Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!

Absolutely! Sikuelewa toka mwanzo kwanini waliamini kuwa Rais ambaye hakuwa na ajenda ya Katiba Mpya muda wote wa kampeni (na miaka ishirini kabla yake) hatimaye ameona mwanga na sasa angeweza kuwa msimamizi mzuri wa mchakato wa kuelekea Katiba mpya.

Chadema pekee ndio wanaweza kuwa wasimamizi wazuri wa machakato wa katiba mpya???

Aisee mna akili sana??? hivi chadema ndio another super party in making
 
Point kubwa hapa ni kuwa CHADEMA walishindwa kuitumia kanuni ya 86 effectively kuzuia muswada, na hivyo kwa kuondoka kwao wakaruhusu muswada upite kirahisi. Nitafurahi na kushukuru sana iwapo atajitokeza mtu anielemishe hicho kifungu cha 86 kinasemaje

Naweka kifungu kizima cha 86 cha Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la 2007


86.-(1) Siku ambayo Muswada wa Sheria uliokwisha kujadiliwa na Kamati umepangwa kwenye Orodha ya Shughuli, Waziri,
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mwenyekiti wa Kamati au Mbunge mwenye Muswada husika atawasilisha hoja kwamba Muswada wa Sheria ambao atautaja kwa jina Kusomwa Mara ya Pili.
(2) Hoja ya Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili itakuwa
kama ifuatavyo:-
“Kwamba, Muswada wa Sheria uitwao….. sasa usomwe mara ya pili”. Au kadri itakavyokuwa; “Kwamba, Muswada uitwao ……………… kama ulivyorekebishwa kwa mujibu wa jedwali la marekebisho au kama ulivyochapishwa upya sasa usomwe mara ya Pili.”
(3) Haitakuwa halali katika hatua hii kuleta hoja ya kufanya mabadiliko katika hoja isipokuwa tu kwamba:-
(a) mabadiliko bila kutoa sababu yanaweza kutolewa kwa kusema: “Kwamba, Muswada huu usisomwe mara ya Pili sasa na badala yake usomwe baada ya ….. kuanzia …..”, na hapo muda ambao Muswada huo unaokusudiwa kusomwa utatajwa.
(b) mabadiliko yenye kutoa sababu yanaweza kutolewa kwa kusema: “Kwamba, Bunge hili likatae Muswada huu Kusomwa
Mara ya Pili kwa sababu zifuatazo …….”, na hapo sababu za kupinga Muswada Kusomwa Mara ya Pili zitatajwa kwa ukamilifu.
(4) Iwapo hoja itatolewa chini ya fasili ya 3(a) na (b) ya Kanuni hii, Spika atalihoji Bunge ili kufikia uamuzi.
(5) Mwenyekiti wa Kamati iliyopelekewa Muswada wa Sheria au Mjumbe mwingine wa Kamati aliyeteuliwa kwa ajili hiyo, atatoa
maoni ya Kamati kuhusu Muswada husika.
(6) Ikiwa Muswada wa Sheria unaohusika ni Muswada wa Serikali, basi Msemaji wa Kambi ya Upinzani atatoa maoni yake juu ya
Muswada husika na endapo ni Muswada Binafsi au Muswada wa Kamati, basi msemaji wa Serikali atatoa maoni yake.
(7) Mjadala wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili utahusu ubora na misingi ya Muswada huo tu.
(8) Majadiliano juu ya hoja kuhusu Muswada kama yapo yatahusu maneno yanayohusiana na hoja tu.
(9) Mbunge yeyote au Waziri anaweza, wakati wa mjadala huo, kumshauri Mtoa hoja afanye mabadiliko katika Muswada, ama
mabadiliko ya jumla au yale atakayoyataja Mbunge.
(10) Katika hatua hii iwapo mtoa hoja anataka kufanya marekebisho au mabadiliko katika Muswada wa Sheria kutokana
na ushauri uliotolewa ama katika Kamati au wakati wa Muswada wa Sheria Kusomwa Mara ya Pili au kwa sababu nyingine yoyote,
iwapo Muswada huo ni wa Serikali atamjulisha Mwandishi Mkuu wa Sheria na iwapo Muswada husika ni wa Kamati au Binafsi
atamjulisha Mshauri Mkuu wa Bunge wa Mambo ya Sheria ili atayarishe na kumkabidhi Katibu ambaye atagawa kwa kila
Mbunge nakala ya:-
(a) Muswada wa Sheria uliochapishwa upya ukiwa na marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika; au
(b) Jedwali la Marekebisho au mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika.
(11) Kamati au Mbunge anaweza kuwasilisha kwa Katibu, kwa maandishi, mabadiliko anayokusudia kuyafanya katika Muswada
huo wakati wa Kamati ya Bunge Zima akionesha bayana mabadiliko yanayokusudiwa kufanyika katika kila Ibara inayohusika.

Pasco anaamini kuwa kwa kutumia kifungu cha 86:3b kwamba Lissu alitakiwa kutoa hoja kwa kutumia kanuni hiyo na mara moja mjadala ungesitishwa. Tatizo ni kuwa kifungu cha 4 cha ibara hiyo kinaweka mtego kuwa hata hoja ya kukataliwa kwa mjadala haisababishi kusitishwa kwa jumla kujadili mswada. Kinachotokea ni kuwa mtoa hoja atapewa nafasi ya kuelezea kwanini mswada usitishwe.

Sasa fikiria kuwa Lissu ametumia ibara hiyo na kupewa nafasi ya kuelezea kwanini mkataba ukataliwe na akaeleza kwa kirefu hoja zake zote. Mwisho akimaliza ibara ya 86:4 inatumika: Yaani,

4) Iwapo hoja itatolewa chini ya fasili ya 3(a) na (b) ya Kanuni hii, Spika atalihoji Bunge ili kufikia uamuzi.

Kumbe, Lissu akimaliza kutoa hoja zote za kuzuia Spika ataliuliza Bunge lifanye uamuzi wa kukataa au kukubali mswada ukataliwe au la. Nani anafikiria kuwa CCM wangeweza kushawishika kukubali hoja ya Zitto kukataa mswada? Maana hoja alizozitoa kwenye hotuba zingekuwa ni karibu zile zile (kama siyo zile zile) ambazo angezitoa kutaka mswada ukataliwe.

Kwa maneno mengine Ibara ya 86 isingeweza kufanya hoja ya CDM ifanikiwe kuzuia mjadala wa mswada kuendelea. Ingeweza tu kumpa Lissu nafasi ya kuelezea kwanini mswada ukataliwe lakini ultimately Bunge lingeulizwa na Spika kama waukatae na sote tumeona kuwa mswada usingeweza kukataliwa na Wabunge wa CCM kwani hata bila hoja za Lissu wao CCM wangeweza kuukataa wenyewe na hawakufanya hivyo!
 
@Topical, hapo kwenye red. hapana. Nadhani unachanga kamati za kudumu za bunge na party caucuses. Kamati za kudumu za bunge zinakuwa na wabunge wa vyama mbalimbali na kamati zinaongozwa na mwenyekiti (sio chief whip). Cauceses ina-apply kwa chama kimoja kimoja. Na kwa chama chochote (unless kina ugomvi wa kuua mtu) kabla ya kwenda kwenye mjadala wowote lazima wawe na vikao vya ndani ili kuweka msimamo. Hapo ndio tunakuwa na chief whip (mshika kifimbo). Kwa ccm ni Lukuvi na CHADEMA ni Lissu. Hao wengine sijui nani.

Sure, mkuu muswada uliporudi kutoka bungeni kila wakati tulikuwa tunaonyeshwa wabunge wakifanya semina na wataalamu wa sheria, akina Shivji, etc ili kupata maoni na kuboresha muswada kabla ya kwenda wakiwemo wabunge wa chadema ...

Waziri wa sheria (kivuli) ana haki sawa kuuliza mchakato wote anytime prior to bunge (aseme kama kweli alinyimwa hizo fursa??)

otherwise anatafuta media attettion hana la maana la kutuambia..
 
Chadema pekee ndio wanaweza kuwa wasimamizi wazuri wa machakato wa katiba mpya???
Aisee mna akili sana??? hivi chadema ndio another super party in making

CHADEMA hawapingi ili wao waongoze, wanachotaka ni kufuata taratibu, na taratibu zinasema muswada unaanza kwa kuchukuwa maoni ya wananchi. Shida CCM walishaamua siku nyingi kwamba wao ndio wana akili.

Binafsi ningependa kufuata utaratibu unawashirikisha wananchi ili kuhakikisha kumbe mbeleni hatutakaa tuwe na chama chochote (CCM, CHADEMA, CUF, TLP ,DOVUTWA etc etc) kinakuwa na utawala wa kifalme kama wa sasa. Ni vizuri kurudisha mamlaka kwa wananchi ili wawe na nguvu ya kuwajibisha viongozi mara moja wanapokwenda kinyume tofauti na sasa na hii itatuletea neema wote (ccm included).
 
CHADEMA hawapingi ili wao waongoze, wanachotaka ni kufuata taratibu, na taratibu zinasema muswada unaanza kwa kuchukuwa maoni ya wananchi. Shida CCM walishaamua siku nyingi kwamba wao ndio wana akili.

Binafsi ningependa kufuata utaratibu unawashirikisha wananchi ili kuhakikisha kumbe mbeleni hatutakaa tuwe na chama chochote (CCM, CHADEMA, CUF, TLP ,DOVUTWA etc etc) kinakuwa na utawala wa kifalme kama wa sasa. Ni vizuri kurudisha mamlaka kwa wananchi ili wawe na nguvu ya kuwajibisha viongozi mara moja wanapokwenda kinyume tofauti na sasa na hii itatuletea neema wote (ccm included).

Utaratibu uliopitishwa sasa unakunyima vipi kutokufikia hicho unachotaka?? yaani katiba nzuri uipendayo??

Usije na speculations? kwamba ccm vile na vile??
 
Kila jambo linaanza na 1,2,.... Huu muswada ulitakiwa kusomwa kwa mara ya kwanza. Maana ya kusoma muswada kwa mara ya kwanza ni kwamba unawekwa kwenye national gazzette na wananchi wanatoa maoni, baada ya kupata maoni (kwa utaratibu wa bunge) unasomwa kwa mara ya pili. Hatua hii inawapa wawakilishi wa wananchi (wabunge) kujadili kitu kizima kwa maana ya kupitia maoni ya wananchi na kuboresha ili usomwe kwa mara ya tatu - kupitishwa.
Aksante sana Mkuu
hivi hili National gazeete linapatikan wapi? . nadhai ni kila muswada kabla ya kuwa sheria lazima utangazwe kwenye national gazeete lakini huwa hasa sijui ni lipi hasa na linaptaikanaje kwa wananchi. hii katiba ya mkoloni naona kuna vitu tumerithi wengi hatuvielewi. Kama hii natonal gazzeti huwa nasikia sana lakini sijui sura yake. Au ndio Daily News????11111

Now, kwa bahati mbaya ccm imekuwa inaendesha hii nchi kwa mazoea bila kusoma/kujali sheria na taratibu zilizopo! Huu muswada ilipelekwa bungeni mwezi March kwa njia 'DHARURA! (dharura ya nini kwenye katiba ya nchi?). Hata hivyo ulikataliwa kwa sababu ulikuwa mbovu mbovu, na mbaya zaidi ulikuwa umeendikwa kwa lugha ya kiingereza! Spika Makinda akatoa tamko utolewa uboroshwe na wapate maoni ya wananchi. Wakubwa kabla ya kuboresha na hata kuundika kwa kiswahili wakaamua kupata maoni chap chap Dar, Zanzibar na Dodoma kwa siku kama tatu tu! Mikoa mingine wakaachwa sijui wako Kenya?
Duh hii basi kali wanafanya Pilot testing hata kwenye katiba. Hapa sasa ndio naanza kukusoama na kuona Tatizo


Hata hivyo hatua hii ilikuwa pre-mature kwa sababu bado muswada ulikuwa kwa lugha ya kiingereza hivyo wananchi wengi wasingejua nini kimeandikwa. Wajumbe wa kamati walipoomba kwenda mikoa mingine walau 10 Spika akazuia.
hili nalo ni Tatizo lingine sababu hata bunge letu ni la vyama vya siasa. watu hawaruhusiwi kugombea bila vyama . Sina tatizo kubwa na hili lo lakini nataka kuonyesha kuwa na bunge letu lisisijahau likadhani lenyewe ndio driving seat kwenye katiba mpya. Na bunge letu linahitaji kuwa reformed wenye katiba mpya......

Muswada wa sasa umetafsiriwa week chache kabla ya bunge kuanza, na haujapata maoni ya wananchi kama taratibu zinavyoelekeza. Na unanekana kumpa rais nguvu ya kuamua katiba iweje akishirikiana na rais wa wanzibar na wakubwa wachache (i.e mwanasheria mkuu). Kwa kifupi huu naweza kuufananisha na waraka toka kwa Mugabe kwenda kwa Morgan Tsvangirai= umekaa vibaya sana huu muswada.
mkuu hapa sasa ndio nilitaka kujua right sequce ya event ilitaiwa kuwaje. Nani anataiwa kuusanya maoni. nani anataiwa kumteau nani . Yaani Nani anatakiw kuform structure na muundo na wajumbe wa katiba mpya. Wajumbe wapatikane vipi?

Yaani kuna maswali najiuliza sipati majibu sabbau kama ni bunge linangozwa CCM ukitumia demokrasia ya bunge Cm watakuwa washini wa kile wanachota ndio kiitakuwa .

Je hili suala si sahihi lisimmiwe na Sheria na majaji na Mahakama . Wanasisa na vyama vya siasa kiwemo rais Vikae pembeni. Badala ya bunge la katiba basi iwe ni Mahakama ya Katiba. Inawezekana ni carzy idea lakini naon bunge lenyewe kama alivyo rais JK wawezeshe tu kuunda muswada wa kuunda mahaaKama ya katiba ambayo May be Jaji mkuu ndiyo atajua How, Who,when etc nyingine
 
Sure, mkuu muswada uliporudi kutoka bungeni kila wakati tulikuwa tunaonyeshwa wabunge wakifanya semina na wataalamu wa sheria, akina Shivji, etc ili kupata maoni na kuboresha muswada kabla ya kwenda wakiwemo wabunge wa chadema ...

Waziri wa sheria (kivuli) ana haki sawa kuuliza mchakato wote anytime prior to bunge (aseme kama kweli alinyimwa hizo fursa??)

otherwise anatafuta media attettion hana la maana la kutuambia..


Kuoneshwa wabunge wakikutana na some interesting professor hakukufanyi wewe mwananchi uwe umeshiriki! Taratibu zinasema wananchi washirikiwe, na sio wananchi-maprofessor tu! Ni vizuri viongozi wakajenga utamaduni wa kuheshimu wananchi hasa pale wanapoanza kulalamika. Topical Tanzania ina mikoa 27, hawa wakubwa wamefanya kikao Dodoma, Dar na Unguja. basi. Tena wakati huo wanatembeza muswa ulikuwa umeendikwa kwa lugha ya kiingereza! Kwa kitu nyeti kama katiba kwa nini ulipue namna hii, tena huku watu wakikuambia unalipuwa? Kisiwa chote cha Pemba hawajaulizwa na kama mtu hana TV basi atakuwa hajaona hata hayo mahojiano ya kamati na ma-professor!

Hapa ndio naona CCM wamewaongezea CHADEMA mtaji. Tabia zao za kufanya mambo kwa ujanjaujanja sasa zimeanikwa.
 
Kuoneshwa wabunge wakikutana na some interesting professor hakukufanyi wewe mwananchi uwe umeshiriki! Taratibu zinasema wananchi washirikiwe, na sio wananchi-maprofessor tu! Ni vizuri viongozi wakajenga utamaduni wa kuheshimu wananchi hasa pale wanapoanza kulalamika. Topical Tanzania ina mikoa 27, hawa wakubwa wamefanya kikao Dodoma, Dar na Unguja. basi. Tena wakati huo wanatembeza muswa ulikuwa umeendikwa kwa lugha ya kiingereza! Kwa kitu nyeti kama katiba kwa nini ulipue namna hii, tena huku watu wakikuambia unalipuwa? Kisiwa chote cha Pemba hawajaulizwa na kama mtu hana TV basi atakuwa hajaona hata hayo mahojiano ya kamati na ma-professor!

Hapa ndio naona CCM wamewaongezea CHADEMA mtaji. Tabia zao za kufanya mambo kwa ujanjaujanja sasa zimeanikwa.

Mimi nafikiri hatua inayofuata ndio hasa sisi wananchi tutashirikishwa kutoa maoni kwenye tume itakayoundwa...

Na logic ni kwamba bunge linawakilisha wananchi katika muswada yote..hata hii ya katiba.
 
Narudia tena:

Nadhani kupiga kura inayohalalaisha upuuzi ni kubaya zaidi kuliku kutohusika kupiga kura hiyo; hata kama kura yako itakuwa inalipinga jambo hilo, bado rekodi zitaonyesha kuwa na wewe ulikuwa ni sehemu ya wale waliohalalisha upuuzi huo.
 
Naweka kifungu kizima cha 86 cha Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la 2007




Pasco anaamini kuwa kwa kutumia kifungu cha 86:3b kwamba Lissu alitakiwa kutoa hoja kwa kutumia kanuni hiyo na mara moja mjadala ungesitishwa. Tatizo ni kuwa kifungu cha 4 cha ibara hiyo kinaweka mtego kuwa hata hoja ya kukataliwa kwa mjadala haisababishi kusitishwa kwa jumla kujadili mswada. Kinachotokea ni kuwa mtoa hoja atapewa nafasi ya kuelezea kwanini mswada usitishwe.

Sasa fikiria kuwa Lissu ametumia ibara hiyo na kupewa nafasi ya kuelezea kwanini mkataba ukataliwe na akaeleza kwa kirefu hoja zake zote. Mwisho akimaliza ibara ya 86:4 inatumika: Yaani,



Kumbe, Lissu akimaliza kutoa hoja zote za kuzuia Spika ataliuliza Bunge lifanye uamuzi wa kukataa au kukubali mswada ukataliwe au la. Nani anafikiria kuwa CCM wangeweza kushawishika kukubali hoja ya Zitto kukataa mswada? Maana hoja alizozitoa kwenye hotuba zingekuwa ni karibu zile zile (kama siyo zile zile) ambazo angezitoa kutaka mswada ukataliwe.

Kwa maneno mengine Ibara ya 86 isingeweza kufanya hoja ya CDM ifanikiwe kuzuia mjadala wa mswada kuendelea. Ingeweza tu kumpa Lissu nafasi ya kuelezea kwanini mswada ukataliwe lakini ultimately Bunge lingeulizwa na Spika kama waukatae na sote tumeona kuwa mswada usingeweza kukataliwa na Wabunge wa CCM kwani hata bila hoja za Lissu wao CCM wangeweza kuukataa wenyewe na hawakufanya hivyo!

Mwanakijiji nimekupata, kuwa mwamuzi wa miwsho hapo ni spika aliyeteuliwa na JK, Ila nadhani wangekataa tu ili wananchi wajuwe moja kuwa ilkataliwa.

Unajuwa sometimes the message you send to the people matters big times...It signals what direction they should take.
 
Mhe. Lissu akanijibu kwa kusoma para ya pingamizi kwenye hotuba yake!. Jee kanuni hiyo ya 86 ndivyo ilivyoelekeza?!. Lissu alikosea pingamizi ni pingamizi tena amewekewa mpaka maneno ya kutamka na hivyo kusitisha process nzima!.
Mhe. Lissu aliposoma hotuba ya kambi ya upinzani, alimaanisha ameikubali hoja ya mtoa hoja, hivyo ku complete the process!.

Msifikiri Watanzania ni kama Wamisri, Walibya au Wasyria, Watanzania ni kama kondoo!. Wanaomkumbuka mwanaharakati wa UDSM enzi zile, Bi Sikitiko Kapile alisema Watanzania tuna nidhamu ya ukondoo na hivyo ndivyo tulivyo. Kama Chadema ina bank on peoples powers!, wait for surprises, they are wrong again and again and again!.
Pasco, kama Lissu angeweka pingamizi kwanza na baadaye akapewa fursa ya kusoma hotuba ya wapinzani ni kitu gani kingefuata? Nadhani hapo ndipo panapotatiza. Ukishasema tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kusema Lissu alikuwa sahihi au alikosea

Pili, katiba ni yetu na katika mazingira ya kawaida haikutakiwa tusikie CCM au Chadema. Kilichotokea ni kuwa CDM wameona uporaji wa haki kama walivyoporwa hoja na JK, wanatueleza sisi wenye katiba. Sisi wote tunapaswa tu-bank katika peoples power kwasababu ndiyo silaha yetu kwa sasa. Kwa mantiki hiyo tujadili namna ya kuikoa katiba yetu na si katiba ya CDM.
 
Utaratibu uliopitishwa sasa unakunyima vipi kutokufikia hicho unachotaka?? yaani katiba nzuri uipendayo??
Usije na speculations? kwamba ccm vile na vile??


Unampa rais mamlaka ya kunichagulia nani akusanye maoni yangu. Hiyo huyu alipewa kazi na rais atareport kwa boss wake = rais na sio mimi =mwananchi. Mimi (wananchi wa Tanzania) simwamini rais kusimamia hela zangu (bank kuu - EPA) au kumamia mali zangu nyingeni (wanyama hai - Qarta, Kagoda,etc) itakuwaje nimwamini asimamie ujenzi wa nyumba yangu? Cement itabaki kweli?
 
Pasco, kama Lissu angeweka pingamizi kwanza na baadaye akapewa fursa ya kusoma hotuba ya wapinzani ni kitu gani kingefuata? Nadhani hapo ndipo panapotatiza. Ukishasema tutakuwa kwenye nafasi nzuri ya kusema Lissu alikuwa sahihi au alikosea

Pili, katiba ni yetu na katika mazingira ya kawaida haikutakiwa tusikie CCM au Chadema. Kilichotokea ni kuwa CDM wameona uporaji wa haki kama walivyoporwa hoja na JK, wanatueleza sisi wenye katiba. Sisi wote tunapaswa tu-bank katika peoples power kwasababu ndiyo silaha yetu kwa sasa. Kwa mantiki hiyo tujadili namna ya kuikoa katiba yetu na si katiba ya CDM.
Ameshasema watanzania ni makondoo,hilo la people's power liondoe kwenye msamiati wake....
Pasco said:
Msifikiri Watanzania ni kama Wamisri, Walibya au Wasyria, Watanzania ni kama kondoo!. Wanaomkumbuka mwanaharakati wa UDSM enzi zile, Bi Sikitiko Kapile alisema Watanzania tuna nidhamu ya ukondoo na hivyo ndivyo tulivyo. Kama Chadema ina bank on peoples powers!, wait for surprises, they are wrong again and again and again!.
 
kitendo cha oversight ya opportunies provided by kifungu cha 86 cha kanuni za bunge kuuzuia huo muswada,

(a) Kanini hawakitumia kanuni ya 86 kuuzuia muswada usisomwe?.

(a). Amenisomea hitimisho la hotuba yake. Kanuni ya 86 ilimtaka Mhe. Lissu awasilishe pingamizi na sio hotuba!.

Mkubwa, hebu tuanikie hapa kanuni ya Bunge inayosema Mbunge mmoja anaweza kuzuia muswada usisomwe mara ya pili.

Usitaje namba ya kifungu tena, umeshakitaja, itandike hapa hiyo kanuni neno kwa neno tuione.
 
Unampa rais mamlaka ya kunichagulia nani akusanye maoni yango. Hiyo huyu alipewa kazi na rais atareport kwa boss wake = rais na sio mimi =mwananchi. **** mimi (wananchi wa Tanzania) simwamini rais kusimamia hela zangu (bank kuu - EPA) au kumamia mali zangu nyingeni (wanyama hai - Qarta, Kagoda,etc) itakuwaje nimwamini asimamie ujenzi wa nyumba yangu? Cement itabaki kweli?

Wananchi wote kwa pamoja wanawezaje kukusanya maoni yao??

Nani anaweza kuchagua watakaokusanya maoni kutoka kwa wananchi?? kwa niaba yao???
 
Mumwi, niko kwenye mobile hivyo sijaweza kuona status yako humu hivyo na presume wewe ni mgeni. Kumfananisha memba wa jf na yoyote ni kosa linaloitwa name calling na adhabu yake ni ban. Humu kwenye jujwaa la siasa tuna discuss issues na ideas hatujadili watu!.
Majukwaa ya kujadili watu pia yapo unaweza kuuliza na utajibiwa.

Mkuu soma thread yako, wewe mleta mada amesema mwenyewe yeye ndio uliuliza hayo maswali na umedai lissu amepiga chenga kukujibu wakati ulijibiwa vizuri tu.
Ila nakataa wanaokuita mnafiki, snitch nk mana kupishana mtazamo ni jambo la kawaida ndio ukubwa huo. Umetoa mtazamo wako na umetumia haki yako.
Tukuelimishe tu kuwa Chadema hawajakosea.
 
Mimi nafikiri hatua inayofuata ndio hasa sisi wananchi tutashirikishwa kutoa maoni kwenye tume itakayoundwa...
Na logic ni kwamba bunge linawakilisha wananchi katika muswada yote..hata hii ya katiba.

Kwa taratibu zilivyo (miswada) wabunge wanatakiwa wajadili muswada baada ya kupata maoni ya wananchi. Ni sawa na kwenda hotelini mhudumi anakuletea ugali bila kujua unakata chakula gani. Kumbe akitakiwa alete menu, wewe mteja unachagua anachotaka ndio ampe taarifa mpishi mengine yanafuata. Wabunge wa ccm wanajua tuna nini sisi wananchi?
 
Wananchi wote kwa pamoja wanawezaje kukusanya maoni yao??

Nani anaweza kuchagua watakaokusanya maoni kutoka kwa wananchi?? kwa niaba yao???

Kumbe walifanyaje walikwenda kwenye hiyo mikoa 3? Walipiga mbiu?
 
Back
Top Bottom