Kati mamba, simba na chatu yupi mrahisi kuokoka tukikutana naye?

Simba kama ni dume jitahidi kumnyemelea Kisha mpige dole la kati kwenye sungilo/puru lazima atoke mbio mambo ya LGBQ hapendi, Kwa upande wa mamba jitahidi upapase jicho lake lazima akuache
wewe jamaa hivi mamba ushawahi kukutana nae uso kwa uso?

Mamba mkubwa ana uzito wa kilogram 800 hadi 1000

Huku kwetu mwaka jana alimuua jamaa yetu wakaitwa wazee kutoka Ukerewe wakamuwekea mtego(kuna ndoano mahususi kwa ajili ya mamba) akanasa, aliliwa kata nzima

Ule mdude una nguvu mno
 
wewe ulichoandika ni ukweli 1000% mimi mpaka wa leo nipo kisiwani

Mwaka jana wameua watu wengi sana mixer mbwa na ng'ombe

Wameacha majeruhi wengi sana

Hao viumbe ni hatari

Wao hawali sehemu ngumu wanakula kuanzia tumboni mpaka kwenye sehemu za siri na matako, kichwa na miguu wanatunza

Na mamba hali peke yake lazima akupeleke kwenye familia yake ili wasaidiane kukata nyama

Mungu fundi
 
sasa hivi wamezagaa ziwa Victoria wengi mno, halafu ni madude balaa sio tudogo
 
Ukikutana na simba na hilo panga lako uanze kujikata mwenye vipande vidogo vya nyama uwe unamrumshia mpaka pale mwenyewe atakapoamua aanze kukutafuna mwenyewe
 
Tiger hana ukaribu na Chui ana ukaribu na Simba hata kimwil wanauzito unaokaribiana Chui ni mdogo.

Simba anaweza hata kumpanda Tiger na kuzaa Mtoto aitwae Liger👇

View attachment 2929283
Jifunze kusoma kwa ufahamu. Jifunze lugha yako ya kiswahili. TIGER kwa Kiswahili anaitwa Chui Milia na sio hilo jina lako, Umeelewa?.
 
Hivi umkazie Simba macho wakati hujawahi kuexperience kuwa nae karibu unadhani ni rahisi ??

Wakati huo unamkazia macho anaunguruma muungurumo mkali kama piki piki za BMW utabaki salama kaka ?

Lazima ujikojolee ama kupoo kabisa na machozi yatakutoka bila kutarajia
 
Jifunze kusoma kwa ufahamu. Jifunze lugha yako ya kiswahili. TIGER kwa Kiswahili anaitwa Chui Milia na sio hilo jina lako, Umeelewa?.
JF Hili ni Jukwaa la kuongezeana maarifa na sio kulazimishana watu waliotunga hilo jina walikuwa na uelewa mdogo.
 
Kuna mtu aliwahi pigwa "kofi" na simba kuanzia kwenye kwapa hadi matakoni ikabakia mifupa tu
 
Nasikia kanyegere kavulana kana wivu kiasi kwamba kakimwona binadamu yupo nyuma ya nyegere jike kanahisi labda binadamu anataka penzi kwa demu wake, katakufukuza kweli.
Sijui ni kweli au stori!
Hiyo ni kama pie27
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…