua kumsitiri ili kudumisha amani nyumbani kwenu......

Usiongee ukamaliza ndugu.......watu hubadilika muda na wakati wowote......
 
Ndugu yangu
Kumpata mwenza aliyetulizana kwa nyakati hizi ni BARAKA, NEEMA na BAHATI kubwa.....hivyo unapaswa kumshukuru mola wako kwa hiyo lakini usiongee hadharani kwa watu Kwa kuvimba kwani mwanadamu hajakamilisha na anaweza kuteleza muda wowote ukaingia aibu kwa maneno yako......

Pengine watu wanayajua ya mkeo ambayo wewe huyajui na kwa heshima yako wameamua kumsitiri ili kudumisha amani nyumbani kwenu......

Usiongee ukamaliza ndugu.......watu hubadilika muda na wakati wowote......
Nlikuwa nataka nifike nae huko huko kanikimbia njiani binadam aaminiki hata uyo anaemuamin uwenda kamzid mbinu ovu ila muda haujafika tu na uzuri siku yakumwagika atakuwa shahid wa kwanz yey mwenyw atakumbuka kujimambafayi kwake.
 
Mumeacha Sheria Za Mungu za kuwavurumishia mawe mpaka wakate kamba hao wazinifu walioko kwenye ndoa. Anza kuwadunda mawe uone kama heshima ya ndoa haitaimarika.
Hiyo sheria ya Mungu labda usubiri ukifa ukaitekeleze mbinguni maana humu duniani utajikuta upo sehemu mbaya na mamlaka za kidunia.....
 
Habari za muda huu waungwana wa hapa jukwaani.

Sijui ni mimi peke yangu tu ama ni macho ya wengi pia yanatazama kama nitazamavo mimi....

Nimekuwa nikishuhudia matukio kadhaa ya kustaajabisha, kushangaa lakini pia yana hudhunisha kuhusu matukio ya wanandoa kutoka nje ya na vile vile namna ambavyo walengwa wanavyochukulia kuwa ni hali ya kawaida kabisa..

Katika mikusanyiko ya watu na vijiwe vya kahawa nasikia baadhi ya watu wakitoa mitazamo yao kuhusu jambo hilo yenye kushangaza kuogofya kwenye masikio ya waungwana..

Jamaa anasema..." siku hizi hakuna mwanamke wa peke yako kaka, kikubwa kuheshimiana tu afanye nisije Tu"

Dada mmoja naye anasema kuwa.."Hakuna mwanaume asiyetoka na mwanamke nje ya mkewe... kikubwa heshima tu akafanyie huko uchafu wake"

Yaani imefikia hatua mpaka wanandoa wanajua kabisa kuwa kwenye muunganiko huu kuna wengine wa ziada na nafsi zao zimeridhika na hilo

Thamani ya muunganiko mtakatifu wa ndoa iko wapi?

Dhumuni hasa la ndoa liko wapi ikiwa mtu anaweza kuyafanya machafu yaliyomsukuma kufunga ndoa ili apate stara?

Ni heshima ipi inayozungumziwa na hawa wanandoa Hali ya kuwa unajua fika kuwa unafanya lile lisilompendeza mwenzi wako?

Muendelezo wa matendo machafu haya yanapelekea vijana kutoona umuhimu wa kuoa ikiwa anawaona wanandoa wanafanya yale wanayoyafanya wao.

Tumefikaje huku..?
Mkuu kwanza habar za miaka tele.
Katika hili dunia imechanganyikiwa na waliomo ndani yake wamevurugwa. Mmomonyoko wa maadili ndio umetawala. Uzinzi sio suala la kuogofya Tena.
Na ukimhoji anayechepuka kuwa kwanini anafanya hvyo hana jibu la msingi la kukupa ni kwamba ameamua tu
 
Mkuu kwanza habar za miaka tele.
Katika hili dunia imechanganyikiwa na waliomo ndani yake wamevurugwa. Mmomonyoko wa maadili ndio umetawala. Uzinzi sio suala la kuogofya Tena.
Na ukimhoji anayechepuka kuwa kwanini anafanya hvyo hana jibu la msingi la kukupa ni kwamba ameamua tu
Njema mkuu......

Kwa kweli hali inatisha na tuendapo ndio kubaya zaidi ya sasa.....
 
Mumeacha Sheria Za Mungu za kuwavurumishia mawe mpaka wakate kamba hao wazinifu walioko kwenye ndoa. Anza kuwadunda mawe uone kama heshima ya ndoa haitaimarika.
Mungu yupi ulomkudia na alosema mzinifu aligwe mawe wafe?
 
Ndoa za siku hizi fashion na kizungumkuti

Thamani ya ndoa kama zamani hakuna kabisa[emoji3577]
 
CHAPA ILALE kama huwezi kuvumilia kuchapiwa!!!

Unaogopa kuishi mwenyewe huo ushamba wenu ndio mnaanza kufa na mawazo kisa kulazimisha kuishi na washenzi au unajikuta unafanya mauaji wakati ukiishi mwenyewe unachapa unasogeza unachapa mwendo mdundo. Tena kama hutaki JAM UNAENDA UNAFUNGA KIZAZI🤗

Hutapata kesi za kijanga jinga mara dawati la jinsia mara sijui mahakamani mnakabana mashati kuhusu CHILD SUPPORT.Wewe mtu akikubambikia straight mbaenda mahakani na vithibitisho na daktari anatoa ushahidi kuwa wewe unatumia uzazi wa mpango🤗🤗🤗

Ni humu tuuu kwanza faida ya uzazi iko wapi watu wanakufa kila siku huko Gaza na pia kuna majanga ya kidunia kila uchwao so wewe kuzaa au kutokuzaa ni nothing huongezi wala hupunguzi chochote dunia tiyari iko balanced ,ukichoka KUZICHAPA unatulia unasubiri kufa kwa amani!!!

📌Kataa ndoa,ndoa ni utapeli!!!
Umetisha Sana mkuu 😂
 
Kwasababu ukitazama kwa jicho lingine tafsiri ya ndoa kwangu naweza kusema ni challenge ya watu wawili kupambana kuweza kuishinda asili.

Asili gani hapa nayoizungumzia.

Maisha ya binadamu yamezungukwa na mambo mengi na katika hayo mambo yapo ambayo hayatoki nje yake bali yapo ndani yake kwa maana ni asili ambayo inaishi ndani yake.

Na moja ya hiyo asili ni "kinai"

Kukinai ni jambo la kiasili la mtu kupunguza matamanio dhidi ya jambo fulani.

Kwasababu mahusiano ni kitu ambacho kinaishi kwenye circle ya hisia, hisia ambazo zinaweza kuwa affected na "Kinai" basi hapa ndio tunaweza kuona outcome ya mambo mengi ikiwemo cheating, Talaka nk.

Kinai inaweza kutokea kwa mazingira mengi lakini ile iliyo kuu mara nyingi hutokea baada ya mtu kukizoea sana kitu.

Ukikizoea sana kitu automatically unapunguza hisia za kimshangao na ule msisimko unapotea kabisa.

Ukimpenda sana mtu akakuvutia na hisia zako zitakuwa juu sana hususan pale ambapo unakuwa na shauku ya kutaka kufanya jambo fulani litaloweza kustawisha upendo wako kwake halafu hiyo nafasi ikawa haipatikani kirahisi.

Mfano siku ya kwanza kumzimikia manzi unakuwa na hisia kali sana na pale ambapo unamvizia ili uteme sumu halafu ukakutana na mazingira yake kuwa ni geti kali na ulinzi mwingi.

Hapo ndio hisia zinazidi kuwa juu kwasababu ile desire ya kutaka kumuona halafu nafasi hiyo hauipati ndio inayochochea hisia zizidi kupanda.

Hii ndio moment ambayo wengine wanasema hawawezi kuishi bila hao wenza wanaowafukuzia.

Lakini suddenly ukamuoa, na sasa ukawa unapata airtime ya kutosha ya kumuona kila siku na sio tu hivyo mkawa mnala kila kitanda kimoja, mnazagabuana na vitu kama hivyo.

Baada ya miezi michache mbele ukikaa chini utagundua zile hisia ambazo ulikuwa nazo kipindi chenu cha dating ni tofauti na hizi hisia ulizonazo baada ya miezi kadhaa ya ndoa.

Kipindi chenu cha dating inawezekana alikuwa anaku turn on kwa tabasamu lake tu. Lakini saizi hata akuvulie unaweza usidise.

Umemchoka.

Hata awe Beyonce au Miss world utamchoka tu na kuna time unaweza ukawa unajiona mjinga ukikumbuka kipindi unamfukuzia uliwahi kumwambia upo tayari kufa kwa ajili yake.

Ukifikia hatua ya kukinai utajiona mjinga ukikumbuka kipindi unamfukuzia uliwahi kukosana na rafiki zako wa tangu utotoni kisa yeye.

Ukimchoka ndio kinai yenyewe hiyo.

Kwa kiwango kipi? Hii SI Unit ya kiwango ndio maana halisi ya ndoa.

Wapo waliokinai ila wakaweza kutulia kwenye ndoa zao ili kutunza maadili ya ndoa na kiapo.

Wapo waliokinai wakashindwa kuendelea na mahusiano ambayo kila mmoja hana hisia na mwenzake hivyo wakaafikiana kupeana talaka. (Na muda mrefu wa talaka ambao watakuwa separated unaweza ku restore hisia zao tena)

Na hao wengine ndio hao ambao wana cheat.
Hakika umeeleza vizuri Sana mkuu
 
Back
Top Bottom