Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

DED mkubwa japokuwa sio bosi wa DAS, Ila ni mkubwa kwa kuwa pale wilayani DED hana bosi wake Ila yeye ndo top, Ila DAS pale wilayani ana bosi wake ambaye ni DC.
 
Mbona shughuli zao nyakati hizi wala hazionekani. Kipindi cha Nyuma nadhani kuanzia miaka ya tisini kurudi nyuma, ukisikia Katibu Tarafa anakuja kijijini ujue ni 'kimuemue'!!
Kwakweli hawana kazi ya kueleweka kwani Maafisa Watendaji wa kata wanatosha. Unajua kipindi kile cha chama kimoja maagizo au utekelezaji ulikuwa unapitia kW DC. Sasa hivi unapitia kwa DED anashusha kwa WEO na Village Executive Officers.

Hawa WEOs ni wasomi. Qualification zao ni diploma na baadhi ni degree holders. VEOs ni certificate. Kwa hiyo wanauwezo wa kumudu kazi zao na hawahitaji msaada wa Afisa Tarafa.

Ikumbukwe kuwa Afisa Tarafa anareport kwa DAS na Afisa Mtendaji wa kata (WEO) anaripoti kwa DED. Ila baadhi ya council wanawashirikisha Maafisa taarifa kwenye vikao vya Halmashauri.
 
DED mkubwa japokuwa sio bosi wa RAS, Ila ni mkubwa kwa kuwa pale wilayani DED hana bosi wake Ila yeye ndo top, Ila RAS pale wilayani ana bosi wake ambaye ni DC.
Mkuu nafikiri unamaanisha DAS. RAS ni Boss wa watumishi wote katika Mkoa including wa mashirika na Taasisi zote za Serikali na za umma.
 
Kwenye awamu hii wote wameteuliwa na rais.
Zamani TAMISEMI ilipokuwa ofisi ya waziri mkuu ndio ilikuwa DED anateuliwa na PM.

Siku hizi tamisemi IPO ofisi ya rais.

Zipo wilaya zenye halmashauri zaidi ya moja, DED -2, but DAS mmoja.

Wana majukumu tofauti, at one point DED anareport kwa DAS.
DAS anahudhuria vikao vya CMT kama mshauri, pia anahudhuria vikao vya baraza LA madiwani but hawajibiki kwao.

DAS line yake ya utendaji wa kila Siku iko sana kwa maafisa tarafa na wenyeviti wa vijiji/ vitongoji na mitaa , vyombo vyote vya ulinzi na usalama wilayani. He can surmon all government agencies in the district ( TRA,tanesco na taasisi nyingine zote kutoka wizara mbalimbali zilizo wilayani kwake) wakati DED anadeal zaidi na watumishi wa idara mbalimbali wakiwemo watendaji kata/ vijiji + madiwani. Na mamlaka ya DED yanaishia kwenye taasisi zilizo chini ya tamisemi tu.
Kisiasa imedeatelty juu ya DED yupo mwenyekiti wa halmashauri/ meya wakati kwa DAS yupo DC.

DAS yupo kidola zaidi wakati DED yuko kiutumishi/ umma zaidi.

DED ana nafasi kubwa ya kufa akiwa tajiri wakati DAS ana nafasi kubwa sana ya kufa maskini.
Hakuna wilaya zenye halmashauri mbili, bali wilaya yenye majimbo mawili
 
Kwa dhana ya "Wilaya" dhidi ya "halmashauri," mimi nadhani DAS yuko juu kiitifaki kuliko DED kwa mchanganuo ufuatao:-

DAS ni mtumishi wa wilaya. (Wilaya moja, DAS mmoja).

DED ni mtumishi wa halmashauri (kwenye Wilaya moja kunaweza kuwa na halmashauri zaidi ya moja).

Kwa maana hiyo tunaweza kusema kwamba "Wilaya moja, DAS mmoja".

Na pia tunaweza kusema, "Wilaya moja halmashauri moja au mbili na hivyo DED mmoja au wawili"

Katika mazingira haya simuoni DED akiwa juu ya DAS.
Wilaya gani ina halmashauri mbili na ded wawili?
 
DAS ni mfanyakazi wa mkuu wa Mkoa.
DC ni mfanyakazi wa mkuu wa Mkoa.
RAS ni mfanyakazi wa mkuu wa mkoa.
DED ni mfanyakazi wa TAMISEMI ambaye yupo chini ya Halmashauri ya wilaya/manispaa/mji (council as a whole).
DED hawezi kuwa chini ya DAS wala DAS kuwa chini ya DED.
DED hawezi hata kuwa chini ya DC, wala RC au RAS. Hawamuhusu kihivyo, bali katika kuwapa ripoti.
DED anaweza kumweka mtu selo kama DC anavyoweza au RC anavyoweza. Haingiliani na DAS,
Rc, RAS zipo chini ya wizara gani? Sio tamisemi? (Tawala za mikoa na serikali za mitaa?)
Niliona Jafo akiagiza Ma RC.

Pia mbona nilishaona RC akimsimamisha ded kwa uchunguzi?
 
DED mkubwa japokuwa sio bosi wa RAS, Ila ni mkubwa kwa kuwa pale wilayani DED hana bosi wake Ila yeye ndo top, Ila RAS pale wilayani ana bosi wake ambaye ni DC.
Dc sio boss wa RAS,
RAS ni mkubwa sana kuliko DC
 
DED na DAS wanapoteuliwa wote kwa pamoja na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara.?
 
Nimepata mkanganyiko kujua nani bosi wa mwenzake kati ya DAS na. DED naomba kuelemishwa mwenye kujua.
Leo umeamua kuja kivingine Moderators wakakugundua!😀😀😀

Kwa nini una obsession sana na issue ya DED na DAS?

1533722893816.png

DED na DAS wanapoteuliwa wote kwa pamoja na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara.?
 
DAS wa wilaya ya nyamagana na DAS wa wilaya ya ilemela. Tambua halmashauri ya jiji la mwanza iliundwa na wilaya mbili tajwa hapo juu na baraza la madiwani lilikuwa moja, meya mmoja na mkurugenzi mmoja.

Basi hiyo ni special case mkuu WILAYA MBILI kuwa na HALMASHAURI moja, BARAZA LA MADIWANI moja na MKURUGENZI kwa maana ya DED mmoja. Japokua kwenye pointi ya DAS naona bado tupo pamoja kwa maana ya kwamba DAS ni wa wilaya (wilaya moja, DAS mmoja) kama ambavyo idadi ya wilaya mbili ulizozitaja inavyokwenda sawa na idadi ya maDAS uliyoitaja pia.
 
Wilaya gani ina halmashauri mbili na ded wawili?

Zipo nyingi tu mkuu, ila kwa kukujibu tu ngoja nitumie Mkoa wa Mtwara kwa mujibu wa takwimu za wizara ya TAMISEMI za leo hii tarehe 08-08-2018 ni kama ifuatavyo:-

Takwimu za Haraka
  • Idadi ya Watu = 1,356,800
  • Ukubwa wa Eneo = 16,720 (Km square)
  • Eneo la Kilimo = Hekta 1,400,000
  • Idadi ya Wilaya = 5
  • Idadi ya Halmashauri = 9
  • Idadi ya vyuo Vikuu = 02
  • Idadi ya Shule za Sekondari = 147
Soma hapo kwenye idadi ya wilaya (5) dhidi ya idadi ya halmashauri (9).
Na moja kati ya wilaya zenye halmashauri zaidi ya moja mkoani Mtwara ni Wilaya ya Mtwara (halmashauri ya manisapaa ya Mtwara almaarufu kama Mikindani na halmashauri ya mtwara vijijini) pia wilaya ya Masasi inazo halmashauri mbili.
 
Zipo nyingi tu mkuu, ila kwa kukujibu tu ngoja nitumie Mkoa wa Mtwara kwa mujibu wa takwimu za wizara ya TAMISEMI za leo hii tarehe 08-08-2018 ni kama ifuatavyo:-

Takwimu za Haraka
  • Idadi ya Watu = 1,356,800
  • Ukubwa wa Eneo = 16,720 (Km square)
  • Eneo la Kilimo = Hekta 1,400,000
  • Idadi ya Wilaya = 5
  • Idadi ya Halmashauri = 9
  • Idadi ya vyuo Vikuu = 02
  • Idadi ya Shule za Sekondari = 147
Soma hapo kwenye idadi ya wilaya (5) dhidi ya idadi ya halmashauri (9).
Na moja kati ya wilaya zenye halmashauri zaidi ya moja mkoani Mtwara ni Wilaya ya Mtwara (halmashauri ya manisapaa ya Mtwara almaarufu kama Mikindani na halmashauri ya mtwara vijijini) pia wilaya ya Masasi inazo halmashauri mbili.
Nisaidie link mkuu!!
Idadi ya madc ni 5 pia?
 
DED na DAS wanapoteuliwa na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara kumzidi mwenzake.?
 
Back
Top Bottom