JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 7,808
- 16,972
Tangu lini DED akateuliwa na waziriDC anateuliwa na Rais wa Jamhuri lakini DED anateuliwa na Waziri wa TAMISEMI. DC anakazi zake na DED anakazi zake, hawaingiliani.
Tayari umejibu maana Halmashauri ipo ndani ya WilayaHakuna wala hawahusiani kabisa.
DAS ni kiongozi wa Wilaya DED ni mtendaji wa Halmashauri!
Zinashindwa kwa sababu ya siasa uchwara za ccm.Una haki ya kuchanganyikiwa mkuu,hata mimi huwa nachanyikiwa,lakini naona kama wako at par,ingawa wakati mwingine naona kwa vile DAS ndiye kiongozi wa watumishi wote Wilayani,basi DED yuko chini ya DAS.Inachanganya kwa kweli.
Mimi huwa nadhani kuna haja ya kufuta mfumo wa kuwa na Halimashauri, ili kuondoa huo mkanganyiko ambao kiukweli unaleta misuguano na mikanganyiko isiyo ya lazima na hivyo kukwamisha utendaji kwa ujumla.Hivi kwa nini tusiwe na DC na DAS tu na chini ya DAS kukawa na idara mbali mbali ambazo zitashuhulikia issues za Willaya?Huu mfumo wa kuwa na Halimashauri unaongeza tu bureaucracy,matumizi ya fedha yasiyo ya lazima,ugumu wa udhibibiti na hivyo kuongeza uwezekano wa upigaji.Kwa ujumla mfumo huu uko inefficient.
Binafsi sioni faida za msingi za Halimashauri,infact naona kama they are just a liability to the government.
Halimashauri zetu zimeshindwa kabisa ku-meet expectations za Watanzania.
Kwa dhana ya "Wilaya" dhidi ya "halmashauri," mimi nadhani DAS yuko juu kiitifaki kuliko DED kwa mchanganuo ufuatao:-
DAS ni mtumishi wa wilaya. (Wilaya moja, DAS mmoja).
DED ni mtumishi wa halmashauri (kwenye Wilaya moja kunaweza kuwa na halmashauri zaidi ya moja).
Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba "Wilaya moja, DAS mmoja".
Na pia tunaweza kusema, "Wilaya moja halmashauri moja au mbili na hivyo DED mmoja au wawili"
Katika mazingira haya simuoni DED akiwa juu ya DAS.
Hili neno karani si zuri kulitumia kwa sasa. Enzi za ukoloni karani alikuwa MTU muhimu sana BA,akitesa wenzake kwa maslahi ya wakoloni. Lkn baada ya Uhuru enzi za ushirika kukawepo makarani walioiba sana fedha za wakulima kwa wananchi wenzetu. Noma sana Hawa.Ninavyojua hapo mwenye hela na budget ni DED huyo DAS anaishia kuwa kalani tu!
Sababu kubwa inayozifanya Halimashauri zetu zishindwe kutimiza majukumu yao ni matumizi mabaya ya resources walizo nazo, ikiwa pamoja na fedha.Siasa sio sababu mkuu.Inaelekea wewe huzifahamu Halimashauri,ni wapigaji kweli kweli.Tena hata afadhali sasa,wanaogopa kidooogo.Kwenye awamu ya tatu na nne ndio ilikuwa mbaya zaidi,wengine hata wanadiriki kusema upigaji ni sehemu ya ajira zao! Funny,upigaji ni sehemu ya ajira?Yaani ulipoajiriwa uliambiwa upigaji ni sehemu ya majukumu yako?Ebo.Zinashindwa kwa sababu ya siasa uchwara za ccm.
Mwanza kabla ya kuundwa manispaa ya ilemela, kulikuwa na mkurugenzi mmoja wa halmashauri ya jiji iliyounganisha wilaya nyamagana na ilemela ambapo madas walikuwa wawili. So hoja yako haina mashiko
Nilikosea, DED anateuliwa na Rais baada ya kushauriana na commission. Kifungu cha 22 Government Service Act, 1982.Tangu lini DED akateuliwa na waziri
Asante mkuu kwa maelezo yako.Kifungu cha 16 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa kinamtambua DAS kama principal adviser (yaani mshauri mkuu) wa DC.
Aisee...mimi nilidhani vyeo hivi vilishafutwa.Maafisa Taarafa
Ukimuingizia DED pia shughuli za ulinzi na Usalama...kazi za maendeleo hazitafanyika.halafu hiki cheo kinacho itwa Sijui mkuu wa wilaya sijui mkoa. vifutiliwe mbali havina maana zaid ya ulaji tu
Bado vipo MkuuAisee...mimi nilidhani vyeo hivi vilishafutwa.
DAS wa wilaya ya nyamagana na DAS wa wilaya ya ilemela. Tambua halmashauri ya jiji la mwanza iliundwa na wilaya mbili tajwa hapo juu na baraza la madiwani lilikuwa moja, meya mmoja na mkurugenzi mmoja.Kama kulikua hakuna kitu kinachoitwa Ilemela na Nyamagana vyenye hadhi ya manispaa, je hao maDAS wawili walikua ni DAS wa wapi/nini ?
Mbona shughuli zao nyakati hizi wala hazionekani. Kipindi cha Nyuma nadhani kuanzia miaka ya tisini kurudi nyuma, ukisikia Katibu Tarafa anakuja kijijini ujue ni 'kimuemue'!!Bado vipo Mkuu
DAS ni mfanyakazi wa mkuu wa Mkoa.Asante mkuu kwa maelezo yako.
Nimesoma neno kwa neno post zote toka post ya kwanza ya uzi huu nikitafuta majukumu ya DAS.
Mpaka hapa nimepata majukumu mawili tu. Kuwa DAS 1) ni Mshauri mkuu wa DC 2) Ni mkuu wa watumishi wote wa Wilaya
Ila hilo jukumu la pili limenichanganya...! Atakuwaje mkuu wa watumishi wa wilaya wakati hawawajibiki kwake ?
Kama kuna majukumu mengine naomba kufahamishwa tena kwa maelezo ya kina.