Dr Akili
JF-Expert Member
- Aug 21, 2011
- 5,119
- 4,569
Haya yanayotokea siyo kwa sababu katiba yetu ni mbovu, la hasha. Wala si kwa sababu tuna sheria mbovu, la hasha. Wala si kwamba tuna wanasheria wabovu, la hasha. Kazi ya mwanasheria ni kumwandalia kile ambacho mteja wake anataka, na matakwa hayo ya mteja wake mwanasheria atayatetea hadi mwisho.Wanabodi,
Hizi kelele za wanasheria manguli wabobezi na wabobevu kuhusu hii IGA ya DPW na Bandari zetu, sio za kuzipuuzia!. Katiba hii mbovu tuliyonayo!, Sheria zetu mbovu tuliyonayo, mikataba mibovu ya kimataifa tunayoingia, mwisho wa siku tunajikuta tumepigwa!, tunafunguliwa mashitaka, tunashindwa, tunapigwa tozo za mabilioni ya fedha!, ambazo ni lazima tulipe.
Haya yote ni matokeo ya kazi ya wanasheria wabovu na baadhi yao vilaza!. Leo nimeianza siku kwa bad news kutoka Marekani, Tanzania tumeshindwa kesi, tunadaiwa tozo ya dola za Marekani zaidi ya Millioni 100!, na lazima tulipe!.
Soma taarifa hii hapa chini
View attachment 2692021
Mungu ibariki Tanzania
- Kama Tanzania tulipitisha sheria kuwa kwenye uwekezaji hakuna mashauri yoyote ya nje ya nchi!. Mashauri yote ni hapa nchini kutumia sheria za Tanzania!, sasa haya mashauri yanaendelea vipi kupelekwa nje?.
- Hii maana yake ni ama tuna sheria mbovu, ama tuna wanasheria wabovu wanaotunga sheria mbovu, zinazotupa mikataba mibovu, na mwisho wa siku tunaishia kupigwa na kutozwa matozo ya ajabu ajabu!.
- Huku kila siku kushindwa kesi za kimataifa na kupigwa tozo nako ni ama tuna sheria mbovu za mikataba mibovu ama kama sheria ni nzuri, then tuna wanasheria wabovu wasio na uwezo wa kushauri the right thing to do!, hivyo serikali yetu inavunja mikataba kitutusa na mwisho wa siku tunaishia kuumizwa kwa kushindwa kesi na kupigwa tozo!.
- Kabla ya kuvunja mkataba wowote, serikali yetu inaomba ushauri wa kisheria kufanya kitu kinachoitwa mitigation, wanasheria hawa huishauri vibaya serikali yetu, mwisho wa siku, tunaishia kuumizwa!.
- Issues ya Richmond, Dowans, tukaunda tume, ikatoa matokeo kwa mbwembe kuwa Richmond ni kampuni hewa hata tukivunja mkataba, hatutashitakiwa popote!.
- Tukamfanya Edward Lowassa ni mbuzi wa kafara, tukavunja mkataba!.
- Tukashitakiwa tukashindwa, tukapigwa tozo!. Waliotushauri tuvunje mkataba wakajiapiza "over my dead body!, hatulipi". Tulilipa kisiri siri every cent!. Hawa wanasheria walifanywa nini?
- Mitambo ya Richmond ikanunuliwa na Simbion, tukaingia nao mkataba ule ule na tukawalipa!.
- Chuma JPM, alipoingia tukavunja mkataba wa Simbion, tukashitakiwa, tukashindwa, tukapigwa tozo, Chuma JPM, akagoma hatulipi!
- Mama kaingia, tumelipa fasta fasta, kimya kimya!. Wanasheria waliotufikisha hapa walifanywa nini?!.
- Tulipotunga sheria mbovu, watu humu tulishauri Zita Act Retroactively? Tutavunja Mikataba Yote Iliyopo? Can we Stand? Do we have the Guts?, leo baada ya kutuletea hii IGA mbovu, watu tumeeleza matatizo yake kibao!.
- Wanasheria hawa hawa, Bunge letu hili hili wanaipitisha hivyo hivyo ilivyo, wanaiambia serikali yetu hii IGA ni nzuri, safi na haina matatizo yoyote!.
- Wanasheria hawa wanao tufikisha hapa, tukiwaita ni wanasheria wabovu au vilaza, itakuwa ni kuwaonea?.
- Tanzania tutaendelea kufanywa shamba la bibi na kichwa cha Mwendawazimu na wanasheria wabovu na vilaza wa aina hii hadi lini?!.
Paskali
Haya yanayotutokea ni kwa sababu ya mikataba mibovu tunayoingia na wawekezaji wa nje. Wa kulaumiwa kwa mikataba hii mibovu ni watawala wetu (wanasiasa), wanasheria hutekeleza kile ambacho watawala wanataka.
Sheria zetu zinazohusu wawekezaji wa nje ni nzuri. Sheria zetu, kwa nia njema ya kuvutia wawekezaji wa nje ziliridhia Conventions za Umoja wa Mataifa za kulinda (guarantee) mikataba hii ya uwekezaji haswa kwa nchi zinazoendelea na hivyo kuzifanya conventions hizo kuwa sheria ya nchi yetu. Na ni karibu nchi zote duniani zilifanya hivyo. Conventions hizi ni zile za Multilateral Investment Guarantee Agency (MIGA) na ile ya International Center for Settlement of Investment Disputes (ICSID). Hivyo hata huyu DP World hakupaswa kuwa na wasi wasi wa kutafuta protection nyingine ya kwake tu kwa uwekezaji wake nchini kwetu.
Ni jambo bora kabisa kuvunja hiyo mikataba mibovu na kulipa hiyo USD 100m kuliko kuendelea kupoteza hayo madini yetu yote ya nickel yenye thamani ya mabillion ya dollars za marekani.
Hilo liwe funzo kwetu kuwa makini sana na mikataba ya uwekezaji tunayoingia. Timu za negotions tunazoziteua zinapaswa kufuatiliwa kwa karibu na security system yetu wakati zinapofanya majadiliano hayo kwani kick back ya 10m USD kwa kila member wa timu hiyo is just peanut kwa hawa foreign investors. Na timu hizi zinapaswa kusheheni wachumi wabobezi na watalaam wa mipango waliobobea, siyo wanasheria. Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali ndiyo inapaswa ku draft makubaliano hayo na kumshauri rais wetu. Na si vibaya wananchi na bunge letu wakashirikishwa kwenye hatua za mwisho za maandalizi ya mikataba hii hasa ile mikubwa. La sivyo tutaendelea kupigwa na vitu vizito.