Katazo la shule kutoendelea na masomo wakati wa likizo ni la kitoto sana. Pia likizo ndefu moja ifutwe

Kupumzika kuwe na kiasi. Unafahamu kuwa mtoto akisoma siku 180 kwa mwaka maana yake anasoma nusu mwaka na nusu mwaka anapumzika? Uliona wapi mtu anapumzika nusu mwaka!!?
Hizo hesabu zako umefanyafanyaje, Likizo hii waliyopo sahivi wanakaa wiki km 5 tu, hiyo ni siku km 35 tu. Mwezi wa 12 wakizidi sana ni wiki 6 ambayo ni siku 42, jumla siku 77, wiki 11 tu. Hizo siku 180 umezikokotoa vipi? Acheni upotoshaji na udanganyifu kwa maslahi yenu
 
Wewe huna akili unadhani Mwalimu ana mshahara ni mdogo ?? Kwa taarifa Mwalimu ana mshahara mzuri Sana kama hutaki acha
Mbona umepanic hivi mwalimu mwenye kujitambua kweli anaweza lalamika kwanini wanafunzi wanafunga shule wanaolalamika ni wale wanaopenda kukaaa shule
 
Watoto wa tz wanapumzika sana. Wanasoma siku chache sana kwa mwaka ukilinganisha na nchi zilizotuacha mbali kiuchumi.
Toa mfano wa hizo nchi

Ukiongea onesha mfano.

Marekani wanasoma siku 160-180
Finland wanasoma siku 190

Wanasoma siku 5 tu za wiki

Kule hawakaririshi.

Tanzania napo hutakiwi zidi siku 194
 
Ahahah
Huyu ni mwalimu mwenye mtindio wa ubongo
 
Kuna shule moja ya kata hapa mbeya mjini Mwl yupo slow sana kufundisha, kipindi cha likizo anang'ang'ana watoto wasifunge, wakati huu ndo mda wa kufanya shughuli zake zingine
 
Vipi kuhusu issue ya kubadili mazingira kurudi kwao?

Naongea hivyo kwani mimi nlisoma shule hizi za bweni za serikali.
Na bahati mbaya hiko chakula chake mkuu.. Ziache hizo likizo tu mkuu, tena ikibidi hata ziongezwe.

Ni magereza yale

Vipi kuhusu issue ya kubadili mazingira kurudi kwao?

Naongea hivyo kwani mimi nlisoma shule hizi za bweni za serikali.
Na bahati mbaya hiko chakula chake mkuu.. Ziache hizo likizo tu mkuu, tena ikibidi hata ziongezwe.

Ni magereza yale
Tatizo la chakula litatuliwe la chakula. Wengine kwao hawali kabisa, afadhali shule wana uhakika wa kula.
 
Umelinganisha na nchi gani?

Unadhani hatuna ndg ambao watoto wanahitaji kuwatembelea na kujumuika kama njia ya kujenga upendo kwenye ukoo.
Angalia nchi zinazofanya vizuri kwenye elimu. Taiwan, Japan, Israeli na South Korea.
 
Mwalimu naona unatetea ulaji wako, punguza njaa
 
Hivi sister kwa akili yako ni sahihi mwanafunzi kutumka nusu mwaia kupumzika?
 
Mwaka nzima watoto wanakalili kuchora panzi na kusoma historia za uongo
Upuuzi tu
Ingekua wanafundishwa mambo ya maana namna ya kuyakabili maisha baada ya kutoka shule ingekua sawa
Ila kwa huu upuuzi wa mitaala yetu hakuna huo umuhimu
 
Pamoja na kuwa kuna walimu wanaojitambua ila ukweli ni kwamba walimu wengi ni vichwa maji

Kweli mtu unalilia likizo ipunguzwe?? badala ya kulilia mshahara na marupurupu??
Wewe kama mama mwenye watoto, unafikiri ni sawa kwa wanao kusoma siku 180 kwa mwaka na kupumzika zingine 180?
 
Juma mosi na jumapili siku 104 kwa mwaka. Bado likizo za mwezi wa tisa na tatu. Siku zote hizi mwanafunzi kapumzika.
 
Si bure! Una matatizo katika uwezo wako wa kuchanganua mambo.
 
Tatizo la chakula litatuliwe la chakula. Wengine kwao hawali kabisa, afadhali shule wana uhakika wa kula.
Ni kweli,

Lakini unaongelea watu 2/100.
Nyumbani ni nyumbani mkuu.

Likizo ziheshimiwe mkuu
 
Nimemuelewa jamaa anajumlisha na weekendi zote, maana weekend hazisomwi pia.

Lakini isue ya likizo ziheshimiwe.
Huwezi ukamcremisha mtu awe anawaza kusoma tu bila mapumziko marefu.
Awafeel pia watu wa shule za bweni
 
Ndugu sikubaliani nawe, naomba ufanye uchunguzi zaidi.

Nikupe taarifa:-

1. Education (learning) and schooling are two different things.

2. Kusoma muda mrefu au kuwa na vipindi vingi au masomo mengi au kukaa shule muda mrefu SIO ELIMU.

3. Kupumzika na kucheza kwa mwanafunzi ni muhimu kama ilivyo kusoma.
Likizo ni muhimu kwa wanafunzi na walimu pia.

4. Mitihani sio kigezo cha kupima Elimu wala ubora wa elimu. Kwa sasa watoto wanafundishwa kukariri na kujibu mitihani; hawapewi elimu wala kujenga ubunifu, maarifa na nidhamu.

5. Tanzania ni moja ya nchi zenye masomo mengi, vipindi vingi, mitihani mingi na kiwango cha chini cha elimu.

Kuna Rasimu Mpya ya Mitaala ya elimu itakayoanza mwakani, hiyo itajaribu kupunguza baadhi ya hizi kero.
Utafute huo mtaala uupitie zaidi.
 
Points nyingi umeweka zina maana sana hapa. Lakini huoni kuwa kupumzika kwa miezi sita katika mwaka ni muda mrefu sana? Maana tafiti zimeonyesha kuwa kunauhusiano mkubwa wa kusoma muda mrefu na "Uelewa" na hata kufanikiwa kimasomo, kama kufika chuo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…