Katiba inasemaje kuhusu uteuzi wa Bashiru Ally?

Katiba inasemaje kuhusu uteuzi wa Bashiru Ally?

Hii pia siyo hoja kwa sababu kuwa kwako mtumishi katika chama haikuondolei haki ya kuhudumu kama mtumishi wa umma.
Ndiyo maana tuna watumishi wa umma ni makada wa vyama mbalimbali lakini hatuwahukumu kwa vyama vyao tutawahukumu kwa namna watakavyotekeleza kanuni na miongozo ya utumishi wa umma

..kwa hiyo mtu anaweza kuwa Katibu Mkuu wizara ya ulinzi, halafu akawa m-nec wa Chadema?🤣
 
Sijafuatilia kiapo chake ila nijuavyo Balozi ni mtumishi wa serikali, mara nyingi tumeona watumishi wa serikali wana teuliwa kuwa wabunge na kuteuliwa kuwa mawaziri muda huo huo na kesho yake wanaapishwa na Rais kuwa mawaziri kwa kiapo kimoja.

Pia kuwa Balozi sio lazima upangiwe kituo cha uwakilishi , ile ni uwakilishi na pia ni heshima ambayo mtumishi anaweza akapatiwa na Rais kwa utumishi wake ulio tukuka.

..hao lazima waende wakaape na bungeni.

..ninavyoelewa mimi balozi anakuwa na kituo, au anakuwa mkurugenzi makao makuu ya wizara.

..pia wako wengine ambao wamekuwa seconded kutumikia mahala fulani, lakini bado wanakuwa wanapanda ngazi za utumishi wizarani na hivyo kuwa mabalozi.

..ubalozi wa heshima sijawahi kuushuhudia hapa Tanzania.
 
Hebu soma post #12 hapo juu...

Ukiisha soma, je wewe unaweza kutuambia hii ina maana gani?

".....kutakuwa na Katibu Mkuu Kiongozi atakayeteuliwa toka miongoni mwa watumishi waandamizi walio katika Utumishi Wa umma...."

1. Huyu Bashiru Ally Lyakurwa, alikuwa ni afisa mwandamizi aliye katika Utumishi Wa umma?

2. Au Je, kuna kipengere cha katiba kinachoi - counter attack IBARA hii ya katiba ili kumpa Rais nguvu/mamlaka ya kumteua huyu ndugu kushika wadhifa huo kinyume na mwongozo na maelekezo ya ibara hii ya katiba...?

NOTE: By the way, kumbuka kuwa huu ni mjadala tu wa kujengeana ufahamu. Hakuna mtu mwenye tatizo binafsi na Ndg Bashiru Ally Lyakurwa au Rais John Pombe Magufuli...

Na in fact mjadala huu unaweza usibadili chochote katika hiki kilichokwisha kutendeka na kuamuliwa na Rais Magufuli hata kama tutajadili mpaka tuvue na nguo zetu...

Lakini all in all, hii haiwazuii watu kujadiliana na kuhoji...
we ndo umeweka uzio mzuri wa nini hoja ya msingi. bahat mbaya wanasheria na wajuvi weng hutawaona hapa kila kitu wanawazia kulipwa fee. na mbaya zaid wachangiaj weng hawajikiti kwenye hoja mana ufaham mdogo. tunaotaka kujifunza tunapotea njia mara. mijadala mirefu labda ihusu pipi mahaba! turud hapa.. MR BASHIRU ANAINGIA KUNDI LA WATUMISHI WA UMMA WAANDAMIZI?
 
Naomba kuuliza.hivi yule katibu mkuu kiongozi Martin luhanjo Naye alikua balozi?.kwakifupi ili mtu awe katibu mkuu kiongozi lazima awe balozi?
 
..kwa hiyo mtu anaweza kuwa Katibu Mkuu wizara ya ulinzi, halafu akawa m-nec wa Chadema?🤣
ideally inawezekana kabisa, ila mamlaka za teuzi kama zimekaa kisiasa basi zitaona tatizo, lakini kama tuko politicaly matured inawezekana!
Ndiyo maana Kitila Mkumbo alikuwa katibu mkuu wa wizara ya maji kabla ya kujivua uanachama wa ACT.
Alikuja kujivua baadae
 
Naomba kuuliza.hivi yule katibu mkuu kiongozi Martin luhanjo Naye alikua balozi?.kwakifupi ili mtu awe katibu mkuu kiongozi lazima awe balozi?
..huko nyuma tumewahi kuwa na makatibu wakuu kiongozi ambao sio mabalozi.

..na ambao walikuwa mabalozi ni kwasababu walipata kuwa watumishi wa wizara ya mambo ya nje.
 
ideally inawezekana kabisa, ila mamlaka za teuzi kama zimekaa kisiasa basi zitaona tatizo, lakini kama tuko politicaly matured inawezekana!
Ndiyo maana Kitila Mkumbo alikuwa katibu mkuu wa wizara ya maji kabla ya kujivua uanachama wa ACT.
Alikuja kujivua baadae

..Je, haiwezekani kuwa uteuzi wa Kitila Mkumbo nao ulikuwa na matatizo?
 
Katiba gani hiyo? Awamu ya 5 katiba ni kimtokacho raisi kinywani kwake
 
..hao lazima waende wakaape na bungeni.

..ninavyoelewa mimi balozi anakuwa na kituo, au anakuwa mkurugenzi makao makuu ya wizara.

..pia wako wengine ambao wamekuwa seconded kutumikia mahala fulani, lakini bado wanakuwa wanapanda ngazi za utumishi wizarani na hivyo kuwa mabalozi.

..ubalozi wa heshima sijawahi kuushuhudia hapa Tanzania.
Huapa bungeni baada ya Rais kuwaapisha na kuendelea na shughuli zao kama mawaziri, hakuna sehemu kikatiba inayosema uwape kwanza kwa kiapo fulani ndipo uwape cha pili ili uwanze kazi. Hivyo sijaona tatizo la Dk bashiri kuteuliwa kuwa balozi na katibu kiongozi kwa wakati mmoja. Labda kama kuna agenda ambayo haijulikani.
 
..huko nyuma tumewahi kuwa na makatibu wakuu kiongozi ambao sio mabalozi.

..na ambao walikuwa mabalozi ni kwasababu walipata kuwa watumishi wa wizara ya mambo ya nje.
Hoja iwe ni kushika nafasi mbili za utumishi je ni halali kisheria?

Hoja pia iwe ni je baada ya Bashiru kuapishwa kuwa katibu mkuu kiongozi, ubalozi wake umekoma?

Hoja iwe ni je kwenye payrol ataingia kama balozi au katibu mkuu kiongozi?

Nahisi hayo ndo maswali matatu ya msingi ya kujiuliza lakini siyo uhalali wa kumteua, kwenye kumteua kuwa Katibu mkuu kiongozi hajavunja katiba wala sheria
 
..Je, haiwezekani kuwa uteuzi wa Kitila Mkumbo nao ulikuwa na matatizo?
Uteuzi wa Kitila haukuwa na tatizo kwa sababu alimtoa ofisi moja ya utumishi ambayo ni (Lecturer kwenye chuo cha umma) na kumpeleka kwenye ofisi nyingine ya umma(ukatibu mkuu).
Watumishi wa umma kuhamishwa ofisi ni jambo la kawaida.

Utumishi wa Umma haupo kwa watu wasio na vyama peke yao, bali ni haki ya kila mtanzania mwenye vigezo bila kujali mrengo wake wa kisiasa
 
Huapa bungeni baada ya Rais kuwaapisha na kuendelea na shughuli zao kama mawaziri, hakuna sehemu kikatiba inayosema uwape kwanza kwa kiapo fulani ndipo uwape cha pili ili uwanze kazi. Hivyo sijaona tatizo la Dk bashiri kuteuliwa kuwa balozi na katibu kiongozi kwa wakati mmoja. Labda kama kuna agenda ambayo haijulikani.

..lakini wamekula viapo viwili.

..je, unao ushahidi kwamba Dr.Bashiru amekula viapo viwili?

..na kiapo cha balozi ni sawa na kiapo cha katibu mkuu kiongozi?
 
..basi tuletee kifungu ambacho ni sahihi, na kinachohalalisha uteuzi huu.

Ndugu yangu, huyu ndugu hana lolote anachojua...

Yeye yuko hapa kutetea chochote anachofanya Mr. President. Ni marufuku kuhoji. Why?

Ni kwa sababu wao wanaamini kuwa, mtu mwenye cheo cha Urais ni kila kitu kwa lolote analoamua, kufikiri na kutenda ñi sahihi...

Wanashindwa kabisa kuelewa kuwa, Rais amepewa mamlaka hayo ya "Urais" wa nchi hii na sisi wananchi wa Tanzania na tukampa/mwekea mwongozo wenye limits ndani ya katiba ili ku - execute madaraka na mamlaka yake moja baada nyingine kwa amani na furaha...

Sisi siyo shamba la wanyama (Animal Farm). Sisi ni nchi. Sisi ni watu..
 
Hakuna Katiba wala ibara yoyote iliyo vunjwa.
Inaonekana kuna baadhi ya watu wanaweweseka, maaana moto wa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dr. Bashiru sio wa mchezo.
 
..basi tuletee kifungu ambacho ni sahihi, na kinachohalalisha uteuzi huu.
Ahaa mkuu JokaKuu ibara ya 116 ya katiba ya JMT inazungumzia Court of appeal ya JMT.
Screenshot_20210227-203321.png
 
Back
Top Bottom