Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Katiba Mpya: NEC ya CCM yatoa tamko kuwa serikali 2 ndio msimamo wa chama!

Wananchi wanataka serikali mbili. Ila vibaraka wa wazungu wakiongozwa na dr slaa ndo wanataka kulazimisha serikali tatu
Kabisa kabisa wanachi wote wanataka serikali mbili vibaraka wa wazungu kwa ulevi wao wa gongo eti serikali tatu sifa au?
 
Hii kali! Muungano tena basi. Serikali hii ya CCM ndio iliyoshindwa kuilinda na kuitetea Katiba ya sasa ya JMT pale Zanzibar ya Amani Karume ilipoamua kuivuruga.

Jakaya pamoja na viapo vyote akakaa kimya. Bunge la JMT nalo likakaa kimya badala ya kumchukulia hatua Jakaya.

Tundu Lissu aliwaambia wazi kilichofanywa Zanzibar kule Bungeni Dodoma. Hawakumsikiliza.
Unazmzungumzia Lisu gani? Huyu huyu aliyegaragazwa na Albert Msando, kijana mdogo kabisa hadi akaomba poo pale alipoomba watumie lugha ya kiswahili badala ya kiingereza?
 
Mpendwa Simiyu yetu, nakiri nimechanganyikiwa kidogo, mnaposema serikali mbili inamaana serikali ya Zanzibar na serikali ya Muungano au na serikali ya Tanganyika?
Kama sio na ya Tanganyika, kwa nini?
Ahsante!
 
SI KWELI , TENA UKOME KABISA KUPOTOSHA , TUWEKEE idadi YA WANACCM NCHI NZIMA , HAO MIL 2 WATAWEZAJE KUTUSEMEA SISI WOTE 45 ML ?
We mburula naona unataka kupasuka unapingana na ukweli ccm ya watanzania hutaki unaacha.
 
Msimamamo wa CCM ndio msimamamo wa wanyonge na wazalendo!

Hivi kuna mtu mnyonge ndani ya ccm?mbona wote ni wanene sana,hata Nape alipopewa ukuu wa wilaya alikuwa amekonda lakini ghafla alipoteuliwa na Baba Mwenye nyumba kushika wadhifa huu wa msema chochote ndani ya chama nae kabadilika,amenona kweli,na kuhusu wazalendo hawapo kabisa,Ze Marcopolo
 
Mpendwa Simiyu yetu, nakiri nimechanganyikiwa kidogo, mnaposema serikali mbili inamaana serikali ya Zanzibar na serikali ya Muungano au na serikali ya Tanganyika?
Kama sio na ya Tanganyika, kwa nini?
Ahsante!
Yaani umeishi miaka yote leo hujui muungano tunaoupenda wananchi?
 
Kikao cha siku 2 cha NEC ya Chama cha Mapinduzi(CCM) kimemalizika na kutoa taarifa kupitia katibu wa Itikadi na uenezi wa chama hicho,bwana Nape Nnauye kuwa wamekubaliana kuendelea na msimamo wa kuunga mkono serikali 2.

Pia,bwana Nape ameongeza kuwa watafanyia kazi changamoto za muungano zinazolalamikiwa.

Katika hatua nyingine,Nape amesema hawatishiwa na hatua ya vyama vingine kwenda kwa wananchi kwani hata wao(CCM) wanaweza kwenda kwa wananchi na kuwaeleza jambo hilo.


CHANZO:ITV

MY TAKE:
Hatua hii ni sawa na kutangaza mgogoro mapema!

NATABIRI - KIKAO hiki CHA BUNGE HUENDA NDIYO KIKAWA CHA MWISHO KABISA , KWA MSIMAMO HUU WA CCM NI LAZIMA KITANUKA TU , HAKUNA ATAKAYEKUBALIANA NA UJINGA HUO .
 
Mpendwa Simiyu yetu, nakiri nimechanganyikiwa kidogo, mnaposema serikali mbili inamaana serikali ya Zanzibar na serikali ya Muungano au na serikali ya Tanganyika?
Kama sio na ya Tanganyika, kwa nini?
Ahsante!
Mkuu nashukuru kwa kujielewa,
wewe ni mdau wa siasa kwa mda mrefu hapa jukwaani siku zote tunaongelea serikali zipi?
 
NATABIRI - KIKAO hiki CHA BUNGE HUENDA NDIYO KIKAWA CHA MWISHO KABISA , KWA MSIMAMO HUU WA CCM NI LAZIMA KITANUKA TU , HAKUNA ATAKAYEKUBALIANA NA UJINGA HUO .
Utasubiri sana mkuu,
haya hayatatokea watanzania wanajitambua siyo majuha.
 
Back
Top Bottom