Kati ya mahakama na benki ni ipi ina wajibu wa kumkabidhi msimamizi wa mirathi pesa za marehemu alizoacha benki au SimuPesa?

Kati ya mahakama na benki ni ipi ina wajibu wa kumkabidhi msimamizi wa mirathi pesa za marehemu alizoacha benki au SimuPesa?

Nilikwenda juzi kufuatilia BANK YA POSTA wakagoma kabisa hata kunipa Bank statements!
Sikuelewa kwanini wakati niliwaonesha barua ya kuteuliwa na mahakama pamoja mihutasari ya vikao!

Walidai sheria haiwaruhusu kudisplay information kwa mtu ambaye siyo mteja wao!
Wakaomba nirudi mahakamani nikawaletee Akaunti ya mahakama!
Halafu hakimu ndo atanipatia pesa kama zimo!
Nilihisi usumbufu
Hii ni sahihi. Ndo maana baada ya kufanya transfer kwenda kwenye akaunti za mahakama unalazimika kupeleka swift message/uthibitisho wa fedha na kiasi kilicho hamishwa kwenda mahakamani. Na kwa utashi inaweza ikaambatanishwa na statement itakayo onyesha mwenendo wa akaunti kwa siku za karibuni mpaka ilipofungwa
 
Option zipo mbili

Either apewe msimamizi kabsa au ipitie mahakama,, japo mahakamani mzunguko wake ni balaa.
Kumbuka msimamizi wa mirathi sio lazima akawa mnufaika pekee wa mali za marehemu. Kuweka fedha yote kwenye akaunti binafsi ni kuhalalisha matumizi binafsi.

Ndo maana anaitwa MSIMAMIZI WA MIRATHI napo pia anaweza kuwa miongoni mwa WARITHI pia
 
Kumbuka msimamizi wa mirathi sio lazima akawa mnufaika pekee wa mali za marehemu. Kuweka fedha yote kwenye akaunti binafsi ni kuhalalisha matumizi binafsi.

Ndo maana anaitwa MSIMAMIZI WA MIRATHI napo pia anaweza kuwa miongoni mwa WARITHI pia
Maana ya kikao cha familia kumteua inamaana wamemwamini

Pia katika fomuya kujaza pesa uende wapi mnaweza kuweka AC zenu wote watoto wa marehemu huku mkiapa mmekubaliana hivo au ziingie sehemu moja then zikitpka mtamalizana wenyewe wanafamilia.
 
Maana ya kikao cha familia kumteua inamaana wamemwamini

Pia katika fomuya kujaza pesa uende wapi mnaweza kuweka AC zenu wote watoto wa marehemu huku mkiapa mmekubaliana hivo au ziingie sehemu moja then zikitpka mtamalizana wenyewe wanafamilia.
Hii mara ya mwisho mmetumia lini mkuu?. Inawezekana ni kweli unachokisema. Ila ninacho kifahamu na kuona kikifanya kazi haswa kama sehemu ya mali ya marehemu itajumuisha akaunti alizokuwa nazo basi ni kupitia akaunti ya mahakama.

Na hii inatumika zaidi ili kuondoa dhuluma ambazo kimsingi watu wamekumbana nazo haswa linapokuja swala la mirathi.
 
Ooh je usahihi wa pesa zinazotumwa mahakaman huwa uko wazi kiasi gani kwa msimamizi wa mirathi?
Usahihi wa pesa lazima uwe wazi. Benki inatakiwa itoe taarifa ya pesa za marehemu. Mgao nani apate kiasi gani unaamuliwa na mahakama kwa kutumia wosia (kama upo). Mahakama inatakiwa iwape wahusika kufuata wosia au maamuzi ya mgao wa mahakama. Hapa huwa hakuna siri maana kila mmoja anajuwa haki yake kufuatana na uamuzi/hukumu ya mahakama.
 
Hii mara ya mwisho mmetumia lini mkuu?. Inawezekana ni kweli unachokisema. Ila ninacho kifahamu na kuona kikifanya kazi haswa kama sehemu ya mali ya marehemu itajumuisha akaunti alizokuwa nazo basi ni kupitia akaunti ya mahakama.

Na hii inatumika zaidi ili kuondoa dhuluma ambazo kimsingi watu wamekumbana nazo haswa linapokuja swala la mirathi.
Isije kuwa nae muelekeza anatoka familia ya extended family.

Nyie kama mlizaliwa baba mmoja mama mbalimbali
Au mama mmoja baba mbalimbali then baba akafariki hapo lazima pesa iingie kwenye Ac ya mahakama.
 
Ushauri tu, Kama ikiwezekena hizi nywila unampatia mtu mmoja mwaminifu ambapo ni rahisi kuwithdraw pesa pindi inapotokea hali Kama hii. Nimejifunza kutoka kwa Mzee yeye alikuwa msiri sana, ikitokea amefariki ghafla ikawa shida sana kutoa pesa mpaka zilipoanza process za mirathi.
Never ever do that. Wewe tumia hiyo process ya mahakanma, lakini nzuri kuliko vyote ni kuacha wosia. Wosia uataifanya kazi ya mahakama na msimamizi wa mirasthi kuwa rahisi. Lakini hii ya kumuamini mtu ina matatizo. Kwanza watu hubadilika. Anaweza kuwa mwaminifu leo, lakini akiona kitita cha pesa uaminifu ukamtoka. Pili, anaweza akawa mwanifu kweli, lakini akazuliwa maneno na ndugu kuwa kiasi kilichoonekana ni kidogo kuliko walichokuwa wanajuwa marehemu anacho. Kutakuwa na maneo mengine, eti alichota kwanza na ndiyo aklatuambia kiasi kilicho huko benki. Kuepuka haya yote acha wosia na msimamizi afuate wosia na uamuzi wa mahakama.
 
Never ever do that. Wewe tumia hiyo process ya mahakanma, lakini nzuri kuliko vyote ni kuacha wosia. Wosia uataifanya kazi ya mahakama na msimamizi wa mirasthi kuwa rahisi. Lakini hii ya kumuamini mtu ina matatizo. Kwanza watu hubadilika. Anaweza kuwa mwaminifu leo, lakini akiona kitita cha pesa uaminifu ukamtoka. Pili, anaweza akawa mwanifu kweli, lakini akazuliwa maneno na ndugu kuwa kiasi kilichoonekana ni kidogo kuliko walichokuwa wanajuwa marehemu anacho. Kutakuwa na maneo mengine, eti alichota kwanza na ndiyo aklatuambia kiasi kilicho huko benki. Kuepuka haya yote acha wosia na msimamizi afuate wosia na uamuzi wa mahakama.
Umemaliza kila kitu mzee japo wosia siyo utamaduni wetu. Japo kifo kipo kuacha wosia binafsi nikili tu hapo ndo ushamba wangu ulipo. Huwa nahisi ni kuingia mkataba na kifo. Kama ulivyoshauri ni taratibu zinafuatwa kwa uzuri kila kitu kinakuwa sawa.
 
Umemaliza kila kitu mzee japo wosia siyo utamaduni wetu. Japo kifo kipo kuacha wosia binafsi nikili tu hapo ndo ushamba wangu ulipo. Huwa nahisi ni kuingia mkataba na kifo. Kama ulivyoshauri ni taratibu zinafuatwa kwa uzuri kila kitu kinakuwa sawa.
Swala la wosia kutokuwa sio utaratibu wetu ni jambo la kubadilika sasa. Ni kitu kizuri sana kukifanya ukiwa hai. Unaepusha mambo mengi.

Jambo la msingi ni usiri wa wosia ili kutoleta migogoro ya kifamilia pindi unapokuwa hai au kusababisha watu wakutangulize/ watu hubadilika.

Pitia ofisi za RITA utapata elimu sana kwa maswala ya wosia. Ni elimu muhimu sana. Pia jaribu tembelea tovuti yao
 
Je bank haiwezi kudanganya kiasi kilichoachwa na marehemu?
 
Back
Top Bottom