Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Mkuu Lunyungu, kwanza heshima kwako, pili naomba msamaha binafsi kwako, mimi ni miongoni mwa wanajf wabaya kabisa wasio na utu, baada ya zile pm kuhusu hali ya afya yako, waugwana tulitakiwa tufanye follow up, sio tunawasiliana tuu katika uzima!. Pole na thank God uko on line ni ishara tosha ya buheri wa afya.

Back kwenye mada, nimesoma primary na sekondari enzi za chama kimoja, Mtoto wa Nyerere ni personal friend wangu. Mtoto wa Mkapa ni class mate wangu Tambaza sambamba na Dr. Mwinyi ni school mate. Mtoto wa JK ni personal friend tangu UDSM, hivyo nimekuwa na access kwa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na JK. Kama mwandishi ninewafanyia personsl intreview marais wote tena interviwew ya mwisho ya Nyerere nilifanya nae Bern nchini Uswisi na mimi ndio ninayo one and only!. Hivyo ningepata preferential treatment kama ningejiunga CCM!, hata kawilaya nisinge kosa!.

Nilipoendesha kipindi cha Kiti Moto enzi zile, hakuna anaejua kwa nini kipindi kile kiliuwawa!. Mimi ndio najua. Nilijiunga TBC, hakuna anaejua ni kwa nini niliondoka!. Mimi ndie ninaejua!.

Kosa langu kubwa ni kuwa too frank. Ukweli unauma ila una cost!. Mimi umeisha ni cost sana hivyo siogopi kuwaambia Chadema ukweli kwa sababu mnaona kama 2015 ni mbali sana, sasa mimi nawaambia ukweli mchungu kabla, na kama mwendo wenyewe ndio huu!, ni hakika, 2015 mtalia tena!.

Mzee Lunyungu, nakuhakikishia kama kipimo cha kuingia mbinguni/peponi kwa kutofungamana na upande wowote, nakuhakikishia nikifa leo au kesho, mimi ni straight mbinguni!.

Ila pia Chadema ina wanachama, mashabiki, wapenzi na wafuasi ambao wao ni waumini wakiabudu kuwa Chadema is always right, siamini kama nawe ni mmoja wao, hivyo kila anayepingana na Chadema basi ni CCM au katumwa.

Nape, January, Kippi ni marafiki zangu kama alivyo Zitto, JJ. Mnyika, Lissu na Freeman, sambamba na Mtatiro, Jussa na Hamad Rashid. Mimi nasimama kama Pasco wa Jf siko upande wowote, mtakaodhania, endeleeni kudhania!.

Nakuomba Mkuu Lunyungu, tafuta post zangu kuhusu CCM, CUF na Chadema halafu fanya conclussion!.
 


@Paso nadhani wewe unaamini kuwa kifungu 86 on its own kingetosha kusitisha huu muswada kusomwa. Lakini kama utaangalia taratibu kabisa hicho kifungu kwenye kipengele cha nne (angalia mchango wa mwanakijiji) kuna 'speed governor' Spika atahoji wabunge ili waafiki au wakatae. Ni hili limefanyika sana kwenye kipindi hiki cha Spika Makinda na kwa bahati mbaya mara nyingi hoja za CHADEMA zimekuwa zinakatiliwa (wengi wape). Mfano ni hoja ya Myina kuhusu EPZ na msamaha wa kodi, hoja ya Lissu ya kutoruhusu wakuu wa mikoa/wilaya (mhimili wa mmoja) kusimamia nidhamu ya mahakama (mhimili mwingine).

Lakini kichekesho kwenye huu muswada Spika Makinda was more daring, hakutaka hata kuruhusu mtu kuongea! Kumbuka bunge la sasa limejaa hila.
 

Pasco, nimeyapenda majibu yako kwa Lunyungu umeonyesha uungwana Mungu akubariki,
sasa nataka kujua msimamo wako mara baada ya mwanakijiji kukuonyesha hicho kipengele cha 86 na mapungufu yake ktk kuhusimamisha mjadala mzima ??
 
Pasco, nimeyapenda majibu yako kwa Lunyungu umeonyesha uungwana Mungu akubariki,
sasa nataka kujua msimamo wako mara baada ya mwanakijiji kukuonyesha hicho kipengele cha 86 na mapungufu yake ktk kuhusimamisha mjadala mzima ??
Politiki, nitajibu kila hoja, ndio nimemaliza harusi ya kijana wangu Jerry Muro, niko kwenye night life mahali, nikirudi home kama ikitokea hazijapanda kichwani, nitajibu hoja zote hakuna kulala!.
 
Pasco,

Mie kwenye mambo ya sheria nina tongotongo sana na hiyo inanisaidia sana kwenye mjadala huu zaidi yenu msio na tongotongo.

Ukiangalia maneno yako, unakubali kabisa kuwa Chadema wamefanya kosa la mwaka na hasa ukiangalia katiba ilivyo. Na hilo kosa hasa kwenye nchi za kawaida na zenye Demokrasia na nidhamu kwa viongozi, utaona na kukubali kuwa ni kosa kubwa sana. Nchi kama hiyo, Kikwete asingelikuwa Rais. Nchi kama hiyo, Lowassa asingelikuwa kiongozi. Nchi kama hiyo, Chenge, Jairo, Mbunge wa Igunga (Kafumu), Prof. Mwandosya, Magufuli nk kwa ufisadi ambao ulishawahi kufanyika na wao wakiwa vingozi wa Serikali/Chama, leo hii walikuwa wanatakiwa kuwa jela. Ila kwa Tanzania, wote bado wanapeta.

Sasa basi ukiwa katika nchi kama Tanzagiza, kila kitu kinawezekana. Mwenyewe unafahamu kabisa kuwa ni Rostam Azziz kamuweka Spika Makinda na pia alimuweka Samuel Sitta na kumuondoa. Kuna dalili kabisa kuwa Rostam Azziz si tu Makinda kamuweka ila ni zaidi ya Makinda.

Hii katiba kama ikianza na iwe ya wananchi, Rostam Azziz anaweza kujikuta anafungwa jela, Barrick Gold wakafukuzwa na kulipa faini kubwa na watu/makampuni mengine mengi yakafuata. Wao milele katiba mpya itakuwa ni Msumari. Ni vizuri sana kusikia waziwazi kuwa Rostam Azziz ndiye alimuweka Sitta/Makinda na wao ndiyo hao wanataka kutuletea eti katiba mpya.

Ukiangalia maelezo yako mwenyewe na maelezo ya Mzee Mwanakijiji, utaona kuwa hicho kifungu hakingelisaidia kabisa. Kama kweli Makinda alishaambiwa na Rostam Azziz apinge hicho kifungu, basi hata angelikuja Obama na kusoma na kuweka pingamizi, nina imani Makinda angelifoka hadi apoteze meno kwa hasira. Angeliweza hata kutoka mbio na rungu la Spika na kumfuata Obama ili am-NYUKE nalo na kuwambia akome kabisa kuja Tanzania na kuleta kalufundi kake ka Sheria za USA hapa.

Ili unielewe kwa ufupi, ni sawa na MJADALA wa kumhusu Lowassa/RA uwe unafanyika na Spika wake ni Bashe. Atatowa kila kisingizio hata cha kusema "wewe, hicho kifungu umekisoma na lafudhi ya Kinyatunzu, na hiyo katiba hairuhusu......" Angelikufukuza kwa kosa hilo na kusema hata kama utajitetea vipi. Mambo mengine hutakiwi kuwa na Karai la Kifipa ili kuona nini kitatokea hapo mbele ya safari. Labda kwa hili ndipo wewe na class mate wako Lissu mmepishana. Yeye kwa kujua nini kitafuata, akaanza kwanza kwa kutumia hiyo nafasi yake mapema na kuweka hotuba yake yote. Badala ya CCM kumsikiliza, akina Rage ndiyo kwanza walikuwa wanazidi kuchukia kwa kuambiwa ukweli wakati wao wanataka wamalize mambo harakaharaka. Kama alivyotegemea Lissu, zikaja siku nne za yeye kutukanwa wakati mtani wangu Makinda, anachekacheka tu utafikiri wamemwambia kuwa mchana kuna Lunch ya nyama ya Pitbull mnono sana.
 
Pasco, nimeyapenda majibu yako kwa Lunyungu umeonyesha uungwana Mungu akubariki,
sasa nataka kujua msimamo wako mara baada ya mwanakijiji kukuonyesha hicho kipengele cha 86 na mapungufu yake ktk kuhusimamisha mjadala mzima ??
Asante Politiki, nitamjibu Mzee Mwanakijiji yeye bado anajenga hoja kwenye presumpmtion ambayo ndio utopia politics, kama maandiko yanasema "tafuteni mtapata", " ombeni mtapewa" au " bisha hodi utafunguliwa!", kama msipotafuta, hampati!, msipoomba hampewi', na msipo bisha hodi, hamfunguliwi!. Kuna kitu Mhe. Tundu Lissu alipashwa kufanya, hakutimiza wajibu wake!, as a result Chadema lost the argument for good!, sasa huu utetezi wa Mzee Mwanakijiji eti hata kama wangeli ... wasingeli kubaliwa!, doesn't hold water!.
Miongoni mwa sheria ambazo mimi nimespecialize ni International Law na Private International Law ambazo zinasisitiza lazima u exohaust existing home remedies ndipo uingie kwenye international law, Mhe. Lissu had a chance hakuitumia!. There must be credible reasons ambazo ni justified kwa why not hizo sababu za Mzee Mwanakijiji ni scapegoat tuu na ni superficial tuu, hakuna sababu zozote za maana zaidi ya uzembe!.

Assumption yangu Chadema banked on Lissu talented gifted genious lawyer!. Ku addmit weakness au kukubali makosa, kwataka moyo!. This time Chadema was wrong!.
 
hawa cdm sio wise hata kidogo kwa sababu historia inajionesha hawa ccm mkisusia bunge wao ndio wanachukua adavantage
 

Pasco, unakubali kuwa kwa kutumia kanuni ya 86:3b Lissu angepewa nafasi ya kuelezea sababu za kwanini mswada ule ukataliwe na Spika angempa nafasi hiyo?
 

Pasco kumbuka kuwa wengine humu si wanasheria na hata basi kuelewa hawataki, nwengune ni waandishi wa vijarida vya internet, hiyo ni tofauti kubwa iliyopo baina yako na wao, wewe ni muandishi lakini umesomea na sheria kama ulivyoainisha.

Umenena vizuri sana kwenye hii mada na hakuna ubishi ispokuwa watu hapa wanapinga kiuchama tu na si kiusomi.

Huwezi kwenda bungeni kwa "assumptions" nakuunga mkono kwa hilo, lakini ndio hivyo tena, wengine huwa wagumu sana kuelewa.

Kitu nilichokiona mimi ni kuwa, Magwanda walikuwa hawana sababu yoyote ya msingi ya kususia bunge, hiyo inaonesha kuwa si wanasiasa. Mwanasiasa mzuri huwa ana "reason".

Chadema kuna wakati walikuwa na hoja nzuri sana za kisiasa lakini niliwaona hawafai walipoanza mchezo wao wa kususasusa, hivi unamsusia nani? ni nani atakudekeza kwenye siasa. Mmmesusa mara moja haitoshi? inakuwa ndiyo kila siku, Rais mumsusie, Bunge mlisusie, sherehe mzisusie. Sasa hizo ni siasa kweli?

Hivi juzi haswa walichokisusia nini haswa? wanasusia mswaada? ili iweje? waonewe huruma na wananchi? hiyo imewafanya waonekane ni watu wa fujo tu na hawana lolote zaidi. Wendi wapenzi wa Chadema nnaojuwana nao hilo wameliponda sana.

Na hapa kwa hii hoja ulioleta utawaona tu. Watasusa sasa hivi.
 
Pasco, unakubali kuwa kwa kutumia kanuni ya 86:3b Lissu angepewa nafasi ya kuelezea sababu za kwanini mswada ule ukataliwe na Spika angempa nafasi hiyo?
Mkuu Mzee Mwanakijiji, with due respect, Bunge linaendeshwa kwa sheria, taratibu na kanuni, kama kanuni inasema mbunge alete pingamizi, spika is obliged kusitisha na kusikiliza pingamizi, ndivyo kanuni inavyotamka, Mhe. Lissu hakutoa pingamizi na badala yake katoa hotuba ya kambi ya upinzani, kinachofuatia hotuba ya kambi ya upinzani ni majadiliano, mlitaka spika afanye nini?..

Nimeuliza kwa nini Mhe. Lissu hakutoa pingamizi?. hakuna jibu!. Nimeuliza kwa nini Lissu amesoma hotuba ambayo hakupaswa kuisoma in the first place?. Pia hakuna majibu!. Hivi Mzee Mwanakijiji unajua hotuba ile ni passport ya mjadala kuendelea?. Hivi unaelewa hotuba ya kambi ya upinzani ni pre requisite kwa muswada wa serikali kupita?. Jee unajua bila hotuba hiyo muswada unasitishwa na kurudishwa kwenye kamati?.
 
Pasco for the time being let us make an assumption that Tindu Lissu is wrong.
Swali ni kuwa kama angeweka pingamizi kufuatana na kifungu 86 na spika akalikubali kwa muda huo,sheria na kanuni zinasema kitu gani kiendelee? hicho ndicho kinatakiwa ufafanuzi.
 

Unachodai wewe ni kuwa kama pingamizi lingewekwa basi mswada ungesitishwa. Inaonekana unachojali ni kusitishwa tu kwa mjadala kwa sababu kanuni inafuatwa. Lakini husemi kama wangefuata kanuni nini kingetokea? Au ulitaka wafuate kanuni kama ishara tu kuwa wamefuata hata kama wangekuwa overruled na Bunge?


Hapana, hii hoja ya mwisho sidhani kama ni sahihi. Kanuni gani inakufanya uamini kuwa pingamizi likiwekwa basi mswada unarudishwa kwenye kamati? Labda miye nimeiruka nisaidie niipitie niko tayari kusahihishwa. Nilivyosoma - na uelewa wangu finyu - ni kuwa pingamizi lingewekwa Spika angeliuliza Bunge kutoa uamuzi. Hili la kuwa pingamizi ikiwekwa mswada unarudishwa kwenye kamati liko wapi?
 

Kumbe wewe ndo Paschal Mayala...
 
Kumbe wewe ndo Paschal Mayala...

jamani toka mwanzoni ndio inavyofahamika kwani si hilo jina la kwanza analotumia kwenye JF sasa kuendelea kushangaa sio
muhimu tutakuwa kama CCM sasa badala ya kujadili hoja tunajadili majina ya watu. FLY is an extra ordinary contributer kwenye JF kwahiyo naamini utakuwa umeelewa kwani toka kwy article yake ya kwanza amesema yeye ni nani baada ya kusema yeye ndio
alikuwa muhuliza swali la kifungu cha 86.
 

Hivi Pasco na Paschal ni sawa?
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji, nakuheshimu sana, nakuomba usiingie kwenye undermining languages, "na uelewa wangu finyu", naomba tusianzishe ...ya rejareja!

Kuhusu swali lako, nieleze unaelewa nini kuhusu kifungu 86.6?.
(6) Ikiwa Muswada wa Sheria unaohusika ni Muswada wa Serikali,
basi Msemaji wa Kambi ya Upinzani atatoa maoni yake juu ya
Muswada husika na endapo ni Muswada Binafsi au Muswada wa
Kamati, basi msemaji wa Serikali atatoa maoni yake.

Bila maoni ya kambi ya upinzani, muswada hausongi mbele!. Hapa naomba unijibu pia Mhe. Lissu alipotoa maoni ya kambi ya upinzani, aliyatoa hayo maoni ili iweje, what does it mean kutoa maoni?, jee alitakiwa kutoa maoni au kupeleka pingamizi?.

[FONT=Helvetica, Calibri, Verdana, Geneva, sans-serif]
[/FONT]
 

Mkuu Mzee Mwanakijiji, nakuheshimu sana, nakuomba usiingie kwenye undermining languages, "na uelewa wangu finyu", naomba tusianzishe ...ya rejareja!


Heshima za kutishana si heshima. Nimesema nikimaanisha hivyo. Wewe umejitaja ni mtaalamu wa sheria za kimataifa na mimi sikujali kama unajidai au unaelezea ukweli. Niliamini unaelezea ukweli. Sasa mimi kudai nina uelewa finyu ndivyo nilivyo ndio maana nauliza maswali. Sina tabia ya kurusha reja reja.



Sasa swali halijibu swali. Kipengele hicho cha sita kina presume kipengele cha 4 kimeamuliwa kwa Bunge kukubali hoja ya kukataa kama itakavyokuwa imetolewa. Na ukumbuke kipengele cha 86.3b ambacho unakitumia hakimtaji kiongozi wa upinzani. Mbunge yeyote anaweza kukitumia kutoa maelezo yakukataa mswada. Sasa kama hoja ya 86:4 inatimizwa - kwamba baada ya Spika wa Bunge kuliuliza Bunge na Bunge linakubaliana na maelezo ya mbunge aliyetoa hoja chini ya kifungu kidogo cha 3b basi ndio ama kinafuata kifungu cha tano au cha sita. Nisahihishe kama uelewa wangu hauko sahihi. Kwamba kifungu cha sita na kile cha tano kinategea uamuzi unaofukiwa chini ya kifungu cha 4.

Bila maoni ya kambi ya upinzani, muswada hausongi mbele!. Hapa naomba unijibu pia Mhe. Lissu alipotoa maoni ya kambi ya upinzani, aliyatoa hayo maoni ili iweje, what does it mean kutoa maoni?, jee alitakiwa kutoa maoni au kupeleka pingamizi?.

Sidhani kama unafanya sahihi. Hivi kwa mfano msemaji wa upinzani (lissu) angesimama na kusema kuwa "Kambi ya Upinzani haina maoni yoyote tunaomba mjadala uendelee" ina maana Spika angewalazimisha watoe maoni? Kifungu cha sita ndicho ambacho Lissu alikitumia kutoa maoni yake kwa niaba ya upinzani. Na alitumia kwa sababu hakukuwa na sababu ya kukataa mswada kwani hata wangekataa hawakuwa na kura ya kuzuia mswada usiendelee. Waliamua kusubiri muda wa kutoa maoni yao (chini ya hicho kifungu kidogo cha sita) na well.. WALITOA MAONI YAO!

Baada ya kutoa maoni yao wakijua kuwa hawana kura ya kuzuia mswada usiendelee waliamua kutoka Bungeni in protest. Yote hayo yakiwa ndani ya uwezo wao wa kidemokrasia. Hawakufanya kosa lolote.
 

Pasco you might be right. lakini at the end of the day, kwa wingi wa CCM, hata kama ungezuiwa na kuomba maoni ya bunge, CCM wangepita na muswada ungeliendelea. Sijui kanuni za bunge zinasemaje, lakini nadhani kura ingepigwa na wabunge. CCM kwa wingi wao wangepita tu. Hivyo naona ni sahihi CDM kususia. CCM wana ajenda yao kuhakikisha wanahodhi katiba mpya. Kikwete will never make a mistake kuunda tume huru. Ataweka watu ambao atahakikisha wanapokea maagizo yake na CCM. Hivyo nikupambana tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…